Watanzania tungeshika bango kama Masoud Kipanya

Mpitagwa

JF-Expert Member
Feb 10, 2012
2,339
1,119
WanaJF, nimefuatilia kwa kina jinsi watanzania wa kawaida kwa nafasi yetu kama waajili wa serikali na kugundua kuwa tunafanya uzembe mkubwa wa kusimamia serikali yetu kwa kukubali kubadilishiwa CD kila uchwao. Lakini Mtanzania mwenzetu kipanya yeye amejipambanua tofauti kwa kung'ang'ania hoja ya kwanza na kugoma kusikia CD ifuatayo. Tokea limetokea tatizo la mgao wa umeme yeye aliamua kuwa cartoon zake zote zitakuwa na dack background ikiwa ni alama ya kuwakumbusha viongozi kuwa tunatatizo la umeme bado lipo na umepita zaidi ya mwaka bado analia na giza la mgao wa umeme na sasa mgao unarudi tena. Je watanzania wote tungekomaa kila mtu kwa nafasi yake tatizo la umeme lingefika hapa? Watanzania matatizo yetu ni mengi na hawezi kwisha kwa pamoja au kwa kubadilishawa CD. Sasa hivi ni muda mwafaka kwa wote kukomalia tatizo moja then likitatuliwa ndoo tuhamie lingine. Hongera Kipanya kwa hili na kwa kutukumbushia suala la hatima ya wabunge waliofukuzwa na vyama vyao, na mengine mengi unayotujuza.
 
Ktk katuni yake amekuwa akimaanisha hii nchi ni giza, kila kitu ni giza!
 
...Ndiyo, yaani Mabwepande -giza, CV za waheshimiwa -giza, tume (huru?) za uchunguzi wa mauaji-giza, bodi za mikopo ya wanafunzi-giza, zahanati na mahospitalini giza, Kagame CUP -giza yaaaaaaniii everything
 
Kweli nchi hii tuko gizani kwa mambo mengi, mikataba tusaini kama tuko gizani, yaani kila kitu ni giza x 10000000
 
Raisi Giza, Wabunge Giza, MAwaziri Giza,.......


MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
hasa vyombo vya habari vinatuangusha kama magazeti na TV na redio walitakiwa washike bango kweli kweli na kuandaa midahalo hasa ya viongozi kuulizwa maswali na wanachi kusiana na mambo ya msingi na yenye utata kama wenzetu dunia ya kwanza wanavyofanya kenya naona wanajitahidi kweli
 
Giza bado linaendelea, Arusha kioo cha ndege kinapasuka, majinia ajali za meli zinakuwa za kawaida sasa na barabarani tumezoea kabisaa. Sasa hivi watu kupoteza maisha imekuwa kitu cha kawaida. Tunaelekea wapi? Bado giza linazidi kuongezeka.
 
Jamaa kiuhalisia anajitahid sana na c katka suala la umeme tu hata katika mambo meng kama kuhusu migodi au huduma za kijamii kama maji na hulka za wanasiasa, binafsi nimekuwa nikifuatilia katuni anazochora kupitia Twaweza na huwa zinarushwa mara nyingi kupitia Star tv. Sio siri jamaa anajua na anaweza na binafsi nazikubali sana kazi zake.
 
Mimi ninafanya hivyo pia. Kila ninapopata nafasi hata kama ni katika mazingira hatarishi namna gani, huwa ninaulazimisha ubongo wangu kufikiri kwa kasi namna ya kufikisha ujumbe wa umuhimu wa kuiondoa CCM madarakani bila kujisababishia matatizo ya kiusalama.
 
Back
Top Bottom