Watanzania tuelezwe kulikuwa na sababu gani za msingi kunasa mazungumzo ya simu ya Makamba kama waziri katika Serikali na viongozi wengineo

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Jumuiya ya Watanzania kwa ujumla inasahau kwamba lilikuwa kosa la jinai kwa mazungumzo binafsi ya simu kati ya kina Makamba, Nape nk kunaswa na kurekodiwa? Je walikuwa wakipelelezwa na vyombo vya usalama nchini? Kulikuwa na kibali cha Mahakama kwamba simu zao ziwekwe katika vyombo vya kunasa mazungumzo yao?

Na kama Raisi Magufuli ametumia njia haramu ambayo haikubaliki kisheria kunasa mazungumzo binafsi ya simu, yeye ndiye alipaswa kuwa wa kwanza kuwaomba msamaha kina Makamba na Tanzania kwa ujumla.

Ni haramu kisheria na kimaadili kunasa mazungumzo binafsi ya simu ya watu bila kibali au sababu za msingi za kiusalama, lakini inaonekana hili linafanywa na awamu ya tano kwa kawaida na hawaoni kama ni tatizo!

Je, watanzania tuelewe kwamba sasa imefikia serikali ya awamu ya tano imekuwa ikinasa mazungumzo ya viongozi wa kitaifa na watu wengine bila ridhaa zao au amri ya mahakama? Hivi kwa nini Watanzania hatulioni hili bali fikra zote tumezielekeza kwenye tarumbeta zinazopigwa juu ya watu kuomba msamaha kwa raisi? Ukweli ni kwamba serikali yeyote inapofikia hatua ya kuanza kunasa mazungumzo ya simu ya viongozi wa kitaifa, hiyo ni serikali ya kidikteta.

Ni kosa kisheria na katika haki za binadamu kufanya hivyo. Raisi Magufuli atueleze kwa mfano, kwa nini serikali ilikuwa ikinasa mazungumzo ya Makamba akiwa waziri katika serikali? Je alikuwa akipelelezwa? Mahakama ilitoa kibali? Na habar iliyopo na kwa maneno yake mwenyewe, Raisi Magufuli ameenda mbali na hata kueleza hadharani kwamba mbali na mawaziri, anafanya hivi hata kwa majaji, kwamba wanachoongea katika simu au email zao sio siri kwake. Ni kwa nini haya yanafanyika? Katiba yetu inampa Raisi mamlaka hayo?

Na hivyo hivyo mazungumzo ya Kinana na Makamba Junior. Raisi Magufuli atoe maelezo ya kina kwa nini serikali iliona kuna umuhimu wa kuwa wananasa mazungumzo yao ya simu, na kwa kutumia sheria ipi ya usalama, na kama walikuwa washukiwa wa uhaini.

Nawashauri viongozi kutia ndani mawaziri muwe makini sana katika suala la kuongea na simu rasmi zenu maana tumeingiliwa. Tumieni simu ambazo hazijasajiriwa katika majina yenu na ambazo mtawapa namba zake watu mnaowaamini tu, kwa kuwa inaonekana serikali ya awamu ya tano imeamua kufanya mambo kama vile kichaa kapewa rungu.

Haikubaliki kabisa kunasa maongezi ya simu ya watu bila sababu za msingi au amri ya mahakama. Na ni wazi kwamba viongozi wote wa kitaifa pamoja na wastaafu simu zenu zinanaswa, au "kudukuliwa" kama wanavyosema mitaani.
 
Kumbe kwa kurekodi mazungumzo ya simu ya kina Nape na Makamba, Raisi Magufuli anaweza kuwa anavunja katiba ya Tanzania, kama kawaida yake.

Article 16 of the Constitution of the United Republic of Tanzania gives the right to privacy, respect and protection of his person and matrimonial life and respect and protection of his residence and private communications. The Constitution further state that;

For the purpose of preserving the person's right in accordance with this Article, the state authority shall
lay down legal procedures regarding the circumstances, manner and extent to which the right to privacy, security of his person, his property and residence may be encroached upon without prejudiceto the provisions of this Article.


