Nyakarungu
JF-Expert Member
- May 1, 2011
- 472
- 375
Wanabodi,
Nawaomba Sana na kuwasihi Watanzania wenzangu tuitunze na kuienzi tunu yetu ya taifa inayoakisi malezi na maadili yetu ya kitanzania ambayo Ni heshima na uungwana kwa binadamu wenzetu.
Hivi karibuni kuna magenge yanazuka mitandaoni yakimkosoa Rais wa JMT Mh. Samia Suluhu Hassan, kwa bahati mbaya sana wanamkosoa kwa kumsodoa kwa maneno yasiyo na sitaha kwa kiongozi wa nchi, tabia hii haifai kabisa na sio nidhamu tuliyofunzwa Watanzania.
Ikiwa twahitaji kumkosoa Rais Basi na tufanye hivyo kwa lugha yenye staha na heshima, na tukumbuke kuwa huyu Ni Rais wa nchi yetu, huzuni yake Ni yetu pia, heshima yake ni yetu na akidhalilika Ni taifa linadhalilika, ukimdhalilisha Rais wako Ni Nani unayemtegemea amheshimishe?
Tuvumilie na tufunike hisia zenye hasira ndani yetu Kisha tukosoe kwa staha.
Nawasihi sana, Uhuru wa kuongea na kuonyesha hisia zetu usigeuke kuwa Uhuru wa kutukana na kuonyesha hasira zetu.
Mwisho:
Tuna wajibu wa kumsikiliza Rais na kuamini kwamba hakuna mama anayeweza kuwapa watoto wake sumu, hisia za mama ni nzito sana kwa watoto.
Nawaomba Sana na kuwasihi Watanzania wenzangu tuitunze na kuienzi tunu yetu ya taifa inayoakisi malezi na maadili yetu ya kitanzania ambayo Ni heshima na uungwana kwa binadamu wenzetu.
Hivi karibuni kuna magenge yanazuka mitandaoni yakimkosoa Rais wa JMT Mh. Samia Suluhu Hassan, kwa bahati mbaya sana wanamkosoa kwa kumsodoa kwa maneno yasiyo na sitaha kwa kiongozi wa nchi, tabia hii haifai kabisa na sio nidhamu tuliyofunzwa Watanzania.
Ikiwa twahitaji kumkosoa Rais Basi na tufanye hivyo kwa lugha yenye staha na heshima, na tukumbuke kuwa huyu Ni Rais wa nchi yetu, huzuni yake Ni yetu pia, heshima yake ni yetu na akidhalilika Ni taifa linadhalilika, ukimdhalilisha Rais wako Ni Nani unayemtegemea amheshimishe?
Tuvumilie na tufunike hisia zenye hasira ndani yetu Kisha tukosoe kwa staha.
Nawasihi sana, Uhuru wa kuongea na kuonyesha hisia zetu usigeuke kuwa Uhuru wa kutukana na kuonyesha hasira zetu.
Mwisho:
Tuna wajibu wa kumsikiliza Rais na kuamini kwamba hakuna mama anayeweza kuwapa watoto wake sumu, hisia za mama ni nzito sana kwa watoto.