Elections 2010 Watanzania tusikubari propagannda hizi! Ni hatari sana!

mshikachuma

JF-Expert Member
Dec 2, 2010
2,853
626
Nikiwa kama mtanzania wa kawaida ambae ninaipenda nchi yangu,sina budi nikitoa maoni yangu.
Nimejaribu kufatilia sana siasa za Tanzania tokea uchaguzi wa vyama vingi mwaka 1995 kipindi cha kampeni. Nakumbuka uchaguzi wa mwaka huo chama kikuu cha upinzani kilikuwa ni Nccr mageuzi
ya akina Mrema against chama tawala ccm ambacho mgombea wake alikua Benjamini mkapa.

Ukiachilia vyama vyote vya upinzani wakati huo,chama ambacho kilikubarika na watu ni Nccr mageuzi
Ccm walipogundua kuwa Nccr ni hatari na nitishio kwao,wakaenda mafichoni,waliporudi wakaja na pro
paganda ya kuwa Nccr mageuzi ni chama cha kikabila [wakimaanisha wachaga] na maana ya NCCR ni
Ni Chama Cha Rabsha. Kwakua kipindi hicho baadhi ya watanzania wengi tulikuwa na mawazo mgando
tukainyima kura Nccr na Mrema wake. Tukaipa kura ccm na mkapa akashinda japo si kwa kishindo.

Uchaguzi wa mwaka 2000 ikatokea chama kingine chenye nguvu na sera mzuri against ccm nacho ni
CUF,kikiongozwa na mh.Lipumba kwa huku Bara na visiwani kikiwakirishwa na Seif sharif Hamadi.
Ccm kama kawaida yao walipoona CUF inakubarika na wananchi,wakaingia tena mafichoni, waliporudi
tu wakaja na bonge la propaganda ya kuwa CUF ni chama cha kidini [hapa walilenga uwislaam].

Haitoshi wakaagizia mapanga nje ya nchi na yakaja kwenye contena yakiwa yana bendera za CUF.
wakaviita vyombo vya habari kuja kushuhudia ugaidi wa Cuf! kumbe si kweli bali propaganda tu!.
Kwahiyo yale ya mwaka 95 yaliyomkuta Lyatonga na Nccr yake,ndio yaliyemkuta mh.Lipumba na
cuf yake. Watanzani tukaigopa Cuf kama ukoma na kura zote tukaipa ccm,na wakashinda tena kwa
propaganda zao

Uchaguzi wa mwaka 2005 nao ukaja na vitukovyake. kwanza wapinzani hawakuwa na nguvu kama
chaguzi zilizopita. kwahiyo ccm kama kawida yao wakazama mafichoni,walivyorudi huko wakaja na uo
ngo unaofanana na propaganda kwa wadanganyika [walikuja na vitu 3] ili tuwachague tena.
Kwanza walisema chagua ccm maisha bora kwa kila mtanzania.Pili wakasema mgombea wao [mh.kikwete] ni 'handsome'yaani ni mzuri ki umbo. Tatu wakasema kikwete ni chaguo La mungu. Wadanganyika tukaichagua ccm,na kikwete akashinda kwa kishindo.kumbe uongo mtupu!

Lakini mambo yaliyotokea ndani ya miaka hiyo mitano hakuna asiyejua! ni vurugu tupu hakuna cha
maisha bora wala babu yake maisha tamu! Badala yake tukashuhudia ufusadi wa kutisha na maisha
kuendelea kuwa magumu kwa watanzania tulio wengi.

Uchaguzi uliyopita wa mwaka huu 2010 ulikuwa wa aina yake kwa wananchi wengi kuwa na mwitikio.
Pamoja na vyama vyote vilivyoshiriki uchaguzi huo,chama ambacho kilikuwa na nguvu ya ajabu na kukubarika na wanchi kwa kasi ya ajabu ni Chadema ambacho kwenye kampeni zake kiliongozwa na
Dr Slaa na timu yake iliyo makini. Hakika hiki ni Chama cha upinzani ambacho hakijawai tokea Tanzania. Chama ambacho kilikuja na sera mzuri,viongozi imara,wasomi na wenye uchungu wa Tanzania na raia wake! Hakika waliichambua serikali ya ccm kuanzia utosini hadi unyayoni na watanzania tukaamka for first time.

