Watanzania tujifunze uzalendo...

Moony

JF-Expert Member
Apr 16, 2011
1,599
435
Inatia aibu na kusikitisha pale watanzania hasa vijana waliozaliwa tangu enzi za Mwinyi na Mkapa pale wanaposhindwa kuwa na adabu.

Inaonyesha ukosefu wa maadili na uzalendo pale unaposhuhudia ama kusikia hawa vijana jinsi wanavyoongea au jinsi wanavyo react kwenye mada nyingi humu JF.

Kumdharau Rais wetu JK pindi anapohudhuria dhifa ama tafrija nje na ndani ya nchi inasikitisha sana.
Ndugu JKikwete anatambulika na kuheshimika duniani, inakuwaje sisi watanzania tunashindwa kutambua hata mchango wake japo hata kama ni mdogo katika maisha ya Watanzania/

Wenzetu nje wanatu judge kwa kauli zetu na matendo yetu. Kwanza waropokaji wengi ni watoto wa mafisadi ambao wameneemeka kupitia mgongo wa serikali.

Tujiheshimu jamani, tumjaji Kikwete kwa hoja, kama ni critical analysis ya utendaji wake, ama personal life, basi iwe ni kwa FACTS na FIGURES.
Tumekuwa wachache wa shukrani kama watu waliolelewa maporini. Mnamsema sema Kagame lakini sisi je, tuna tabia gani nzuri ku reflect UTANZANIA wetu?
Huku Nambia na kwingineko Watanzania tulikuwa tukisifika kwa upendo na heshima kumbe UNAFIKI, UCHOYO, UCHAWI, KIJICHO vimetuzunguka.

Mtu akifanikiwa kidogo hufanyi utafiti ujue kafanikiwa vipi, ila utaanza kumwita kila aina ya majina. Nadhani ni Tanzania pekee duniani ukipita mitaani asubuhi unakuta watu wamekaa barazani wakicheza bao au wakiomba mia tano au kupanda daladala mwanzo hadi mwisho kwa nauli ya kuomba bila kuwa na sababu ya kwendea mjini.

Mrema uko wapi? Kawawa uko wapi, Sokoine uko wapi? nguvu kazi iko wapi ??? tuokoe vijana katika hili janga la uvivu na unafiki?
Kazi kushinda na simu kuchati umbea na kupost matusi kwenye blogs!

Hatujui kuappreciate kazi ya CCM wala mchango wa CHADEMA na Vyama vingine katika maendeleo ya nchi yetu.

Hongera Kikwete, umejitahidi sana, pamoja na kejeli, kashifa na matusi unayopewa, YOU HAVE PLAYED YOUR PART!
 
Inatia aibu na kusikitisha pale watanzania hasa vijana waliozaliwa tangu enzi za Mwinyi na Mkapa pale wanaposhindwa kuwa na adabu.

Inaonyesha ukosefu wa maadili na uzalendo pale unaposhuhudia ama kusikia hawa vijana jinsi wanavyoongea au jinsi wanavyo react kwenye mada nyingi humu JF.

Kumdharau Rais wetu JK pindi anapohudhuria dhifa ama tafrija nje na ndani ya nchi inasikitisha sana.
Ndugu JKikwete anatambulika na kuheshimika duniani, inakuwaje sisi watanzania tunashindwa kutambua hata mchango wake japo hata kama ni mdogo katika maisha ya Watanzania/

Wenzetu nje wanatu judge kwa kauli zetu na matendo yetu. Kwanza waropokaji wengi ni watoto wa mafisadi ambao wameneemeka kupitia mgongo wa serikali.

Tujiheshimu jamani, tumjaji Kikwete kwa hoja, kama ni critical analysis ya utendaji wake, ama personal life, basi iwe ni kwa FACTS na FIGURES.
Tumekuwa wachache wa shukrani kama watu waliolelewa maporini. Mnamsema sema Kagame lakini sisi je, tuna tabia gani nzuri ku reflect UTANZANIA wetu?
Huku Nambia na kwingineko Watanzania tulikuwa tukisifika kwa upendo na heshima kumbe UNAFIKI, UCHOYO, UCHAWI, KIJICHO vimetuzunguka.

