Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,708
- 5,711
Kama kuna taifa ambalo Mungu amelibaliki ni taifa la Tanzania. Maana udini na ukabila ni vitu ambavyo havina nafasi kabisa.
Naongea maisha ambayo ni uhalisia wa maisha yetu sisi watanzania. Ukisoma na mtu awe na dini au kabila tofauti huyo anakuwa ndugu yako. Mimi najua kila mtanzania analifahamu hili ndio maana leo hii unaweza ukawa na rafiki Muislamu na wewe ni Mkristo, msaada wake ukawa mkubwa zaidi ya ndugu yako wa damu.
Leo baraza la mawaziri limetangazwa lakini watu badala ya kujadili mtu aliyeteuliwa kama anafaa au la watu wanajadili dini na makabila ya wateuliwa. Hii ni picha mbaya sana hasa kwa watu wanaofikiri kwa akili timamu.
Alipokuwa madarakani Mzee Ally Hassan Mwinyi baadhi ya watu wasio makini walimtuhumu kuwa ni mdini tena anakumbatia waislamu watupu. Mbaya zaidi alijisahau akaruhusu Zanzibar/ Tanzania visiwani ikajiunga Oic. Lakini ukweli ni kuwa mzee mwinyi hakuwa mdini au mkabila. Waziri mkuu wake alikuwa mkristo tena Mgogo. Na hata Cabinet yake ilikuwa na wakristo wengi kuliko waislamu.
Historia ipo wazi,hata Mwl JKN watu walimtuhumu kuwa mkatoliki na hashauliki na hii ni sababu watu wanatoa maoni kwa hisia bila kujali ukweli na uhalisia.
Leo hii Cabinet imetangazwa,lakini badala ya watu kujadili uwezo wa mtu aliyeteuliwa kama anaweza kutumikia watanzania watu wanaanza kujadili kabila na dini za wateuliwa. Huku ni kukosa busara na kupungukiwa akili za kufikiri.
Wapi katiba ya JMT imetamka juu ya kuwa na uwiano sawa wa kidini au kikabila? Hili taifa halina dini wala kabila. Tunapojadili masuala ya msingi ya taifa letu tutumie busara na hekima.
Naongea maisha ambayo ni uhalisia wa maisha yetu sisi watanzania. Ukisoma na mtu awe na dini au kabila tofauti huyo anakuwa ndugu yako. Mimi najua kila mtanzania analifahamu hili ndio maana leo hii unaweza ukawa na rafiki Muislamu na wewe ni Mkristo, msaada wake ukawa mkubwa zaidi ya ndugu yako wa damu.
Leo baraza la mawaziri limetangazwa lakini watu badala ya kujadili mtu aliyeteuliwa kama anafaa au la watu wanajadili dini na makabila ya wateuliwa. Hii ni picha mbaya sana hasa kwa watu wanaofikiri kwa akili timamu.
Alipokuwa madarakani Mzee Ally Hassan Mwinyi baadhi ya watu wasio makini walimtuhumu kuwa ni mdini tena anakumbatia waislamu watupu. Mbaya zaidi alijisahau akaruhusu Zanzibar/ Tanzania visiwani ikajiunga Oic. Lakini ukweli ni kuwa mzee mwinyi hakuwa mdini au mkabila. Waziri mkuu wake alikuwa mkristo tena Mgogo. Na hata Cabinet yake ilikuwa na wakristo wengi kuliko waislamu.
Historia ipo wazi,hata Mwl JKN watu walimtuhumu kuwa mkatoliki na hashauliki na hii ni sababu watu wanatoa maoni kwa hisia bila kujali ukweli na uhalisia.
Leo hii Cabinet imetangazwa,lakini badala ya watu kujadili uwezo wa mtu aliyeteuliwa kama anaweza kutumikia watanzania watu wanaanza kujadili kabila na dini za wateuliwa. Huku ni kukosa busara na kupungukiwa akili za kufikiri.
Wapi katiba ya JMT imetamka juu ya kuwa na uwiano sawa wa kidini au kikabila? Hili taifa halina dini wala kabila. Tunapojadili masuala ya msingi ya taifa letu tutumie busara na hekima.