Watanzania Waasia kwenye vyombo vya Usalama

Nakabiliwa na maswali machache:

a. Kwanini Watanzania wenye asili ya Uhindi au Uarabuni hawaingii kwenye vikosi vya usalama? Zamani nakumbuka tulikuwa tunawatania kuwa wao ni "watoto mayai" hawawezi kazi za shurba lakini nikagundua kuwa hata kule Uhindi na Uarabuni kuna majeshi na POlisi na wao wanapewa mafunzo ya kijeshi na kuhenyeka kama sisi. Hivyo suala la "umayai" halipo.

b. Ni juhudi gani zinafanyika kurecruit Watanzania hawa hasa kutokana na ujuzi wao wa mambo ya biashara, utaalamu wa IT, n.k n.k na hivyo kuleta vipaji ambavyo vinahitajika sana kwenye vyombo vyetu hivi?

c. NI kwa kiasi gani familia za ndugu zetu hawa zinawa encourage watoto wao kuitumikia nchi yao kwa zaidi ya siasa na biashara na kuingia kwenye utumishi wa umma. Watakuwa wanaendelea kutoa misaada tu mpaka lini.

Wahindi ni lazima wabadilike hilo halina ubishi...Wafanye tathmini wenyewe kwenye jumuiya zao waone ni kwa jinsi gani wataweza kufanya mambo ya kulisaidia Taifa na wananchi wao given the position they withhold in our society...Hilo tutalisimamia in any means neccessary....Na si kutowa misaada kwa ccm ambayo inaishia kwa mafisadi na rushwa kwenye uchaguzi ili kuendelea kuyalinda maslahi ya kibiashara nk.

Badala ya mawazo yao kuwa kwenye kuchuma na kupeleka nje na hatimaye kuhamia huko moja kwa moja...Wafikirie namna ya kuikwamua jamii ambayo imewawezesha kuupata utajiri wanaoupeleka nje ya nchi...Pia kuwa na utu na kuwathamini watu weusi na bila kuwanyanyapaa kwasababu zisizo za kimsingi.

Assimilation ni muhimu hilo halina ubishi kwetu tusiokuwa na mitizamo yoyote ya tofauti na uafrika halisi kwamba maslahi ya Afrika na mwafrika kwanza.

Katika nchi yeyote inayojidai kuwa ni demokrasia, uhuru wa raia wake kuchagua jinsi gani ya kutumikia taifa lake ni sacrosant. Mchango wowote atakaoutoa, katika nyanja yeyote ile ni lazima ithaminiwe. Tunapoanza kamchezo ka kusema kuwa utumishi katika sehemu fulani ndiyo uthaminiwe zaidi tutajiingiza kwenye matatizo. Mfanyabiashara anayewekeza na kutoa ajira kwa wanachi wake anastahili heshima sawa na mwanajeshi aliye klindoni katika mipaka ya nchi. Tusisahau kuwa utumishi katika hivi vyombo vya usalama si kila wakati ni matokeo ya uzalendo bali ni mtu kujipima uwezo wake ( shule aliyosoma, watu anaowajua n.k.) na kuona huko kuna uwezekano mkubwa wa kumpatia riziki. Vile vile mtu anayeamua kuingia katika biashara ni hivyo hivyo. Mara nyingi anafanya hivyo kutokana na sababu hizo hizo. Uwezo wake, network yake na kukosa nyenzo za kuingia sehemu nyingine. Mbona wengi tu baada ya vita vya Kagera, pamoja na kuahidiwa vyeo jeshini, tulikataa kujiunga? Utasema na sisi tulikosa uzalendo?

Kama tunaona tuna haja ya kuwa nao (kutokana na ujuzi,vipaji vyao au contact zao na si rangi yao au kabila yao) tuwatafute na kuwatongoza kujiunga na vyombo hivyo vya usalama kama vile ambavyo tunatakiwa kufanya kwa mtanzania mwengine. Rangi, uasili zitumike pale tu tunapoona kuwa hivyo vitatusaidia katika malengo yetu fulani. K.m. kama lengo letu ni kufanya espionage India basi bila shaka kuwa na mtu mwenye asili ya huko itasaidia. Au kama tunatarajia kuwa siku moja tutapigana na Oman, basi bila shaka kuwa na mtu mwenye asili ya huko kutasaidia. Lakini si vinginevyo. Kufanya vingine ni institutional racism. Kwetu sisi na sio kwa wao.

Hii institutional racism iko wazi katika tunavyojiangalia kama jamii. Kila kitu tunafanya kama vile mtanzania ni yule anayefanana na sisi. Hivi tumewahi kujiuliza ni vitu gani kati hizi institutions vinaendana tofauti na jadi zao? Wahindi wengi hawali nyama lakini katika vyombo hivi kama hauli nyama utakufa njaa! Si hicho tuu, sehemu nyingine utategemewa kushiriki katika kuchinja wanyama hawa. Mhindi leo umwambie achinje ng'ombe! Uchanganyikaji wa kijinsia katika vyombo hivyo inaweza ikawa kikwazo kingine. Si siri kuwa kama angetokeza mtoto wa Kihindi au Mwarabu wakati wetu wa JKT angegombewa na walafi kama mpira wa kona! Mzazi gani mwenye mapenzi na mtoto wake atamwachia aingie huko kama ana uwezo wa kumwepusha? Masingasinga dini yao inawakataza kukata nywele. Vyombo vyetu vya usalama, wembe ndiyo moja ya vitu vya kwanza ambavyo kichwa chako kitakutana nacho. Wanaume wote tuliopitia JKT tulinyoa mfano wa mustini! Institutional racism hii inaonekana vile na jinsi sisi tunavyowaangalia hawa jamaa kama vile wote ni matajiri na sleki. Akionekana mhindi, kitu cha kwanza kinachotuingia kichwani ni namna gani tunavyoweza kumminya ili atukatie kitu kidogo. Akitokea mhindi, mawazo yetu yote ni kuwa huyu ni lazima mkali wa hesabu na huko ndiko tunakompeleka. Katika vyama vingi vya professionals, nafasi ambazo wahindi wanapata bila matatizo mengi ni uweka hazina! hapana, wakuu, matatizo yako kwetu.

Katika dunia ya sasa hatuzungumzii asimilation bali integration. Katika assimilation unatakiwa ukane ulikotoka na uchukue identity ya nchi iliyokupokea. Katika integration, unategemewa kukubaliana na value za msingi lakini kubakia na tamaduni na lugha (yako ya asili na hiyo ya ugenini) n.k. Kwa wenzetu wanachukua hizi tofauti kama resources na si kikwazo. Canada wachina wa Vancouver wameiwezesha nchi yao mpya kupata biashara kibao na China n.k. Sisi kwetu tunaona mtu kupenda asili yao ni kukosa uzalendo. Leo tunamshangilia Obama ambae hafanyi siri ya kuwa na mapenzi makubwa na ukoo wa baba yake. Baba aliye mtelekeza.

Matumizi yetu ya majina kama mhindi, mwarabu, tukimzungumzia mtu ambae kwa generations amekuweko kwetu ni moja ya dalili ya kutowakubali hao. Wenzetu wanawatofautisha wananchi wao wenye asili ya nje kwa kutumia hyphens, African-Americans, Irish-Americans, Asian-Americans, Black-Britons n.k. Ni lini tutamwona mtanzania mwenye asili ya bara lingine na rangi iliyo tofauti na sisi kuwa anahaki sawasawa na sisi watengo? Haki hiyo ikiwa ni pamoja na kujichagulia wapi atakapotoa mchango wake kwa taifa lake!

Sisi tulio majority katika nchi hii. Inatubidi sisi tuwape nafasi na kuwahakikishia kuwa tunawathamini kama tunavyomthamini mtu mwingine. Ishara ya kuthamini huko ni jinsi tutakavyoheshimu utamaduni na imani zao kama vile tunavyoheshimu za wadengereko wenzetu.

Amandlaa........
 
Wako wachache ndiyo lakini angalia ni asilimia gani ya pesa wanazoihujumu nchi yetu kwa ufisadi. Katika mafisadi kumi golo, (Golo ni jinsi Watanzania weusi tunavyoitwa na hawa wahindi) kuna Mhindi mmoja ambae ndiyo mastermind na ndiyo mwenye kuchota asilimia tisini na tisa! Ni mpaka hapo Watanzania hawa wenye asili ya kihindi watakapoamua kuacha tabia yao ya kuweka mguu mmoja hapa Tanzania na mguu mwingine Uingerza au Canada ndipo tutaona mabadiliko. Kwa sasa generation hii ya kihindi bado haijaamua na hawana uzalendo na nchi yetu, wao ni pesa tu. Wataingia bungeni ili kuchunga masilahi yao binafsi ya kiuchumi na siyo ya nchi.
 
Wako wachache ndiyo lakini angalia ni asilimia gani ya pesa wanazoihujumu nchi yetu kwa ufisadi. Katika mafisadi kumi golo, (Golo ni jinsi Watanzania weusi tunavyoitwa na hawa wahindi) kuna Mhindi mmoja ambae ndiyo mastermind na ndiyo mwenye kuchota asilimia tisini na tisa! Ni mpaka hapo Watanzania hawa wenye asili ya kihindi watakapoamua kuacha tabia yao ya kuweka mguu mmoja hapa Tanzania na mguu mwingine Uingerza au Canada ndipo tutaona mabadiliko. Kwa sasa generation hii ya kihindi bado haijaamua na hawana uzalendo na nchi yetu, wao ni pesa tu. Wataingia bungeni ili kuchunga masilahi yao binafsi ya kiuchumi na siyo ya nchi.

Haya ni yale yale ya kuhukumu jamii nzima kwa vitendo vya wachache wao. Kama katika mafisadi kumi tisa ni wenzetu kwa nini tumshupalie huyu mmoja badala ya kuwalaumu hawa wengine kwa kuweza kurubuniwa na huyu mmoja? Wangapi kati yetu humu ndani ambao tuna uraia wa nchi nyingine au watoto wetu wana uraia wa nchi nyingine? Mbona hatuhukumiwi kuwa tunakosa uzalendo. Badala yake wengine tunaitwa hata kushika nafasi za juu katika serikali! Utawezaje kuangalia maslahi ya nchi bila kuangalia maslahi yako binafsi? Mafanikio yeyote ya nchi si yatakuwa lazima na impact katika maslahi yako binafsi? Vile vile mafanikio yako binafsi si ndiyo mafanikio ya nchi? Au unataka kutuambia kuwa uchumi wa nchi na uchumi wa wananchi wake ni vitu viwili tofauti?

Hatutaweza kuendelea hadi hapo tutakapoacha victim mentality na kuondokana na miwani ya ubaguzi. Tukubali mapungufu yetu na sio kila wakati kutafuta mchawi. Tuwakubali na kuwakumbatia wale wote ambao ni wananchi wenzetu na wanaoitakia mema nchi yetu bila kujali rangi yao, kabila yao, jinsia yao, ulemavu wao n.k. Vile vile tuwatenge, tuwakemee na kuwashughulikia wale wote wanaoturudisha nyuma katika safari yetu ya kutafuta maendeleo kwa wananchi wetu bila kujali rangi yao, kabila lao, jinsia yao n.k. Tuwalaani wakina Jeetu Patel si kwa sababu ni wahindi bali kwa sababu ni wezi. Tuwasherehekee wakina Issa Shivji si kwa sababu ni wahindi bali kwa sababu ni wenzetu katika vita ya kujikomboa.

Amandla....
 
Tuwalaani wakina Jeetu Patel si kwa sababu ni wahindi bali kwa sababu ni wezi. Tuwasherehekee wakina Issa Shivji si kwa sababu ni wahindi bali kwa sababu ni wenzetu katika vita ya kujikomboa.

Nakubaliana na wewe kuwa vitendo vibaya vya kifisadi vinafanywa na "wenzetu" wahindi wachache. Je hao majority waliobaki ni nani ataewahamasisha wawe kama akina Alnoor Kassam, Issa Shivji na Amir Jamal? The ball is in their court. Ningefurahi kuona kachero wa kihindi akipiga patrol mitaani!
 
Tuwalaani wakina Jeetu Patel si kwa sababu ni wahindi bali kwa sababu ni wezi. Tuwasherehekee wakina Issa Shivji si kwa sababu ni wahindi bali kwa sababu ni wenzetu katika vita ya kujikomboa.

Nakubaliana na wewe kuwa vitendo vibaya vya kifisadi vinafanywa na "wenzetu" wahindi wachache. Je hao majority waliobaki ni nani ataewahamasisha wawe kama akina Alnoor Kassam, Issa Shivji na Amir Jamal? The ball is in their court. Ningefurahi kuona kachero wa kihindi akipiga patrol mitaani!

Umekosea.The ball is in OUR court. Kwani huyo kachero unayemuona kila siku unamuuliza kabila lake kabla ya kuwa na imani yake? Kama sio, basi kwa nini lazima umuone wa kihindi? Kama wachina wanavyosema," rangi ya paka si muhimu ili mradi anakamata panya"! Hii obsession na rangi haitatufikisha popote.
 
Tuwalaani wakina Jeetu Patel si kwa sababu ni wahindi bali kwa sababu ni wezi.

Pole pole mkuu, innocent until proven guilty maana mkianza haya maneno ambayo ni irresponsible, akishinda kesi ambayo inaweza kua haina strong ushahidi, then utasema nini?

Mambo mengine ni kutumia akili kidogo tu kabla ya kuandika, kushitakiwa wizi ni one thing na ku-prove kwenye sheria ni absolutely another ishu.
 
Pole pole mkuu, innocent until proven guilty maana mkianza haya maneno ambayo ni irresponsible, akishinda kesi ambayo inaweza kua haina strong ushahidi, then utasema nini?

Mambo mengine ni kutumia akili kidogo tu kabla ya kuandika, kushitakiwa wizi ni one thing na ku-prove kwenye sheria ni absolutely another ishu.

Kaka yangu sijui uliondoka lini bongo, lakini in short legal system yetu imeparaganyika sana. Kuna uwezekano mkubwa kabisa kuwa ruling imeshatolewa hii kuwapeleka mahakamani ni formality tu. Wanayosema watu zinaweza kuwa ni irresponsibe statements, lakini zinatokana na actualities za behaviour za hawa watanzania wenzetu on the ground. Siungi mkono maneno ya kibaguzi dhidi ya Jeetu kwa sababu sio rangi yake imefanya awe hapo alipo, kwa kuna wengine wengi tu wenye rangi za kibongo mbona wako uraiani wanapeta ndani ya mashangingi na kupewa ulinzi juu. I can feel pessmism ya watu kama hawa, tusiwalaumu sana.
 
Hakuna kitu kinachoonesha utii wa mtu kwa nchi yake kama utayari wake kufa kwa ajili ya nchi hiyo. Ni kipimo cha juu kabisa cha mapenzi ya mtu kwa nchi yake. Lakini pia kuitumikia nchi katika nafasi mbalimbali kunaonesha jinsi gani mtu anavyolipenda Taifa lake.

Mojawapo ya vitu ambavyo havionekani sana katika Taifa letu ni Watanzania wenzetu wenye asili ya Asia (wahindi, Waarabu, n.k) kujiunga na vyombo vyetu vya usalama hasa majeshi yetu ya Ulinzi na Usalama.

Nikikumbuka vizuri baada ya uasi mwaka 1964 ni maafisa wachache wa kizungu ambao waliendelea na jeshi na ni mmoja ambaye aliendelea kuitumikia kwa muda mrefu tu. Sifahamu sasa hivi kama kuna maafisa wowote wa JWTZ ambao aidha wana asili ya Uhindi au Uarabuni.

Kwa upande wa Polisi kumekuwepo na maafisa kadhaa wa Kihindi na wenye asili ya Uarabuni lakini nadhani sasa hivi wengi watakuwa wameshastaafu. Nafahamu wapo vijana wachache ambao waliingia huko (namkumbuka Bi. Khadija K. binti wa kiarabu aliyejiunga toka Tanga) na pia Insp. Khan ambao at the time nilikuwa nashangaa kweli kuwaona kwenye jeshi letu.

Hata kwenye taasisi nyingine (ukiondoa za Kitaaluma) bado jamii hii ya Watanzania inakosekana sana. Sijui idadi yao kwenye TRA, Public service n.k

Kwa upande wa Magereza ndiyo sijui kabisa kama kuna watanzania wenye asili ya nje ya bara letu ambao wanaitumikia nchi yao hivyo. Wakati ambao nakumbuka tuliweza kuwaona Wahindi na Waarabu wengi ni wakati wa JKT ule. Sijui katika JKT hiii ya kujitolea inakuwaje.

BIla ya shaka unajiuliza "what is the point". Point yangu ni kuwa inaonekana aidha kwa makusudi au by default mchango wa Watanzania hawa unataka kuishia kwenye siasa na biashara au sekta binafsi na siyo kwenye utumishi wa umma.

Nakabiliwa na maswali machache:

a. Kwanini Watanzania wenye asili ya Uhindi au Uarabuni hawaingii kwenye vikosi vya usalama? Zamani nakumbuka tulikuwa tunawatania kuwa wao ni "watoto mayai" hawawezi kazi za shurba lakini nikagundua kuwa hata kule Uhindi na Uarabuni kuna majeshi na POlisi na wao wanapewa mafunzo ya kijeshi na kuhenyeka kama sisi. Hivyo suala la "umayai" halipo.

b. Ni juhudi gani zinafanyika kurecruit Watanzania hawa hasa kutokana na ujuzi wao wa mambo ya biashara, utaalamu wa IT, n.k n.k na hivyo kuleta vipaji ambavyo vinahitajika sana kwenye vyombo vyetu hivi?

c. NI kwa kiasi gani familia za ndugu zetu hawa zinawa encourage watoto wao kuitumikia nchi yao kwa zaidi ya siasa na biashara na kuingia kwenye utumishi wa umma. Watakuwa wanaendelea kutoa misaada tu mpaka lini.


Thanks Mwanakjj kwa kuleta hii thread. Well Ntaanzia Zimbabwe, siku zote na mara nyingi watu wanaoijadili Zimbabwe, Mugabe, na siasa za huko huwa wanamiss this point and I am again glad Mkjj u brought it up.

Ishu ya Zimbabwe na wazungu wao ex wakoloni wao in this perspective ni tofauti kabisa na hapa kwetu. I remember uo as recenty as yr 2000 kulikuwa na polisi wa chini kabisa wazungu, askari magereza wazungu, wanajeshi wazungu, makarani wa mahakama wazungu, mahakimu wazungu, waiters na waitresses wazungu, walimu katika shule za serikali wazungu, majaji wazungu hata postmen (Wale jamaa wanaoleta barua nyumbani wakipitisha nyumba hadi nyumba na vibaskeli) wazungu. N hata kulikuwa na madereva wa malori wazungu, manesi etc. In my opinion that was a true rainbow country.

Pamoja na kwamba wazungu wengi wameondoka lakini bado serikali ina waajiriwa wazungu although ni wachache sana. Wengi wa hawa watu hawajaondoka eti kwa sababu hawaipendi Zimbabwe, au they are not proud of being Zimbabweans bali ni kutokana na siasa chafu zilizowafanya wengi wao wawe ni victims of the system. Most of them are the countries bordering Zimbabwe wakisubiri hali iwe restored. Sitopenda kuingia kiundani kwenye hili japo najua tayari kuna watu watakuwa wanahoji uzalendo wa hao so called wazungu. Lakini tukumbuke Kuna wazungu ni wabunge wa upinzani kama Trudy Stevenson na Mr. Bennet, na maeconomist, wahandisi etc.

Hali hii ya intergration nchini Zim iliwezesha ile national healing kutoka kwenye ukoloni ambao ulikoma just in 1980. Nakumbuka that time hata Mugabe angemchagua mzungu mwenye sifa kuwa jaji mkuu ilionekana ni kawaida tu.......... Wtu wote bila kujali rangi, background walishirikiana kuijenga Zim na ikasifika kama ilivyokuwa.

Kubwa katika hoja hii ni ile hali ya kutotiliana wasiwasi, kutokujenga chuki na hasa zile state sponsored dhidi ya jamii fulani kwa manufaa binafsi ya kisiasa (Ndio hasa Mugabe anachokifanya), na kubwa zaidi kushiriki pamoja katika ujenzi wa taifa ambalo linakuwa ni promising for our grand, and grand kids.