The Constitution provides the outstanding meaning of what privacy means and its limits. What the Constitution remain silence is on the aspect of privacy in digital environment.
 
Na pia sheria za kimataifa na haki za binadamu

Article 4 of the African Charter on Human and People’s Rights speaks about right to respect the life and integrity of his person. This means of the act of a person to respect the life and integrity of another person, automatically infringing someone‟s privacy can be against the right to respect the said. Because when you respect someone‟s privacy, you also respect his life and integrity

Also Article 12 of the Universal Declaration of Human Rights articulates that; No one shall be subjected to arbitrary interference with his privacy, family, home or correspondence, nor to attacks upon his honour and reputation. Everyone
has the right to the protection of the law against such interference or attacks.The Article provide a good basis of what privacy means, and as the fact that the Constitution adhere to the principles established by this Declaration, then
as stated earlier the Declaration provides a good basis for the definition of privacy.

Article 8 of the European Convention on Human Rights, protects "the right to respect for private and family life, "and to the European Union's new Charter of Fundamental Rights, which demonstratively features articles on both "Respect for Private and Family Life" and "Protection of Personal Data." The Convention creates the right to respect privacy of family and protection of someone‟s data, particularly personal data which may include health, financial, medical and political data.
 
Tatizo kubwa nionalo mimi ni udhaifu alionao bwana mkubwa.bado haamini kama anakubalika na serikali anayoiongoza kwahiyo hofu alonayo inamsababisha aweke mitego mingi kuwaangalia wanaomuwinda. Kimsingi kuna makosa ya kisheria kuingilia "privacy" za watumiaji wa simu lakini kwa sababu ni mkubwa kataka hakuna namna ni kuikanyaga na kuisigina tu katiba.
 
Jumuiya ya Watanzania kwa ujumla inasahau kwamba lilikuwa kosa la jinai kwa mazungumzo binafsi ya simu kati ya kina Makamba, Nape nk kunaswa na kurekodiwa? Je walikuwa wakipelelezwa na vyombo vya usalama nchini? Kulikuwa na kibali cha Mahakama kwamba simu zao ziwekwe katika vyombo vya kunasa mazungumzo yao?

Na kama Raisi Magufuli ametumia njia haramu ambayo haikubaliki kisheria kunasa mazungumzo binafsi ya simu, yeye ndiye alipaswa kuwa wa kwanza kuwaomba msamaha kina Makamba na Tanzania kwa ujumla.

Ni haramu kisheria na kimaadili kunasa mazungumzo binafsi ya simu ya watu bila kibali sababu za msingi za kiusalama, lakini inaonekana hili linafanywa na awamu ya tano kwa kawaida na hawaoni kama ni tatizo!

Je, watanzania tuelewe kwamba sasa imefikia serikali ya awamu ya tano imekuwa ikinasa mazungumzo ya viongozi wa kitaifa na watu wengine bila ridhaa zao au amri ya mahakama? Hivi kwa nini Watanzania hatulioni hili bali fikra zote tumezielekeza kwenye tarumbeta zinazopigwa juu ya watu kuomba msamaha kwa raisi? Ukweli ni kwamba serikali yeyote inapofikia hatua ya kuanza kunasa mazungumzo ya simu ya viongozi wa kitaifa, hiyo ni serikali ya kidikteta.

Ni kosa kisheria na katika haki za binadamu kufanya hivyo. Raisi Magufuli atueleze kwa mfano, kwa nini serikali ilikuwa ikinasa mazungumzo ya Makamba akiwa waziri katika serikali? Je alikuwa akipelelezwa? Mahakama ilitoa kibali?

Na hivyo hivyo mazungumzo ya Kinana na Makamba Junior. Raisi Magufuli atoe maelezo ya kina kwa nini serikali iliona kuna umuhimu wa kuwa wananasa mazungumzo yao ya simu, na kwa kutumia sheria ipi ya usalama, na kama walikuwa washukiwa wa uhaini.

Nawashauri viongozi kutia ndani mawaziri muwe makini sana katika suala la kuongea na simu rasmi zenu maana tumeingiliwa. Tumieni simu ambazo hazijasajiriwa katika majina yenu na ambazo mtawapa namba zake watu mnaowaamini tu, kwa kuwa inaonekana serikali ya awamu ya tano imeamua kufanya mambo kama vile kichaa kapewa rungu.

Haikubaliki kabisa kunasa maongezi ya simu ya watu bila sababu za msingi au amri ya mahakama. Na ni wazi kwamba viongozi wote wa kitaifa pamoja na wastaafu simu zenu zinanaswa, au "kudukuliwa" kama wanavyosema mitaani.

Mosi, unamfahamu mdukuaji? Kama ndiyo mpeleke mahakamani.
Pili, kuna nchi imeshawahi kukemea au kuonesha nia ya kumpeleka mwanzilishi wa Wikileaks mahakamani kwa kuwa ameweka wazi nyaraka za siri hususan za Marekani zinazohusu mambo ya ndani ya nchi hiyo? Binafsi niliona Marekani akihaha kumsaka mtu huyo kwa kuanikwa uovu wake. So why mnamtaka Rais, tena aliyesemwa aanze kufanya kitu ambacho ninyi wenyewe mnajijua msingefanya? He opted to remain silent, they followed him.
Tatu, unataka sisi Watanzania tuelezwe nini ikiwa wahusika wanajua ni wapi walikosea na wameomba radhi? Kwa nini usingewashauri waende mahakamani?
Nne, una ushahidi gani kuwa mawasiliano yalinaswa na serikali? Basi mimi na wewe pia tupelekwe mahakamani maana tumezisikia na kuzisambaza sauti hizo baada ya kuzipata kwenye social media. Unless wewe ni mgeni kwenye masuala ya Technology ya habari, lakini tambua kuwa kuna watu ambao furaha yao ni kuona kuwa wanaingilia mifumo ya watu wengine hata kama hawalipwi au kupata faida yoyote kifedha. Kwanini tusiwalaumu Makampuni ya simu kwa kuwa na mifumo dhaifu kiusalama?

Watanzania tuna mambo mengi ya kufanya, wahusika wamekiri kosa; why tujipendekeze kuumia sisi?
 
Tuna wanasheria wengi sana, manguli nchini hapa wanaoweza kupeleka swala hili mahakamani wakapata Point 3. Wafanye hivyo sasa, badala ya kila siku kuletwa vifungu vya sheria kibao as if sisi ndio watoa hukumu.

Fungueni kesi mahakamani ili tupate mahali pa kuanzia kwa mustakabali wa vizazi vijavyo.
 
Mosi, unamfahamu mdukuaji? Kama ndiyo mpeleke mahakamani.
Pili, kuna nchi imeshawahi kukemea au kuonesha nia ya kumpeleka mwanzilishi wa Wikileaks mahakamani kwa kuwa ameweka wazi nyaraka za siri hususan za Marekani zinazohusu mambo ya ndani ya nchi hiyo? Binafsi niliona Marekani akihaha kumsaka mtu huyo kwa kuanikwa uovu wake. So why mnamtaka Rais, tena aliyesemwa aanze kufanya kitu ambacho ninyi wenyewe mnajijua msingefanya? He opted to remain silent, they followed him.
Tatu, unataka sisi Watanzania tuelezwe nini ikiwa wahusika wanajua ni wapi walikosea na wameomba radhi? Kwa nini usingewashauri waende mahakamani?
Nne, una ushahidi gani kuwa mawasiliano yalinaswa na serikali? Basi mimi na wewe pia tupelekwe mahakamani maana tumezisikia na kuzisambaza sauti hizo baada ya kuzipata kwenye social media. Unless wewe ni mgeni kwenye masuala ya Technology ya habari, lakini tambua kuwa kuna watu ambao furaha yao ni kuona kuwa wanaingilia mifumo ya watu wengine hata kama hawalipwi au kupata faida yoyote kifedha. Kwanini tusiwalaumu Makampuni ya simu kwa kuwa na mifumo dhaifu kiusalama?

Watanzania tuna mambo mengi ya kufanya, wahusika wamekiri kosa; why tujipendekeze kuumia sisi?
Jibu kwa maswali yako ni rahisi sana - huruhusiwi kutumia na kuweka hadharani taarifa zinazoonyesha wazi kulikuwa na udukuaji haramu. Hapa kimsingi Raisi Magufuli alipaswa ahitakiwe kwa kudukua kwa sababu yeyey ndie amekamatwa na kuku wa wizi.

La sivyo hapaswi kutuia kwa faida yake udukuaji uliofanywa kwa njia haramu
 
Vyombo vyote vya ujasusi dunia nzima, vinafanya udukuzi kwa yeyote ama for udukuzi tuu ama for security reasons kinyume cha sheria, kuanzia simu zao, sms zao, emails zao na barua zao, ikiwemo yeye mwenyewe rais Magufuli kudukuliwa na wadukuaji wenye uwezo mkubwa zaidi yetu wa udukuzi, kwa vile udukuzi huo hua unafanyika kinyume cha sheria, hawakupaswa ku leak hizo info to the public domain.

Kwa vile rais Magufuli ni mkweli kupindukia, aliusema ukweli uliopitiliza kuhusu udukuaji wa mawasiliano ya yule msaliti na akatoa maelezo wasaliti huwa wanafanywa nini vitani na kusisitiza huwezi kuwa msaliti ukaachwa hivi hivi una survive...,

Pia rais Magufuli aliwahi kuuzungumzia udukuzi kwa majaji hadi kwenye accounts zao, wanapokwenda likizo nje ya nchi wanasafiri daraja gani, wanafikia hoteli gani za kiasi gani, wanaspend kiasi gani na kwenye accounts zao wana kiasi gani, kitu ambacho ni kweli TISS wetu wanakifanya lakini rais kama CinC hakupaswa kukisema public.

Kwangu mimi as a security conscious citizen, kudukuliwa sio issue, kwangu issue kwa nini wame leak clips za udukuzi na hakuna aliyekemea?.

Kwenye hili la udukuzi niliwahi kulizungumza siku nyingi humu


Huu utaratibu kwa watu waliokosewa kwa kudukuliwa kinyume cha sheria, halafu wao ndio wanaomba msamaha kuwa ni wakosaji, kunajenga nidhamu mpya ya mawasiliano ya simu za mkononi, sasa watu wanaongea kwa heshima na adabu.
P
 
Mosi, unamfahamu mdukuaji? Kama ndiyo mpeleke mahakamani.
Pili, kuna nchi imeshawahi kukemea au kuonesha nia ya kumpeleka mwanzilishi wa Wikileaks mahakamani kwa kuwa ameweka wazi nyaraka za siri hususan za Marekani zinazohusu mambo ya ndani ya nchi hiyo? Binafsi niliona Marekani akihaha kumsaka mtu huyo kwa kuanikwa uovu wake. So why mnamtaka Rais, tena aliyesemwa aanze kufanya kitu ambacho ninyi wenyewe mnajijua msingefanya? He opted to remain silent, they followed him.
Tatu, unataka sisi Watanzania tuelezwe nini ikiwa wahusika wanajua ni wapi walikosea na wameomba radhi? Kwa nini usingewashauri waende mahakamani?
Nne, una ushahidi gani kuwa mawasiliano yalinaswa na serikali? Basi mimi na wewe pia tupelekwe mahakamani maana tumezisikia na kuzisambaza sauti hizo baada ya kuzipata kwenye social media. Unless wewe ni mgeni kwenye masuala ya Technology ya habari, lakini tambua kuwa kuna watu ambao furaha yao ni kuona kuwa wanaingilia mifumo ya watu wengine hata kama hawalipwi au kupata faida yoyote kifedha. Kwanini tusiwalaumu Makampuni ya simu kwa kuwa na mifumo dhaifu kiusalama?

Watanzania tuna mambo mengi ya kufanya, wahusika wamekiri kosa; why tujipendekeze kuumia sisi?
Bavicha wanaangaika sana katika hili
 
Jibu kwa maswali yako ni rahisi sana - huruhusiwi kutumia na kuweka hadharani taarifa zinazoonyesha wazi kulikuwa na udukuaji haramu. Hapa kimsingi Raisi Magufuli alipaswa ahitakiwe kwa kudukua kwa sababu yeyey ndie amekamatwa na kuku wa wizi.

La sivyo hapaswi kutuia kwa faida yake udukuaji uliofanywa kwa njia haramu

Nani aliweka hadharani? Mpeleke mahakamani basi, maana lawama zinakwenda kwa Rais as if aliweka kwenye account yake. Yeye pia anatumia mitandao kama mimi na wewe so lazima azipate.

Onesha account yoyote ya Rais ambayo ilisambaza sauti hizo, kama hutaishia kuona kwamba account yako mwenyewe ndio ilisambaza.

Umefikirika ulichoandika kweli?
 
Jumuiya ya Watanzania kwa ujumla inasahau kwamba lilikuwa kosa la jinai kwa mazungumzo binafsi ya simu kati ya kina Makamba, Nape nk kunaswa na kurekodiwa? Je walikuwa wakipelelezwa na vyombo vya usalama nchini? Kulikuwa na kibali cha Mahakama kwamba simu zao ziwekwe katika vyombo vya kunasa mazungumzo yao?

Na kama Raisi Magufuli ametumia njia haramu ambayo haikubaliki kisheria kunasa mazungumzo binafsi ya simu, yeye ndiye alipaswa kuwa wa kwanza kuwaomba msamaha kina Makamba na Tanzania kwa ujumla.

Ni haramu kisheria na kimaadili kunasa mazungumzo binafsi ya simu ya watu bila kibali sababu za msingi za kiusalama, lakini inaonekana hili linafanywa na awamu ya tano kwa kawaida na hawaoni kama ni tatizo!

Je, watanzania tuelewe kwamba sasa imefikia serikali ya awamu ya tano imekuwa ikinasa mazungumzo ya viongozi wa kitaifa na watu wengine bila ridhaa zao au amri ya mahakama? Hivi kwa nini Watanzania hatulioni hili bali fikra zote tumezielekeza kwenye tarumbeta zinazopigwa juu ya watu kuomba msamaha kwa raisi? Ukweli ni kwamba serikali yeyote inapofikia hatua ya kuanza kunasa mazungumzo ya simu ya viongozi wa kitaifa, hiyo ni serikali ya kidikteta.

Ni kosa kisheria na katika haki za binadamu kufanya hivyo. Raisi Magufuli atueleze kwa mfano, kwa nini serikali ilikuwa ikinasa mazungumzo ya Makamba akiwa waziri katika serikali? Je alikuwa akipelelezwa? Mahakama ilitoa kibali?

Na hivyo hivyo mazungumzo ya Kinana na Makamba Junior. Raisi Magufuli atoe maelezo ya kina kwa nini serikali iliona kuna umuhimu wa kuwa wananasa mazungumzo yao ya simu, na kwa kutumia sheria ipi ya usalama, na kama walikuwa washukiwa wa uhaini.

Nawashauri viongozi kutia ndani mawaziri muwe makini sana katika suala la kuongea na simu rasmi zenu maana tumeingiliwa. Tumieni simu ambazo hazijasajiriwa katika majina yenu na ambazo mtawapa namba zake watu mnaowaamini tu, kwa kuwa inaonekana serikali ya awamu ya tano imeamua kufanya mambo kama vile kichaa kapewa rungu.