Lakini kama kawada ya ccm,wakaenda mafichoni waliporudi huko wakaja na bonge la propaganda lenye sumu kali. Wakasema Chadema ni chama cha kidini [hapa walilenga ukristo]na ukabila.
Kwa watu kama sisi ambao tunazijua propaganda za ccm tukasema Nooo! thiz time we have to vote for change,na tukaipa kura chadema. Ila kwa wale waliokuwa teyari kuipa kula chadema wakati huo huo hawazijui propaganda za ccm 'hasa vijijini' waliposikia sumu za ccm wakabadilisha mawazo na wakaipa kura ccm au hawakwenda kabisa kupiga kura. kwahiyo ikawa faida na neema kwa ccm na
hasara kwa Chadema. ccm ikashinda tena japo si kwa kishindo kama chaguzi zilizopita.

Narudia tena, Chadema ni chama ambacho hakijawahi tokea Tanzania bara! kimetuonyesha kina
sera mzuri,uongozi imara,na kina future ya Tanzania tunayoitaka! kimepata wabunge wengi bara kuliko chama chochote cha upinzani. Ni chama ambacho kimekubarika pande zote za Tanzania bara!
Na isingekuwa propaganda za ccm,basi Chadema ingeshika Dola na leo ingekuwa story nyingine.

Hitimisho langu ni-
Watanzania tusikubari propaganda hizi za Ccm! Ni hatari sana hawa watu hasa wanapoona kuna chama cha upinzani makini na chenye uongozi imara,hapo wao wako teyari waivuruge nchi kwa
propaganda za sumu ili mladi waendelee kutawala! Camooon guys tuamkeni watanzania! hii ni
nchi yetu wote na tunawajibu ya kuipigania kwa manufaa ya walio wengi! Ahsanteni.

Nawakilisha.
 
umenena mkuu wangu, kikwete ajaribu kufikiri ingawa yeye ni zumbukuku, je 2005 alishinda kwa 80% leo ame -drop below 50% udini unatoka wapi? acha propaganda wewe mkwere umeangukia pua kwa kutoa ahadi kibao, my take, nasikia unaandaa mzanzibar kuwa mrithi wako kama ulivyo wafanyia uvccm , na kumwengua sita bungeni, wewe ni mtu dhaifu sana haijawahi kutokea katika historia ya taifa hili, KUMBE NYERERE ALIKUWA SAHIHI KUKUKATAA NA HAKUWAHI KUSEMA UTAKUA KWANI TAYARI ULIKUWA KIJEBA
 
Article nzuri.
Nyongeza: Tusikubali pia propaganda za Dr. Slaa kuwa kura zake zimeibiwa mpaka atuonyeshe vidhibiti.
 
