figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,890
Salaam Wakuu,
Pamoja na mapungufu ya mambo ya vyama vya Siasa na Malalamiko ya Demokrasia, safari hii nafuu kuliko wakati ulopita.
Rais Samia anaiongoza Tanzania. Na hatoki kwani bado anautamani Urais na ziara za hapa na pale.
Watu wanaojipanga kumtoa kwenye kiti chake kwa karatasi, msitegemee atawaletea uji kwenye kijiko cha dhahabu, Munatakiwa Mjipange kiakili ikibidi ombeni msaada nje ya Nchi, ongea na Waasisi wa Nchi hii ili wawasaidie kumshawishi matakwa yenu.
Vinginevyo mtaishia kupiga kelele. Kikwete aliwahi kusema, Kelele za Mlango, hazimzuii mwenye nyumba kulala.
Kwa Upande wangu Namshukuru Mungu kwa kutoondolea balaa, Janga na jitu lisilofungwa Kengele.
Asingekuwa Mungu, yule Baba angetutoa roho.
Thread hii nimeiandika kichwani Mwangu nikiwa Mifereji ya damu inayotiririka ya Watanzania Ben Saanane, Alfonce Mawazo na Wengine wengi.
Zama za majizi za kuchukua pesa kwenye akaunti za beni za Wavuja jasho kisha kuwafungulia kesi za uhujumu uchumi na kuwataka waombe msamaha, imekwenda na maji. Sasa akaunti unaacha hela kesho asubuhi ukiamka unaikuta salama.
Mungu ni mwema
Pamoja na mapungufu ya mambo ya vyama vya Siasa na Malalamiko ya Demokrasia, safari hii nafuu kuliko wakati ulopita.
Rais Samia anaiongoza Tanzania. Na hatoki kwani bado anautamani Urais na ziara za hapa na pale.
Watu wanaojipanga kumtoa kwenye kiti chake kwa karatasi, msitegemee atawaletea uji kwenye kijiko cha dhahabu, Munatakiwa Mjipange kiakili ikibidi ombeni msaada nje ya Nchi, ongea na Waasisi wa Nchi hii ili wawasaidie kumshawishi matakwa yenu.
Vinginevyo mtaishia kupiga kelele. Kikwete aliwahi kusema, Kelele za Mlango, hazimzuii mwenye nyumba kulala.
Kwa Upande wangu Namshukuru Mungu kwa kutoondolea balaa, Janga na jitu lisilofungwa Kengele.
Asingekuwa Mungu, yule Baba angetutoa roho.
Thread hii nimeiandika kichwani Mwangu nikiwa Mifereji ya damu inayotiririka ya Watanzania Ben Saanane, Alfonce Mawazo na Wengine wengi.
Zama za majizi za kuchukua pesa kwenye akaunti za beni za Wavuja jasho kisha kuwafungulia kesi za uhujumu uchumi na kuwataka waombe msamaha, imekwenda na maji. Sasa akaunti unaacha hela kesho asubuhi ukiamka unaikuta salama.
Mungu ni mwema