Ng'wamapalala
JF-Expert Member
- Jun 9, 2011
- 6,808
- 6,500
Tanzania hatutapata tena "GOLDEN CHANCE" kama hii iliyotokea ya kupata katiba mpya na kuachana na hili "DUDU" linaloitwa MUUNGANO.
Kudai muungano usiwepo kwenye katiba ijayo 2014 kwa sasa siyo kosa. Lingehesabika ni kosa kisheria kama tungekuwa tunaweka viraka tena katika katiba hii mbovu ya mwaka 1977, kama ilivyo katika ibara ya 1 na 2(i).
1. Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.
2.-(1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo.
Sijasikia hata chama kimoja cha siasa, Asasi za kisiasa na Wanasiasa mmoja mmoja wakija na hoja ya REFERENDUM ili kujisimika kwa wapiga kura kwa vile kwa sasa kuna OMBWE la hoja ya msingi kuhusu muungano.
Kama kitatokea chama kwenye uchaguzi mkuu ujao 2015 kikaja na hoja yenye ABSOLUTE PROMISE ya referendum sina pasi shaka kitapata kura maelfu kwa mamilioni kwa wananchi wa pande zote za muungano.
Huhitaji kufanya research kujua wananchi wa pande zote mbili za muungano wamechoka na hili 'ZIGO' la muungano ambalo liko UNBALANCED kwa pande zote. Kila pande zinalalamika lakini kwa sababu ambazo haziko wazi na hazieleweki huku wanasiasa wetu wakiwa wameziba midomo na masikio.
Tarehe 30 Aprili, 1992, Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais wa wakati ule, John Samuel Malecela alibainisha katika bunge la Muungano matatizo ya muungano ambayo alisema mwarobaini wake ni UTEKELEZI.
John Samuel Malecela alisema, ninanukuu,
Miaka 49 kwa sasa, matatizo siyo kwamba bado ni yale yale bali pia yameongezeka. Repoti zaidi ya 39 kuhusiana na muungano zimeandikwa na viraka zaidi ya 10 vimewekwa bila kupata mwarobaini wa matatizo achilia mbali utekelezaji. Kwa jinsi hali inavyoonekana, things will only get worse before getting more worse. Ikumbukwe kuwa mfumo wa muungano wa Ireland ya Kaskazini uliotumika kama BENCHMARK kuandika Hati ya Muungano wetu lakini imegundulika mfumo huu una matatizo ambayo hata nchi za Ireland Kaskazini mpaka ninaandika hii mada bado zina matatizo makubwa na Mwingereza kwa maana kuwa, hii hati ya muungano ina matatizo ya msingi ambayo hayawezi kumalizwa na vikao vya bunge na repoti mbali mbali, bali yatamalizwa na REFERENDUM kama UK walivyonyosha mikono juu na kuamua baada ya uchaguzi mkuu ujao kuwepo na referendum kuhusu uhuru wa Waskotishi na uanachama wa muungano wa nchi za ulaya.
Wakati wa vuguvugu la G55, Rais Mwinyi aliwahi kutamka kuwa mwerekeo wa CCM na sera zake ni kutoka serikali mbili kuelekea serikali MOJA. Kwa sasa jinsi matatizo yalivyokuwa makubwa, hata hiyo sera ya CCM ya serikali moja haiwezekani tena.
Kwa sasa tumefikia sehemu ambayo hata Jaji Mkuu na Waziri Mkuu hawana uhakika kama Zanzibar ni nchi au Mkoa. Matatizo ni makubwa yamefikia kiwango cha nchi kutokuaminiana kutokana na matatizo ya hati ya muungano, maslahi kiuchumi na tofauti la ongezeko la watu kati ya nchi mbili ukilinganisha na eneo la nchi. We can't sit in here and keep on fooling ourself. It'll NEVER work.
Swali linalokosa majibu ni DOGO lakini limebeba mabadiliko ya kitaifa kwa manufaa ya wananchi kitaifa kwa leo na kwa kizazi kijacho katika nyanja zote (kisiasa, kiuchumi na kijamii).
