Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,466
- 113,543
Wanabodi,
Asubuhi ya leo, nimepata fursa kuangalia TBC.
Naibu Waziri wa Afya, Mhe. Dr. Faustine Ndugulile yuko live TBC kwenye kipindi cha Jambo Tanzania.
Amesema "Watanzania hatuna utamaduni wa kupima afya zetu, mtu kwenda hospitali ni mpaka aumwe na kuandikiwa vipimo na daktari, hivyo tunaishi kwa kudra tuu za Mwenyezi Mungu!"- Dr. Ndugulile. Jee hii ni kweli?.
Dr. Ndugulile amesema kutokea kwa vifo vya ghafla kwa baadhi ya watu, kunachangiwa na watu wengi kuishi na magonjwa hatari yanayotibika bila wao kujijua, na kusema kunapofanyika upimaji wa jumla kwenye matukio mbalimbali, kuna mtu amekutwa na presha juu ya 200 na anadunda tuu bila yeye kujijua!.
Dr Ndugulile ametoa wito kwa Watanzania tujenge utamaduni wa kupima afya zetu kwa hiari mara kwa mara, na sio kusubiri hadi tuumwe, ndipo twende hospitali kupimwa na kutibiwa.
Dr. Ndugulile, pia alizungumzia mambo mengi makubwa mazuri ambayo serikali ya awamu ya 5 imeyafanya na inaendelea kuyafanya kuboresha sekta ya afya nchini.
Pia alizungumzia hali ya ugonjwa wa ukimwi na maendeleo ya vita dhidi ya ukimwi, amewasisitiza Watanzania kujitokeza kwa wingi na kupima afya zao kwa hiari na haswa wanaume. Wizara yake na taasisi za upimaji wa hiari, zimelenga kila mikusanyiko, na hata juzi kati kwenye mechi ya watani wa jadi, kulikuwepo na kambi ya upimaji wa hiari.
Pia Waziri Ndugulile aliwahakikishia Watanzania kuhusu ubora wa condoms za bure ni ubora ule ule sawa na condoms za kulipia, condoms zote zinazoingizwa nchini, zinapimwa kiwango cha ubora, hizo condoms za bure, zinatolewa bure kwa sababu kuna watu wamezilipia ruzuku, na sio za bure kwa sababu zina ubora hafifu hivyo hazina thamani, na zile condoms za gharama, zina gharama sio kwa sababu ya ubora, bali ni sababu za kibiashara tuu kwa kuongeza ladha, vikorombwezo na rangi mbalimbali ili tuu kuvutia mtumiaji lakini ubora wa condoms zote ni ule ule.
Pia Dr. Ndugulile alizungumzia baadhi ya changamoto za sekta ya afya na namna ya kuzikabili, changamoto kuu ni nguvu kazi, tuna wafanyakazi wachache kuliko mahitaji, na kutolea mfano wataalamu wa X-Ray ni wachache, hivyo sasa serikali imeanzisha Digital X-Ray machines ambazo, sasa X-Ray zitapigwa hospitali zote nchini na kutumwa kwenye a reading centre ambayo kutakuwa na wataalamu, na hapo hapo wanarudisha majibu kule ilikopigwa. Huu sasa ndio mwanzo wa Tanzania kufanya telemedicine.
My Take
Kwa maoni yangu, Dr. Ndugulile is good kwenye kujieleza, anafaa sasa awe awe waziri kamili, na waziri wake atafutiwe pengine pa kwenda. Ingekuwa na waziri wake ana uwezo kama huu, Watanzania wangeilewa vizuri zaidi awamu hii ya tano na mambo mazuri inayowatendea Watanzania kwenye sekta ya afya, such that come 2020, they will do the right thing.
Tufike mahali serikali yetu iendeshwe kwa proffesionalism, Waziri wa Afya awe MD, anamchukua mwanasheria na kumpa wizara ya Afya!, halafu naibu ndio MD, matokeo naibu ndio the right person wa kuelezea masuala la kiafya kuliko Waziri wake, a lawyer!.
Kama ilivyo kwenye wizara ya sheria, yuko mwanasheria bingwa, mambo ya ndani yuko polisi, Habari yuko mwanahabari, ulinzi alipaswa awe mjeshi etc. Kuwaweka mawaziri professionals kwenye technical ministries zinazohitaji professionalism kunaongeza productivity hivyo kuleta tija zaidi, kwa sababu sasa tunaelekea kwenye siasa za ukweli, politics of reality na sio politics of propanganda, tunapaswa, tuachane na siasa za propaganda, mabingwa wa kusema sana ndio wanateuliwa mawaziri, tuelekee kwenye politics of reality, ma professionals wenye kuonyesha uwezo wa delivery ndio wapewe vizara zinazohitaji professionals zao, na sio kwenye uwaziri tuu hata makatibu wakuu, mfano Viwanda na Biashara, yupo yule yule mkemia aliyasimamia ile Ph.D ya kemia, kama asante yake kwa kazi nzuri ya ile dissertation wakati tuna ma Ph.D holders kibao wa biashara. Tusiwateua watu kwa shukrani kwenye key technical, ministries na ukombozi wa taifa hili, lets give the key ministries to the key professionals and the best brains that we have halafu zile wizara za blah blah ndio unawaweka watu wa blah blah.
Jumatano njema.
Paskali.
Asubuhi ya leo, nimepata fursa kuangalia TBC.
Naibu Waziri wa Afya, Mhe. Dr. Faustine Ndugulile yuko live TBC kwenye kipindi cha Jambo Tanzania.
Amesema "Watanzania hatuna utamaduni wa kupima afya zetu, mtu kwenda hospitali ni mpaka aumwe na kuandikiwa vipimo na daktari, hivyo tunaishi kwa kudra tuu za Mwenyezi Mungu!"- Dr. Ndugulile. Jee hii ni kweli?.
Dr. Ndugulile amesema kutokea kwa vifo vya ghafla kwa baadhi ya watu, kunachangiwa na watu wengi kuishi na magonjwa hatari yanayotibika bila wao kujijua, na kusema kunapofanyika upimaji wa jumla kwenye matukio mbalimbali, kuna mtu amekutwa na presha juu ya 200 na anadunda tuu bila yeye kujijua!.
Dr Ndugulile ametoa wito kwa Watanzania tujenge utamaduni wa kupima afya zetu kwa hiari mara kwa mara, na sio kusubiri hadi tuumwe, ndipo twende hospitali kupimwa na kutibiwa.
Dr. Ndugulile, pia alizungumzia mambo mengi makubwa mazuri ambayo serikali ya awamu ya 5 imeyafanya na inaendelea kuyafanya kuboresha sekta ya afya nchini.
Pia alizungumzia hali ya ugonjwa wa ukimwi na maendeleo ya vita dhidi ya ukimwi, amewasisitiza Watanzania kujitokeza kwa wingi na kupima afya zao kwa hiari na haswa wanaume. Wizara yake na taasisi za upimaji wa hiari, zimelenga kila mikusanyiko, na hata juzi kati kwenye mechi ya watani wa jadi, kulikuwepo na kambi ya upimaji wa hiari.
Pia Waziri Ndugulile aliwahakikishia Watanzania kuhusu ubora wa condoms za bure ni ubora ule ule sawa na condoms za kulipia, condoms zote zinazoingizwa nchini, zinapimwa kiwango cha ubora, hizo condoms za bure, zinatolewa bure kwa sababu kuna watu wamezilipia ruzuku, na sio za bure kwa sababu zina ubora hafifu hivyo hazina thamani, na zile condoms za gharama, zina gharama sio kwa sababu ya ubora, bali ni sababu za kibiashara tuu kwa kuongeza ladha, vikorombwezo na rangi mbalimbali ili tuu kuvutia mtumiaji lakini ubora wa condoms zote ni ule ule.
Pia Dr. Ndugulile alizungumzia baadhi ya changamoto za sekta ya afya na namna ya kuzikabili, changamoto kuu ni nguvu kazi, tuna wafanyakazi wachache kuliko mahitaji, na kutolea mfano wataalamu wa X-Ray ni wachache, hivyo sasa serikali imeanzisha Digital X-Ray machines ambazo, sasa X-Ray zitapigwa hospitali zote nchini na kutumwa kwenye a reading centre ambayo kutakuwa na wataalamu, na hapo hapo wanarudisha majibu kule ilikopigwa. Huu sasa ndio mwanzo wa Tanzania kufanya telemedicine.
My Take
Kwa maoni yangu, Dr. Ndugulile is good kwenye kujieleza, anafaa sasa awe awe waziri kamili, na waziri wake atafutiwe pengine pa kwenda. Ingekuwa na waziri wake ana uwezo kama huu, Watanzania wangeilewa vizuri zaidi awamu hii ya tano na mambo mazuri inayowatendea Watanzania kwenye sekta ya afya, such that come 2020, they will do the right thing.
Tufike mahali serikali yetu iendeshwe kwa proffesionalism, Waziri wa Afya awe MD, anamchukua mwanasheria na kumpa wizara ya Afya!, halafu naibu ndio MD, matokeo naibu ndio the right person wa kuelezea masuala la kiafya kuliko Waziri wake, a lawyer!.
Kama ilivyo kwenye wizara ya sheria, yuko mwanasheria bingwa, mambo ya ndani yuko polisi, Habari yuko mwanahabari, ulinzi alipaswa awe mjeshi etc. Kuwaweka mawaziri professionals kwenye technical ministries zinazohitaji professionalism kunaongeza productivity hivyo kuleta tija zaidi, kwa sababu sasa tunaelekea kwenye siasa za ukweli, politics of reality na sio politics of propanganda, tunapaswa, tuachane na siasa za propaganda, mabingwa wa kusema sana ndio wanateuliwa mawaziri, tuelekee kwenye politics of reality, ma professionals wenye kuonyesha uwezo wa delivery ndio wapewe vizara zinazohitaji professionals zao, na sio kwenye uwaziri tuu hata makatibu wakuu, mfano Viwanda na Biashara, yupo yule yule mkemia aliyasimamia ile Ph.D ya kemia, kama asante yake kwa kazi nzuri ya ile dissertation wakati tuna ma Ph.D holders kibao wa biashara. Tusiwateua watu kwa shukrani kwenye key technical, ministries na ukombozi wa taifa hili, lets give the key ministries to the key professionals and the best brains that we have halafu zile wizara za blah blah ndio unawaweka watu wa blah blah.
Jumatano njema.
Paskali.