Haikubaliki kabisa kunasa maongezi ya simu ya watu bila sababu za msingi au amri ya mahakama. Na ni wazi kwamba viongozi wote wa kitaifa pamoja na wastaafu simu zenu zinanaswa, au "kudukuliwa" kama wanavyosema mitaani.
Kama unamhujumu raisi hauko salaama vyombo vya ulinzi vipo kazini mda wote,udukuzi kwa watu wanaotaka kuiangusha serikali halali iliyowekwa na wananchi hawatakuwa salaama, usione wameomba msamaha yapo mengi zaidi ya hayo raisi anayajua! Ukiona nape ananyoshanyosha mikono anajua alichokuwa anakifanya na team ile labda yawezekana hujui kilichofanya mwigulu kuenguliwa yapo mengi na yanajulikana wa Kwanza alikuwa mfanyabuashara alieleza yote baada ya kukabwa Koo wakabaki hao vijana wahuni waliofkria chama ni cha Koo zao.NAKUKUMBUSHA KUWA ZILE VOICE NOTE SIYO ZA KUOMBEWA MSAMAHA YAPO MENGI, MKUU MAGOGONI ANAYAJUA NA ANAUSHAHIDI KILA KITU KUHUSIANA NA HAO VIJANA WALICHOKUWA WANAKIFANYA , NA HII YAKUOMBA MSAMAHA NI UNAFIKI WASINGEUMBULIWA KWA MACHACHE YA VOICE NOTE HIZO WASINGEFIKA IKULU KUNYOSHANYOSHA MIKONO YA MSAMAHA! JPM MJANJA UTAONA MBELE ATAKACHO KIFANYA UTAKUJA KUNIKUMBUSHA HUMU:::
 
Vyombo vyote vya ujasusi dunia nzima, vinafanya udukuzi kwa yeyote ama for udukuzi tuu ama for security reasons kinyume cha sheria, ikiwemo yeye mwenyewe rais Magufuli kudukuliwa na wadukuaji wenye uwezo mkubwa zaidi yetu wa udukuzi
Kosa ni pale unaposhikwa ?, hatuwezi kuwalaumu ambao hatujawashika hata kama wanafanya.., tatizo ni pale mtu anapokiri kwa kunufaika na utendaji wa kosa.., hata kama sio yeye aliyetenda kosa basi awashughulikie waliotenda hilo kosa la kudukua.., bila hivyo hii italeta utamaduni wa kwamba kudukua ni sawa...,

Not only must Justice be done; it must also be seen to be done."
 
Kosa ni pale unaposhikwa ?, hatuwezi kuwalaumu ambao hatujawashika hata kama wanafanya.., tatizo ni pale mtu anapokiri kwa kunufaika na utendaji wa kosa.., hata kama sio yeye aliyetenda kosa basi awashughulikie waliotenda hilo kosa la kudukua.., bila hivyo hii italeta utamaduni wa kwamba kudukua ni sawa...,

Not only must Justice be done; it must also be seen to be done."

Mdukuaji ni nani? Mbona mnazunguka tu. Be specific mtaje, na toa ushahidi. Kwani kuna faida gani ambayo Rais ameipata kutokana na udukuzi huo, zaidi ya waliokuwa wakishindwa kulala kupata faida ya usingizi baada ya kusamehewa? Mimi na wewe tumesikiliza, kama alivyofanya Rais na wote tuna wajibu wa kuchukua hatua should there be any kosa.
 
