Watanzania tupunguze maisha ya Video / Drama kwani yanatuaibisha sana!

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,052
107,535
Ni hivi punde tu nimetoka kumtembelea Msanii fulani ( wa Kiume ) ambaye mara nyingi mno huwa hakauki ama Mitandaoni au Luningani au katika Midomo yetu bila kusahau katika Magazeti mengi ya Udaku na hamuwezi amini nimekalia tu katika Kochi lake ( Sofa ) nimegongana na Kunguni wa kufa mtu. Kama na hiyo haitoshi nimeingia katika Gari lake ili anifikishe somewhere ili niweze kutiririka na kuserereka Kitaa na kwenyewe nimekutana na Mende wa kutosha tu.

Cha kusikitisha wakati nikisabahiwa / nikisalimiwa na hao Kunguni na Mende mwenzangu ( Msanii mwenye Sifa ) yeye ndiyo Kwanza hajali na anaona hao Marafiki zake Kunguni na Mende wana haki ya Kuishi katika Nyumba na Gari yake.

Mwisho nimalizie tu kwa kusema Watanzania tupunguze Sifa / Maisha ya Video / Drama / Shobo hasa katika maisha yetu pale tunapokuwa nje ya maeneo yetu ya kuishi kwani kumbe uhalisia wetu haukakisi tunavyoonekana Mitandaoni / Luningani na Magazetini.

Msanii mzima Kwako umejaza Kunguni na katika Gari lako kuna Abiria wengine Mende umewaficha. Sasa kama leo tu nimetoka kumtembelea Msanii huyu na nimekaribishwa Kwake na Mwenyeji Kunguni na Abiria Mende katika Gari lake vipi nikisema nikawatembelee na wengine ambao na wao huku nje wamejawa na Mashauzi kibao?

Nawasilisha na tuishi tu maisha yetu ya asili kisha tupunguze Sifa / Shobo ambazo Kiukweli hatufanani nazo.
 
unajua kwamba kunguni na mende sometimez wanazaliwa kwa sababu ya umasikini na sio uchafu....kama leo hii wewe mleta mada ungenunua kazi ya msanii huyo ni kuachana na habari za kicopy kazi zao ata usingeondoka na mayai ya kunguni nyumbani kwake...cha muhimu ni kuacha unafiki.
 
Chorus
Hatucheki na wewe sababu ya uongo na umbea,

Hatuongei na wewe sababu ya uongo na umbea,

Kwa sababu moja tu ya uongo na umbeeea,

Hook
Uongo na umbea umbea
Uongo na umbea umbea

Omg ft Baraka-Uongo na Umbea
 
Looooo

Ha ha haaaa kunguni na mende tena!!!!

Kwanza kilichokupeleka kwake na kuendelea kukaa inaonyesha unampapatikia sana ha ha haaaa, ni kama unamuona yeye yupo juu..si ungeondoka au kukaa chini.. vipeeee???

Mitandaoni watu wengi yao ni maisha feki feki fekiiiiiii
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom