Ngamanya Kitangalala
JF-Expert Member
- Sep 24, 2012
- 501
- 1,214
Moja ya jambo ambalo Watanzania na Waafrika wenzangukwa ujumla tunapaswa kujiuliza sana.
Je, hivi ni kweli, nchi ya Marekani na vibaraka wake ni watetezi wa demokraaia au ni watetezi wa maslahi yao binafsi?
Kwanini?
Kwa sababu, kumekuwepo na kukosekana kwa usawa (double standard ) zà hali ya juu kabisa ya namna ambavyo, nchi hiyo ya Marekani, ambaye ndio anaonekana ni kinara wa demokraaia na haki za binadamu (human rights) hapa duniani, jinsi anavyoshughulikia huo upatikanaji wa demokraaia na haki za kibinadamu, kwenye mataifa mbalimbali hapa duniani
Kwa mfano kwenye nchi ya Misri ( Egypt) mwaka 2013, ulifanyika uchaguzi wa kwanza wa vyama ving na kidemokrasia nchni humo, ambapo nchi hiyo kwa mara ya kwanza kabisa katika historia yao, ilifanikiwa kupata Rais wa kwanza aliyepatikana kwa njia ya kidemokrasia, marehemu Mohamed Morsikutoka chama cha Muslim Brotherhood
Lakini mwaka mmoja baadaye 2014,Rais huyo aliyepatikana kwa njia ya kidemokrasia, kwa kupigiwa kura na wananchi wa Mirsi, aliondolewa/ kupinduliwa kutoka madarakani na Jenerali Abdel Fattah El Sisi ambaye kabla ya hapo alikuwa ndiye waziri wa ulinzi( Minister of Defence)na ndiye alikuwa Amiri jeshi mkuu (Commander in chief) wa majeshi ya Mirsi, Kwa mujibu wa katiba ya Misri, waziri wa ulinzi ndiye anakuwa pia amiri jeshi mkuu (Commander in chief) na Rais wa Mirsi yeye anakuwa kiongozi mkuu( Supreme Commander) wa vikosi vya ulinzi na usalama vya nchi ya Misri
Lakini kitu cha ajabu kabisa, Rais wa 45 wa Marekani, Donald Trump alipoingia madarakani mwaka 2016, Rais wa kwanza kabisa duniani, kukaribishwa na Rais Trump Oval office, White House (ikulu ya Marekani) alikuwa ni Rais Abdel Fattah El Sisi.
Na mpaka sasa, kwa mujibu wa wizara ya Ulinzi ya Marekani( Pentagon), nchi ya Misri ndio nchi inayopokea misaada mikubwa kabisa ya kijeshi kutoka Marekani bada ya Israel.
toka mwaka 1987 nchi ya Misri, imekuwa ikipokea takribani dola za kimarekani 1.3 bilioni kila mwaka, kwa ajili ya msaada kwa jeshi la Misri,na kufanya nchi ya Misri kuwa na jeshi imara na lenye nguvu kuliko nchi yeyote ile barani Africa.
Na kuonyesha ni kwa namna gani misaada ya kijeshi ya Marekani kwa Misri imekuwa ni muhimu sana kwa jeshi la Misri, taasisi ya Jaffee Centre kupitia kwenye utafiti wake( Strategic Studies, annual middle east strategic balance) ulionyesha Jeshi la Misri ndio jeshi i kubwa zaid kuliko majeshi yote kwnye ukanda huo wa mashariki ya kati (Middle East)
Swali tunalopaswa, kujiuliza je ni kwa nini nchi ya Misri imekuwa ni mshirika mkubwa sana kwa serikali ya Washington?
Kwa sababu kama wengi tunavyojua sera za chama chama cha Muslim Brotherhood na uwepo wa nchi ya Israel kule mashariki ya kati( middle east) na mahusiano ya nchi za Marekani na Israel, katika hali yeyote ile, serikali ya Washington, haiwezi kuruhusu nchi ya Misri kuwa chini ya utawala wa chama cha Muslim Brotherhood.