Ni kweli ingawa pia tunapoingiza wachungaji kwenye siasa inadhihirisha na kuonyesha jinsi tulivyo. Ni kweli lakini pia makanisa yanapojitokeza hadharani na kuipigania chadema inadhirisha kuwa kina ajenda ya UDINI. Ni kweli lakini pia ZITO anapoandamwa sana ndani ya chama ni dhahiri udini unafanya kazi yake. ni kweli lakini pia unaposimamisha mgombea mwenza muislamu mbumbumbu (darasa la saba) ni kielelezo tosha cha kuonyesha waislam watakuwa wakubruzwa tu katika serikali ambayo ingeundwa na chadema. NA HUU NDIO UMAKINI WA VIONGOZI WA CHADEMA. Ni kweli pia hata wana JF wanaoshabikia chadema wana msimamo hasi dhidi ya Waislamu. Ni kweli lakini pia jinsi chadema ilivyojipanga kupambana na CUF inadhirisha na kuamsha maswali mengi. NA HII YOTE HAIHITAJI KUPIGIWA PROPAGANDA NA CCM. Ni ukweli usiofichika. Bado ni kweli hata kadiri tunavyokwenda inadhirisha uchanga wa wanasiasa wa chadema. Bado nasisitiza kuwa UBINAFSI NA UZANDIKI NA UKABILA PAMOJA NA KUKOSEKANA UZALENDO ni miongoni mwa vipaumbele vya viongoi wa chadema. Bado haya yote hayahitaji kupandikizwa na CCM.
Twende mbele turudi nyuma bado wanasiasa wa Chadema hawana vision ya Utaifa bali wanataka kutumia silaha na umasikini pamoja na katiba kufika Ikulu kwa gharama yoyote hata ikigharimu maisha ya watu wengi.
Ningeshawishika kidogo madai ya kusema CCM wamechakachua matokeo ya URAIS ikiwa chadema wangekuja na DATA kamili ya idadi kwa majimbo ya kila mgombea aliyopata - mwezi mmoja sasa baada ya uchaguzi kuisha. TUTAWAAMINI VIPI WAKIYALETA SASA KAMA SI YA KUCHAKACHUA?. JE, KATIKA HILI CCM SI WATAONEKANA BORA ZAIDI ??
NACHANGIA HOJA.
 
Ni kweli ingawa pia tunapoingiza wachungaji kwenye siasa inadhihirisha na kuonyesha jinsi tulivyo. Ni kweli lakini pia makanisa yanapojitokeza hadharani na kuipigania chadema inadhirisha kuwa kina ajenda ya UDINI. Ni kweli lakini pia ZITO anapoandamwa sana ndani ya chama ni dhahiri udini unafanya kazi yake. ni kweli lakini pia unaposimamisha mgombea mwenza muislamu mbumbumbu (darasa la saba) ni kielelezo tosha cha kuonyesha waislam watakuwa wakubruzwa tu katika serikali ambayo ingeundwa na chadema. NA HUU NDIO UMAKINI WA VIONGOZI WA CHADEMA. Ni kweli pia hata wana JF wanaoshabikia chadema wana msimamo hasi dhidi ya Waislamu. Ni kweli lakini pia jinsi chadema ilivyojipanga kupambana na CUF inadhirisha na kuamsha maswali mengi. NA HII YOTE HAIHITAJI KUPIGIWA PROPAGANDA NA CCM. Ni ukweli usiofichika. Bado ni kweli hata kadiri tunavyokwenda inadhirisha uchanga wa wanasiasa wa chadema. Bado nasisitiza kuwa UBINAFSI NA UZANDIKI NA UKABILA PAMOJA NA KUKOSEKANA UZALENDO ni miongoni mwa vipaumbele vya viongoi wa chadema. Bado haya yote hayahitaji kupandikizwa na CCM.
Twende mbele turudi nyuma bado wanasiasa wa Chadema hawana vision ya Utaifa bali wanataka kutumia silaha na umasikini pamoja na katiba kufika Ikulu kwa gharama yoyote hata ikigharimu maisha ya watu wengi.
Ningeshawishika kidogo madai ya kusema CCM wamechakachua matokeo ya URAIS ikiwa chadema wangekuja na DATA kamili ya idadi kwa majimbo ya kila mgombea aliyopata - mwezi mmoja sasa baada ya uchaguzi kuisha. TUTAWAAMINI VIPI WAKIYALETA SASA KAMA SI YA KUCHAKACHUA?. JE, KATIKA HILI CCM SI WATAONEKANA BORA ZAIDI ??
NACHANGIA HOJA.

