Watanzania tukatae Kurogwa tuijenge nchi yetu

Eng. Y. Bihagaze

JF-Expert Member
Sep 8, 2011
1,488
908
Ifike wakati Watanzania Tukatae vichwa vya Kurogwa. Tuikumbuke nchi hii na tuijenge Kwa Upya.

Naomba nisiwachoshe Kwa Takwimu Na mlolongo wa mambo ambayo mnayajua..itoshe kusema tu kwamba Bidii ya Rais wetu kugundua Na kuwachomoa mafunyfunyu ya makontena Na mabilioni ya fedhazetu zilizokuwa zinaingia kwenye mafuko ya wachache badii hii watanzania wenzetu wanaiponda wanasema raisi wetu anakurupuka

Hakurupuki hapo tu kabaini wafanyakazi hewa zaid ya elfu Kumi nchini ambao mabilioni ya fedha Zetu zilitokomea hewani wenzetu hawa wanasema anakurupuka banaaa..

Mafuta yaliingia nchini freely, wafanya biashara walilipa kodi kama walivyotaka, anapakua Lita laki moja anasema kapakua Lita elfu mbili Na nchi inakwenda, kadhibiti mwanya huo ..watanzania wenzetu wanasema anakurupuka bana..

Anatumbua wafanyakazi wasio wajibika kwenye kisma za Madaraka yao ..watanzania wenzetu wanapwayuka ati anapenda sifaa..

Rais anasema wanafunzi zaidi ya elfu Saba waondolewe Chuo kikuu, Kwa sababu heshima ya Chuo kikuu ibakie kutoa shahada Na vyuo vyenye hadhi ya kutoa diploma wanayoihitaji wanafunzi hao Na walimu wabobezi Wa fani zao wapo huko vyuoni sasa Na nafasi huko vyuoni Zipo sasa Kwa nini wanafunzi hao wang'anga'anizwe kusome Chuo kikuu Na walimu walipwe extra Pesa ili wasake materia Na kuwafundisha wanafunzi hao??, Rais Kusema wanafunzi waondolewe Na udahili ufanywe Kwa wenyesifa ya diploma Na wapelekwe kwenye vyuo husika, watu wanapinga.. Wanabishia.. Wanachobishia Na kupinga hakijulikani..

Niwambieni watanzania wenzangu huko ndio kulogwa kwenyewe. MTU ukishalogwa huwezi kuona mazuri hata iweje. Watu wengine wananachefua zaidi .. Wanasema ati Rais hajui siasa.. Anajifunzia siasa ikulu.. Aaah sasa wewe yaani Ile Kuwa Na wafanyakazi hewa kwako ndio siasa, wizi, ufisadi, ubadhirifu huo kwako ndio siasa.. Basi kama Tafsiri ya siasa ndio hiyo ..siasa ni kitu mbaya sana basi..

Watanzania wenzangu mnaojitambua ni SAA ya kuwaondolea uvivu wajinga wachache wasiopenda nchi yetu isonge Mbele Kwa maslahi ya matumbo yao. CCM imetufikisha pabaya, CCM imechanganya madaraka ya SERIKALI Na Yale ya Kichama, MABWENYENYE ndani ya Chama wamejipa uungu watu Na kushika hatamu za serikali.. Rais anachofanya sasa ni kutofautisha wazi kuwatumikia wananchi Na mambo ya Kichama. Tunajisahau sana.. Huyu ni Rais Wa Tanzania ingawa ni mwanachama Wa CCM. Naamini watu wabaya sana wengi wamo CCM ila pia kuna masazo ya watu wengi Wazuri CCM humo humo. Mfano nzuri ni Rais huyu. Kuna watu ndani ya Chama ambao mbali Na Uonzo uliomo chamani wao wamejitenga nao ila kuna wengine wanaamini Chama chote Kimeoza. Upinzani kumuunga mkono Raisi Kwa Mazuri afanyayo sio Dhambi..sio kosa.. Kuwa mpinzani sio Kuwa shetani Wa kupinga kila kitu..

Wananchi wanafurahia uwajibikaji Wa watumishi Wa serikali Kwa sasa, upatikanaji Wa HUDUMA za kijamii ambazo hapo awali ilikuwa ndoto, elimu za watoto wetu, heshima ya mtanzania inayoanza kurejea.. Kisha MTU aliyelogwa Wa Chama chochote anabeza Bidii hizi.. TUTAKUKANYAGA TUU..Watanzania Hatuhitaji CCM, wala CHADEMA, Wala CUF wala Chama chochote .. Tunahitaji nafuu ya maisha Na maendeleo kutoka Kwa MTU yeyote Wa Chama chochote mwenye nia njema Na Sisi ..

Kwa sasa Nchi kwanza Vyama baadae sana huko ikikaribia Uchaguzi..sio Leo
 
Bunge live likirudi itapendeza zaidi ili tuweze kuona bajeti na juhudi hizo za mh. Raisi bungeni
 
Ulitaka kusemaje labda kwa mfano? Kuna swali bado halina majibu Jesca alifikaje chuo kikuu!? Ukitaka maendeleo wewe kuwa nayo tu hujakazwa sisi wengine nchi tunataka kuijenga kuanzia ikulu.
 
Ifike wakati Watanzania Tukatae vichwa vya Kurogwa. Tuikumbuke nchi hii na tuijenge Kwa Upya.

Naomba nisiwachoshe Kwa Takwimu Na mlolongo wa mambo ambayo mnayajua..itoshe kusema tu kwamba Bidii ya Rais wetu kugundua Na kuwachomoa mafunyfunyu ya makontena Na mabilioni ya fedhazetu zilizokuwa zinaingia kwenye mafuko ya wachache badii hii watanzania wenzetu wanaiponda wanasema raisi wetu anakurupuka

Hakurupuki hapo tu kabaini wafanyakazi hewa zaid ya elfu Kumi nchini ambao mabilioni ya fedha Zetu zilitokomea hewani wenzetu hawa wanasema anakurupuka banaaa..

Mafuta yaliingia nchini freely, wafanya biashara walilipa kodi kama walivyotaka, anapakua Lita laki moja anasema kapakua Lita elfu mbili Na nchi inakwenda, kadhibiti mwanya huo ..watanzania wenzetu wanasema anakurupuka bana..

Anatumbua wafanyakazi wasio wajibika kwenye kisma za Madaraka yao ..watanzania wenzetu wanapwayuka ati anapenda sifaa..

Rais anasema wanafunzi zaidi ya elfu Saba waondolewe Chuo kikuu, Kwa sababu heshima ya Chuo kikuu ibakie kutoa shahada Na vyuo vyenye hadhi ya kutoa diploma wanayoihitaji wanafunzi hao Na walimu wabobezi Wa fani zao wapo huko vyuoni sasa Na nafasi huko vyuoni Zipo sasa Kwa nini wanafunzi hao wang'anga'anizwe kusome Chuo kikuu Na walimu walipwe extra Pesa ili wasake materia Na kuwafundisha wanafunzi hao??, Rais Kusema wanafunzi waondolewe Na udahili ufanywe Kwa wenyesifa ya diploma Na wapelekwe kwenye vyuo husika, watu wanapinga.. Wanabishia.. Wanachobishia Na kupinga hakijulikani..

Niwambieni watanzania wenzangu huko ndio kulogwa kwenyewe. MTU ukishalogwa huwezi kuona mazuri hata iweje. Watu wengine wananachefua zaidi .. Wanasema ati Rais hajui siasa.. Anajifunzia siasa ikulu.. Aaah sasa wewe yaani Ile Kuwa Na wafanyakazi hewa kwako ndio siasa, wizi, ufisadi, ubadhirifu huo kwako ndio siasa.. Basi kama Tafsiri ya siasa ndio hiyo ..siasa ni kitu mbaya sana basi..

Watanzania wenzangu mnaojitambua ni SAA ya kuwaondolea uvivu wajinga wachache wasiopenda nchi yetu isonge Mbele Kwa maslahi ya matumbo yao. CCM imetufikisha pabaya, CCM imechanganya madaraka ya SERIKALI Na Yale ya Kichama, MABWENYENYE ndani ya Chama wamejipa uungu watu Na kushika hatamu za serikali.. Rais anachofanya sasa ni kutofautisha wazi kuwatumikia wananchi Na mambo ya Kichama. Tunajisahau sana.. Huyu ni Rais Wa Tanzania ingawa ni mwanachama Wa CCM. Naamini watu wabaya sana wengi wamo CCM ila pia kuna masazo ya watu wengi Wazuri CCM humo humo. Mfano nzuri ni Rais huyu. Kuna watu ndani ya Chama ambao mbali Na Uonzo uliomo chamani wao wamejitenga nao ila kuna wengine wanaamini Chama chote Kimeoza. Upinzani kumuunga mkono Raisi Kwa Mazuri afanyayo sio Dhambi..sio kosa.. Kuwa mpinzani sio Kuwa shetani Wa kupinga kila kitu..

Wananchi wanafurahia uwajibikaji Wa watumishi Wa serikali Kwa sasa, upatikanaji Wa HUDUMA za kijamii ambazo hapo awali ilikuwa ndoto, elimu za watoto wetu, heshima ya mtanzania inayoanza kurejea.. Kisha MTU aliyelogwa Wa Chama chochote anabeza Bidii hizi.. TUTAKUKANYAGA TUU..Watanzania Hatuhitaji CCM, wala CHADEMA, Wala CUF wala Chama chochote .. Tunahitaji nafuu ya maisha Na maendeleo kutoka Kwa MTU yeyote Wa Chama chochote mwenye nia njema Na Sisi ..