Mtu akifanikiwa kidogo hufanyi utafiti ujue kafanikiwa vipi, ila utaanza kumwita kila aina ya majina. Nadhani ni Tanzania pekee duniani ukipita mitaani asubuhi unakuta watu wamekaa barazani wakicheza bao au wakiomba mia tano au kupanda daladala mwanzo hadi mwisho kwa nauli ya kuomba bila kuwa na sababu ya kwendea mjini.

Mrema uko wapi? Kawawa uko wapi, Sokoine uko wapi? nguvu kazi iko wapi ??? tuokoe vijana katika hili janga la uvivu na unafiki?
Kazi kushinda na simu kuchati umbea na kupost matusi kwenye blogs!

Hatujui kuappreciate kazi ya CCM wala mchango wa CHADEMA na Vyama vingine katika maendeleo ya nchi yetu.

Hongera Kikwete, umejitahidi sana, pamoja na kejeli, kashifa na matusi unayopewa, YOU HAVE PLAYED YOUR PART!



Wengi tuna appreciate kazi ya Mh. Kikwete na ccm tatizo ni ubaguzi ambao ccm wamekuwa wakiupandikiza miongoni mwa jamaii. Kwa mfano mm ni Mchagga nitawapenda ccm kweli na kila siku wameweka watu kwenye mitandao kuwatukana wachaga?

Wao kila anayewapinga wanamwita Mchaga, Mkaskazini, Mkristo, Mkanda n.k . Ni haki kweli? Kwani ni lazima wote tuipende ccm?
 
Wengi tuna appreciate kazi ya Mh. Kikwete na ccm tatizo ni ubaguzi ambao ccm wamekuwa wakiupandikiza miongoni mwa jamaii. Kwa mfano mm ni Mchagga nitawapenda ccm kweli na kila siku wameweka watu kwenye mitandao kuwatukana wachaga?

Wao kila anayewapinga wanamwita Mchaga, Mkaskazini, Mkristo, Mkanda n.k . Ni haki kweli? Kwani ni lazima wote tuipende ccm?

Basi pambana na huyo mtu anayewasema sema wachaga ama wakurya si wote
 
Ndugu yangu hapa tulipo na tuendapo sipo.,,hilo hujaliona peke yako.kwa mtazamo wangu wa haraka kuna sababu mbali mbali zinazochangia
[a]Missing in ACTION;Maandishi mengi au vitabu ni sumu kubwa kwa vijana wa sasa,.sio bure aliyesema ukitaka kuficha hela we ficha kwenye kitabu..Hii inasikitisha na kutia aibu.Mfano ni hapo majuzi tu,.nilikuwa nimekaa baa na vijana mbalimbali,.walikuwapo wanafunzi wa vyuo vikuu,wengine wamemaliza na wengine wapo shule ,moja wapo kati ya mada tuliokuwa tunaichambua ilikuwa ni Jumuia ya Afrika Mashariki,wengi walitupa lawama kwa R.Kenyata pia wapo waliokuwa wanamlaumu R.kikwete.
Nikaona kuwa huo ni wakati mzuri wa kupata upembuzi yakinifu na maoni mazuri kutoka kwa vijana hawa,maana walikuwapo wanafunzi wa Political Science.Nikaomba tuzungumzie hutuba ya R.Kikwete aliyoitoa bungeni kuhusu suala la Africa Mashariki halafu ndiotuelekee kwenye,mada .
Amini nanachoandika,.hakuna hata mmoja aliyekuwa akijua R.Kikwete alizungumzia nini,kila mmoja alitoa sababu zake za kutoisikia au kuisoma hiyo hutuba,yupo aliyesema ameisevu kwenye flash akipata muda ataisoma...yupo aliyesema ataitafuta,..na hatimaye mmoja kati yao aliomba niwasimulie ilikuwa inazungumzia nini?! Nlichukia sana ,yaani nageuzwa msimuliaji wa sinema inayoendelea? Mazungumzo hayakuendelea kwa muda mrefu niliaga na kuondoka....Yaaani muda wote mmekaa pamoja,watu wanamtupia lawama kikwete na Uhuru kuhusu A.Mashariki, bila hata kujua J.K alizungumzia nini kuhusu hilo jambo,..wanafuzi wa political science ni wa kujitetea kizombi hivi?sasa lawama zilikuwa za nini?