Hakuna simu isiyorekodiwa duniani, kurekodi simu ni njia mojawapo ya kudhibiti uhalafu wowote unaopangwa au uliopangwa kupitia mitandao. Jaribu kujenga hoja katika misingi ya kueleweka. njama ovu yeyote dhidi ya nchi au Rais ni bora ikadhibitiwa mapema na kwa njia yoyote ili hali ya usalama izidi kutamalaki.

wanaharakati wa hovyo kama ninyi ndio wa kunyimwa vibali kufanya kazi zenu hapa Tanzania. tumeona na tunaendelea kushuhudia matukio na njama ya hovyo zikipangwa duniani kupitia mitandao ya simu ambayo inahatarisha hali ya ulinzi na usalama na ninyi wanaharakati msivyoona haya wala aibu mipango hiyo hamuioni ila mnaitetea kwa kuiita faragha. Faragha ni kuteta watu kwenye simu? faragha ni kutukana mtu? je, hao wanaoteta watu waliomba kibali sehemu cha kuteta watu? je, hawajavunja uhuru wa mwingine?

acheni kujitoa fahamu ninyi wanaharakati mnatuharibia nchi yetu kwa harakati zenu za hovyo zisizo na staha
 
Nani aliweka hadharani? Mpeleke mahakamani basi, maana lawama zinakwenda kwa Rais as if aliweka kwenye account yake. Yeye pia anatumia mitandao kama mimi na wewe so lazima azipate.

Onesha account yoyote ya Rais ambayo ilisambaza sauti hizo, kama hutaishia kuona kwamba account yako mwenyewe ndio ilisambaza.

Umefikirika ulichoandika kweli?
Nashangaa kama unafikiria unachosema! NI kosa la jinai kutumia habari iliyopatikana kwa namna ambayo ni haramu
 
Mdukuaji ni nani? Mbona mnazunguka tu. Be specific mtaje, na toa ushahidi. Kwani kuna faida gani ambayo Rais ameipata kutokana na udukuzi huo, zaidi ya waliokuwa wakishindwa kulala kupata faida ya usingizi baada ya kusamehewa? Mimi na wewe tumesikiliza, kama alivyofanya Rais na wote tuna wajibu wa kuchukua hatua should there be any kosa.
Amekea waliomtukana through udukuzi.., hajakemea udukuzi.., wala kuuliza ile chain ya huo udukuzi kwa kuunda tume na kuangalia leakage imetokea wapi.., after all kama kiongozi wa nchi inabidi kukemea tabia yoyote mbovu pindi tu inapoanza
 
Vyombo vyote vya ujasusi dunia nzima, vinafanya udukuzi kwa yeyote ama for udukuzi tuu ama for security reasons kinyume cha sheria, ikiwemo yeye mwenyewe rais Magufuli kudukuliwa na wadukuaji wenye uwezo mkubwa zaidi yetu wa udukuzi, kwa vile udukuzi huo hua unafanyika kinyume cha sheria, hawakupaswa ku leak hizo info to the public domain.

Kwa vile rais Magufuli ni mkweli kupindukia, aliusema ukweli uliopitiliza kuhusu udukuaji wa mafanikio ya yule msaliti na akatoa maelezo wasaliti huwa wanafanywa nini vitani na kusisitiza huwezi kuwa msaliti ukaachwa hivi hivi una survive...

Pia rais Magufuli aliwahi kuuzungumzia udukuzi kwa majaji hadi kwenye accounts zao, wanapokwenda likizo nje ya nje, wanasafiri daraja gani, wanafikia hoteli gani za kiasi gani, wanaspend kiasi gani na kwenye accounts zao wana kiasi gani, kitu ambacho ni kweli TISS wetu wanakifanya lakini rais kama CinC hakupaswa kukisema public.

Kwangu mimi as a security conscious citizen, kudukuliwa sio issue, kwangu issue kwa nini wame leak clips za udukuzi?.

Kwenye hili la udukuzi niliwahi kulizungumza siku nyingi humu


Huu utaratibu kwa watu waliokosewa kwa kudukuliwa kinyume cha sheria, halafu wao ndio wanaomba msamaha kuwa ni wakosaji, kunajenga nidhamu ya mawasiliano ya simu.
P
Mkuu Pascal, unanifanya niogope sana!
 
Back
Top Bottom