Kwa Tanzania japo kisheria hizo jamii alizozitaja mkjj hazivunji sheria lakini kuna some gap ambayo haizungumzwi hadharani na ni time bomb. Leo hii JK akiteua jai mkuu muhindi itaonekana ni kawaida? Au mkuu wa TRA mwarabu watu watasemaje? Si jambo la ajabu kuona kwamba watanzania wengi wanawaona hawa jamaa kama ni foreigners na mbaya zaidi hata the ruling elite huwa wanajisahau na hata kusema hadharani kwa mfano aah yule mdosi (ikiwa na namna flani ya kibaguzi) tutamshughulikia. Nawafahamu wahindi na waarabu wengi tu hasa tuliosoma nao amabao wana uzalendo wa hali ya juu lakini jamii inawaona they are not one of us!!!!!!!!! Hii ni hatari kwa taifa changa na mskini kama hili ambao hatu ule umoja alioasisi JK snr. umenza kumomonyoka.

The bottom line ni k wamba jamii haiwaamini wahindi, waarabu, wazungu kwamba ni watanzania wenzetu. Na wao pia baadhi huwa hawapendi kuoneaka ni watz by 100%

Kwa hoja ya mkjj hivyo basi sio tu kweenye masuala ya kazi za umma, bali pia makazi, imani za kidini , national events zinapaswa kuwa participated kimchanganyiko. Otherwise halii hii itaremain kuwa time bomb na siku ikierupt tuashindwa kujua nani wa kumlaumu.
 
Pole pole mkuu, innocent until proven guilty maana mkianza haya maneno ambayo ni irresponsible, akishinda kesi ambayo inaweza kua haina strong ushahidi, then utasema nini?

Mambo mengine ni kutumia akili kidogo tu kabla ya kuandika, kushitakiwa wizi ni one thing na ku-prove kwenye sheria ni absolutely another ishu.

Huyo Mkapa mnayemwita Fisadi n.k. ni mahakama gani iliyomtia hatiani? Mimi ninawaasi watu wasimlaani mtu aliyefikishwa mahakamani kwa ajili ya rangi yake bali kwa kitendo anachotuhumiwa kufanya. Wewe mwenzangu mtetezi wa haki za binadamu unamhukumu mtu ambae hata mahakamani hajafikishwa. Wewe uliyewahi kutangaza kwa kujivuna kuwa inapuja wahindi wewe ni mbaguzi wa rangi! Unataka kuniambia kuwa mahakama ikimwona Jeetu kuwa hana hatia wote mtakubaliana nao? Leo hii wewe mzee wa dataz unasimama kupinga maneno irresponsible? Wewe ambae bila kutoa ushahidi ulidai kuwa Rais wetu ameteua mla rushwa akijua kuwa hivyo na kutangaza hivyo hadharani? Jisafishe kwanza mwenyewe kabla ya kuninyooshea kidole.

Hata hivyo nashukuru kwa kunionyesha makosa yangu na ninawaomba watanzania wasimseme Jeetu Patel na mtu yeyote mwingine wanaemshuku kwa kufanya makosa mpaka hapo mahakama itakapowatia hatiani. Kufanya hivyo, kama alivyoeleza, FMeS ni kuonyesha upungufu wa akili!

Amandla......
 
Tuwalaani wakina Jeetu Patel si kwa sababu ni wahindi bali kwa sababu ni wezi.

Jitu Patel, sasa hivi yupo kwenye process ya sheria ku-determine kama ni mwizi au sio, full stop!

Huyo Mkapa mnayemwita Fisadi n.k. ni mahakama gani iliyomtia hatiani? Mimi ninawaasi watu wasimlaani mtu aliyefikishwa mahakamani kwa ajili ya rangi yake bali kwa kitendo anachotuhumiwa kufanya. Wewe mwenzangu mtetezi wa haki za binadamu unamhukumu mtu ambae hata mahakamani hajafikishwa. Wewe uliyewahi kutangaza kwa kujivuna kuwa inapuja wahindi wewe ni mbaguzi wa rangi! Unataka kuniambia kuwa mahakama ikimwona Jeetu kuwa hana hatia wote mtakubaliana nao? Leo hii wewe mzee wa dataz unasimama kupinga maneno irresponsible?

The minute Mkapa, alipokingiwa kifua na rais wa sasa kuwa asisumbuliwe, tayari ukweli ukajiweka wazi kwamba ni fisadi kama alivyosema Dr. Slaa.

Wewe ambae bila kutoa ushahidi ulidai kuwa Rais wetu ameteua mla rushwa akijua kuwa hivyo na kutangaza hivyo hadharani? Jisafishe kwanza mwenyewe kabla ya kuninyooshea kidole. Hata hivyo nashukuru kwa kunionyesha makosa yangu na ninawaomba watanzania wasimseme Jeetu Patel na mtu yeyote mwingine wanaemshuku kwa kufanya makosa mpaka hapo mahakama itakapowatia hatiani. Kufanya hivyo, kama alivyoeleza, FMeS ni kuonyesha upungufu wa akili!

Amandla......

