Watanzania tuwe makini sana na watu kama Dkt. Diallo. Ni watu wa maslahi zaidi

Natoa rai kwa wana CCM wote tuisusie Sahara media ya Antony Dialo kwa sababu ya uasi wake.

Fisadi Dialo hapaswi kuchekewa na yeyote mpenda haki na asiye mnufaika wa magenge ya kihuni ndani ya CCM.

Kidumu chama cha mapinduzi.

Wanaccm wengi ni wazee, au vijana maslahi, hivyo hamna impact yoyote kwenye nchi hii.
 
Natoa rai kwa wana CCM wote tuisusie Sahara media ya Antony Dialo kwa sababu ya uasi wake.

Fisadi Dialo hapaswi kuchekewa na yeyote mpenda haki na asiye mnufaika wa magenge ya kihuni ndani ya CCM.

Kidumu chama cha mapinduzi.
Someone somewhere has said his days are set off and it is part of the sanctions. Very soon he gonna close down everything of economic generation.
 
Mama anaupiga mwingi sana 😂😂😂😂sasa hivi Diallo anaupiga mwingi. Uchaguzi ungekuwa unafanyika mwaka huu Diallo angeteuliwa na wapinzani uchwara kugombea kama rais.
Ni Mkiti sasa,chama aliko siyo uchwara? Akihamia kwingine uchwara
Anadai hela zake mmlipe
 
Narudia tena, alichosema Diallo ni ukweli, na ukweli huo huwa tunausema humu jukwaani mara Kibao. Alichokifanya huyo Diallo ni kwenda kinyume na wanaccm wengi kuficha ukweli unaokidhuru chama chao...
Nakwambia hivi issue sio ukweli hapo bali alichoongea kimewapendeza bila kujali kwamba ni kweli au sio kweli. Huo ndio ukweli wenyewe usiotaka niseme.
 
Et alichoongea ni kweli, tangu lini mkapenda ukweli? alichoongea kimewapendeza ndio maana mnakishabikia ila kama huo mnaoita ukweli ungekuwa unamuhusu Lissu au Mbowe hali ingekuwa tofauti hapa.
 
WEE, ushindwe na ulegee! nisusie sahara media halafu nitaipata wapi STAR TV nyingine ya kuangalia?!!!!!
 
Nakwambia hivi issue sio ukweli hapo bali alichoongea kimewapendeza bila kujali kwamba ni kweli au sio kweli. Huo ndio ukweli wenyewe usiotaka niseme.

Hajaongea kipya, ila ni mwanaccm pekee aliyekiri huo ukweli hadharani. Hayo aliyosema tunayosema kila siku humu, tena yeye bado kakiri ukweli huo kwa kuumauma maneno.

Kwani watu kuporwa fedha na TRA ni uongo, watu kubambikiziwa kesi na kodi ni uongo, rais mwenyewe si kasema watu wamebambikiwa kesi? Watu kuporwa fedha kwenye Bureau de change ni uongo? Kuna uongo gani hapo?
 
Maybe you missed the point..

Kuwa kichaa ulidhani ni hadi mtu akae barabarani na nguo kuukuu?...
Naongezea hata akiwa na suti anakula mahindi ya kuchoma barabarani na kuanza kusema akina mama mnataka kupanuliwa mbele ama nyuma.
 
Alikuwa mwehu ila Diallo pia alishirikiana na mwehu kwahio na yeye ni mwehu na mnafiki pia! Hapo imekaaje!?
Mnafiki? Hapan shaka, alikuwa. Mwehu? 🤔 labda. Lakini naona ni mtu maslahi zaidi.

Unajua watu maslahi wakijua mwehu kashikilia kibubu cha taifa basi watamwimbia nyimbo za utukufu hadi siku kitakapomponyoka. Hapo ndipo fahamu zao za unafiki hugeukia upande wa pili.
 
Natoa rai kwa wana CCM wote tuisusie Sahara media ya Antony Dialo kwa sababu ya uasi wake.

Fisadi Dialo hapaswi kuchekewa na yeyote mpenda haki na asiye mnufaika wa magenge ya kihuni ndani ya CCM.

Kidumu chama cha mapinduzi.
Tayari kishaanza kusuaiwa na watangazaji wake wote watahammia vyombo vingine na huduma zake atazifunga sio muda mrefu.

Alidai atagombea uenyekiti huko Mwanza mwakani, asahau hawamtaki.
 
Huyo Mzee achana naye , he is no longer relevant.
Kwako wakijani ni relevant kwako,ila sii kwa wengi,ukweli mchungu,usioupenda kuusikia na hampendi kuusikia.Kisu chake kiligota kwenye mifupa ya wengi.
 
Uko vyema kuhusu moral authority na chuki binafsi ya Diallo. LAKINI, kasema ukweli wenyewe ambao si rahisi kuukanusha. Unaweza kusema kajisahau karopoka, bado unabakia kuwa ukweli mtupu.

Wakubwa wengi huko CCM wanajua hivyo; wako kimya kwa sababu za kimaslahi au “ustaarabu” tu wakijua leo hii hawana moral integrity ya kumsema mwendazake.
 
Tayari kishaanza kusuaiwa na watangazaji wake wote watahammia vyombo vingine na huduma zake atazifunga sio muda mrefu.

Alidai atagombea uenyekiti huko Mwanza mwakani, asahau hawamtaki.
Unajilisha matango pori tu.

WanaCCM wote wenye akili timamu wanaamini na walikuwa wanjua alichosema Diallo. Amesema ukweli mchungu. Hivyo ndivyo wengi wanvyosema wakiwa uwani.

Kumshambulia Diallo hakubadilishi ukweli.
 
Hajaongea kipya, ila ni mwanaccm pekee aliyekiri huo ukweli hadharani. Hayo aliyosema tunayosema kila siku humu, tena yeye bado kakiri ukweli huo kwa kuumauma maneno. Kwani watu kuporwa fedha na TRA ni uongo, watu kubambikiziwa kesi na kodi ni uongo, rais mwenyewe si kasema watu wamebambikiwa kesi? Watu kuporwa fedha kwenye Bureau de change ni uongo? Kuna uongo gani hapo?
Nasema hivi hoja si ukweli au uongo bali ni mambo ambayo mnapenda kuyasikia, na ndio maana imekuwa issue kubwa ya kufungua nyuzi kibao humu pamoja na kusema si jambo jipya.
 
Wala huna haja ya kuwaambia watu kuwa Dialo ni nani, wengi wanamfahamu, alijitoa sana kupitia vyombo vyake vya habari kumnadi Meko 2015!!na ndio wale wale tu , kwa sasa tujadili hoja hiyo aliyoitoa je ina mashiko?..
Legacy ya Magufuli haiwezi kufutika kwa maneno matupu ya chuki, Magufuli alikuwa mtu wa vitendo na siyo maneno matupu.

Mtu anayeweza kufuta Legacy ya Magufuli ni yule atakayetenda na kuacha alama zaidi ya zile alizoacha Magufuli.

Sent from my itel W6004 using JamiiForums mobile app
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom