Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
- Thread starter
- #121
View attachment 2050551
Wanabodi,
[/LIST]
My Take.
Wanabodi, mnalionaje hili?. DPP afute kesi kwa Nolle, Mbowe aachiwe bila masharti yoyote, Asamehewa tuu bila kuomba msamaha, aachiwe kwa dhamana kesi iendelee, au aendelee kukomaa kama Mandela, no retreat no surrender, akamae nao mpaka kieleweke?
- Kunamsemo wa kizungu, usemao, "you can't eat your cake and have it", you either eat your cake na iishe, its gone, au usiile, uingalie tuu iendelee kuwepo, ila hapa natoa ushauri, unaweza kuila keki yako na ikaendelea kuwepo kwa kuimega kidogo kido na sio kuibugia. Maadam sheria ni zetu na tumezitunga wenyewe, ili kuziridhisha pande zote, tunaweza kuimega kidogo kidogo keki yetu na kuila huku ikiendelea kuwepo.
- Japo lengo la watu kuwekwa mahabusu ni ili kuwazuia wasitoroke na kuna baadhi ya makosa hayana dhamana, ili mtuhumiwa asitutoroke, tuambiane ukweli, hivi Mbowe anaweza kweli kutoroka nchi na kukimbilia uhamishoni aende kuwa mkimbizi wa kisiasa kama wale waoga wawili?. Kama hata kwenye kesi za mauaji hakuna dhamana, lakini kesi ya Ditopile aliyekuwa anatetewa na wakili Nimrodi Mkono, Wakili Mkono, alijenga hoja maridhawa, Ditopile akaachiwa kwa dhamana hadi pale Mungu alipoamua kumalizana nae. Hivyo kama tuna nia njema, Mbowe awe huru, anaweza kuachiwa kwa dhamana hata bila dhamana hiyo kuombwa, akawa anakuja kuhudhuria kesi akitokea nyumbani kwake.
- Kumbe DPP kutenda haki kunawezekana! Hongera sana, kazi umeianza vizuri. Sasa haki sio tu inatendeka, inaonekana! Kazi Iendelee…View attachment 2050632
- Kwa kufanya hivi, tutakuwa tumejibu ombi la 'Askofu Makarios' wetu na wale wote wenye nia njema na mapenzi mema kwa Mbowe kuwa jela ni mbaya, hivyo atakuwa huru uraiani kuungana na familia yake, ndugu jamaa na marafiki, na hata kusafiri kwenda kuhiji Moshi kwenye ile hija maarufu ya Wachagga ya Mwezi Desemba, na hata akiamua kusafiri kidogo hadi Arusha, kupitia Kisongo, kumsalimu yule 'jamaa yetu'.
- Huku hii kesi ya Mbowe, ikiendelea kuna mawili,
1. Serikali inaweza kabisa kuwa imeona inakwenda kushindwa kwa aibu na fedheha, hivyo ili kuepuka aibu ya kushindwa kwa fedheha, hivyo DPP, anaweza kupeleka Nolle. Hili lilifanyika, litamfanya Mbowe kuonekana shujaa, na akiachiwa kwa Nolle, huo moto wake ni usipime!.
2. Mahakama inaweza kabisa ithibitishe Mbowe ni malaika, hivyo alikuwa anasingiziwa tuu, ugaidi, hapo serikali itafedheheka.
3. Ili kuzuia serikali isifedheheke, hata kama in reality Mbowe sio gaidi lakini ili kumuadabisha, then ni lazima atatiwa hatiani na sheria ichukue mkondo wake kwa kula mvua kadhaa, na hapa sasa ndipo mahali Mama Samia mwenye uwezo napo kwa kutoa msamaha kwa wafungwa. Mbowe ataachiwa shingo chini, hataweza kugombea kitu chochote.
Nawatakia Krismasi Njema.
Paskali.
Mkuu NewPage, asante sana kwa kuniuliza na kwa maoni yako, hili la hii kesi ya Ugaidi ya Mbowe, nimeisha liandikia makala, karibu pande hiziKwa kweli kaka yangu ninakuaminia sana kwa kufanya uchambuzi. Hata hivyo ukimya wako kuhusu kufanya uchambuzi na utabiri wa nini itakuwa athari kisiasa kuhusu uamuzi wowote utakaohusisha kesi ya Mbowe.
Kwa mfano kwa sasa tunasubiri iwapo Mahakama itaamua Mbowe na wenzake wana kesi ya kujibu na ikafikia hadi hatua ya utetezi athari zake zitakuwa ni zipi?
Hayo ni mawazo yangu - Je, ndugu yangu Paskali Mayala wewe unalichambuaje suala hili?
P