Kimkakati nchi ya Misri ni muhimu sana kwa nchi za Marekani na mshirika wake wa karibu Israel, kwa sababu ya uwepo wa mfereji wa Suez (Suez Canal ) ambapo Marekani amekuwa akitumia kupirisha meli zake za kivita (US naval vessels) pale kila zinapohitajika kwenye eneo hilo la mashariki ya kati (Middle East)
Lakini pia, kuwepo na mpaka kati ya nchi ya Misri na Israel, mpaka ( boarder) wenye urefu wa maili 170( 270 kilometa), umeifanya nchi ya Misri kuwa muhimu sana kwa Marekani, kwani mara kadhaa serikali ya Misri, imekuwa ikiziruhusu ndege za kivita za Marekani ( US military aircraft) kutumia anga la Misri.
Kwa hayo mawili, inaifanya nchi ya Misri, kuwa nchi muhimu sana (strategic area) kwa serikali ya Washington, kuweza kuendeleza utawala na ubabe wake kwenye eneo hilo muhimu la mashariki ya kati
Kwa hiyo kwa Marekani kufumbia macho ukiukaji wa demokraaia na haki za binadamu nchini Misri, ni kwa sababu ya kulinda maslahi yake ya kiuchumi
Lakini pia, nchi ya Saudi Arabia, moja ya nchi ambayo ni mshiriki mkubwa kabisa wa kibiashara wa Marekani, kumekuwepo na tuhuma nyingi, za ukiukwaji mkubwa kabisa wa haki za binadamu, pasipo kuchukuliwa hatua zozote na huyo kinara wa demokraaia na haki za binadamu( Marekani)
Mfano mwaka October 2018, mwandishi wa habari, wa gazeti la The Washington Post (Moja ya gazeti maarufu kabisa nchini Marekani) na mwanaharakati marehemu Jamal Ahmad Khashoggi, ambaye alikuwa ni raia wa Marekani, mwenye asili ya Saudi Arabia, aliuwawa kikatikili kabisa katika ubalozi mdogo wa Saudi Arabia jijini Instanbul, Uturuki.
Mauaji ambayo yalishutumiwa vikali sana hapa duniani, na kumekuwepo na tuhuma za serikali ya Riyadh (Saudi Arabia) kupitia mwana mfalne( Crown Prince) Mohammed Bin Salman kuhusika na mauaji hayo ya kikatili .
Lakini pia, mwaka 2012 mwana mtandao maarufu nchini Saudi Arabia, Raif Badawi,alihukumiwa miaka 10 jela kwa kosa tu la kuanzisha mjadala mtandaoni kuhusu uhuru wa kujieleza ( Freedom of expression) nchini Saudi Arabia, hukumu ambayo ilishutumiwa vikali na mataifa mbalimbali duniani
Lakini cha ajabu kabisa, pamoja na yote hayo, mpaka leo serikali ya Marekani ( kinara wa demokraaia na haki za binadamu duniani) haijawahi kuchukua hatua zozote dhidi ya serikali ya Riyadh,au hata kutoa kauli tu kupinga ukiukwaji mkubwa huo wa haki za binadamu
Unajua ni kwanini?
Kwa mujibu wa takwimu kutoka ofsi ya wawakilishi wa wafanyabiashara wa Marekani (Office of The United States Trade Representatives ), biashara ya bidhaa na huduma ( Goods & Services) baina ya nchi za Marekani na Saudia Arabia kwa mwaka 2018 ilikuwa na thamani ya dola za kimarekani billioni 48.3, kwa maana hiyo, nchi ya Saudi Arabia, ni mshirika mkubwa wa kibiashara wa nchi ya Marekani, na ndio sababu inayopelekea nchi ya Marekani, kufumba mambo dhidi ya Saudi Arabia
Kwa hayo machache tu, nitamshangaa sana Mtanzania ambaye atakuwa na fikra potofu za kuamini kuwa mabeberu wanaojifanya wako mstari wa mbele kwenye kwenye kutetea demokraaia na haki za binadamu nchini Tanzania, ni kweli wanaipenda sana nchi yetu.
Mabeberu wanafanya hivyo kwa agenda zao (hidden agenda) na ni kwa maslahi yao na nchi zao
Tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu huu,wa tarehe 28 mwezi huu, ni vema watanzania wenzangu tukawa makini sana na watu hawa, tusikubali kudanganywa na mtu au taifa lingine lolote
Mungu ibariki Tanzania
Ngamanya Kitangalala Mwaswala
kngamanya@yahoo.com
Je, hivi ni kweli, nchi ya Marekani na vibaraka wake ni watetezi wa demokraaia au ni watetezi wa maslahi yao binafsi?
