Just Distinctions
JF-Expert Member
- May 5, 2016
- 2,690
- 5,315
Habari wa wakati huu wakuu, tangu janga hili la Corona litukumbe Tanzania kama ilivyo nchi zingine duniani kote kumekuwa na maoni mbalimbali ya watu wakitaka hatua madhubuti zichukuliwe ili kukabiliana na janga hili ikiwamo kuzuia mikusanyiko na misongamano isiyo ya lazima, kufunga shughuli zote ambazo zinahusisha muingiliano wa watu mbalimbali kama shule, kuweka vifaa vya kujikinga na kupunguza maambukizi, na wengine wakaenda mbali zaidi kuwe na zuio la kutotoka ndani kabisa ili kupunguza kusambaa kwa gonjwa hili la hatari.
Baadhi ya hatua zimechukuliwa na serikali kama ambavyo imetangazwa na wote tumeshuhudia kama kusimamisha michezo, kufunga vyuo na shule n.k na baadhi ya hatua pia bado serikali haijafanya hivyo kama kuweka zuio la kutotoka majumbani kama nchi jirani.
Kitu kinachonishangaza ni kuwa Watanzania elimu ya corona tumeipata na njia za kujikinga tunazijua lakini kwa nini kila kitu tulaumu serikali? wewe unajua corona inasambaa baki nyumbani!, ila sasa asilimia ya watu wengi hata humu jamii forum wanasisitiza serikali iweke "lockdown" ilihali wao bado wanafanya mizunguko na wanaenda mjini kama kawaida.
Kujikinga na kuzuia maambukizi kunaanza na wewe, ikiwa wewe hutaki kufanya hivyo mpaka serikali ikulazimishe huo ndio unafiki tunaouzungumza, lockdown inapaswa ianze na wewe kukaa nyumbani na familia yako. sio kulalamika kwenye mitandao ya kijamii serikali iweke zuio ilhali wewe ndio bingwa wa kufanya mizunguko hapa mjini.
Kuwajibika ni kwa wewe kuchukua hatua stahiki sio mpaka ulazimishwe ndio iwe na mashiko inapaswa ujilazimu wewe mwenyewe. inashangaza wale wanaopigania serikali iweke zuio la kubaki majumbani ndio tunapishana nao kila siku mijini sasa mna tofauti gani na wale wasiotaka liwepo hilo zuio?
Mwisho ningependa kuwasihi waTanzania wenzangu, tuchukue tahadhari kwa kujikinga na gonjwa hili na pia tutumie muda huu ambao bado shughuli za kiuchumi hazijasimama kuweka akiba ya fedha na vingine vya muhimu kadri vile inavyowezekana ili kujipanga kwa yote yajayo kwani tuendako changamoto zitazidi kuongezeka. Asante
Sent using Jamii Forums mobile app
Baadhi ya hatua zimechukuliwa na serikali kama ambavyo imetangazwa na wote tumeshuhudia kama kusimamisha michezo, kufunga vyuo na shule n.k na baadhi ya hatua pia bado serikali haijafanya hivyo kama kuweka zuio la kutotoka majumbani kama nchi jirani.
Kitu kinachonishangaza ni kuwa Watanzania elimu ya corona tumeipata na njia za kujikinga tunazijua lakini kwa nini kila kitu tulaumu serikali? wewe unajua corona inasambaa baki nyumbani!, ila sasa asilimia ya watu wengi hata humu jamii forum wanasisitiza serikali iweke "lockdown" ilihali wao bado wanafanya mizunguko na wanaenda mjini kama kawaida.
Kujikinga na kuzuia maambukizi kunaanza na wewe, ikiwa wewe hutaki kufanya hivyo mpaka serikali ikulazimishe huo ndio unafiki tunaouzungumza, lockdown inapaswa ianze na wewe kukaa nyumbani na familia yako. sio kulalamika kwenye mitandao ya kijamii serikali iweke zuio ilhali wewe ndio bingwa wa kufanya mizunguko hapa mjini.
Kuwajibika ni kwa wewe kuchukua hatua stahiki sio mpaka ulazimishwe ndio iwe na mashiko inapaswa ujilazimu wewe mwenyewe. inashangaza wale wanaopigania serikali iweke zuio la kubaki majumbani ndio tunapishana nao kila siku mijini sasa mna tofauti gani na wale wasiotaka liwepo hilo zuio?
Mwisho ningependa kuwasihi waTanzania wenzangu, tuchukue tahadhari kwa kujikinga na gonjwa hili na pia tutumie muda huu ambao bado shughuli za kiuchumi hazijasimama kuweka akiba ya fedha na vingine vya muhimu kadri vile inavyowezekana ili kujipanga kwa yote yajayo kwani tuendako changamoto zitazidi kuongezeka. Asante
Sent using Jamii Forums mobile app