Mkuu kama ni haki hata ss waislaam tumepigia kampeni kikwete kwa sbb ni muislam tena wazwaz, radio zetu zote zilieleza wazi wazi magazeti, misikitini nk . napenda nikukumbushe kwa faida yako kama ww muislam wa kweli nakumbukumbu zako kama hazina vumbi. unakumbuka viongoz wetu wadini walivyokuwa wakieleza ubaya wa ccm? unajua kirefu cha ccm tulivyokuwa tunatafsiliwa? au ww c mwaharakati wa kiislam? iweje leo watuchanganye kuwa ccm nzuri? ndugu zanguni ktk iman tufikirie sana tusije kuwa kama bendela, hawa wanasiasa hufanya kila hila wafanikiwe lengo lao. sasa 2015 ccm wakisimamisha mkristo itakuwaje? tuhame chama? si itakuwa aibu tu kwetu. nawapi ktk quran imeeleza haiuhusiwi kuongozwa na din nyingime? msimamo wangu ntaichukia ccm daima, nautambue watz wamechoka utawala wa ukandamizaji.
 
Mkuu kama ni haki hata ss waislaam tumepigia kampeni kikwete kwa sbb ni muislam tena wazwaz, radio zetu zote zilieleza wazi wazi magazeti, misikitini nk . napenda nikukumbushe kwa faida yako kama ww muislam wa kweli nakumbukumbu zako kama hazina vumbi. unakumbuka viongoz wetu wadini walivyokuwa wakieleza ubaya wa ccm? unajua kirefu cha ccm tulivyokuwa tunatafsiliwa? au ww c mwaharakati wa kiislam? iweje leo watuchanganye kuwa ccm nzuri? ndugu zanguni ktk iman tufikirie sana tusije kuwa kama bendela, hawa wanasiasa hufanya kila hila wafanikiwe lengo lao. sasa 2015 ccm wakisimamisha mkristo itakuwaje? tuhame chama? si itakuwa aibu tu kwetu. nawapi ktk quran imeeleza haiuhusiwi kuongozwa na din nyingime? msimamo wangu ntaichukia ccm daima, nautambue watz wamechoka utawala wa ukandamizaji.
======

Hapo umenena ndugu yangu.
Ndani ya CCM wapo wachungaji na mashehe kama wabunge. Sijasikia CCm hao hao wakijikemea kuwa wana udini kwa kuwa wachungaji wamekuwa wabunge kupitia CCM. Lakini pale 'aliyekuwa' padri alipogombea urais ikawa nongwa.
Maaskofu wanaposema JK ni chaguo la Mungu, CCM haikemei, lakini Askofu mwingine akisimama akasema "Chagua mtu, usichague chama", CCM wanakuja juu kuwa huo ni udini.

Watu wakibaini hizi njama, CCM itahama nchi.
 
hii ndo funga mwaka!! :teeth:

Ni kweli kabisa kabisa... watu waaacheni watoe vinyongo vyao, tuanze 2011 vichwa vimetulia na mambo mapya!
 
ccm ni wabinafsi sijui wanataka waongoze nchi peke yao wanakula na vipofu bado wanamshika mkono rejea yale ya ndugu Kego kung'oa vitasa na kuchukua vitu vingine kwenye ofisi ya mbunge kisa kashindwa ubunge!
 
Mi ni muislam tena swala tano ila kuliko niishabikie au kuchagua ccm bora nile nguruwe japo hacheuwi.ccm ni kama nguruwe hakicheui kile chama wao ni kula tu.ikumbukwe pia nguruwe hula hadi wanae aliowazaa mwenyewe.same like happen to ccm wana sema eti elimu bure haiwezekani wakati wao walisomeshwa na hiyo hiyo ccm bure.SHAME ON YOU CCM NA TEAM NZIMA.
 
Nimepata nafuu kubwa hapa maana watu wamekubali kuweka dini pembeni na kujadili nchi yetu na siasa zake vizuri kabisa. Tungeendelea kuwaza hivi basi tungeweza kuwaelimisha na wengine na nchi hii ingebadilika. Najisikia kufananisha dini moja kati ya Kiislamu na ya Kikiristo kuogopa kuwa na raisi kutoka moja wapo na mawazo yaliyoigubika Marekani wakati alipochaguliwa Obama kuwa raisi wa kwanza mweusi. Wapo waliodhani kuwa hataweza kuwa raisi wa wote. Leo hii wanajiona wajinga sana wala hawasemi tena. Hivi kweli mtu mwenye akili timamu anaweza kudhania kuwa Raisi wa Tanzania awe Muislamu au Mkristu ataweza kupata nafasi ya kugeuza nchi hii kuwa ya dini moja?? Au kupedelea dini moja? Ataanzia wapi?? Ni akili finyu tu ndizo zinaweza kuwaza hilo. Hivyo vyombo vya dola vimechanganyika makabila na dini zote, zipo familia zenye dini zaidi ya moja ndani yake. Awe Shekhe awe Padri hawezi kamwe badili lolote. Uvivu wa kufikiri ni tatizo kubwa kuliko malaria tuliyo nayo Watanzania. NASEMA TUACHANE NA UDINI NA UKABILA WALA TUSIUJADILI, NI MBINU ZA KUTUPOTEZEA MUDA TU, SI CHOCHOTE SI LOLOTE! Mungu ibariki Tanzania.
 
Achana na Kagumyamuheto naye ni pandikizi. Nani hasiyejua ya kwamba tangu kuruhusiwa siasa ya vyama vingi ccm imekuwa ikitumia haswa mbinu za aina tatu kusambaratisha vyama vya upinzani vyenye kuonyesha dalili za kuwa na nguvu. Mbinu hizo nipamojana; kupandikiza vibaraka kwenye vyama hivyo, kuvituhumu kuwa vinachochea uvunjifu wa amani huku ccm yenyewe ikiwa ndiyo inatumia vyombo vya dola na makada wake kufanya hivyo, na mwisho, kuvituhumu kuwa ama ni vyama vya kidini, kama ilivyokuwa kwa cuf, au vinabebwa kwa misingi ya kidini, kama yalivyo madai ya sasa kwa upande wa chadema. Ebu tujiulize kama ni kweli cuf kilikuwa ni chama kilichojengeka kwa msingi wa dini kimewezaje kuubomoa msingi huo kiasi cha kuvifanya vyama hivyo hasimu (cuf na ccm), hivi sasa kuwa maswahiba. Na kwa upande wa chadema, chama hicho kimejipambanua katika kupinga vita maovu yote katika jamii; ikiwemo rushwa, ubadhirifu wa mali za umma, mtindo uliozuka katika miaka ya hivi karibuni ya viongozi kutumia nyadhifa zao kujihudumia wenyewe badala ya kuhumia umma, kama ilivyokuwa huka nyuma ambapo cheo kichukuliwa kuwa dhamana n.k Masuala haya yanashabihana na mafundisho ya dini zote, uwe ukristo uwe uislamu. Kama hivyo ndivyo kwanini dini hizo zisiiunge mkono chadema ambayo ajenda yake na shabaha kuu za dini hizo vinafanana. ukubali husikubali suala la dini katika uchaguzi huu uliokwisha limepandikizwa na ccm baada ya kuona kwamba kwa kuwa chadema ilikuwa na sera zinazovutia dini zote bila ya kupandikiza suala la dini ili kuleta mfarakano ccm itakuwa imekwisha.
 
Nachukia watu wanaoandika r mahali pa l na l mahali pa r 'tusikubari', 'kukubari' nk. Inatia shaka elimu ya mwandishi na by extension hoja yake!
 
Nachukia watu wanaoandika r mahali pa l na l mahali pa r 'tusikubari', 'kukubari' nk. Inatia shaka elimu ya mwandishi na by extension hoja yake!

Utusamehe tu sisi wakurya hatuna L katika vocaburary yetu
 
Ni kweli ingawa pia tunapoingiza wachungaji kwenye siasa inadhihirisha na kuonyesha jinsi tulivyo. Ni kweli lakini pia makanisa yanapojitokeza hadharani na kuipigania chadema inadhirisha kuwa kina ajenda ya UDINI. Ni kweli lakini pia ZITO anapoandamwa sana ndani ya chama ni dhahiri udini unafanya kazi yake. ni kweli lakini pia unaposimamisha mgombea mwenza muislamu mbumbumbu (darasa la saba) ni kielelezo tosha cha kuonyesha waislam watakuwa wakubruzwa tu katika serikali ambayo ingeundwa na chadema. NA HUU NDIO UMAKINI WA VIONGOZI WA CHADEMA. Ni kweli pia hata wana JF wanaoshabikia chadema wana msimamo hasi dhidi ya Waislamu. Ni kweli lakini pia jinsi chadema ilivyojipanga kupambana na CUF inadhirisha na kuamsha maswali mengi. NA HII YOTE HAIHITAJI KUPIGIWA PROPAGANDA NA CCM. Ni ukweli usiofichika. Bado ni kweli hata kadiri tunavyokwenda inadhirisha uchanga wa wanasiasa wa chadema. Bado nasisitiza kuwa UBINAFSI NA UZANDIKI NA UKABILA PAMOJA NA KUKOSEKANA UZALENDO ni miongoni mwa vipaumbele vya viongoi wa chadema. Bado haya yote hayahitaji kupandikizwa na CCM.
Twende mbele turudi nyuma bado wanasiasa wa Chadema hawana vision ya Utaifa bali wanataka kutumia silaha na umasikini pamoja na katiba kufika Ikulu kwa gharama yoyote hata ikigharimu maisha ya watu wengi.
Ningeshawishika kidogo madai ya kusema CCM wamechakachua matokeo ya URAIS ikiwa chadema wangekuja na DATA kamili ya idadi kwa majimbo ya kila mgombea aliyopata - mwezi mmoja sasa baada ya uchaguzi kuisha. TUTAWAAMINI VIPI WAKIYALETA SASA KAMA SI YA KUCHAKACHUA?. JE, KATIKA HILI CCM SI WATAONEKANA BORA ZAIDI ??
NACHANGIA HOJA.

Nashukuru kwa michango yenu ambayo imejali maslahi ya Utaifa Zaidi kuliko udini. ingawa pia nashangazwa na michango yenu pahala pengine ambapo mnajidhirisha mlivyo na chuki dhidi ya dini zingine na hasa Uislamu. Binafsi sioni tatizo la nani atawale nchi hii. Hii ni nchi yetu sote. Pengine tatizo ni dhamira inayojitokeza wakati wa kufanya maamuzi MUHIMU NA NYETI na jinsi tunavyosifia Umakini wa viongozi tunao washabika bila kupima upande wa pili. Hebu tuendelee kujadili.
1.0 Suala la mgombea mwenza wa chadema kuwa mbumbumbu ingawa kweli kuna tatio la kikatiba hapo je, hamkuona kama kumchagua huyo ilikuwa ni Kuwatenga Wazanzibari na Waislamu???. je, hamuoni kwa kufanya hivyo mumekosa kura muhimu za wenye kuyatazama majambo kwa uelewa mzuri??
2.0 Je, Suala la wana JF waliowengi wanaoshabikia Chadema kubeza waislamu hamuoni linahatarisha msingi wa umoja wa Taifa letu?. Je, Chadema inajipambanua vipi kitaifa? mdharau mwiba mguu huota tende! kalagabaho!!!
3.0 Je, suala la Chadema na wanachadema kupambana na CUF hamuoni haileti picha nzuri Kitaifa?
4.0 Madai ya kusema CCM wamechakachua matokeo ya URAIS . Na BADO chadema wameshindwa kuleta DATA kamili ya idadi kwa majimbo ya kila mgombea aliyopata - mwezi mmoja na ushee sasa baada ya uchaguzi kuisha. TUTAWAAMINI VIPI WAKIYALETA SASA KAMA SI YA KUCHAKACHUA?. UMAKINI WA VIONGOI WAPAMBANAJI UKO WAPI???????????????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Haya mambo manne muhimu tujadili kwa kina bila ushabiki. Penye tatizo tuthubutu kusema. Nafahamu wazi CCM wamekuwa na tabia ya kupandikiza propaganda za kuuwa chama chenye nguvu. lakini pia naomba michango yenu katika haya mambo manne. je, CCM inahusika vipi?
Na kama ni kweli basi kuna tofauti gani kati ya CCM na CHADEMA?
Iam more RATIONAL than EMOTIONAL instigated!
 
