Watanzania tunapaswa kuambiwa na kujua ukweli kwamba Gesi inayochimbwa Mtwara si yetu

Mkuu mkulima gwakikolo , kuna maswali mengine, kuwauliza baadhi ya watu sio kuwatendea haki!.
Naomba usinionee bure!.
Swali hili ni kama uko na rafiki yako, anamjua baba yako, halafu mko mbele ya watu, kuna mlevi mmoja watu wanancheka kwa kuzidiwa na kilaji, halafu rafiki yako anaona kabisa huyo ni mzee wako, halafu anakuuliza wewe mbele ya ule umati wa watu, ati yule mlevi ni baba yake nani vile?.
Wewe utajibu?. Mswali mengine sio ya kujibiwa, swali hili ungeniuliza mimi enzi zangu zile za maswali kama haya
ndio ningekujibu.
P
Paskali Bhana...sasa ulipoamua kugombea ubunge ulitaka ukaibadili hii janja ya Chama chenu sio??
 
Mkuu Hakimu Mfawidhi , hili la gesi wewe ndio umelijua leo?.
Hali hiyo ilikuwa zamani, lakini sasa tuna sheria mpya ya madini na extractive industry yoyote, kila kinachopatikana, asilimia 16% ni mali ya Watanzania. Yaani serikali yetu ina own 16% ya migodi yote, hivyo japo ni kweli kila kinachovunwa ni mali ya mmiliki, hivyo Watanzania ni wamiliki wa hiyo 16% ya free carried shares kwenue rasilimali zote za extractive industry.
P
Nyie ndio mnaliponza hili Taifa kwa kundelea kutetea CCM iliyotufikisha hapa.

Hiyo sheria iko tu ila sidhani kama hata inasimamiwa
 
Paskali Bhana...sasa ulipoamua kugombea ubunge ulitaka ukaibadili hii janja ya Chama chenu sio??
Mkuu mkulima gwakikolo , please hear me sababu zangu

Naa baada ya kutupa karata yangu, na nilichoambulia, kwanza nilikubali matokeo
Na kisha nikatoa maoni yangu
Na kweli mwisho wa siku, hicho nilichokizungumza hapo juu, ndicho kimekwenda kutokea, mkono mtupu haulambwi, wenye mikono mirefu ndio walioptishwa with few exceptions, hivyo sasa tusubiri
2025.
P
 
Nyie ndio mnaliponza hili Taifa kwa kundelea kutetea CCM iliyotufikisha hapa.
Mkuu Kishina cha Mshahara, Salary Slip , humu duniani hakuna kitu kizuri kama ukweli, the truth, na ukiwa mkweli mno sometimes, there is a price to pay!. Mimi ni kada wa CCM, ila ni miongoni mwa makada wachache ambao ni makada contemporary toka kundi la ma lumpen proletarians wakati CCM kama chama kimeshikwa, na kundi la ma bourgeoisies ambao ndio huamua kila kitu kwa ajili yetu. Japo ukweli huu ni mchungu ndio ukweli wenyewe, CCM ndio kila kitu!, CCM ndio Tanzania!, bila CCM hakuna Tanzania!. Nakuomba na wewe kuwa tuu mkweli toka ndani ya nafsi yako kwa ukweli kabisa wa dhati ya moyo wako, kuwa ni kweli CCM ndio imetufikisha hapa, lakini kwa vyama vilivyopo, hivi hivi vilivyo, kuna chama gani credible cha kuikabidhi ikulu yetu?. Nakuhakikishia, hakuna!. Sasa kama kilichopo ni CCM only na hakuna kingine, then what?. Jibu ni CCM only!. Kubali, kataa!.
P
 
Kusema eti TPDC ni madalali tu, SIO SAHIHI!

Gesi iliyoanza kuchimbwa kwa miaka kadhaa sasa, ni ya Mnazi Bay.... hii ilichimbwa wakati wa Mkapa, na asilimia kubwa za hisa zilikuwa zinamilikiwa na Artmas waliokuwa wanazalisha umeme hukohuko kusini kabla hawajafungasha virago na kuuza hisa zao!!

Baada ya Artmas kuondoka, kwa sasa mwenye share nyingi zaidi kwenye hiyo gas ni Maurel & Prom wanaomiliki 48.6% ya hisa, Wentworth Resource 31.4%, huku TPDC unaowaita eti MADALALI tu wakimiliki 20% ya hisa!!

Sasa kama TPDC na hisa zao 20% ni MADALALI, hivi ni akina nani wale waliokuwa wanafurahia 16% ya hisa za kampuni za madini?!

Kwahiyo ni sahihi kusema wanamiliki stake ndogo ya hisa lakini sio kweli kusema ni MADALI tu!!

Kama mnaamini Nyerere Dam itawapa umeme wa bei rahisi basi itakuwa MNAJIDANGANYA kupita kiasi!!

REMEMBER, trillions of TZS zinatumika kwenye lile bwawa, na kiasi kikubwa kikiwa ni pesa kutoka private banks!!

Sasa ikiwa Daraja la Kigamboni lililogharimu less than TZS 500 Billion mnalipia ili ku-cover gharama za ujenzi, tena za kumlipa NSSF mwenye pesa zetu wenyewe, who do you expect will carry the burden of trillions being used in Nyerere Dam?

Jibu ni wewe na wenzako mnaodanganyana Nyerere Dam itawapa umeme wa bei rahisi wakati hata kuvuka daraja tu, unakamuliwa hadi watu wanakwepa kupita pale!!

Kama ni ya Msimbati, ndo hiyo ambayo nimekupa percentage ownership na kama ni ya kina kirefu ambacho bado haijachmbwa, yenyewe bado!!

Na kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta na Gas ya mwaka 2015, MMILIKI wa VITALU VYA GESI ni TPDC! Kampuni yoyote, iwe ya nje au ya ndani, ikitaka kuchimba gas inatakiwa KUINGIA UBIA na TPDC, and not otherwise!!

At the time, TPDC itakuwa inafahamika kama National Oil Company, na kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta na Gesi, inatakiwa kumiliki AT LEAST 25% ya share! So that having been said, it's all about TPDC financial ability to acquire even MORE SHARES!!

Man,

Natural Gas Industry may offer more than you think!! The problem watu mnaangalia gas industry katika eneo la uchimbaji peke yake!

Natural Gas Industry is an engine for other sectors of economy, na pia ina maeneo makuu 3:-

1. Upstream
2. Midstream
3. Downstream.

Upstream is very expensive to run, na HAKUNA Mtanzania anayeweza... hapa ndipo pale Muhongo alikuwa anaonekana ni mtu wa ovyo lakini ndo ukweli wenyewe!!

Na ukitaka kufahamu ni namna gani ilivyo expensive ku-run upstream level of the gas industry, ni ile plant inayotoka kujengwa kwa matrilion ya shillings! Hapo ndipo mtu anatakiwa kujiuliza unahitajika uwekezaji wa namna gani kuweza ku-recover zile trillions zinazotaka kuwekezwa just kwenye processing industry!!

Kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta na Gas ya 2015, National Oil Company wamepewa EXCLUSIVE RIGHTS ya ku-run Mid and Lower Stream!!

Wewe ukiweza kuwa na ONLY 10% Market Share of Midstream Level, trust me, utakuwa the biggest billionaire in the country!

What entails Midstream Level?

Kwa mfano, kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta na Gas ya 2015, kabla hatujaanza kukimbilia kufanya gas export, ni lazima taifa liwe limejitosheleza na nishati ya gas!

Na katika mpango uliopo, National Oil Company wanatakiwa kusambaza mabomba ya gas Tanzania YOTE, ili hatimae gas ifike moja kwa moja kwenye nyumba za watu, viwandani, na vituo vya kujazia gesi kwenye magari!

Shughuli ya Usambazaji na/au Usafirishaji wa Gas ni one of the Midstream Activities ambayo sheria inampa National Oil Company Exclusive Right ya ku-run hiyo midstream!!

Upstream, ambayo ndiyo National Oil Company hawajapewa hiyo exclusively right is just about GAS EXTRACTION, and that's it!!!

It's unfortunately nipo safarini, ningeongea mengi kuhusu midstream and downstream, na pia kuongea kwa mapana kuhusu Local Content... yaani Sheria inavyotaka ushiriki wa WATANZANIA kwenye midstream and downstream!!

Na sina shaka mara kadhaa watu wamekuwa wakisema Sheria ya Mafuta ya Gas ya mwaka 2015 ni MBOVU huku am certain wengi wao kama sio WOTE, hawajaisoma hiyo sheria but TRUST ME, shughuli za uchimbaji zikianza, lazima kutakuwa na ATTEMPT kubadili sheria kwa sababu, Google Financial Statement of any Major Global Oil and Gas Company you know, utakuta nyingi ya kampuni hizi huwa zinafanya hadi Midstream Activities huko wanakoendesha shughuli za uchimbaji!

Do that homework!!

Lakini pamoja na hizo Midstream and Downstream Activities ambazo NOC wamepewa exclusive right ya kuziendesha, pia take anothe homework kuangalia byproducts zinazopatikana kutokana na natural gas processing!!

Kukupa mfano mdogo tu, pale Mtwara panataka kujengwa Kiwanda cha Mbolea ambacho thamani yake ni AT LEAST 50% ya gharama za ujenzi wa Nyerere Dam (about TZS 4 Trillion as at 2020)! Tanzania HAKUNA kiwanda chenye thamani ya angalau 25% ya hicho kiwanda kinachotaka kujengwa Mtwara!

Byproducts zinazotokana na Natural Gas Processing, moja ya matumizi yake ni uzalishaji wa mbolea, na ndizo zitalisha hicho kiwanda!!!

To cut a long story short, Gas Industry itashindwa kuwa Game Changer kwa SABABU TU nchi yenyewe hii imejaa viongozi na watendaji wezi!! Wale Waarabu wakati wanaaza wala usidhani kwamba eti walikuwa wanamiliki shares nyiiiiingi kwenye mafuta na gas, hell no but still gas and oil changed The Arab World!! Na wao, ni kama sisi, walikuwa hawana hata ubavu wa kuchimba hayo mafuta/gas, wenyewe!!

Tatizo letu, linaweza kuwa kama Angola na Nigeria. Nchi ni maskini lakini viongozi na watendaji ndo matajiri wakubwa!! Na kama mnadhani Tanzania kuna ufisadi, basi hamjawahi kuona ufisadi! Subirini uchimbaji wa gesi ya kina kirefu ianze kuchimbwa, hapo ndipo hasa mtakapofahamu ni kwanini NIgeria inaitwa ndio Kinara wa Ufisadi!!

In fact, hata Waarabu na wenyewe ni Mafisadi Balaa sema tawala za kifalme zinafanya ufisadi uwe wa wachache, na hao wachache pia wanawafanyia maendeleo wananchi!!

Chukulia mfano mdogo tu wa Ibara ya 219 (1) ambayo inasema:-

Sasa tuseme wewe umepewa tenda ya ku-supply mabomba tu kwenye mradi wa ujenzi wa gas distribution infrastructure nchini kote!!

Ulishawahi kujiuliza hiyo tenda itakuwa na thamani ipi kwako!

Lakini hata kwa ibara ndogo ya pili, inayosema:-

Sasa tuseme unamiliki ONLY 25% ya hiyo kampuni inayoagiza bidhaa kutoka nje, kwa zile bidhaa ambazo hazizalishwi TZ, na kwa kuangalia ukubwa wa gas industry, hivi ulishawahi kujiuliza utakuwa unafanya biashara yenye ukubwa kiasi gani kwa hizo hizo 25% kama kweli ni zako?!

Sasa nikupe tatizo KUBWA la Watanzania!

Tutaendelea kulia lia hivi hivi "tumeibiwa! tumeibiwa" badala ya kujipanga!!

Kuja kushtuka, shughuli zimeshafikia peak, kampuni za uchimbaji zinahitaji supply ya Goods X, lakini HAKUNA Mtanzania hata mmoja mwenye kampuni inayoweza ku-supply kwa sababu miaka yote walikuwa wanalilia tu!!

Kitakachotokea, wanakuja Wajanja Wakenya, wanakuambia muanzishe kampuni ya hiyo wakati pesa HUNA! Lakini kwavile sheria inataka Mtanzania amiliki at least 25% Shares, kwenye MoU na Article Association mnayopeleka BRELA anakuandika unamiliki 25% ambazo kimsingi sio ZAKO, bali ni za Mjanja Mkenya atakayekuwa anakulipa tu vipesa kidogo sijui labda commission from your fake 25% SHARES!!

Hiyo ndo ile Muhongo alikuwa anasema HATUTAKI MADALALI!!

Anyway, keep dreaming kwamba Bwawa La Nyerere will be very special for y'all but whether you like it or not, hamna kitu pale zaidi ya huo umeme!!

Sasa si bora hata huo mnaoita Mradi wa Kifisadi wenye uwezo mkubwa sana wa ku-stimulate other sectors of economies zinazoweza kutoa ajira na fursa ya kibiashara kwa Watanzania wengi zaidi!!

What about Bwawa la Nyerere?! Ndo kwa mfano, umeme huooooo, umeshaanza kuwaka kutoka Bwawa la Nyerere... WHAT NEXT?

Akili za Kuambiwa...
Kuna vitu eidha unachanganya ama unaandika kishabiki.

1. Nisaidie kujua hao artmas walikua wanazalisha umeme kisha wanaupeleka wapi na plant ya kuzalisha umeme ilikua imejengwa wapi?

Kwa kumbukumbu zangu kampuni iliyosaini HGA ni Wentworth mwaka 2004. Kampuni hiyo ikauza hisa zake 51% kwa M&P mwaka 2009 ila hadi kufikia 2015 M&P walikua na 60% na hao Wentworth wakiwa na 40% za exploration ownership ya Mnazi Bay.

Kwa kumbukumbu zangu pia ni kwamba Wentworth anamiliki 31% shares, M&P 48% na TPDC anamiliki 20% ya operations.

Kuna tofauti kati ya exploration ownership na operations ownership.

2. Unalinganisha vitu 2 tofauti, kwamba nani atabeba gharama za bwawa. Ukatolea mfano daraja la kigamboni.

Daraja la kigamboni limejengwa kwa hela za wafanyakazi waliokua wanachangia hela zao NSSF hivyo zile hela sio za nchi, ni za wafanyakazi hivyo lazima zilipaswa kurudishwa. Bwawa la Nyerere linajengwa kwa kodi za wananchi walipa kodi, hizo serikali ina mamlaka ya kuzitumia itakavyo kwa maslahi ya watu wote ama ya nchi.

Hivyo gharama za bwawa tayari zinabebwa na wananchi wote sio kama hela za NSSF hizo ni za wafanyakazi wamekatwa kwenye mishahara yao na sio kodi ile.

Kuna mambo umeandika kishabiki hadi inatia shaka jinsi unavyofikiri. Huoni faida ya bwawa zaidi ya umeme, ila husemi ni umeme wa bei nafuu, umeme wa maji Duniani kote ndio wa bei nafuu kuliko kitu chochote, sasa wewe huelewi kwamba kukiwa na umeme wa kutosha na wa bei nafuu kutasisimua sekta nyingine za uchumi?

Hilo la kwanza, bwana wa mtera lilijengwa anablengo lake ilikua kudhibiti mafuriko ndio baadae ikaja wazo la kuweka ama kuzalisha umeme, je toka Mtera imejengwa umewahi kusikia mafuriko hilo eneo?

Kwa msingi huo bwana la Nyerere litasaidia kuzuia mafuriko kama yale yaliyotokea mwaka jana huko Rufiji, huoni hii kama ni faida, wewe unaona umeme tu?

Ukiachia kudhibiti mafuriko, kuna uvuvi, utalii, kilimo cha umwagiliaji kwani kunakua na uhakika wa maji ya kutosha maeneo ya jirani, hilo huoni kama ni faida, wewe faida unayoiona ni umeme tu.

Jambo la tatu ni kwamba bwana linategemea kuwepo zaidi ya miaka 50 ijayo, hiyo gesi unayoisema ikianza kuchimbwa kwenye large scale haiwezi kuwepo zaidi ya miaka 20, itaisha ila maji hayaishi Duniani.
 
Kuna mambo bado hayajawekwa sawa na yakaeleweka vyema.

Gesi inayochimbwa Mtwara sio ya watanzania, ile gesi ni ya makampuni ya kigeni na sio ya Watanzania.

Ieleweke pia kwamba Gesi ile iko 18% nchi kavu na 82% majini ama baharini kwenye kina kirefu.

Ieleweke zaidi kwamba shirika la mafuta na petroli la Taifa ama TPDC wao ni watu wa kati kati ama middle man wa gesi inayozalisha umeme Tanzania.

TPDC wao wananunua gesi kutoka kwa makampuni ya kigeni yanayochimba gesi na kisha kuiuzia TANESCO, yaani makampuni yanachimba, yanapiga gharama za uchimbaji na faida yake, yanaiuzia TPDC, kisha TPDC anaweka cha juu na yeye anaiuzia TANESCO halafu TANESCO anazalisha umeme anauzia wananchi.

Kwa kiswahili chepesi ni kwamba, kwenye gesi ya mtwara TPDC ni dalali ama machinga wa gesi, yeye mwenyewe hana gesi ila kutokana na sheria za nchi, ana umiliki kidogo wa hisa kwenye hayo makampuni yanayochimba gesi. Serikali ama TPDC hawana kisima hata kimoja cha gesi, wao pia wananunua.

Hivyo basi ifahamike kwamba umeme wa gesi hautakuja kua bei Rahisi Tanzania kwa sababu gesi ina madalali ama inapitia mikono mingi na kila wakala ama dalali anaweka cha juu hadi kumfikia TANESCO na tanesco kuwafikishia walaji ambao ni wanachi.

Hivyo ifahamike zaidi kwamba gesi iliyoko kusini 90% ilishauzwa na wamakonde wakae wakijua hawana gesi pale, sio yao ni ya makampuni ya kigeni.

Na hao unaosikia wanasema uanzishwaji wa kiwanda cha kuchakata gesi utabadili maisha ya watanzania ama wanaita game changer huo ni uongo wa wazi kwani kiwanda hicho faida pekee ambayo tutaipata kwa Tanzania ni ajira, kodi na vitu vidogo vidogo lakini sio hasa keki ama nyama yenyewe ya gesi kwani gesi sio yetu.

Ukitaka kujua kitakachotokea kwenye gesi kwa kujenga mtambo wa LNG ni kuangalia faida tunayopata kwenye viwanda vya sukari, je tunafaidi uwepo wa bei ndogo ya sukari ama tunafaidi vitu vidogo vidogo kama ajira ya watu wachache, kodi na vitu vingine vidogo vidogo ila bei ya sukari iko juu.

Tunapeana matumaini ila ukweli ni kwamba we are fucked up.

Habari ndio hiyo.
Yanekuwa hayo tena! Looooooohhhhhh!
 
Mkuu Kishina cha Mshahara, Salary Slip , humu duniani hakuna kitu kizuri kama ukweli, the truth, na ukiwa mkweli mno sometimes, there is a price to pay!. Mimi ni kada wa CCM, ila ni miongoni mwa makada wachache ambao ni makada contemporary toka kundi la ma lumpen proletarians wakati CCM kama chama kimeshikwa, na kundi la ma bourgeoisies ambao ndio huamua kila kitu kwa ajili yetu. Japo ukweli huu ni mchungu ndio ukweli wenyewe, CCM ndio kila kitu!, CCM ndio Tanzania!, bila CCM hakuna Tanzania!. Nakuomba na wewe kuwa tuu mkweli toka ndani ya nafsi yako kwa ukweli kabisa wa dhati ya moyo wako, kuwa ni kweli CCM ndio imetufikisha hapa, lakini kwa vyama vilivyopo, hivi hivi vilivyo, kuna chama gani credible cha kuikabidhi ikulu yetu?. Nakuhakikishia, hakuna!. Sasa kama kilichopo ni CCM only na hakuna kingine, then what?. Jibu ni CCM only!. Kubali, kataa!.
P
Aseeeeeee! Yaani umemalizia kishabiki kweli! Mungu anakuona lakini MCCM mwenzangu!
 
Nakuelewa sana kaka, ndio maana nasema mwendazake hakuwa na nia njema. Angeamua kutulia na kusikiliza ushauri tungekuwa mbali sana..
Hao watu ni wapotoshaji na genge lao issue ipo hivi.

Chukulia wewe una shamba pori hekari 10000 huna hela za kuliendeleza.

Anakuja mwekezaji na offer ya kukodi matumizi ya shamba faida mgawane mpaka arudishe hela yake.

Sasa akianza kulima hilo shamba kuna economic benefits maana atanunua mbolea, pesticide, ataajiri watu na faida zinazotokana na kilimo.

Upande wa pili ni makubaliano yako na mwekezaji let’s say kuwekeza inabidi atumie billioni 10 ambazo kutoka mfukoni kwake 3 na 7 kakopa bank kwa miaka 15 high interest. Ambapo kila mwaka anatakiwa arudishe million 800 za bank na yeye billion 3 yake kaigawa kwa 15 ambapo kila mwaka anataka millioni 200.

Mavuno ya shamba faida kila mwaka ni billioni 1.8, sasa kabla amjafanya chochote inabidi kwanza mlipe bank million 800 + na millioni 200 yake. Baada ya hapo kwa sababu wewe umetoa hela yako unataka upate millioni 500, yeye apate millioni 300.

Mwaka ambao mavuno sio mazuri labda mmepata billioni 1.4 utaratibu ni uleule bank na yeye lazima watoe billioni 1 yao; na hiyo millioni mia 400 inayobaki kwa sababu aifikii zawadi yake anaweza sema mwaka huu nachukua 300 nakupa 100. Ila 200 iliyobaki mwakani inabidi tufidie on top of 500.

Ni hivi serikali sio kwamba aijui economic benefits, majadiliano yapo kwenye makubaliano kati ya mwekezaji na mwenye shamba wanagawana vipi na ukikosea utaumizwa sana and those finance are more complicated kuliko huo mfano wa shamba.

Hao watu wakiongozwa na Zitto wanapotosha na kutumia hoja za economic benefit za jamii kama pressure serikali iingie kichwa kichwa na kuingia mkataba mmbovu.
 
Kuna mambo bado hayajawekwa sawa na yakaeleweka vyema.

Gesi inayochimbwa Mtwara sio ya watanzania, ile gesi ni ya makampuni ya kigeni na sio ya Watanzania.

Ieleweke pia kwamba Gesi ile iko 18% nchi kavu na 82% majini ama baharini kwenye kina kirefu.

Ieleweke zaidi kwamba shirika la mafuta na petroli la Taifa ama TPDC wao ni watu wa kati kati ama middle man wa gesi inayozalisha umeme Tanzania.

TPDC wao wananunua gesi kutoka kwa makampuni ya kigeni yanayochimba gesi na kisha kuiuzia TANESCO, yaani makampuni yanachimba, yanapiga gharama za uchimbaji na faida yake, yanaiuzia TPDC, kisha TPDC anaweka cha juu na yeye anaiuzia TANESCO halafu TANESCO anazalisha umeme anauzia wananchi.

Kwa kiswahili chepesi ni kwamba, kwenye gesi ya mtwara TPDC ni dalali ama machinga wa gesi, yeye mwenyewe hana gesi ila kutokana na sheria za nchi, ana umiliki kidogo wa hisa kwenye hayo makampuni yanayochimba gesi. Serikali ama TPDC hawana kisima hata kimoja cha gesi, wao pia wananunua.

Hivyo basi ifahamike kwamba umeme wa gesi hautakuja kua bei Rahisi Tanzania kwa sababu gesi ina madalali ama inapitia mikono mingi na kila wakala ama dalali anaweka cha juu hadi kumfikia TANESCO na tanesco kuwafikishia walaji ambao ni wanachi.

Hivyo ifahamike zaidi kwamba gesi iliyoko kusini 90% ilishauzwa na wamakonde wakae wakijua hawana gesi pale, sio yao ni ya makampuni ya kigeni.

Na hao unaosikia wanasema uanzishwaji wa kiwanda cha kuchakata gesi utabadili maisha ya watanzania ama wanaita game changer huo ni uongo wa wazi kwani kiwanda hicho faida pekee ambayo tutaipata kwa Tanzania ni ajira, kodi na vitu vidogo vidogo lakini sio hasa keki ama nyama yenyewe ya gesi kwani gesi sio yetu.

Ukitaka kujua kitakachotokea kwenye gesi kwa kujenga mtambo wa LNG ni kuangalia faida tunayopata kwenye viwanda vya sukari, je tunafaidi uwepo wa bei ndogo ya sukari ama tunafaidi vitu vidogo vidogo kama ajira ya watu wachache, kodi na vitu vingine vidogo vidogo ila bei ya sukari iko juu.

Tunapeana matumaini ila ukweli ni kwamba we are fucked up.

Habari ndio hiyo.
Doo na mradi wa umeme wa MWALIMU NYERERE H.E.P naona unaenda kutupa hadithi zile zile
 
Ngozi nyeusi kwakweli... ni vituko sana duniani...Yani tupo kama takataka tu. Mtu mweusi hawezi mkomboa mweusi mwenzie zaidi ya kuhakikisha vizazi na vizazi vinakaa kwenye umasikini kikubwa yeye na familia yake wamekimbiza mabillioni nje. Kama kweli Mungu yupo kuna watu watapata tabu sana.


Shida ni elimu yetu ya sayansi na teknolojia ni ndogo au ya kukopi au hatuna wataakanu competent katika nyanja nyingi na hatuna UZALENDO toka kwa viongozi hadi sisi wananchi wa kawaida.

Ngoja nikupe mfano hai; hivi sisi kama nchi hatuwezi kuwa na kampuni ya ujenzi inayoweza kutandika mataruma ya reli ya SGR??----- tufanye hatuna hayo makampuni, basi je ilishindikanaje hiyo kampuni inayojenga SGR kupewa Contract ya kujenga kutoka Dar hadi tuseme Moro tu ambapo katika umbali huo Makampuni yetu au wataalamu wetu wa ndani waweze kujifunza namna ya utandikaji ili utandikaji kutoka Moro--- Mwanza---Kigoma tufanye sisi wenyewe!!! , lazima kutakuwa na changamoto, mfano ujenzi wa madaraja na mahandaki, kazi hizo tuna subcontract.

Kifupi ni kwamba Ubinafsi na ujinga vimetuandama mno sisi Waafrika na ndio maana Wazungu wana take advantage.
 
Ok, hao wageni walitupa nini hadi tukawapa hiyo gesi wachimbe? Bila shaka kuna makubaliano na sisi tumefaidika.
Wageni a.k.a Beberu hawana shida na wewe, wao humaliza tu wenye dhamana.


Kwa Africa Viongozi ndio wenye nchi...ndio maana utasikia Nchi inawaambia Viongozi "mkiwa rafiki na sisi hatutaingilia mambo yenu"....na hakuna pepo wanayoipenda Viongozi kama kuachwa huru wafanyie Wananchi wanavyotaka.
 
Kama hujawahi kumiliki alamsiniliyo Mwadui, au Tanzanite iliyo Mererani...

Hata kwa gesi iliyopo Songosongo, Msimbati n.k itakuwa hivyo hivyo
 
TPDC wapewe tu kitambulisho cha machinga, ila na machinga walianzia Mtwara kwa hiyo ni sawa tu hata gesi tukiipata kwa mfumo wa kimachinga
Mnawaonea tuu hao TPDC.. Hivi tuna uwezo wa kuchimba na kusimamia visima vya gesi sisi kweli? Umeme tuu hapa miaka 60 bado unatuhenyesha ndiyo tutaweza visima vya gesi? Hata Waarabu na mafuta yao lakini kuyachimba walitafuta makampuni, sema wenzetu hawakuingia mikataba ya kindezi kama sisi.
 
Kuna mambo bado hayajawekwa sawa na yakaeleweka vyema.

Gesi inayochimbwa Mtwara sio ya watanzania, ile gesi ni ya makampuni ya kigeni na sio ya Watanzania.

Ieleweke pia kwamba Gesi ile iko 18% nchi kavu na 82% majini ama baharini kwenye kina kirefu.

Ieleweke zaidi kwamba shirika la mafuta na petroli la Taifa ama TPDC wao ni watu wa kati kati ama middle man wa gesi inayozalisha umeme Tanzania.

TPDC wao wananunua gesi kutoka kwa makampuni ya kigeni yanayochimba gesi na kisha kuiuzia TANESCO, yaani makampuni yanachimba, yanapiga gharama za uchimbaji na faida yake, yanaiuzia TPDC, kisha TPDC anaweka cha juu na yeye anaiuzia TANESCO halafu TANESCO anazalisha umeme anauzia wananchi.

Kwa kiswahili chepesi ni kwamba, kwenye gesi ya mtwara TPDC ni dalali ama machinga wa gesi, yeye mwenyewe hana gesi ila kutokana na sheria za nchi, ana umiliki kidogo wa hisa kwenye hayo makampuni yanayochimba gesi. Serikali ama TPDC hawana kisima hata kimoja cha gesi, wao pia wananunua.

Hivyo basi ifahamike kwamba umeme wa gesi hautakuja kua bei Rahisi Tanzania kwa sababu gesi ina madalali ama inapitia mikono mingi na kila wakala ama dalali anaweka cha juu hadi kumfikia TANESCO na tanesco kuwafikishia walaji ambao ni wanachi.

Hivyo ifahamike zaidi kwamba gesi iliyoko kusini 90% ilishauzwa na wamakonde wakae wakijua hawana gesi pale, sio yao ni ya makampuni ya kigeni.

Na hao unaosikia wanasema uanzishwaji wa kiwanda cha kuchakata gesi utabadili maisha ya watanzania ama wanaita game changer huo ni uongo wa wazi kwani kiwanda hicho faida pekee ambayo tutaipata kwa Tanzania ni ajira, kodi na vitu vidogo vidogo lakini sio hasa keki ama nyama yenyewe ya gesi kwani gesi sio yetu.

Ukitaka kujua kitakachotokea kwenye gesi kwa kujenga mtambo wa LNG ni kuangalia faida tunayopata kwenye viwanda vya sukari, je tunafaidi uwepo wa bei ndogo ya sukari ama tunafaidi vitu vidogo vidogo kama ajira ya watu wachache, kodi na vitu vingine vidogo vidogo ila bei ya sukari iko juu.

Tunapeana matumaini ila ukweli ni kwamba we are fucked up.

Habari ndio hiyo.
If thst is the case hatuna haja ya kudrill gas yenyewe. Hi ni rasilimali ya maana safi katika maendeleo ya nchi. Shida kama ni utaalamu wa kuchimba gas yenyewe basi tusubiri mpaka tutakapokuwa na wataalamu wetu wenyewe. Kama ni gharama za uchimbaji na mitambo basi pia tusubiri mpaka tutakapokuwa tumekaa vizuri kiuwezo. Hakuna maana wala tija kuyaacha makampuni ya nje kujimilikisha hii rasilimali. Haiozi itasubiri tukiwa tayari.
 
86 Reactions
Reply
Back
Top Bottom