Watanzania tembeeni kifua mbele, mnalia kidogo Rais Samia anawasikia, anawabembeleza

the horse

JF-Expert Member
Sep 27, 2011
652
441
Kwa nchi za wengine tena hata nyingi tu za majirani😂 raia kukaa mtandaoni na kuanza kuinanga Serikali, kuisema na kuibagaza kwa jambo fulani basi angeshikwa au hata Serikali ingeleta jeuri na kiburi isisikilize wananchi na ingeendelea na ilichopanga lakini hiyo haiwezi kutokea Tanzania kwa Mama Samia.

Huu ni usikivu, busara na uongozi wa hali ya juu sana. Watoto wanalalamika tu kwenye mitandao lakini Mama anawasikia na anachukua hatua. Hakuna mtu aliyekwenda polisi, wala kuandamana kushinikiza tozo zipunguzwe lakini Mama amesikia kilio cha hata hao wachache waliosema tu mtandaoni na hatua amechukua. Tembeeni kifua mbele Watanzania.

Comment ya raia mmoja aliyeko ndanindani huko Njombe imetosha kwa Serikali kuchukua hatua na kufanya marekebisho ya tozo. Usikivu wa hali ya juu sana huu.

Mwisho, fikiria hizi tozo si kwamba anakatwa kila mtu, ni watu wachache tuh wanaotuma au kutoa fedha. Sasa fikiri shilingi 50 au 500 yako Wewe mmoja unayokatwa inakwenda kuokoa Jamii nzima ya watu zaidi ya laki 1 ambao hawana kituo cha afya pale Mbinga au kule Newala ndanindani. Fikiria 1000 yako unayokatwa inakwenda kuokoa vijana zaidi ya 100 wasio na darasa pale Kibondo. Swawabu kiwango gani Wewe unaipata? Shilingi 100 yako Wewe mmoja inakwenda kuokoa watu zaidi ya 1000 sehemu. Kwanini usitembee kifua mbele sasa?

Tembeeni kifua mbele Watanzania, mko mikono salama na Mama, mkilia kidogo Mama anakuja anawabembeleza halafu safari ya kujenga Taifa letu inaendelea👍🏿

Bwanku M Bwanku
 
Tanzania tuna Rais msikivu Sana. Anajua kuongoza na kusikiliza watu. Mungu aendelee kumuweka na afya njema Mama Samia
 
Mihimili yote ya serikali ni mfu. Hatuna rais, hatuna bunge na mahakama hatuna. Nchi inaongozwa kizombie zombie kwa matakwa na maamuzi ya wachache waliojimilikisha.

We still have a long way to go. Sehemu moja muhimu ya ku deal nayo ni bunge. Hapo ndio kila kitu.
 
Kwa nchi za wengine tena hata nyingi tu za majirani😂 raia kukaa mtandaoni na kuanza kuinanga Serikali, kuisema na kuibagaza kwa jambo fulani basi angeshikwa au hata Serikali ingeleta jeuri na kiburi isisikilize wananchi na ingeendelea na ilichopanga lakini hiyo haiwezi kutokea Tanzania kwa Mama Samia.

Huu ni usikivu, busara na uongozi wa hali ya juu sana. Watoto wanalalamika tu kwenye mitandao lakini Mama anawasikia na anachukua hatua. Hakuna mtu aliyekwenda polisi, wala kuandamana kushinikiza tozo zipunguzwe lakini Mama amesikia kilio cha hata hao wachache waliosema tu mtandaoni na hatua amechukua. Tembeeni kifua mbele Watanzania.

Comment ya raia mmoja aliyeko ndanindani huko Njombe imetosha kwa Serikali kuchukua hatua na kufanya marekebisho ya tozo. Usikivu wa hali ya juu sana huu.

Mwisho, fikiria hizi tozo si kwamba anakatwa kila mtu, ni watu wachache tuh wanaotuma au kutoa fedha. Sasa fikiri shilingi 50 au 500 yako Wewe mmoja unayokatwa inakwenda kuokoa Jamii nzima ya watu zaidi ya laki 1 ambao hawana kituo cha afya pale Mbinga au kule Newala ndanindani. Fikiria 1000 yako unayokatwa inakwenda kuokoa vijana zaidi ya 100 wasio na darasa pale Kibondo. Swawabu kiwango gani Wewe unaipata? Shilingi 100 yako Wewe mmoja inakwenda kuokoa watu zaidi ya 1000 sehemu. Kwanini usitembee kifua mbele sasa?

Tembeeni kifua mbele Watanzania, mko mikono salama na Mama, mkilia kidogo Mama anakuja anawabembeleza halafu safari ya kujenga Taifa letu inaendelea👍🏿

Bwanku M Bwanku
Mbona mwigulu alisema ni Sheria imeshasainiwa na bunge so hawawezi Rudi nyuma. Imekuwaje sasa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom