Watanzania wenzangu mie nafikiri kwa hali ilivyo tete kuhusu mgomo wa madaktari, tuna haki na sababu ya msingi ya kumbana Rais Kikwete atuhakikishie usalama wetu na hatma ya afya zetu. Yeye mwenyewe kwa hiari yake alitupigia magoti akatuomba tumchague kuongoza serikali na akatuahidi maisha bora kwetu sote. Hata kama hatukumchagua sote au kama isemwavyo kwamba alichachua matokeo ila pia alikula kiapo cha kutimiza hayo. Na ili kumwezesha yeye kutuletea hayo maisha bora sisi Watanzania tunamlipa kodi.
Katika hili la mgomo Raisi Kikwete ndo mdaiwa wetu kwani ndo tuna mkataba naye na sio madaktari!
Nawasilisha wakuu!
Katika hili la mgomo Raisi Kikwete ndo mdaiwa wetu kwani ndo tuna mkataba naye na sio madaktari!
Nawasilisha wakuu!