FACTS na FIGURES.
zitatolewa wapi Mzee iwapo maandishi yamegeuka kimeta? mtu anaona bora asimuliwe kuliko kupoteza muda kusoma mwenyewe.

Ligi mpya inayoendelea kwenye CHADEMA watu wamegawanyika pande mbili ,..wapo wanaouunga mkono uongozi wa Chadema,wapo wanaomuunga mkono Zitto Kabwe.na ubishi ni wa kufa mtu ,...Ukulizia nini maana ya waraka na ulikuwa unazungumzia nini?, lengo lake kuu ni nini? wengi hawaujui zaidi ya kurukia usaliti,...mara huyu kanunua Nyumba ,huyu Viongozi hawataki hesabu zikaguliwe,...USALAMA....

UKWELI TUNARUDI PALE PALE









Tujiheshimu jamani, tumjaji Kikwete kwa hoja, kama ni critical analysis ya utendaji wake, ama personal life, basi iwe ni kwa FACTS na FIGURES.
Tumekuwa wachache wa shukrani kama watu waliolelewa maporini. Mnamsema sema Kagame lakini sisi je, tuna tabia gani nzuri ku reflect UTANZANIA wetu?
Huku Nambia .,,,,,
 
Siungi mkono matusi na dharau kwa watu wazima!!!!

Ila hii hali ni kuonesha kutoridhishwa na haki ya kimaisha kama litaangaliwa kwa jicho la tatu! !!!! Laiti maandamano yangekuwa ni tabia ya Watanzania hali ingekuwa tofauti kabisa.

Namuonea huruma zaid Rais ajaye ndio atakaa kwa wakati mgumu zaidi kama hali ya kimaisha haitakuwa ya kuridhisha!!!!!!! Sababu attitude za Watanzania zinabadilika kwa kasi sana sijui ni kujitambua au kupoteza uvumilivu! !!!???

Na huo uzalendo unaouhubiri ukimea mioyoni mwa Watanzania na wakatambua haki zao basi amini usiamini mtu asiye na uvumilivu atafunga,kutia ulemavu na kuua raia wengi sana maana uzalendo na vurumai vinapishana kidogo sana kwa kweli maana mzalendo akishalipa kodi hatokuelewa kumwambia dawa imeisha (Hospitali), sijui visima vinasafishwa (Mgao) , mara oonh sijui Ruvu chini kumefanyaje( Maji hakuna)!!!!!!!!!

Uzalendo unahitaji a matured system to accommodate the ingredients!!!!!
 
Wengi tuna appreciate kazi ya Mh. Kikwete na ccm tatizo ni ubaguzi ambao ccm wamekuwa wakiupandikiza miongoni mwa jamaii. Kwa mfano mm ni Mchagga nitawapenda ccm kweli na kila siku wameweka watu kwenye mitandao kuwatukana wachaga?

Wao kila anayewapinga wanamwita Mchaga, Mkaskazini, Mkristo, Mkanda n.k . Ni haki kweli? Kwani ni lazima wote tuipende ccm?

nmeshangaa sana kuna mnywa vroba wa bavcha alpost..namnukuu..tupo kwenye kongamano la bavcha landmark hotel waache ccm na uhuru wao..huyu anaonyesha ameamka na vroba na sumu ipo mfukoni..Mungu atusaidie tujtambue na tuwe wazalendo...
cc..rtz..marcopolo..pasco..wazalendo wote ...bavcha
 
Back
Top Bottom