Kwanini?
Kwa sababu, kumekuwepo na kukosekana kwa usawa (double standard ) zà hali ya juu kabisa ya namna ambavyo, nchi hiyo ya Marekani, ambaye ndio anaonekana ni kinara wa demokraaia na haki za binadamu (human rights) hapa duniani, jinsi anavyoshughulikia huo upatikanaji wa demokraaia na haki za kibinadamu, kwenye mataifa mbalimbali hapa duniani
Kwa mfano kwenye nchi ya Misri ( Egypt) mwaka 2013, ulifanyika uchaguzi wa kwanza wa vyama ving na kidemokrasia nchni humo, ambapo nchi hiyo kwa mara ya kwanza kabisa katika historia yao, ilifanikiwa kupata Rais wa kwanza aliyepatikana kwa njia ya kidemokrasia, marehemu Mohamed Morsikutoka chama cha Muslim Brotherhood
Lakini mwaka mmoja baadaye 2014,Rais huyo aliyepatikana kwa njia ya kidemokrasia, kwa kupigiwa kura na wananchi wa Mirsi, aliondolewa/ kupinduliwa kutoka madarakani na Jenerali Abdel Fattah El Sisi ambaye kabla ya hapo alikuwa ndiye waziri wa ulinzi( Minister of Defence)na ndiye alikuwa Amiri jeshi mkuu (Commander in chief) wa majeshi ya Mirsi, Kwa mujibu wa katiba ya Misri, waziri wa ulinzi ndiye anakuwa pia amiri jeshi mkuu (Commander in chief) na Rais wa Mirsi yeye anakuwa kiongozi mkuu( Supreme Commander) wa vikosi vya ulinzi na usalama vya nchi ya Misri
Lakini kitu cha ajabu kabisa, Rais wa 45 wa Marekani, Donald Trump alipoingia madarakani mwaka 2016, Rais wa kwanza kabisa duniani, kukaribishwa na Rais Trump Oval office, White House (ikulu ya Marekani) alikuwa ni Rais Abdel Fattah El Sisi.
Na mpaka sasa, kwa mujibu wa wizara ya Ulinzi ya Marekani( Pentagon), nchi ya Misri ndio nchi inayopokea misaada mikubwa kabisa ya kijeshi kutoka Marekani bada ya Israel.
toka mwaka 1987 nchi ya Misri, imekuwa ikipokea takribani dola za kimarekani 1.3 bilioni kila mwaka, kwa ajili ya msaada kwa jeshi la Misri,na kufanya nchi ya Misri kuwa na jeshi imara na lenye nguvu kuliko nchi yeyote ile barani Africa.
Na kuonyesha ni kwa namna gani misaada ya kijeshi ya Marekani kwa Misri imekuwa ni muhimu sana kwa jeshi la Misri, taasisi ya Jaffee Centre kupitia kwenye utafiti wake( Strategic Studies, annual middle east strategic balance) ulionyesha Jeshi la Misri ndio jeshi i kubwa zaid kuliko majeshi yote kwnye ukanda huo wa mashariki ya kati (Middle East)
Swali tunalopaswa, kujiuliza je ni kwa nini nchi ya Misri imekuwa ni mshirika mkubwa sana kwa serikali ya Washington?
Kwa sababu kama wengi tunavyojua sera za chama chama cha Muslim Brotherhood na uwepo wa nchi ya Israel kule mashariki ya kati( middle east) na mahusiano ya nchi za Marekani na Israel, katika hali yeyote ile, serikali ya Washington, haiwezi kuruhusu nchi ya Misri kuwa chini ya utawala wa chama cha Muslim Brotherhood.