Nashukuru kwa michango yenu ambayo imejali maslahi ya Utaifa Zaidi kuliko udini. ingawa pia nashangazwa na michango yenu pahala pengine ambapo mnajidhirisha mlivyo na chuki dhidi ya dini zingine na hasa Uislamu. Binafsi sioni tatizo la nani atawale nchi hii. Hii ni nchi yetu sote. Pengine tatizo ni dhamira inayojitokeza wakati wa kufanya maamuzi MUHIMU NA NYETI na jinsi tunavyosifia Umakini wa viongozi tunao washabika bila kupima upande wa pili. Hebu tuendelee kujadili.

1.0 Suala la mgombea mwenza wa chadema kuwa mbumbumbu ingawa kweli kuna tatizo la kikatiba hapo je, hamkuona kama kumchagua huyo ilikuwa ni Kuwatenga Wazanzibari na Waislamu???. je, hamuoni kwa kufanya hivyo mumekosa kura muhimu za wenye kuyatazama majambo kwa uelewa mzuri??

2.0 Je, Suala la wana JF waliowengi wanaoshabikia Chadema kubeza waislamu hamuoni linahatarisha msingi wa umoja wa Taifa letu?. Je, Chadema inajipambanua vipi kitaifa? mdharau mwiba mguu huota tende! kalagabaho!!!

3.0 Je, suala la Chadema na wanachadema kupambana na CUF hamuoni haileti picha nzuri Kitaifa?

4.0 Madai ya kusema CCM wamechakachua matokeo ya URAIS . Na BADO chadema wameshindwa kuleta DATA kamili ya idadi kwa majimbo ya kila mgombea aliyopata - mwezi mmoja na ushee sasa baada ya uchaguzi kuisha. TUTAWAAMINI VIPI WAKIYALETA SASA KAMA SI YA KUCHAKACHUA?. UMAKINI WA VIONGOZI WAPAMBANAJI UKO WAPI???????????????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Haya mambo manne muhimu tujadili kwa kina bila ushabiki. Penye tatizo tuthubutu kusema. Nafahamu wazi CCM wamekuwa na tabia ya kupandikiza propaganda za kuuwa chama chenye nguvu. lakini pia naomba michango yenu katika haya mambo manne. je, CCM inahusika vipi?
Na kama ni kweli basi kuna tofauti gani kati ya CCM na CHADEMA?
Iam more RATIONAL than EMOTIONAL instigated!
 
Article nzuri.
Nyongeza: Tusikubali pia propaganda za Dr. Slaa kuwa kura zake zimeibiwa mpaka atuonyeshe vidhibiti.

Nadhani DR slaa na Chadema kwa ujumla ni wauungwana sana, wangetoa chochote ambacho kingekuwa uthibitisho wa wizi wa kura mara tu baada ya uchanguzi, inawezekana watu wangefanya funjo, ni bora walivyo kaa kimya mpaka hali itulie!
 
Nadhani DR slaa na Chadema kwa ujumla ni wauungwana sana, wangetoa chochote ambacho kingekuwa uthibitisho wa wizi wa kura mara tu baada ya uchanguzi, inawezekana watu wangefanya funjo, ni bora walivyo kaa kimya mpaka hali itulie!
Kwa kutoa hivyo vithibitisho naamini Watahatarisha amani na utulivu wetu tuliojijengea maana imeshasemwa wazi hali ni tete.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom