Watanzania tukubali kubadilika

Omuchimati

JF-Expert Member
Aug 23, 2014
427
202
Namshukuru Mungu kwanza kabisa kwa kunipa uhai na kuniwezesha kupumua hadi leo hii ni wengi nimeshawapoteza ndugu jamaa na marafiki, achilia mbali walioko mahospitalini na jela, hakika ni vyema kumshukuru MUNGU.
Sitaki kwenda nje ya mada hapo juu,watanzani wakati tunamtafuta Rais wa awamu ya tano tulihubiri mabadiliko, nilipita vijiweni huko kinondoni, sinza, Makumbusho kijitonyama, watu wote walikuwa wakihubiri mabadiliko,iliwabidi wanasiasa wacheze kulingana na ala ya wimbo huo nao wakaanza kuhubiri mabadiliko,lakini kumbe tulikuwa hatupo tayari kwa mabadiliko.

Baada ya Mhe John Joseph Pombe Magufuli kuikamata awamu ya tano amesafisha nyumba kwa kuwatimua watumishi walioshindwa kusimamia misingi ya maadili, kwani wengi wao walitumia vyeo vyao kwa manufaa yao wenyewe, achilia mbali watumishi wa umma, wafanyabiashara wabadhirifu na wahujumu wa uchumi, wembe umewagusa wanalia ,wanamlilia Magufuli wanasema anaendesha nchi kwa media, anakurupuka, hana huruma na wafanyabiashara na watumishi wa umma,Je ni mabadiliko gani enyi wana wa Tanzania mliyataka? Mlitaka nchi iendelee kunyonywa na watu wachache? Mlitaka pengo kati ya maskini na matajiri lizidi kuwa kubwa? Nchi isingekalika......amani ingetoweka kwani maskini wangeshindwa kuvumilia,anachokifanya JPM haya ndio mabadiliko ya kweli,mimi namuunga mkono, wewe je?
 
Namshukuru Mungu kwanza kabisa kwa kunipa uhai na kuniwezesha kupumua hadi leo hii ni wengi nimeshawapoteza ndugu jamaa na marafiki, achilia mbali walioko mahospitalini na jela, hakika ni vyema kumshukuru MUNGU.
Sitaki kwenda nje ya mada hapo juu,watanzani wakati tunamtafuta Rais wa awamu ya tano tulihubiri mabadiliko, nilipita vijiweni huko kinondoni, sinza, Makumbusho kijitonyama, watu wote walikuwa wakihubiri mabadiliko,iliwabidi wanasiasa wacheze kulingana na ala ya wimbo huo nao wakaanza kuhubiri mabadiliko,lakini kumbe tulikuwa hatupo tayari kwa mabadiliko.

Baada ya Mhe John Joseph Pombe Magufuli kuikamata awamu ya tano amesafisha nyumba kwa kuwatimua watumishi walioshindwa kusimamia misingi ya maadili, kwani wengi wao walitumia vyeo vyao kwa manufaa yao wenyewe, achilia mbali watumishi wa umma, wafanyabiashara wabadhirifu na wahujumu wa uchumi, wembe umewagusa wanalia ,wanamlilia Magufuli wanasema anaendesha nchi kwa media, anakurupuka, hana huruma na wafanyabiashara na watumishi wa umma,Je ni mabadiliko gani enyi wana wa Tanzania mliyataka? Mlitaka nchi iendelee kunyonywa na watu wachache? Mlitaka pengo kati ya maskini na matajiri lizidi kuwa kubwa? Nchi isingekalika......amani ingetoweka kwani maskini wangeshindwa kuvumilia,anachokifanya JPM haya ndio mabadiliko ya kweli,mimi namuunga mkono, wewe je?

Nakuunga mkono kwa hii mada yako, lakini inabidi nikuambie ukweli. Hata kama nchi ingeendelea kunyonwa na wachache bado utulivu ungeendelea kuwepo kwani utulivu unaletwa kwa kutumia jeshi la polisi hata kama hatukubaliani na mambo. Nchi hii ukijaribu kuangalia kwa jicho la tatu haina amani bali ina makondoo wengi na hapo ndipo utulivu unapopatikana na sio amani katika uhalisia wake. Sisi maskini wa nchi hii bado sio wavulimivu bali ni waoga na hatujui kudai haki zetu. Mifano nitakupa hapa chini
  1. Bei ya mafuta imeshuka kwenye soko la dunia tena kwa kiwango cha kutisha lakini hapa nchini ni kunyume chake. Hili nalifananisha pindi mafuta yakipanda bei kwenye soko la dunia kesho yake mamlaka husika utasikia wanapandisha bei haraka
  2. Bei ya umeme imeendelea kuwa juu hata baada ya bunge kutoa maazimio kwamba bei hii tunapigwa. Kinatokea kichekesho eti wanashusha bei kwa 1%. Toka lini ukasikia umeme umepanda bei kwa 1%?
  3. Pembejeo na bei ya mazao ya mkulima ndio imekuwa kifo na uduni wa maisha ya mkulima. Leo hii katika nchi inayojinasibu kwamba 80% ya wananchi wake ni wakulima lakini huko ndio kwenye umaskini wa kutupwa. Kwa maneno marahisi ukitaka kuwa maskini vizuri nchi hii nenda kalime. Huku kwenye kilimo usishangae mkulima kukopwa na serekali na akiilipwa analipwa nusu ili aendelee kulima tena. Madalali wamejaa kwenye mazao ya wakulima matokeo yake unakuta dalali ana maisha bora wakati mkulima anakufa kwa njaa.
Katika mazingira haya unaweza kujisifia mabadiliko ya kuona watu wanafukuzwa kazi wakati ufukazaji huo hauna matokeo ya moja kwa moja na maisha ya wananchi? Tunataka mabadiliko kwenye maisha yetu ya kila siku na sio mabadiliko ya kuona watu wanafukuzwa kazi. Ni kweli kufukuza watumishi wasiotekeleza wajibu wao ni jambo jema, lakini ukimfukuza mtumishi wa umma kazi ndio pembejeo inakuwa na bei nafuu? Umeme unakuwa na bei halali? Mafuta yanashuka bei kulingana na soko la dunia? Ama mwenzetu wewe mabadiliko yako unayazungumzia katika nyanja ipi?
 