Kimkakati nchi ya Misri ni muhimu sana kwa nchi za Marekani na mshirika wake wa karibu Israel, kwa sababu ya uwepo wa mfereji wa Suez (Suez Canal ) ambapo Marekani amekuwa akitumia kupirisha meli zake za kivita (US naval vessels) pale kila zinapohitajika kwenye eneo hilo la mashariki ya kati (Middle East)
Lakini pia, kuwepo na mpaka kati ya nchi ya Misri na Israel, mpaka ( boarder) wenye urefu wa maili 170( 270 kilometa), umeifanya nchi ya Misri kuwa muhimu sana kwa Marekani, kwani mara kadhaa serikali ya Misri, imekuwa ikiziruhusu ndege za kivita za Marekani ( US military aircraft) kutumia anga la Misri.
Kwa hayo mawili, inaifanya nchi ya Misri, kuwa nchi muhimu sana (strategic area) kwa serikali ya Washington, kuweza kuendeleza utawala na ubabe wake kwenye eneo hilo muhimu la mashariki ya kati
Kwa hiyo kwa Marekani kufumbia macho ukiukaji wa demokraaia na haki za binadamu nchini Misri, ni kwa sababu ya kulinda maslahi yake ya kiuchumi
Lakini pia, nchi ya Saudi Arabia, moja ya nchi ambayo ni mshiriki mkubwa kabisa wa kibiashara wa Marekani, kumekuwepo na tuhuma nyingi, za ukiukwaji mkubwa kabisa wa haki za binadamu, pasipo kuchukuliwa hatua zozote na huyo kinara wa demokraaia na haki za binadamu( Marekani)
Mfano mwaka October 2018, mwandishi wa habari, wa gazeti la The Washington Post (Moja ya gazeti maarufu kabisa nchini Marekani) na mwanaharakati marehemu Jamal Ahmad Khashoggi, ambaye alikuwa ni raia wa Marekani, mwenye asili ya Saudi Arabia, aliuwawa kikatikili kabisa katika ubalozi mdogo wa Saudi Arabia jijini Instanbul, Uturuki.
Mauaji ambayo yalishutumiwa vikali sana hapa duniani, na kumekuwepo na tuhuma za serikali ya Riyadh (Saudi Arabia) kupitia mwana mfalne( Crown Prince) Mohammed Bin Salman kuhusika na mauaji hayo ya kikatili .
Lakini pia, mwaka 2012 mwana mtandao maarufu nchini Saudi Arabia, Raif Badawi,alihukumiwa miaka 10 jela kwa kosa tu la kuanzisha mjadala mtandaoni kuhusu uhuru wa kujieleza ( Freedom of expression) nchini Saudi Arabia, hukumu ambayo ilishutumiwa vikali na mataifa mbalimbali duniani
Lakini cha ajabu kabisa, pamoja na yote hayo, mpaka leo serikali ya Marekani ( kinara wa demokraaia na haki za binadamu duniani) haijawahi kuchukua hatua zozote dhidi ya serikali ya Riyadh,au hata kutoa kauli tu kupinga ukiukwaji mkubwa huo wa haki za binadamu
Unajua ni kwanini?
Kwa mujibu wa takwimu kutoka ofsi ya wawakilishi wa wafanyabiashara wa Marekani (Office of The United States Trade Representatives ), biashara ya bidhaa na huduma ( Goods & Services) baina ya nchi za Marekani na Saudia Arabia kwa mwaka 2018 ilikuwa na thamani ya dola za kimarekani billioni 48.3, kwa maana hiyo, nchi ya Saudi Arabia, ni mshirika mkubwa wa kibiashara wa nchi ya Marekani, na ndio sababu inayopelekea nchi ya Marekani, kufumba mambo dhidi ya Saudi Arabia
Kwa hayo machache tu, nitamshangaa sana Mtanzania ambaye atakuwa na fikra potofu za kuamini kuwa mabeberu wanaojifanya wako mstari wa mbele kwenye kwenye kutetea demokraaia na haki za binadamu nchini Tanzania, ni kweli wanaipenda sana nchi yetu.
Mabeberu wanafanya hivyo kwa agenda zao (hidden agenda) na ni kwa maslahi yao na nchi zao
Tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu huu,wa tarehe 28 mwezi huu, ni vema watanzania wenzangu tukawa makini sana na watu hawa, tusikubali kudanganywa na mtu au taifa lingine lolote
Mungu ibariki Tanzania
Ngamanya Kitangalala Mwaswala
kngamanya@yahoo.com