Kwa nini swala la muungano linakuwa ni SIRI?. Kwa nini wananchi wasipewe REFERENDUM wakajiamulia mwerekeo wao?.
Wananchi wana haki ya kuambiwa na kujua mwelekeo wa nchi zao kwa matakwa yao na kwa manufaa yao na kizazi kijacho. Hizi ni zama za UWAZI na UKWELI kama Rais Mkapa alivyochagiza baada ya kuingia madarakani mwaka 1995. LAZIMA TUAMBIZANE.
Kama wanasiasa wetu wanahubiri kuwa nchi ina DEMOKRASIA, huku wakijua demokrasia maana yake ni utawala wa watu au madaraka kwa manufaa ya watu. Kwa nini wanashindwa kuishi kwenye maneno yao?.
Kwa sasa inavyoonekana wananchi wanataka mwerekeo mwingine kisiasa, kiuchumi na kijamii, kwa hiyo lazima wasikilizwe. Njia mbadala kwa sasa ni kura kwa njia ya REFERENDUM.
GIVE US A REFERENDUM to vote YES MUUNGANO or NO MUUNGANO.
Hatuwezi kuukimbia UKWELI. Kufanya hivyo ni kuwa kama ngamia anayezika kichwa kwenye mchanga.
Kudai muungano usiwepo kwenye katiba ijayo 2014 kwa sasa siyo kosa. Lingehesabika ni kosa kisheria kama tungekuwa tunaweka viraka tena katika katiba hii mbovu ya mwaka 1977, kama ilivyo katika ibara ya 1 na 2(i).
1. Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.
2.-(1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo.
Sijasikia hata chama kimoja cha siasa, Asasi za kisiasa na Wanasiasa mmoja mmoja wakija na hoja ya REFERENDUM ili kujisimika kwa wapiga kura kwa vile kwa sasa kuna OMBWE la hoja ya msingi kuhusu muungano.
Kama kitatokea chama kwenye uchaguzi mkuu ujao 2015 kikaja na hoja yenye ABSOLUTE PROMISE ya referendum sina pasi shaka kitapata kura maelfu kwa mamilioni kwa wananchi wa pande zote za muungano.
Huhitaji kufanya research kujua wananchi wa pande zote mbili za muungano wamechoka na hili 'ZIGO' la muungano ambalo liko UNBALANCED kwa pande zote. Kila pande zinalalamika lakini kwa sababu ambazo haziko wazi na hazieleweki huku wanasiasa wetu wakiwa wameziba midomo na masikio.
Tarehe 30 Aprili, 1992, Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais wa wakati ule, John Samuel Malecela alibainisha katika bunge la Muungano matatizo ya muungano ambayo alisema mwarobaini wake ni UTEKELEZI.
John Samuel Malecela alisema, ninanukuu,
Mwisho wa kunukuu.Na bila ya kuyaficha baadhi ya matatizo hayo ni mambo yanayohusu suala la uraia, milki ya fedha za kigeni, ukusanyaji na mgawanyo wa mapato kutokana na kodi na ushuru wa forodha,tatizo la formula ya kuchangia gharama za Muungano. Hakuna shaka kwamba haya ni matatizo na mara nyingine yanakera:
Hata hivyo, kwa heshima zote kwa Tume Waheshimiwa Wabunge watakubaliana nami kuwa utatuzi au ufumbuzi wa matatizo hayo, hautapatikana kwa kuanzishwa Shirikisho la Serikali tatu. Kinyume chake hiyo itakuwa ni chanzo cha kufifia umoja wa mshikamano wa Tanzania uliojengeka tango mwaka 1964. Inatoa mwanya kwa wasiopenda umoja huo hatimaye kuuvunja. Hiyo siyo kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania nzima. (Makofi) Mheshimiwa Spika, matatizo ni
lazima yatatuliwe. Hivyo ni azma ya Chama Cha Mapinduzi na Serikali kueleza nguvu zake zote katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo hayo. Serikali na Chama zitaendelea kutafuta ufumbuzi wa matatizo bayo halisi na kuyaondoa kwa manufaa ya wananchi wote wa Tanzania chini ya mfumo wa sasa. Hivyo kwa sasa Serikali inayafanyia kazi maeneo Yanayohusika. Uhusiano wa Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na hasa katika maeneo yanayohusu matatizo niliyoyaainisha.