Kwa sasa Nchi kwanza Vyama baadae sana huko ikikaribia Uchaguzi..sio Leo

kama Rais keshaingiwa na hofu ya kutawala? anaishia kwnda makanisa ya ajabu ajabu? hiyo nchi mtaijengaje?
 
Bunge live likirudi itapendeza zaidi ili tuweze kuona bajeti na juhudi hizo za mh. Raisi bungeni
Bunge Liko Live.. Labda live ipi unaiongelea..TBC wanaonyesha bunge live Kwa redio ..sio Kwa Runinga.. Labda useme kwamba unataka kuona sio kusikiliza .. Uone walivyovaa , mikogo yao wakati wanaongea, n.k.. Hapo sawa..lakini kama ni kusikia hoja TBC radio iko Live mbona ..
 
kama Rais keshaingiwa na hofu ya kutawala? anaishia kwnda makanisa ya ajabu ajabu? hiyo nchi mtaijengaje?
Huku ni kumdhalilisha kiongozi Wa nchi..Jambo hili likemewe haraka.. Rais ni Rais Wa Watanzania wote.. Ana Uhuru Wa kwenda KANISA lolote Na dhehebu lolote Na dini yoyote kusali atakavyo..akienda kesho msikiti Wa Mtoro utasema kachanganyikiwa .. Wewe MTU mbaya sana ..mbaguzi ..hufai Kuwa Mzalendo Wa nchi hii
 
Eti "amegundua madudu bandari na issue ya wafanyakazi hewa"

Naddhani wewe umelogwa na aliyekuloga amehamia Syria.
Kwani wafanyakazi hewa na ubadhirifu wa bandari umesemwa mara ngapi bungeni na wapinzani in the last 10 yrs?
Sema ameamua kujitahidi ku act unlike msoga boy aliyeamua kufumbua macho pamoja na wanunge wote wa CCM na mawaziri wao na wakuu wa mikoa wao.


CCM ni ileile mjomba.....
 
Huku ni kumdhalilisha kiongozi Wa nchi..Jambo hili likemewe haraka.. Rais ni Rais Wa Watanzania wote.. Ana Uhuru Wa kwenda KANISA lolote Na dhehebu lolote Na dini yoyote kusali atakavyo..akienda kesho msikiti Wa Mtoro utasema kachanganyikiwa .. Wewe MTU mbaya sana ..mbaguzi ..hufai Kuwa Mzalendo Wa nchi hii

Ulishamwona kikwete anakwenda kuswali idd kidongo chekundu? angekwenda kusali St peter wali tusinge sema? ila katoka kusali? karudi Ikulu? halafu kachomoka tena kwenda kusali duuuuuu!!!
 
Makanisa ya ajabu ndio yapi.

Na yasiyo ya ajabu ndio yapi.

Acha fikra finyu......
Makanisa ya ajabu ni yale yaliyosajiliwa kama NGO na siyo kama kanisa likiwemo hilo la Mzee wa upako na ndio maana makanisa hayo hayapewi free airtime au vipindi vya bure kwenye tv ya Taifa siku za jumapili.

Serikali tu yenyewe imeshindwa kuyatambuwa kwa hiyo mdau yuko sahihi kuyaita ya ajabuajabu it means from no where.
 
Makanisa ya ajabu ni yale yaliyosajiliwa kama NGO na siyo kama kanisa likiwemo hilo la Mzee wa upako na ndio maana makanisa hayo hayapewi free airtime au vipindi vya bure kwenye tv ya Taifa siku za jumapili.

Serikali tu yenyewe imeshindwa kuyatambuwa kwa hiyo mdau yuko sahihi kuyaita ya ajabuajabu it means from no where.
Kwa hiyo quality ya kanisa(nyumba ya Mungu ambayo ni ya kiroho) , hupimwa kwa makaratasi ya usajili ??

Yesu akirudi leo, watu kama nyie atawatandika viboko tu.
 
Usisahau pia ni serekali ambayo imewafukuza kazi vijana 597 wa NIDA bila kuwapa stahiki zao tena wakiwazungusha na kuwaacha solemba wakilia hadharani
 
Ulishamwona kikwete anakwenda kuswali idd kidongo chekundu? angekwenda kusali St peter wali tusinge sema? ila katoka kusali? karudi Ikulu? halafu kachomoka tena kwenda kusali duuuuuu!!!
Watanzania baadhi yetu tunachosha..
 
Eti "amegundua madudu bandari na issue ya wafanyakazi hewa"

Naddhani wewe umelogwa na aliyekuloga amehamia Syria.
Kwani wafanyakazi hewa na ubadhirifu wa bandari umesemwa mara ngapi bungeni na wapinzani in the last 10 yrs?
Sema ameamua kujitahidi ku act unlike msoga boy aliyeamua kufumbua macho pamoja na wanunge wote wa CCM na mawaziri wao na wakuu wa mikoa wao.


CCM ni ileile mjomba.....
Watanzania Mnataka nini??? Mnamtaka Nani? Nani awaongozeni.. Na mnatakaje..
 
Back
Top Bottom