Rohombaya
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 13,055
- 10,337
Watanzania wenzangu mimi naona wakati umefika wa kutonunua bidhaa za makampuni ya mafuta yalioyokuwa vinara wa mgomo wa kuuza mafuta mara baada ya bei kupunguzwa. Kwa mawazo yangu mimi kile kiasi kilichopunguzwa kwa kiasi kikubwa hakikuwa ni sehemu ya faida yao bali tozo zilizokuwa zinaingia serikalini hii inamaana kwamba kuna ukwepaji mkubwa wa malipo ya tozo hizo ndio maana wanafaidika nazo. Wao walijali maslahi yao zaidi wakakosa utu na wakasahau kuwa "mteja ni mfalme".
Tuwasusie, tusinunue bidhaa zao wajue kuwa nasi ni sehemu muhimu kwenye biashara zao ili wawe na adabu siku zijazo.
Nawasilisha
Tuwasusie, tusinunue bidhaa zao wajue kuwa nasi ni sehemu muhimu kwenye biashara zao ili wawe na adabu siku zijazo.
Nawasilisha