Sina mpango wa personal na wewe ni waste of time ya wananchi wengine, nina-deal na hoja, Jitu Patel ndio kwanza amefikishwa kwenye mkono wetu wa sheria hajahukumiwa kwa hiyo kumuita mwizi kama ulivyofanya simply wrong, mimi sijawahi kumhukumu mtuhumiwa yoyote aliyeko kwenye mikono ya sheria kwua ni guilty tayari kwa sababu unaweza kuwa-influence mahakimu wetu wakatoa hukumu ambayo ni biased, that is all hayo mengine ni yako hayanihusu! Na sina time ya kuwapotezea wananchi wengine hapa na nonesense!
 
Halafu unashangaa kwa nini Forum yako imedoda

ule mtego wako watu washaustukia na hiyo ndio faida mojawapo ya kusoma shule ya Msingi ya Kisarawe pale Kariakoo

watoto wa mjini huwa wanastukia mambo kwa mbaaali


sie wengine ndio watu ha HIA HIA kule kwako tutakuwa tunakuoan kama wakwe zetu tuuu

Let me wonder for a second

chimpanzee_thinking_poster.jpg


Sijui ni nani aliyekuwa na kimbelembele cha kuutangazia ulimwengu "mwanakijiji kaanzisha forum yake" bila kuomba au kujiuliza kwanini mwenyewe sikuamua kuitangaza hapa...
 
... .
Nakabiliwa na maswali machache:

a. Kwanini Watanzania wenye asili ya Uhindi au Uarabuni hawaingii kwenye vikosi vya usalama? Zamani nakumbuka tulikuwa tunawatania kuwa wao ni "watoto mayai" hawawezi kazi za shurba lakini nikagundua kuwa hata kule Uhindi na Uarabuni kuna majeshi na POlisi na wao wanapewa mafunzo ya kijeshi na kuhenyeka kama sisi. Hivyo suala la "umayai" halipo.

b. Ni juhudi gani zinafanyika kurecruit Watanzania hawa hasa kutokana na ujuzi wao wa mambo ya biashara, utaalamu wa IT, n.k n.k na hivyo kuleta vipaji ambavyo vinahitajika sana kwenye vyombo vyetu hivi?

c. NI kwa kiasi gani familia za ndugu zetu hawa zinawa encourage watoto wao kuitumikia nchi yao kwa zaidi ya siasa na biashara na kuingia kwenye utumishi wa umma. Watakuwa wanaendelea kutoa misaada tu mpaka lini.

Wakati mwingine naelewa kweli kwanini tunafeli mitihani mirahisi kweli kwa sababu mtu anajadili vitu ambavyo hata hakuulizwa na anaenda so deep kujibu vitu ambavyo hajaulizwa. Nimeuliza maswali matatu tu ambayo yana majibu rahisi na labda ya moja kwa moja. Mojawapo ya majibu ambayo mtu angeweza kutoa ni kusema "Sijui".

Lakini inasikitisha watu wameenda mbali kuanzia ukabila, udini, n.k na hivyo kujidhihirisha kuwa kwanza hawawezi kuangalia nini kimeulizwa na wanajibu vitu kutoka kwenye projection ya hisia zao na siyo mada iliyopo. Lakini la pili ni watu kujibu kitu ambacho wanadhania wameulizwa.

Ningekuwa mimi nakabiliana na maswali hayo ningechukua swali moja na kufanya hivi:

Bw. Mwanakijiji majibu ya maswali yako ni kama ifuatavyo (kwa kadiri ninavyojua)

Swali: 1: Kwanini Watanzania wenye asili ya Uhindi au Uarabuni hawaingii kwenye vikosi vya usalama? Zamani nakumbuka tulikuwa tunawatania kuwa wao ni "watoto mayai" hawawezi kazi za shurba lakini nikagundua kuwa hata kule Uhindi na Uarabuni kuna majeshi na POlisi na wao wanapewa mafunzo ya kijeshi na kuhenyeka kama sisi. Hivyo suala la "umayai" halipo.

Jibu: Mimi nafikiri hawaingii kwenye vikosi hivi kwa sababu x, y, na z. au Si kweli wapo sema kwa sababu ya a, b, na c idadi yao haionekani sana bla bla bla.

Swali 2: b. Ni juhudi gani zinafanyika kurecruit Watanzania hawa hasa kutokana na ujuzi wao wa mambo ya biashara, utaalamu wa IT, n.k n.k na hivyo kuleta vipaji ambavyo vinahitajika sana kwenye vyombo vyetu hivi?

Jibu: Kwa kweli juhudi zinazofanywa ni hizi x, y, z na zinafanywa na idara hizi au zile. au hakuna juhudi zozote zinazofanywa kwa sababu ya b, c, na m. Au Hakuna sababu ya kujaribu kuwarecruit kwa sababu m, n, o, p

Swali 3: NI kwa kiasi gani familia za ndugu zetu hawa zinawa encourage watoto wao kuitumikia nchi yao kwa zaidi ya siasa na biashara na kuingia kwenye utumishi wa umma. Watakuwa wanaendelea kutoa misaada tu mpaka lini

Jibu: Mimi sijui familia zao zikoje kwa kweli ningependa kumuuliza mmoja wa ndugu zetu hawa inakuwaje. AU, Familia zao zinajitahidi kuwahamasisha watoto kuingia kwenye shughuli hizi na zile kuliko hizi za utumishi wa umma hasa katika vyombo vya usalama lakini kutokana na b, x, c inakuwa vigumu bla bla bla.

Lakini watu wameshindwa kuangalia kilichoulizwa na wametoka na kwenda mbali na kuacha maswali yenyewe na kubakia wanabishana kuhusu rangi, dini, siasa, mahakamani, n.k

WELL, I know kwanini forum yangu inadolola! It takes guts to think and move beyond the status quo!
 
Kabla ya Sarakikya alikuwepo Mhindi kwa jina la Col Kashmiri. Huyu ndiye alitakiwa kuwa CDF wa kwanza Mtanganyika. He played an important role kwenye vita za Uganda pamoja na Col Marealle. Palikuwepo pia na wahindi kenye jeshi la Polisi.


..hivi colonel kashmir naye alienda vitani....huyu jamaa ni mzalendo kweli ...alikuwa na offer ya kupewa uraia wa uingereza kutokana na mke wake kuwa raia wa uingereza akakataa..na akaamua kumuacha mkewe ili abaki tanzania...tunaongelea miaka ile ya ujamaa ......... kama jeshi lingekuwa na nia ya kweli ya kupata minority recruits jeshini colonel kashmir angeweza kuwa ..agent mzuri wa kusajili minorities wenye uzalendo wa kweli kama wake...mimi najuwa wapo ..kwa sababu nimekaa na wengi....najuwa..

..i also see col.marealle retired ..and others..some of these officers ..with what ever they served ..none of them could be considered for any sort of generals....for the same case we discussed of nyarenda and morisho sareakikya..and other officers...
 
PM, what interest is there for the government to recruit minorities to join the public service especially the security organs or law enforcement agencies such as Police, TPDF, TISS FIU, PCCB, NPS?
 
Lakini watu wameshindwa kuangalia kilichoulizwa na wametoka na kwenda mbali na kuacha maswali yenyewe na kubakia wanabishana kuhusu rangi, dini, siasa, mahakamani, n.k

WELL, I know kwanini forum yangu inadolola! It takes guts to think and move beyond the status quo!

Mzee Mwanakijiji.

With all due respect etc. etc. hii ni www na si shule ambayo mwenzetu ni mwalimu! Maswali yakiwekwa humu yana-provoke debate ambayo hakuna anayejua itaelekea wapi au itaishia wapi! Kwangu mimi huu ndiyo mvuto wake. Kwa mfano kwa jinsi ulivyolileta swali lako ni lazima suala la ubaguzi lingeingia kwenye mjadala! Sasa, Mkuu, unatuambia tungekujibu kwa namna ulivyotaka tungefika kweli kurasa ya 10 ya ushee? Mimi nadhani forum itadolola kama watu watabakia kujibu maswali kama yalivyoulizwa au kama muulizaji angependa yajibiwe! Tofauti na shule ni kwamba ukileta swali haujui majibu utakayoyapata. Kwangu mimi hiki ninakifurahia maana napata nafasi ya kujifunza mengi. Tukibaki unakotaka (kama nimekuelewa vyema) ndiyo tutabaki kwenye Status Quo na kushindwa kufikiri nje ya box!

Amandla.......
 
Sina mpango wa personal na wewe ni waste of time ya wananchi wengine, nina-deal na hoja, Jitu Patel ndio kwanza amefikishwa kwenye mkono wetu wa sheria hajahukumiwa kwa hiyo kumuita mwizi kama ulivyofanya simply wrong, mimi sijawahi kumhukumu mtuhumiwa yoyote aliyeko kwenye mikono ya sheria kwua ni guilty tayari kwa sababu unaweza kuwa-influence mahakimu wetu wakatoa hukumu ambayo ni biased, that is all hayo mengine ni yako hayanihusu! Na sina time ya kuwapotezea wananchi wengine hapa na nonesense!

Touche!

Nilichosema ni hiki " Tuwalaani wakina Jeetu Patel si kwa sababu ni wahindi bali kwa sababu ni wezi." Nimemtumia Jeetu Patel kama mfano wa jamii na si yeye binafsi ndiyo maana nilitumia neno wakina na sio tuwalaani Jeetu Patel kama ambavyo ulivyoelewa. Nakubali hata hivyo nilistahili kuli-phrase better ama sivyo watu wangechukulia kuwa Jeetu Patel na wenzake ni wezi wakati mahakama haijatoa hukumu. Nashukuru umeliona hili na umesimama kidete kutetea uhuru wa mahakama na haki za watuhumiwa mbele ya sheria. Lakini, kwa mtazamo huo basi zile nyuzi zote zinazojadili swala la watuhumiwa wa kesi ya EPA ni makosa maana mahakimu na majaji wanaweza kuzipitia na kuwa influenced katika maamuzi yao? Kwa sababu wengine pengine ni wanachama humu, tunaweza kuwapotosha wakawa biased katika kuhukumu? Au hata zile zinazozungumzia maswala yaliyoundiwa tume tayari ni hatari maana zinaweza kuwapotosha members wa tume hizo? Watu kama Mzee Mwanakijiji wanatakiwa walaaniwe kwa kushikia bango ishu ya vifo vya watoto wa Tabora wakati tume ikiendelea na kazi ya kuchungua kilichotokea?

Hiyo sentensi yako ya mwisho sina matatizo nayo isipokuwa hilo neno la mwisho! Kuna ka-e umekaongezea. Ninasema hivi kwa vile umelitumia mara nyingi na mara zote unakosea spelling. Kwa hali hiyo sitegemei majibu kutoka kwako maana si najua haupendi kubishana na fools kama mimi kwa kuhofia kuwa wasomaji hawataweza kutofautisha nani ni fool!

Amandla........
 
kule kwa mwanakijiji forum hatuendi na mwenyewe anajua hilo. Mtu anaendekeza udini bila sababu zzote zilizo na msingi bwana!

jamani ule ni mtego sie tuta kufa humu humu na huyu invisible wetu

kule sie tutakuwa tunapita njia tuu lakini ndani hatuingiii
 
Mzee Mwanakijiji.

With all due respect etc. etc. hii ni www na si shule ambayo mwenzetu ni mwalimu! Maswali yakiwekwa humu yana-provoke debate ambayo hakuna anayejua itaelekea wapi au itaishia wapi!



Debate inapotoka kwenye hoja na kuanza kuwa vioja kama mtoa hoja ninayo haki ya kuurejesha mjadala ili uelekeee kule ambako naamini ulipaswa kuwa. Na kwa vile hii ni www mtu akiona anataka kujadili kitu kingine anao uhuru wa kuanzisha thread nyingine to deal with that particular issue.

Kwangu mimi huu ndiyo mvuto wake. Kwa mfano kwa jinsi ulivyolileta swali lako ni lazima suala la ubaguzi lingeingia kwenye mjadala!

Siyo lazima, isipokuwa mtu anapolazimisha suala la ubaguzi kwa sababu swali langu halihusiani hata chembe na ubaguzi isipokuwa pale mtu anapoproject his/her own biases.

Sasa, Mkuu, unatuambia tungekujibu kwa namna ulivyotaka tungefika kweli kurasa ya 10 ya ushee?

Kulikuwa na ulazima wa kufika kurasa 10 na ushee kwa majibu yasiyohusiana na swali?


Mimi nadhani forum itadolola kama watu watabakia kujibu maswali kama yalivyoulizwa au kama muulizaji angependa yajibiwe!

Hapana forum itaonesha ukomavu kwani watu watakuwa hatimaye wanajadili issue na siyo kupiga soga tu alimradi wajaze kurasa.


Tofauti na shule ni kwamba ukileta swali haujui majibu utakayoyapata.

Hii ni flawed, swali likiulizwa majibu yake hayajalishi yanatoka wapi majibu hayo kama ni ya kweli yatafanana. Tofauti itakuwa ni jinsi yanavyotolewa kwani shuleni yanatolewa kwa msingi wa lugha na mtindo wa kitaaluma wakati kwenye mtandao ni free style.
Kwangu mimi hiki ninakifurahia maana napata nafasi ya kujifunza mengi. Tukibaki unakotaka (kama nimekuelewa vyema) ndiyo tutabaki kwenye Status Quo na kushindwa kufikiri nje ya box!

Tatizo ni kuwa wakati mwingine watu wanapojaribu kufikiri nje ya box wanajikuta wamejiingiza kwenye box jingine kumbe walichofanya ni kutoka kwenye box dogo na kuingia kwenye box kubwa. Kwangu mimi haitoshi kufikiri nje ya box tu bali kwenda mbali na box kabisa!


Amandla.......

ngaetu!
 
kule kwa mwanakijiji forum hatuendi na mwenyewe anajua hilo. Mtu anaendekeza udini bila sababu zzote zilizo na msingi bwana!

jamani ule ni mtego sie tuta kufa humu humu na huyu invisible wetu

kule sie tutakuwa tunapita njia tuu lakini ndani hatuingiii

kwanza, hukaribishwi; na ukija utatimuliwa summarily! Ndiyo raha ya kuwa dikteta mkarimu!
 
Re: Watanzania Waasia kwenye vyombo vya Usalama

Siyo lazima, isipokuwa mtu anapolazimisha suala la ubaguzi kwa sababu swali langu halihusiani hata chembe na ubaguzi isipokuwa pale mtu anapoproject his/her own biases.

With all due respect, etc etc. Mzee Mwanakijiji. Unakuwa disingenuous unaposema swali lako halihusiani hata chembe na ubaguzi. Kichwa chenyewe cha thread kimekaa kibaguzi. Au unataka kutuambia makabila yote 120 ya nchini mwetu yanawakilishwa kwenye vyombo vya usalama? Kwa nini uone kuwa ni watanzania waasia ndiyo hawamo kwenye vyombo hivyo? Kwa nini usiulizie wamatengo wengine? Kwa nini usiulize waztanzania wazungu? Hapana, Mkuu, swali lako limekaa kibaguzi ndiyo maana sisi wengine kila wakati tutakurudisha huko. Na ndiyo uzuri mwingine wa www. Hata kama mwenye hoja hatapendezewa wachangiaji wana uhuru wakuipeleka hoja wanakotaka!

Haya, dikteta mkarimu. Mbona siioni forum yako? Au hautaki mafundi mchundo huko?

Amandla......
 
Back
Top Bottom