Miaka 49 kwa sasa, matatizo siyo kwamba bado ni yale yale bali pia yameongezeka. Repoti zaidi ya 39 kuhusiana na muungano zimeandikwa na viraka zaidi ya 10 vimewekwa bila kupata mwarobaini wa matatizo achilia mbali utekelezaji. Kwa jinsi hali inavyoonekana, things will only get worse before getting more worse. Ikumbukwe kuwa mfumo wa muungano wa Ireland ya Kaskazini uliotumika kama BENCHMARK kuandika Hati ya Muungano wetu lakini imegundulika mfumo huu una matatizo ambayo hata nchi za Ireland Kaskazini mpaka ninaandika hii mada bado zina matatizo makubwa na Mwingereza kwa maana kuwa, hii hati ya muungano ina matatizo ya msingi ambayo hayawezi kumalizwa na vikao vya bunge na repoti mbali mbali, bali yatamalizwa na REFERENDUM kama UK walivyonyosha mikono juu na kuamua baada ya uchaguzi mkuu ujao kuwepo na referendum kuhusu uhuru wa Waskotishi na uanachama wa muungano wa nchi za ulaya.
Wakati wa vuguvugu la G55, Rais Mwinyi aliwahi kutamka kuwa mwerekeo wa CCM na sera zake ni kutoka serikali mbili kuelekea serikali MOJA. Kwa sasa jinsi matatizo yalivyokuwa makubwa, hata hiyo sera ya CCM ya serikali moja haiwezekani tena.
Kwa sasa tumefikia sehemu ambayo hata Jaji Mkuu na Waziri Mkuu hawana uhakika kama Zanzibar ni nchi au Mkoa. Matatizo ni makubwa yamefikia kiwango cha nchi kutokuaminiana kutokana na matatizo ya hati ya muungano, maslahi kiuchumi na tofauti la ongezeko la watu kati ya nchi mbili ukilinganisha na eneo la nchi. We can't sit in here and keep on fooling ourself. It'll NEVER work.
Swali linalokosa majibu ni DOGO lakini limebeba mabadiliko ya kitaifa kwa manufaa ya wananchi kitaifa kwa leo na kwa kizazi kijacho katika nyanja zote (kisiasa, kiuchumi na kijamii).
Kwa nini swala la muungano linakuwa ni SIRI?. Kwa nini wananchi wasipewe REFERENDUM wakajiamulia mwerekeo wao?.
Wananchi wana haki ya kuambiwa na kujua mwelekeo wa nchi zao kwa matakwa yao na kwa manufaa yao na kizazi kijacho. Hizi ni zama za UWAZI na UKWELI kama Rais Mkapa alivyochagiza baada ya kuingia madarakani mwaka 1995. LAZIMA TUAMBIZANE.
Kama wanasiasa wetu wanahubiri kuwa nchi ina DEMOKRASIA, huku wakijua demokrasia maana yake ni utawala wa watu au madaraka kwa manufaa ya watu. Kwa nini wanashindwa kuishi kwenye maneno yao?.
Kwa sasa inavyoonekana wananchi wanataka mwerekeo mwingine kisiasa, kiuchumi na kijamii, kwa hiyo lazima wasikilizwe. Njia mbadala kwa sasa ni kura kwa njia ya REFERENDUM.
GIVE US A REFERENDUM to vote YES MUUNGANO or NO MUUNGANO.
Hatuwezi kuukimbia UKWELI. Kufanya hivyo ni kuwa kama ngamia anayezika kichwa kwenye mchanga.