Watanzania tusipomuunga mkono Rais Magufuli tutakuja kulia kwa kusaga meno kama walibya

Developer IOS

JF-Expert Member
Jun 20, 2017
1,457
1,409
Aslam aleykum, bwana Yesu asifiwe wana board,

Kwanza naomba nimshukuru Mungu kwa kutuamsha tena katika Jumapili tulivu sana kwenye nchi yetu iliojaa amani.

Africa ni bara lililojaliwa rasilimali nyingi sana lakini ndio bara masikini kuliko mabara yote hii ni kutokana na aina ya uongozi wa rushwa ufisadi na wizi ambao rasilimali hunufaisha watu wachache waliopo kwenye system.

Wakuu ni marachache sana Africa inakuwa inapata viongozi wenye mapenzi ya kweli na uzalendo dhidi ya nchi zao viongozi wenye dhamira ya zati ya kuzikomboa nchi zao dhidi ya ufisadi rushwa na unyonyaji dhidi ya neo-colonialism.Siku zote ukiingilia maslai ya mzungu especial dollar lazima utengenezewe visanga na wapandikizwe wasaliti wachache ili wakung'oe.

Tunaona Gadaffi alivyoingia cha kwanza alisimamia rasilimali ya mafuta iwanufaishe walibya wote wazungu walipogoma aliwaambia kama walibya waliishi miaka zaid ya 47 bila mafuta basi wataweza kuishi tena bila mafuta same to Rais Magufuli kwenye madini pili Gadaffi alizuia matumizi ya dollar na kutaka kuintroduce pesa mpya ili waafrika waache kutumia dollar same to Rais Magufuli alivyopiga marufuku matumizi ya dollar.

NATO wakamtengenezea kikundi cha wasaliti wakajifanya wanataka demokrasia uchwara wakampindua na kumuua Gadaffi kikatili na kinyama sana walishangilia sana lakini leo Libya sio Libya ile ya Gadaffi wa libya leo wanalia sana rasilimali zote zinaibiwa hazinufaishi tena walibya.

The same to Tanzania baada ya kutangaza vita za kiuchumi tunaanza kuhujumia especial kwenye uchumi na shilingi yetu bila kusahau wanawatumia upinzani uchwara kudai madai yaleyale ya demokrasia uchwara.

Tumeshuhudia majaribio kadhaa yakigonga mwamba kama vile operesheni UKUTA yenye lengo la kusababisha vurugu kama Libya. Naomba kuwahusia watanzania wenzangu kuwa kuna msemo unasema we dont know what we have until you lose it. Tuweni makini rais tumepata hivyo tusikubali kurubuniwa watanzania hatuli demokrasia tunakula chakula. First piority yetu ni maendeleo sio bunge live, sio mikutano ya kisiasa na wala sio freedom ya kutukana viongozi wetu.
 
Kwanin mnatumia nguv kubwa sana kutaka watz tumpende rafiki wa m7? Akili ni nywele na kila mtu anazake. Leo nikisema watz wasipowaunga mkono upinzani watakuja kulia na kusaga meno, kwan ni lazma wapinzan waungwe mkono? Msitupangie cha kufanya coz wenye akili tushamjua mapema sana.
 
Msing'ang'anie kuungwa mkono.hoja zinazotolewa na wasiounga mkono muwe mnazijibu. Tuanzie kwa rais kuweka pembeni katiba

Amesema mwenyewe Magu kwamba miaka yote tumekuwa tukisaga meno,sasa kuna kipya kipi katika usagaji wa meno. Mnataka kumfanya kama Mungu vile wakati mtu mwenyewe mweupe tu. Hivi kafanya kipi cha ajabu hapo
 
Tulipokubali Demokrasia tulikubali kutofautiana mawazo..

Hivyo basi Rais hawezi ungwa mkono na kila mmoja kamwee..

Ila nadhani tutumie akili zetu tuu maana yapo mambo yanayofanywa kwa ustawi wa nchi yetu yanayopaswa kuungwa mkono, utofauti wetu uwe katika siasa ila linapokuja suala la nchi tukemee wote anapokosea na tumuunge mkono anapopatia.
 
Kiongozi mzalendo na imara husikiliza anaowaongoza na kutoa uamuzi makini na wabusara. Kiongozi anayetaka kulazimishwa kusifiwa kana kwamba yeye hakuwahi kuwa fisadi alishushwa kutoka mbinguni hivyo kuwa tenda wenzake ambao pengine walikuwa wakishirikiana naye kabla hajapata cheo na kujifanya msafi kana kwamba hakuwa kwenye mfumo mbovu pengine ndio uliomuweka hapo alipo siyo sahihi.
 
Kwanin mnatumia nguv kubwa sana kutaka watz tumpende rafiki wa m7? Akili ni nywele na kila mtu anazake. Leo nikisema watz wasipowaunga mkono upinzani watakuja kulia na kusaga meno, kwan ni lazma wapinzan waungwe mkono? Msitupangie cha kufanya coz wenye akili tushamjua mapema sana.
Mtakuja kujuta na sijui mtakimbilia wapi chukueni mfano kwa majirani zenu. I support magufuli 100%
 
Mku hii ndo hoja uliyokuja nayo. Yaani kuwatisha watu kwa nchi iliyohuru ni Kesi. Kumbuka hiyo Libya unayoizungumzia hujui matatizo yaliko anzia ingia ktk gugo tafuta kitu kinaitwa Six sister ndo utajua cNJhochoko ziliko anzia.
Wache watu waongee kwani wanajenga hoja na sisi tuwapinge kwa hoja sio kwa Kejeli ambazo huzaa maswali kwa raia waliowengi ambao wanauelewa wa kupambanua mambo.
 
Mtu anayesema hadharani haki za binadamu sio kipaumbele siwezi kumuunga mkono hata akianza kutulipa 5m kila mtanzania. Mleta mada aje kujibu
Haki za binadamu zinatakiwa zianzie nyumbani kwako kwanza je unazitimiza? Je huwa huwachapi watto wako/ mke wako. Sasa haki za binadamu ziko wapi
 
Tulipokubali Demokrasia tulikubali kutofautiana mawazo..

Hivyo basi Rais hawezi ungwa mkono na kila mmoja kamwee..

Ila nadhani tutumie akili zetu tuu maana yapo mambo yanayofanywa kwa ustawi wa nchi yetu yanayopaswa kuungwa mkono, utofauti wetu uwe katika siasa ila linapokuja suala la nchi tukemee wote anapokosea na tumuunge mkono anapopatia.
hatukukubali demokrasia ya kutukana na kuwakebei viongozi sio utamaduni wetu hatukukubali demokrasia ya kurudisha nyuma maendeleo
 
hawa mapandikizi Mungu alishaamua kuwaumbua, Libya hatuwezi fika. Tunajua wapo hao mapandikizi wa wawazungu, wanafanya kazi ya kutetea wazungu, lengo lao ni kuivuruga nchi.
Swali. Uchumi wa Mwl. Nyerere ulianguka na Ujamaa tukauyumbisha,hivyo naye alikuwa pandikizi? Tatizo kubwa ni ubinafsi wetu viongozi hasa wa Kiafrika. Mtu anaomba kura,na anaahidi kushirikiana na kila mtu atakpochaguliwa. Akishachaguliwa,anabadilika na kusema"Nisikilizeni mimi tu na yeyote asiongee,matatizo yenu yote nayafahamu". Je,hiyo ni kweli?
 
Wapinzani tupo kwaajiri ya kuikosoa serekali sasa tukimuunga mkono nani atamkosoa!!!! Nyie ndo wale wale hamtaki ushindani
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom