Watanzania tunahitaji katiba mpya, "Hili halina mjadala" lakini ni nani wa kutuongoza?

kimazinka

Member
Aug 15, 2016
77
64
Ni ukweli usiopingika kuwa Watanzania tunayo hamu kubwa ya kupata katiba mpya. Lkn ni ukweli usiopingika kwamba CCM kama chama na si watu hawako tayari kuliona tamanio hilo likitimia!!

Nimeamua kuna na hoja hii baada ya vilio vya hivi karibuni vya wana wa UKAWA kufuatia kipigo kikali kutoka kwa wana wa CCM japo bado siamini kama katiba ya sasa ndio iliyosababisha kipigo hicho. Lkn mwisho wa siku Watanzania tunahitaji katiba mpya ambayo itakuwa imerekebisha mambo mengi yakiwemo ya uchaguzi n.k.!

Lkn tatizo ninalo liona ni kuwa pamoja na kuwepo matamanio hayo, bado wana hawa Watanzania wanakosa mtu kwenye nia ya dhati ya kuwaongoza kuhakikisha tamanio hili linatimia! Kwanini?

Mwaka 2010 Mara baada ya uchaguzi CDM walibeba jukumu hhili, mapingamizi yalianza mapema kabisa akianza waziri wa sheria wa wkt huo mama Cellina Kombani( mungu amrehemu) yeye alisema hatuhitaji katiba mpya Bali iliyokuwepo ilikidhi mahitaji na kama ingetokea bac ingepigwa vilaka tu!

Cellina kombani alikuwa waziri wa sheria tamko lake lilimanisha tamko la serikali, yaani huo ndo ulikuwa msimamo wa JK na serikali yake. Lkn CDM wakiungwa mkono na makundi mabalimbali ya kijamii hawakukata tamaa, nakumbuka nkwenye moja ya vyuo vikuu pale Dodoma kwenye moja Gobless Lema ktk tukio moja alituongoza kufanya maandamano kabla ya kukutana na kipigo cha Police. Hatukuwa tumejali uwezekano wa kupigwa na Police kwa sababu tuliona katiba mpya kama jambo lenye maslahi kwa taifa, hatukuangalia nani aliyekuwa anatuongoza bali tuliangalia nia thabiti ya huyo!

Baada ya pressure kuzidi hatimaye Jakaya Kikwete alimgeuka Waziri wake na wanaCCM wengine wengi, akatangaza mchakato wa katiba mpya. Nimeanza na utangulizi huu mrefu kuonyesha kuwa jambo hili halikuja kirahisi na hatuwezi kufika hapo tunapotamani kirahisi.

Tofauti na mwanzoni ambapo tatzo lilikuwa kwa wahafidhina wa CCM safari hii limeongezeka tatzo lingine, ni kwamba hatuna mtu wa kusimama na kutuongoza katika mapambano hayo ambayo kama nilivosema so mepesi! Kwanini!?

Wote tunajua jinsi uchaguzi wa mwaka Jana ulivoacha vurugu katk vyama vyetu, kuanzia CCM hadi CUF, vurugu hizo zimesababisha watu kujikuta wakiwa ktk maeneo wasiyositahili huku wengine wakiondoka ktk maeneo wanayostahili.

Uchaguzi umetupa raisi ambaye ameweka wazi kuwa kwake katiba mpya si kipaumbele, ikumbikwe Rais aliyepita aliunga mkono hoja ya katiba mpya kabla ya kutugeuka dakika za mwisho baada ya kuwekwa kikaangoni!!
Wote tunajua nguvu za rais chini ya katiba ya sasa hvo kulazimisha kupata jambo asilolitaka linahitaji kuwa na viongozi kwenye nia thabiti, je tunao hao?

Lkn pia uchaguzi huo umewaingiza baadhi ya watu waliokuwa wakitegemewa ktk upatikanji wa katiba mpya ndani ya serikali, serikali ambayo katiba mpya si kipaumbele, hawa hawawezi tena kuthubutu kuwa mstari wa mbele!!!

Lkn upande wa pili nako hali si shwari, CDM ile, CUF ile sasa hazionekani, hawa simu hizi wanaweza kupigwa mkwara na Paul Makonda na wakanywea.

Kibaya zaidi watu walioikata hadharani katiba ya Warioba, watu ambao ushahidi wa wazi unaonyesha dhahili walishiliki kikamilifu kuhakisha katiba ya Warioba inakwama,sasa ndo vinara wa upande huu, bahati mbaya yangu tuwakaribishe hawajawahi kutuomba msamaha juu ya Yale waliyotenda wakiwa Kyle, hawajawahi kutoka hadharani na kusema sasa wana msimamo gani juu ya katiba mpya!

Hawa wanaonekana wakitumia nguvu nyingi sana kuelekea uchaguzi wa 2020, hawataki kuangalia mstakabali wa nchi kwa mda mrefu kama ss tunavyoangalia, hawa wakija na kelele za katiba mpya hawezi tena kuaminiwa, rekodi zao zipo wazi na hata tukiacha rekodi zao matendo yao yanatuonesha wanangalia 2020 hivyo hata wakipiga kelele za katiba mpya wengi tutashindwa kuwaamini, kwa sababu ukweli ni kuwa watakuwa wanazitumia kama mwavuli tu wa 2020, HAWA HATUWEZI KUWAAMINI HATA KIDOGO na hawana legitimacy tena ya kubeba jukumu hilo, uchu wa kuingia magogoni 2015 umewaondolea uhalali huo!

Kule CUF ndo usiseme wanashinda mitandaoni wakiitana majina ya ajabu ajabu kweli.
Zitto anaoeneka anaweza kulibeba jukumu hilo, tatzo hawa wengine watakubali ajipatie ujiko huo?, chama chake kina watu na rasilimali za kulisimamia hilo!?

Hebu ona NGOS nazo ziko hoi, hawa nao kama wanachungulia kwanza wenzao waanze wao ndo wanajifanya kupiga kelele, labda TLHRC wangeweza kutusimamia, lkn Yule mama namuona mwepesi mno, akipigwa mkwara mdogo ananywea, lkn sioni kama kuna Manpower yanye weledi na moyo wa uzalendo pale inayoweza kusimama naye hata kama angethubutu!

Deus Kibamba wa jukwa la Katiba anoaonekana mtu strong, lkn NGO yake sioni kama ina nguvu za kutosha( fund na manpower), mmmmhhhh!!!

Nikasema bac vyombo vya habari, thubutuu!!
Huku nako mambo si mambo, baada ya uchaguzi huku wameamua kuchagua pande, ss wametuacha, sasa wanapiga ngoma za wanaowalipa!

Kinachobaki ni sisi Watanzania kubaki na matamanio yetu, huku tukiomba kudura za Allah atokee shujaa wa kujitoa mhanga na kutuongoza ktk kutimiza haja yetu hii mhimu, "KUPATA KATIBA MPYA"
 
Ni ukweli usiopingika kuwa Watanzania tunayo hamu kubwa ya kupata katiba mpya. Lkn ni ukweli usiopingika kwamba CCM kama chama na si watu hawako tayari kuliona tamanio hilo likitimia!!

Nimeamua kuna na hoja hii baada ya vilio vya hivi karibuni vya wana wa UKAWA kufuatia kipigo kikali kutoka kwa wana wa CCM japo bado siamini kama katiba ya sasa ndio iliyosababisha kipigo hicho. Lkn mwisho wa siku Watanzania tunahitaji katiba mpya ambayo itakuwa imerekebisha mambo mengi yakiwemo ya uchaguzi n.k.!

Lkn tatizo ninalo liona ni kuwa pamoja na kuwepo matamanio hayo, bado wana hawa Watanzania wanakosa mtu kwenye nia ya dhati ya kuwaongoza kuhakikisha tamanio hili linatimia! Kwanini?

Mwaka 2010 Mara baada ya uchaguzi CDM walibeba jukumu hhili, mapingamizi yalianza mapema kabisa akianza waziri wa sheria wa wkt huo mama Cellina Kombani( mungu amrehemu) yeye alisema hatuhitaji katiba mpya Bali iliyokuwepo ilikidhi mahitaji na kama ingetokea bac ingepigwa vilaka tu!

Cellina kombani alikuwa waziri wa sheria tamko lake lilimanisha tamko la serikali, yaani huo ndo ulikuwa msimamo wa JK na serikali yake. Lkn CDM wakiungwa mkono na makundi mabalimbali ya kijamii hawakukata tamaa, nakumbuka nkwenye moja ya vyuo vikuu pale Dodoma kwenye moja Gobless Lema ktk tukio moja alituongoza kufanya maandamano kabla ya kukutana na kipigo cha Police. Hatukuwa tumejali uwezekano wa kupigwa na Police kwa sababu tuliona katiba mpya kama jambo lenye maslahi kwa taifa, hatukuangalia nani aliyekuwa anatuongoza bali tuliangalia nia thabiti ya huyo!

Baada ya pressure kuzidi hatimaye Jakaya Kikwete alimgeuka Waziri wake na wanaCCM wengine wengi, akatangaza mchakato wa katiba mpya. Nimeanza na utangulizi huu mrefu kuonyesha kuwa jambo hili halikuja kirahisi na hatuwezi kufika hapo tunapotamani kirahisi.

Tofauti na mwanzoni ambapo tatzo lilikuwa kwa wahafidhina wa CCM safari hii limeongezeka tatzo lingine, ni kwamba hatuna mtu wa kusimama na kutuongoza katika mapambano hayo ambayo kama nilivosema so mepesi! Kwanini!?

Wote tunajua jinsi uchaguzi wa mwaka Jana ulivoacha vurugu katk vyama vyetu, kuanzia CCM hadi CUF, vurugu hizo zimesababisha watu kujikuta wakiwa ktk maeneo wasiyositahili huku wengine wakiondoka ktk maeneo wanayostahili.

Uchaguzi umetupa raisi ambaye ameweka wazi kuwa kwake katiba mpya si kipaumbele, ikumbikwe Rais aliyepita aliunga mkono hoja ya katiba mpya kabla ya kutugeuka dakika za mwisho baada ya kuwekwa kikaangoni!!
Wote tunajua nguvu za rais chini ya katiba ya sasa hvo kulazimisha kupata jambo asilolitaka linahitaji kuwa na viongozi kwenye nia thabiti, je tunao hao?

Lkn pia uchaguzi huo umewaingiza baadhi ya watu waliokuwa wakitegemewa ktk upatikanji wa katiba mpya ndani ya serikali, serikali ambayo katiba mpya si kipaumbele, hawa hawawezi tena kuthubutu kuwa mstari wa mbele!!!

Lkn upande wa pili nako hali si shwari, CDM ile, CUF ile sasa hazionekani, hawa simu hizi wanaweza kupigwa mkwara na Paul Makonda na wakanywea.

Kibaya zaidi watu walioikata hadharani katiba ya Warioba, watu ambao ushahidi wa wazi unaonyesha dhahili walishiliki kikamilifu kuhakisha katiba ya Warioba inakwama,sasa ndo vinara wa upande huu, bahati mbaya yangu tuwakaribishe hawajawahi kutuomba msamaha juu ya Yale waliyotenda wakiwa Kyle, hawajawahi kutoka hadharani na kusema sasa wana msimamo gani juu ya katiba mpya!