Nakuunga mkono kwa hii mada yako, lakini inabidi nikuambie ukweli. Hata kama nchi ingeendelea kunyonwa na wachache bado utulivu ungeendelea kuwepo kwani utulivu unaletwa kwa kutumia jeshi la polisi hata kama hatukubaliani na mambo. Nchi hii ukijaribu kuangalia kwa jicho la tatu haina amani bali ina makondoo wengi na hapo ndipo utulivu unapopatikana na sio amani katika uhalisia wake. Sisi maskini wa nchi hii bado sio wavulimivu bali ni waoga na hatujui kudai haki zetu. Mifano nitakupa hapa chini
  1. Bei ya mafuta imeshuka kwenye soko la dunia tena kwa kiwango cha kutisha lakini hapa nchini ni kunyume chake. Hili nalifananisha pindi mafuta yakipanda bei kwenye soko la dunia kesho yake mamlaka husika utasikia wanapandisha bei haraka
  2. Bei ya umeme imeendelea kuwa juu hata baada ya bunge kutoa maazimio kwamba bei hii tunapigwa. Kinatokea kichekesho eti wanashusha bei kwa 1%. Toka lini ukasikia umeme umepanda bei kwa 1%?
  3. Pembejeo na bei ya mazao ya mkulima ndio imekuwa kifo na uduni wa maisha ya mkulima. Leo hii katika nchi inayojinasibu kwamba 80% ya wananchi wake ni wakulima lakini huko ndio kwenye umaskini wa kutupwa. Kwa maneno marahisi ukitaka kuwa maskini vizuri nchi hii nenda kalime. Huku kwenye kilimo usishangae mkulima kukopwa na serekali na akiilipwa analipwa nusu ili aendelee kulima tena. Madalali wamejaa kwenye mazao ya wakulima matokeo yake unakuta dalali ana maisha bora wakati mkulima anakufa kwa njaa.
Katika mazingira haya unaweza kujisifia mabadiliko ya kuona watu wanafukuzwa kazi wakati ufukazaji huo hauna matokeo ya moja kwa moja na maisha ya wananchi? Tunataka mabadiliko kwenye maisha yetu ya kila siku na sio mabadiliko ya kuona watu wanafukuzwa kazi. Ni kweli kufukuza watumishi wasiotekeleza wajibu wao ni jambo jema, lakini ukimfukuza mtumishi wa umma kazi ndio pembejeo inakuwa na bei nafuu? Umeme unakuwa na bei halali? Mafuta yanashuka bei kulingana na soko la dunia? Ama mwenzetu wewe mabadiliko yako unayazungumzia katika nyanja ipi?
Hakika umenena kweli tindo: kuna haja kabisa serikali kumulika masoko ya bidhaa, afya na elimu kwa darubini yenye uwiano ili kuweza kuleta tija kwa watu wenye kipato cha chini,wameanza vizuri kwa sukari,Afya na Elimu, tunaomba hayo mambo wayasimamie yapate kunyanyua maisha ya mtu wa chini au kumletea unafuu.

Lakini pia na sie watz tupaze sauti kwa mambo ya msingi.
 
Nakuunga mkono kwa hii mada yako, lakini inabidi nikuambie ukweli. Hata kama nchi ingeendelea kunyonwa na wachache bado utulivu ungeendelea kuwepo kwani utulivu unaletwa kwa kutumia jeshi la polisi hata kama hatukubaliani na mambo. Nchi hii ukijaribu kuangalia kwa jicho la tatu haina amani bali ina makondoo wengi na hapo ndipo utulivu unapopatikana na sio amani katika uhalisia wake. Sisi maskini wa nchi hii bado sio wavulimivu bali ni waoga na hatujui kudai haki zetu. Mifano nitakupa hapa chini
  1. Bei ya mafuta imeshuka kwenye soko la dunia tena kwa kiwango cha kutisha lakini hapa nchini ni kunyume chake. Hili nalifananisha pindi mafuta yakipanda bei kwenye soko la dunia kesho yake mamlaka husika utasikia wanapandisha bei haraka
  2. Bei ya umeme imeendelea kuwa juu hata baada ya bunge kutoa maazimio kwamba bei hii tunapigwa. Kinatokea kichekesho eti wanashusha bei kwa 1%. Toka lini ukasikia umeme umepanda bei kwa 1%?
  3. Pembejeo na bei ya mazao ya mkulima ndio imekuwa kifo na uduni wa maisha ya mkulima. Leo hii katika nchi inayojinasibu kwamba 80% ya wananchi wake ni wakulima lakini huko ndio kwenye umaskini wa kutupwa. Kwa maneno marahisi ukitaka kuwa maskini vizuri nchi hii nenda kalime. Huku kwenye kilimo usishangae mkulima kukopwa na serekali na akiilipwa analipwa nusu ili aendelee kulima tena. Madalali wamejaa kwenye mazao ya wakulima matokeo yake unakuta dalali ana maisha bora wakati mkulima anakufa kwa njaa.
Katika mazingira haya unaweza kujisifia mabadiliko ya kuona watu wanafukuzwa kazi wakati ufukazaji huo hauna matokeo ya moja kwa moja na maisha ya wananchi? Tunataka mabadiliko kwenye maisha yetu ya kila siku na sio mabadiliko ya kuona watu wanafukuzwa kazi. Ni kweli kufukuza watumishi wasiotekeleza wajibu wao ni jambo jema, lakini ukimfukuza mtumishi wa umma kazi ndio pembejeo inakuwa na bei nafuu? Umeme unakuwa na bei halali? Mafuta yanashuka bei kulingana na soko la dunia? Ama mwenzetu wewe mabadiliko yako unayazungumzia katika nyanja ipi?

Kila kitu kinaenda kwa hatua. Hata kama ingekua wewe hapo usingeweza kufanikisha zoazi la kuleta mbadiliko kwa wiki au mweziau mwaka mmoja. Inabidikwanza kusafishwe na serikali ionyeshe meno yake makali, then ikusanye kupato cha kutosha then ndio yanakuja masuala mengine ya umeme na pembejeo.
Mleta mada alichosema ni kweli, hali inabadilika taratibu, na kwa kasi hii kama tutashikana mikono nina uhakika baada 3 years tutaua mbali. Kuwanza tupiganie huduma ya Afya, Maji na elimu iboroshwe,. Bila elimu bila afya hatutafanya lolote
 
Namshukuru Mungu kwanza kabisa kwa kunipa uhai na kuniwezesha kupumua hadi leo hii ni wengi nimeshawapoteza ndugu jamaa na marafiki, achilia mbali walioko mahospitalini na jela, hakika ni vyema kumshukuru MUNGU.
Sitaki kwenda nje ya mada hapo juu,watanzani wakati tunamtafuta Rais wa awamu ya tano tulihubiri mabadiliko, nilipita vijiweni huko kinondoni, sinza, Makumbusho kijitonyama, watu wote walikuwa wakihubiri mabadiliko,iliwabidi wanasiasa wacheze kulingana na ala ya wimbo huo nao wakaanza kuhubiri mabadiliko,lakini kumbe tulikuwa hatupo tayari kwa mabadiliko.

Baada ya Mhe John Joseph Pombe Magufuli kuikamata awamu ya tano amesafisha nyumba kwa kuwatimua watumishi walioshindwa kusimamia misingi ya maadili, kwani wengi wao walitumia vyeo vyao kwa manufaa yao wenyewe, achilia mbali watumishi wa umma, wafanyabiashara wabadhirifu na wahujumu wa uchumi, wembe umewagusa wanalia ,wanamlilia Magufuli wanasema anaendesha nchi kwa media, anakurupuka, hana huruma na wafanyabiashara na watumishi wa umma,Je ni mabadiliko gani enyi wana wa Tanzania mliyataka? Mlitaka nchi iendelee kunyonywa na watu wachache? Mlitaka pengo kati ya maskini na matajiri lizidi kuwa kubwa? Nchi isingekalika......amani ingetoweka kwani maskini wangeshindwa kuvumilia,anachokifanya JPM haya ndio mabadiliko ya kweli,mimi namuunga mkono, wewe je?
Safi sana ila nimetambua binadamu wana kazi. lakini nimetambua kuwa wasiokubaliana ni wachache mnooooooo. Ila nimebaini kuwa hao wachache ndio wale wenye pesa , lakini nina hakika kuwa wana pesa si za jasho lao bali za wizi kwa kutumia ujanja ujanja. Ila kingine nimebaini kuwa hao wachache asilimia kubwa wanaexposure hivyo wana uwezo mkubwa wa kudanganya watu. Wana uwezo hata wa kuajiri watu kukaa mitandaoni na kupinga kila kitu kizuri ili mradi tu mkono uende kinywani. Ni watu hatari tuungaane kuwapinga. Naomba nieleweke kukosoa haizuiliwi ila kukosoa hata jema kabisa kwa asilimia kubwa ya wananchi. Haikubaliki. Juzi nilisikiliza kipindi cha ITV nilisikia Mzee mmoja akisema Mh. Magufuli aongezewe muda wa miaka 300! Nadhani alimaanisha atawale milele. Hivyo go Mh. Magufuli go. Wengi tunakuunga mkono!
 
Safi sana ila nimetambua binadamu wana kazi. lakini nimetambua kuwa wasiokubaliana ni wachache mnooooooo. Ila nimebaini kuwa hao wachache ndio wale wenye pesa , lakini nina hakika kuwa wana pesa si za jasho lao bali za wizi kwa kutumia ujanja ujanja. Ila kingine nimebaini kuwa hao wachache asilimia kubwa wanaexposure hivyo wana uwezo mkubwa wa kudanganya watu. Wana uwezo hata wa kuajiri watu kukaa mitandaoni na kupinga kila kitu kizuri ili mradi tu mkono uende kinywani. Ni watu hatari tuungaane kuwapinga. Naomba nieleweke kukosoa haizuiliwi ila kukosoa hata jema kabisa kwa asilimia kubwa ya wananchi. Haikubaliki. Juzi nilisikiliza kipindi cha ITV nilisikia Mzee mmoja akisema Mh. Magufuli aongezewe muda wa miaka 300! Nadhani alimaanisha atawale milele. Hivyo go Mh. Magufuli go. Wengi tunakuunga mkono!
Umeeleweka kwa uzuri mwana tukiungana wote kumpa moyo Mhe. Rais atapata nguvu hata za kuwatafuna mapapa.
 
Safi sana ila nimetambua binadamu wana kazi. lakini nimetambua kuwa wasiokubaliana ni wachache mnooooooo. Ila nimebaini kuwa hao wachache ndio wale wenye pesa , lakini nina hakika kuwa wana pesa si za jasho lao bali za wizi kwa kutumia ujanja ujanja. Ila kingine nimebaini kuwa hao wachache asilimia kubwa wanaexposure hivyo wana uwezo mkubwa wa kudanganya watu. Wana uwezo hata wa kuajiri watu kukaa mitandaoni na kupinga kila kitu kizuri ili mradi tu mkono uende kinywani. Ni watu hatari tuungaane kuwapinga. Naomba nieleweke kukosoa haizuiliwi ila kukosoa hata jema kabisa kwa asilimia kubwa ya wananchi. Haikubaliki. Juzi nilisikiliza kipindi cha ITV nilisikia Mzee mmoja akisema Mh. Magufuli aongezewe muda wa miaka 300! Nadhani alimaanisha atawale milele. Hivyo go Mh. Magufuli go. Wengi tunakuunga mkono!

Tanzania na Afrina nzima kinachotuangusha si utawala bora, ni uwizi, tamaa, na uongo. Nilikua sipendi CCM na wala sisemi kua naipenda kwa sasa lakini nimeipenda kazi na utaratibu wa mh. Raisi. Kuna mapungufu ambayo yanahitaji kurekebishwa kwani sisi ni binadamu.
Kitu kimmoja tujiulize je ilashawahi kutokea utawala kama huu hapa tanzania na afrika nzima? Utawala wa kupambana na rushwa, na isitoshe tunawekewa kiasi cha mapato mara kwa mara na maelezo ya hizo fedha jinsi zitakavyo tumika. Je iliwahi kutokea hapo awali?
Kama usemavyo wanao pinga utawala huu ni hao wenye majipu na hao wanao shabikia mradi ni CCM basi inakua ni kupinga tu.
Inabidi watanzania tujitokeze kwa wingi kupambana ni rushwa na ufisadi. Pammoja na hao madaktari na manesi wanao sababisha vifo kwa ajili ya uzembe. Hata daktari wa Michael Jackson ametiwa jela kwa ajili ya uzembe.
Tujitahidi kutundika majina na sehemu za kazi za hao wanao kula rushwa au wanao zembea kwenye kazi. Mwanzo mgumu lakini tutafika.
Mishahara na mzingira ya kazi ni mbaya lakini tukijikaza watoto wetu na wajukuu watakuja kufaidi.
 
Back
Top Bottom