Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,440
- 113,448
- Thread starter
- #181
Kwa vile mpaka sasa Mungu bado hajasema ...Wanabodi,
Hivyo mimi naunga mkono hoja ya rais mwanamke ile 2025, kwasabubu kiukweli kabisa, wanawake wana uwezo sana wa uongozi na wengine kuliko hata wanaume, ila siku zote, tumekuwa tukiwakandamiza kutokana na kutawaliwa na mfumo dume kwa miaka nenda miaka rudi, na mpaka Mungu alipoingilia kati. Kama Mungu asingeingilia kati na JPM akaendelea hadi 2025, CCM isingemsimamisha mgombea mwanamke, lakini baada ya Mungu kuingilia kati na Tanzania kwa mara ya kwanza tukapata rais mwanamke, na Mama Samia ameisha onyesha na kuthibitisha pasipo shaka kuwa wanawake wanaweza, then why not 2025 asiwe mwanamke sasa sio tena kwa kudra za Mwenyeenzi Mungu bali kwa chaguo la Mungu kwa Tanzania na kupata endorsement ya Watanzania kwenye sanduku la kura, kumchagua rais mwanamke na wabunge na madiwani wanawake wa kutosha. Na hili likifanyika na likakamilika kikamilifu, uchaguzi wa 2025 tukapata 50/50 ya wabunge na madiwani wanawake wa kutosha. Kazi ya kwanza ya Bunge jipya ni kufuta viti maalum, vitakuwa havihitajiki tena, vikiendelea kubaki ni wastage of time, money and resources.
Marais wa Nchi Hupangwa na Mungu, hata JPM alikuwa ni Chaguo la Mungu kwa Tanzanzia, ila Mungu huweza kulikatiza chaguo lake wakati wowote na kumchagua mwingine, hii haikuanza leo, toka enzi za Nabii Musa, alikatizwa hakuingia nchi ya ahadi Canan, kwa sababu fulani. Everything happens for a reasons anazojua Mungu mwenyewe, hivyo hata Samia ni mpango wa Mungu kwa Tanzania labda hadi 2025 ni Mungu tuu mwenyewe anajua. Kama Samia ni mpango wa Mungu kwa Tanzania 2025 -2030, then Mungu atasema nasi hapa katikati kabla ya 2025, kwasababu hata JPM, hakuna aliyejua Mungu alipanga nini, vivyo hivyo kwa Samia 2025, ni Mungu tuu pekee ndiye ajuaye amepanga nini na amempangia nani, lakini kwa utaratibu wa CCM, urais huu wa sasa wa Mama Samia ulioletwa kwa kudra tuu za Mwenyezi Mungu, hii ni awamu yake ya kwanza, hivyo kila mtu anajua utaratibu wa CCM, anajua uchaguzi wa 2025 ndio awamu yake ya pili ya Mama Samia but only if ndivyo na YEYE alivyopanga!.
Swali linabaki, Jee Samia ndio mpango wa Mungu kwa Tanzania, 2025 ....
2025 Twende na Mwanamke!.
Paskali
Update
Kuna HII sauti imeibuka!.
Naunga mkono hoja Hongera Spika Dkt. Tulia Ackson. Kuna haja MaSpika wetu iwe lazima kuwa Wanasheria?Spika Tulia kaiva sana kwenye suala kutafiri Sheria, naangalia hapa Bunge live wanapitisha muswada wa tume ya uchaguzi naona anamtoa knout mpaka AG huyu dada ni balaa wabunge wote wanampigia makofi.
Mbeya tunasema Tulia mitano tena.
Tena sio Tulia mitano tena bali 2025 could be ni Dr. Tulia!.
Angalia tulikotoka nae
1. Hivyo japo ni mimi niliyemtabiria Dr. Tulia uspika, Voices from within: Nimesikia sauti, Dr. Tulia Ackson ndiye Spika ajaye! Sauti hiyo imenieleza Ndugai, japo atatamani aendelee lakini...
2. Fursa ya Spika mpya ilipojitokeza, niliwaomba CCM Kujiuzulu kwa Ndugai ni mpango wa Mungu kwa Tanzania ili tupate Spika Bora. CCM itateua Spika Bora au Bora Spika kama kawa?
3. Hivyo Dr Tulia aliposhinda nikamshauri Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana!
4. Kwa vile Rais Samia amesisitiza 2025 twende na Mwanamke Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye! wengi wanadhani Mwanamke wa 2025 ni lazima awe Rais Samia, anaweza kuwa ni Dr. Tulia!.
5. Sababu ya kwanini 2025 anaweza kuwa ni Dr. Tulia ni HII
P