Hawa wanaonekana wakitumia nguvu nyingi sana kuelekea uchaguzi wa 2020, hawataki kuangalia mstakabali wa nchi kwa mda mrefu kama ss tunavyoangalia, hawa wakija na kelele za katiba mpya hawezi tena kuaminiwa, rekodi zao zipo wazi na hata tukiacha rekodi zao matendo yao yanatuonesha wanangalia 2020 hivyo hata wakipiga kelele za katiba mpya wengi tutashindwa kuwaamini, kwa sababu ukweli ni kuwa watakuwa wanazitumia kama mwavuli tu wa 2020, HAWA HATUWEZI KUWAAMINI HATA KIDOGO na hawana legitimacy tena ya kubeba jukumu hilo, uchu wa kuingia magogoni 2015 umewaondolea uhalali huo!

Kule CUF ndo usiseme wanashinda mitandaoni wakiitana majina ya ajabu ajabu kweli.
Zitto anaoeneka anaweza kulibeba jukumu hilo, tatzo hawa wengine watakubali ajipatie ujiko huo?, chama chake kina watu na rasilimali za kulisimamia hilo!?

Hebu ona NGOS nazo ziko hoi, hawa nao kama wanachungulia kwanza wenzao waanze wao ndo wanajifanya kupiga kelele, labda TLHRC wangeweza kutusimamia, lkn Yule mama namuona mwepesi mno, akipigwa mkwara mdogo ananywea, lkn sioni kama kuna Manpower yanye weledi na moyo wa uzalendo pale inayoweza kusimama naye hata kama angethubutu!

Deus Kibamba wa jukwa la Katiba anoaonekana mtu strong, lkn NGO yake sioni kama ina nguvu za kutosha( fund na manpower), mmmmhhhh!!!

Nikasema bac vyombo vya habari, thubutuu!!
Huku nako mambo si mambo, baada ya uchaguzi huku wameamua kuchagua pande, ss wametuacha, sasa wanapiga ngoma za wanaowalipa!

Kinachobaki ni sisi Watanzania kubaki na matamanio yetu, huku tukiomba kudura za Allah atokee shujaa wa kujitoa mhanga na kutuongoza ktk kutimiza haja yetu hii mhimu, "KUPATA KATIBA MPYA"
Usiulize Nani wa kuidai katiba mpya Bali mm na wewe ndo wenye kuidai hiyo katiba.tuunde movement ya kuidai katiba mpya pamoja na tume huru ya uchaguzi. Namba zangu Ni 0753111826 nawe weka zako tutafutane mie Niko Arusha.
 
Kwa sasa vyama vya upinzani havitakiwi kuingia kwenye uchaguzi wa aina yoyote ile halafu wanaposhindwa waje kulia lia..
Katiba mpya tu ndio iwe agenda kwa sasa.
 
Usiulize Nani wa kuidai katiba mpya Bali mm na wewe ndo wenye kuidai hiyo katiba.tuunde movement ya kuidai katiba mpya pamoja na tume huru ya uchaguzi. Namba zangu Ni 0753111826 nawe weka zako tutafutane mie Niko Arusha.
Ni kweli mkuu mm na ww ndo wahusika wakuu, lkn mambo makubwa na magumu kama haya yanahitaji kiongoz, kiongoz mwaminifu ili aweze kutuongoza ss,Nazi yetu ni kumuunga mkono, shida hiyo MTU huyo kwa sasa simuoni!!
 
Ni ukweli usiopingika kuwa Watanzania tunayo hamu kubwa ya kupata katiba mpya. Lkn ni ukweli usiopingika kwamba CCM kama chama na si watu hawako tayari kuliona tamanio hilo likitimia!!

Nimeamua kuna na hoja hii baada ya vilio vya hivi karibuni vya wana wa UKAWA kufuatia kipigo kikali kutoka kwa wana wa CCM japo bado siamini kama katiba ya sasa ndio iliyosababisha kipigo hicho. Lkn mwisho wa siku Watanzania tunahitaji katiba mpya ambayo itakuwa imerekebisha mambo mengi yakiwemo ya uchaguzi n.k.!

Lkn tatizo ninalo liona ni kuwa pamoja na kuwepo matamanio hayo, bado wana hawa Watanzania wanakosa mtu kwenye nia ya dhati ya kuwaongoza kuhakikisha tamanio hili linatimia! Kwanini?

Mwaka 2010 Mara baada ya uchaguzi CDM walibeba jukumu hhili, mapingamizi yalianza mapema kabisa akianza waziri wa sheria wa wkt huo mama Cellina Kombani( mungu amrehemu) yeye alisema hatuhitaji katiba mpya Bali iliyokuwepo ilikidhi mahitaji na kama ingetokea bac ingepigwa vilaka tu!

Cellina kombani alikuwa waziri wa sheria tamko lake lilimanisha tamko la serikali, yaani huo ndo ulikuwa msimamo wa JK na serikali yake. Lkn CDM wakiungwa mkono na makundi mabalimbali ya kijamii hawakukata tamaa, nakumbuka nkwenye moja ya vyuo vikuu pale Dodoma kwenye moja Gobless Lema ktk tukio moja alituongoza kufanya maandamano kabla ya kukutana na kipigo cha Police. Hatukuwa tumejali uwezekano wa kupigwa na Police kwa sababu tuliona katiba mpya kama jambo lenye maslahi kwa taifa, hatukuangalia nani aliyekuwa anatuongoza bali tuliangalia nia thabiti ya huyo!

Baada ya pressure kuzidi hatimaye Jakaya Kikwete alimgeuka Waziri wake na wanaCCM wengine wengi, akatangaza mchakato wa katiba mpya. Nimeanza na utangulizi huu mrefu kuonyesha kuwa jambo hili halikuja kirahisi na hatuwezi kufika hapo tunapotamani kirahisi.

Tofauti na mwanzoni ambapo tatzo lilikuwa kwa wahafidhina wa CCM safari hii limeongezeka tatzo lingine, ni kwamba hatuna mtu wa kusimama na kutuongoza katika mapambano hayo ambayo kama nilivosema so mepesi! Kwanini!?

Wote tunajua jinsi uchaguzi wa mwaka Jana ulivoacha vurugu katk vyama vyetu, kuanzia CCM hadi CUF, vurugu hizo zimesababisha watu kujikuta wakiwa ktk maeneo wasiyositahili huku wengine wakiondoka ktk maeneo wanayostahili.

Uchaguzi umetupa raisi ambaye ameweka wazi kuwa kwake katiba mpya si kipaumbele, ikumbikwe Rais aliyepita aliunga mkono hoja ya katiba mpya kabla ya kutugeuka dakika za mwisho baada ya kuwekwa kikaangoni!!
Wote tunajua nguvu za rais chini ya katiba ya sasa hvo kulazimisha kupata jambo asilolitaka linahitaji kuwa na viongozi kwenye nia thabiti, je tunao hao?

Lkn pia uchaguzi huo umewaingiza baadhi ya watu waliokuwa wakitegemewa ktk upatikanji wa katiba mpya ndani ya serikali, serikali ambayo katiba mpya si kipaumbele, hawa hawawezi tena kuthubutu kuwa mstari wa mbele!!!

Lkn upande wa pili nako hali si shwari, CDM ile, CUF ile sasa hazionekani, hawa simu hizi wanaweza kupigwa mkwara na Paul Makonda na wakanywea.

Kibaya zaidi watu walioikata hadharani katiba ya Warioba, watu ambao ushahidi wa wazi unaonyesha dhahili walishiliki kikamilifu kuhakisha katiba ya Warioba inakwama,sasa ndo vinara wa upande huu, bahati mbaya yangu tuwakaribishe hawajawahi kutuomba msamaha juu ya Yale waliyotenda wakiwa Kyle, hawajawahi kutoka hadharani na kusema sasa wana msimamo gani juu ya katiba mpya!

Hawa wanaonekana wakitumia nguvu nyingi sana kuelekea uchaguzi wa 2020, hawataki kuangalia mstakabali wa nchi kwa mda mrefu kama ss tunavyoangalia, hawa wakija na kelele za katiba mpya hawezi tena kuaminiwa, rekodi zao zipo wazi na hata tukiacha rekodi zao matendo yao yanatuonesha wanangalia 2020 hivyo hata wakipiga kelele za katiba mpya wengi tutashindwa kuwaamini, kwa sababu ukweli ni kuwa watakuwa wanazitumia kama mwavuli tu wa 2020, HAWA HATUWEZI KUWAAMINI HATA KIDOGO na hawana legitimacy tena ya kubeba jukumu hilo, uchu wa kuingia magogoni 2015 umewaondolea uhalali huo!

Kule CUF ndo usiseme wanashinda mitandaoni wakiitana majina ya ajabu ajabu kweli.
Zitto anaoeneka anaweza kulibeba jukumu hilo, tatzo hawa wengine watakubali ajipatie ujiko huo?, chama chake kina watu na rasilimali za kulisimamia hilo!?

Hebu ona NGOS nazo ziko hoi, hawa nao kama wanachungulia kwanza wenzao waanze wao ndo wanajifanya kupiga kelele, labda TLHRC wangeweza kutusimamia, lkn Yule mama namuona mwepesi mno, akipigwa mkwara mdogo ananywea, lkn sioni kama kuna Manpower yanye weledi na moyo wa uzalendo pale inayoweza kusimama naye hata kama angethubutu!

Deus Kibamba wa jukwa la Katiba anoaonekana mtu strong, lkn NGO yake sioni kama ina nguvu za kutosha( fund na manpower), mmmmhhhh!!!

Nikasema bac vyombo vya habari, thubutuu!!
Huku nako mambo si mambo, baada ya uchaguzi huku wameamua kuchagua pande, ss wametuacha, sasa wanapiga ngoma za wanaowalipa!

Kinachobaki ni sisi Watanzania kubaki na matamanio yetu, huku tukiomba kudura za Allah atokee shujaa wa kujitoa mhanga na kutuongoza ktk kutimiza haja yetu hii mhimu, "KUPATA KATIBA MPYA"

Well said mku
 
Upinzani unapaswa kuondoa tofauti zao na kuweka maslahi ya taifa mbele. Tudai katiba mpya kwanza yenye tume huru ya uchaguzi. Hili ni la dharura. Hili litawapa uhuru wanaoshikiliwa kinyume cha utaratibu, litawaweka polisi sehemu wanapostahili, litatofautisha masuala ya sheria tokea katika matamko ya wanasiasa, mahakama zitakuwa huru, tutahoji kwa mantiki na kusikilizwa kuhusiana na wanaopotea, nk nk.

Angalia Kenya:

ODM MPs rebuke Uhuru for belittling Raila

Nchi hii si ya mtu mmoja wala si ya kikundi cha watu. Mkuu aliapa kulinda katiba ya nchi. Tutafautishe katiba ya nchi na katiba za chama.
 
Kwa sasa vyama vya upinzani havitakiwi kuingia kwenye uchaguzi wa aina yoyote ile halafu wanaposhindwa waje kulia lia..
Katiba mpya tu ndio iwe agenda kwa sasa.
Mkuu huoni jinsi wanavyoelekeza nguvu kubwa kwenye uchaguz wa 2020, badala ya katiba mpya ambayo tukiipata inaweza kuwa mwarobaini wa matatizo mengi yakiwemo ya uchaguzi, swali langu ni je hao unaowasema wasusie uchaguzi hadi katiba ipatikane bado wanaletimacy ya kusimama mbele ya Watanzania na kudai katiba mpya!!
 
Upinzani unapaswa kuondoa tofauti zao na kuweka maslahi ya taifa mbele. Tudai katiba mpya kwanza yenye tume huru ya uchaguzi. Hili ni la dharura. Hili litawapa uhuru wanaoshikiliwa kinyume cha utaratibu, litawaweka polisi sehemu wanapostahili, litatofautisha masuala ya sheria tokea katika matamko ya wanasiasa, mahakama zitakuwa huru, tutahoji kwa mantiki na kusikilizwa kuhusiana na wanaopotea, nk nk.

Angalia Kenya:

ODM MPs rebuke Uhuru for belittling Raila

Nchi hii si ya mtu mmoja wala si ya kikundi cha watu. Mkuu aliapa kulinda katiba ya nchi. Tutafautishe katiba ya nchi na katiba za chama.
Mkuu unadhani bado wana legitimacy ya kutuongoza Watanzania ktk hilo!?
Unadhani wanayo nia thabiti ya kudai katiba mpya au wanaweza tu kuitumia kama political platform kuelekea 2020!?
 
Mkuu unadhani bado wana legitimacy ya kutuongoza Watanzania ktk hilo!?
Unadhani wanayo nia thabiti ya kudai katiba mpya au wanaweza tu kuitumia kama political platform kuelekea 2020!?

Mkuu uko na hoja ila kutokana na ilivyo muhimu kupata katiba thabiti ya wananchi na tume huru ya uchaguzi hatuna namna. Hawa pekee ndiyo tulio nao sasa kwani CCM wao wamekana wazi wazi kuwa katiba si kipa umbele chao ya kuwa wako kwenye kunyoosha nchi. Hili ni kipaumbele na nchi inanyooshwa kwa katiba tena katiba bora kabisa.

Ilikuwa heri kuachana na agenda ya 2020 tukadai katiba kwa nguvu zote. Bila hiyo chaguzi zote ni kupoteza muda.

Ilikuwa heri kuacha marumbano yasiyo na tija tuwekeze katika hoja hii yenye mashiko na tija kwa taifa hili kwa miaka lukuki mbele. Katiba mpya, katiba ya wananchi itadhibiti Udikteta uchwara, wizi wa kura, matamko yasiyo na tija, kuwekana ndani holela, na kero zote tunazozishuhudia.

Tuachane na agenda ya 2020 tutafute katiba mpya katiba ya wananchi itakayosimika tume huru ya uchaguzi. Kuwekwa ndani kwa hili ni sawa lakini haya mengine ya kuitana mashoga -- yanatia ukakasi.
 
Wanabodi,

Heshima mbele, Wakati Taifa letu likiwa katika sintofahamu kuhusiana na Mchakato wa Katiba Mpya ambao ulisimama,Ni dhahiri kuwa Tunahitaji Mchakato ule kurejeshwa tukianzia pale ambapo Tulikwamia.

Kimsingi tukijikita katika uhalisia na mahitaji ya Taifa,Tunapaswa kuwa na Katiba ambayo itakuwa muarobaini katika mfumo mzima, unaozalisha ukiukuaji wa maadili ya Uongozi,Nakupelekea uwapo wa mwenendo unaozalisha upotefu wa rasilimali za Taifa.

Katiba Mpya ni zaidi ya Itkadi zetu za kisiasa,Tunapaswa kutanguliza utaifa mbele,Sioni Tanzania bila ufisadi pasipo Katiba Mpya inayoakisi kwa upana mahitaji na Changamoto mbalimbali za Kiulimwengu.

Kimsingi yanayojiri sasa katika awamu hii ambayo ni utashi wa mtu yanazaa mawaa na msingi usio endelevu kwa maslahi ya Taifa.Watanzania Tushikamane Tanzania ni yetu sote 2020 bila katiba mpya ni anguko lingine la la kimaadili na midingi ya utawala bora.
 
Wakulifanya hilo wapo wengi ila tatizo wanapenda kuandaliwa badala ya kutafuta njia ya kuipata kwani watu wao ambao ndo mtaji wao. Na muda ndo huo unaondoka mwisho lawama wakati ni sasa tukumbuke kwenye Vitisho kuna majibu mazuri
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom