Watanzania: Tunataka rais mkali, dictator, Je kuna dalili za kumpata mwenye sifa hizi CCM?

mcfm40

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
4,452
3,150
Mara nyingi watanzania walipokuwa wanaulizwa aina ya rais wanayemtaka, wamekuwa wakisema wanataka rais mkali kwa mafisadi na wabadhirifu, rais atakayeogopwa na waliochini yake. kwa lugha nyingine wanamtaka rais mwenye hulka ya kidikteta kidogo katika kusukuma mambo.

Hili linaonekana ni kutokana na huyu rais anayemaliza muda wake kutokuwa serious katika mambo mengi na pia kuonekana kutoogopwa na waliochini yake. Mfano , aliwahi kusema wezi wa Epa wakirudisha pesa atawasamehe, mapaka leo hatujui nani walirudisha na nani hawajarudisha na hatua gani zimechukuliwa.

Aliwatetea mafisadi wa Escrow badala ya kuonesha ukali kuwaondoa na kuwashitaki. Kinyume chake alidai fedha za escroe hazikuwa za umma. Mpaka leo kina Seith na Rugemalila pamoja na kutoa rushwa kwa viongozi wa serikali hawajachukuliwa hatua yoyote. Zaidi sana pesa zilizowekwa kwenye akaunti ya Stanbic mpaka leo hawajulikani waliozibeba na magunia na sandarusi. Hajaoekana kujali na hili limewafanya wengi wahisi naye ni mnufaika.

Kuna kipindi Sitta akiwa spika alimwambia aongoze ukali kidogo!
Imemlazimu kuvunja baraza la mawaziri mara nyingi kwa utendaji mbovu wa wateule wake. Na mara zote amefanya haya kwa kushinikizwa na sio kwa hiari yake mwenyewe.

Haya yote yamewafanya wananchi waone kwamba Tanzania inahitaji kiongozi dikteta na mkali ili kusukuma mambo yaende. na mara nyingi hata leo ukiwauliza utapata jibu la namna hii.

Je nje ya upinzani kuna uwezekano wa kupata kiongozi wa namna hii ndani ya CCM kati ya wale wenye uwezekano mkubwa wa kupitishwa? Kwa maneno mengine kuna mwelekeo CCM kuzingatia mawazo haya ya wananchi katika vikao vinavyoendelea huko dodoma?
 
Si mwingine ni Prof Sospeter Muhongo ndugu. Hakuna kazina kama hii kwenye uongozi wa hii nchi si upinzani wala chama tawala ndugu.
 
Tatizo la professor Muhongo ni kwamba hana busara za kiuongozi. Tunataka diketat mwenye busara. Muongo amekuwa nagombana na kila mtu na kuishia kujigamba tu kwamba yeye anajua kila kitu. Kiukweli muhongo hana sifa hata chembe za kuwa rais.
 
Huu uzi ulipotea ghafla sijui nini kilitokea au nyuzi zinamiminika km mvua hapa?
 
Kichwa nyeupe anafaa japo alikuwa na element za ufisadi lakini.....
 
Tatizo la professor Muhongo ni kwamba hana busara za kiuongozi. Tunataka diketat mwenye busara. Muongo amekuwa nagombana na kila mtu na kuishia kujigamba tu kwamba yeye anajua kila kitu. Kiukweli muhongo hana sifa hata chembe za kuwa rais.

very arogant
 
Mwakyembe ndio mwarobaini wa ccm. Ana akili yaani mwanasheria so issue za kustakiwa au kutofata sheria hamna kwake na anamaamuzi angalia alivyotusafishia bandari hadi kikwete kasifia jana na airport ilivyokuwa njia ya madawa
 
Lowasa pekee atosha,yule padri slaa hawezi girfriend wake tu anamuendesha je mafisadi atawaweza?

Maweeee! Ndio wanamleta Membe? Same old story! Watu wanadhani kuchekacheka na kutabasmu vizuri ndio sifa ya kuwa rais!
 
Back
Top Bottom