Uchaguzi 2020 Watanzania sio wajinga, hawatachagua chama ambacho wafuasi, viongozi na wanachama wake sio wazalendo

Ni kweli, ila sio kwa huku jukwaani kwa watu wenye uelewa wa mambo. Kwa huko vijijini na kwa watu wenye uelewa duni wa mambo, mnaweza kuchukua maksi, ila sio kwa watu wanaojitambua. Haya machache yanayofanyika sasa, ni mambo madogo yaliyochelewa. Ndio maana tukiona mmeamka sasa na kuanza kunajisi demokrasia eti kisa kuna hospitali za 1.2b@ tunawaona malimbukeni fulani. Kibaya zaidi mnataka kiongozi asujudiwe kwa mambo madogo hivyo. Hapo ndio ninajua bado mna mitazamo ya kichovu ya kikomunisti.
Hakuna mtu anayetaka kiongozi asujududiwe. Bali tunaeleza mambo mazuri aliyofanya. Ambayo hata wewe unasema yalicheleweshwa. Hakuna ulimbukeni hapo, hivi punde utakuwa unakula treni mpaka Dodoma, fasta tu.
 
Je kwa rasilimali tulizonazo tunastahili kua na maisha haya leo?yanayofanywa na chama tawala ni "wema" ama ni wajibu wao?
Wewe unaonaje? Maana hata Mobutu alikuwa na wajibu wa kuindeleza DRC yenye utajiri wa kutosha wa maliasili. Lakini alihamisha pesa za umma na kupeleka Uswiss.
 
Hakuna mtu anayetaka kiongozi asujududiwe. Bali tunaeleza mambo mazuri aliyofanya. Ambayo hata wewe unasema yalicheleweshwa. Hakuna ulimbukeni hapo, hivi punde utakuwa unakula treni mpaka Dodoma, fasta tu.

Ni mazuri ila ya kawaida sana. Mimi nimezaliwa na kukulia hapa Dar. Nimekaa Sweden 10 consecutive yrs, na sikuwahi kuona kiongozi akitaka kusujudiwa kwa kutimiza wajibu wake. Wala sijawahi kuona huko kiongozi akinajisi chaguzi za nchi hiyo ili chama chake kitangazwe washindi, kisa kuna mambo fulani katekeleza kwenye wajibu wake. Hizo tabia ziko kwenye nchi zenye mitazamo ya kikomunisti, kama China, North Korea nk, ambapo wananchi wanatawaliwa kwa mabavu na shuruti, na kuishi kwa kutii utashi wa viongozi, na viongozi hujiona ndio wenye maono ya nchi.

Hiyo treni inayokutisha ww leo, mimi nimetumia zaidi ya miaka kumi, na wala sikushangaa chochote. Mnaweza kuwatisha malimbukeni wenzenu. Sio kila mtu anasujudia vitu mpaka viwe kigezo cha kunyanyasa wenye mitazamo tofauti na mitazamo/itakadi zenu za kichovu.
 
Ni mazuri ila ya kawaida sana. Mimi nimezaliwa na kukulia hapa Dar. Nimekaa Sweden 10 consecutive yrs, na sikuwahi kuona kiongozi akitaka kusujudiwa kwa kutimiza wajibu wake. Wala sijawahi kuona huko kiongozi akinajisi chaguzi za nchi hiyo ili chama chake kitangazwe washindi, kisa kuna mambo fulani katekeleza kwenye wajibu wake. Hizo tabia ziko kwenye nchi zenye mitazamo ya kikomunisti, kama China, North Korea nk, ambapo wananchi wanatawaliwa kwa mabavu na shuruti, na kuishi kwa kutii utashi wa viongozi, na viongozi hujiona ndio wenye maono ya nchi.

Hiyo treni inayokutisha ww leo, mimi nimetumia zaidi ya miaka kumi, na wala sikushangaa chochote. Mnaweza kuwatisha malimbukeni wenzenu. Sio kila mtu anasujudia vitu mpaka viwe kigezo cha kunyanyasa wenye mitazamo tofauti na mitazamo/itakadi zenu za kichovu.
Sweden nchi ambayo kodi yake inatumika inavyotakiwa. Watu wasiseme kweli kuwa serikali inatimiza wajibu vizuri? Maana Sweden mtu akikosa hata dawa ni kashfa kubwa. Kwa hiyo kutimiza wajibu ipasavyo lazima watu wajadili ukweli.
 
Sweden nchi ambayo kodi yake inatumika inavyotakiwa. Watu wasiseme kweli kuwa serikali inatimiza wajibu vizuri? Maana Sweden mtu akikosa hata dawa ni kashfa kubwa. Kwa hiyo kutimiza wajibu ipasavyo lazima watu wajadili ukweli.
Unakosea sana kusema viongozi wanasujudiwa. Hata Usa Trump amekalia kuti kavu. Lakini Obama alifanya mazuri kama Obamacare na watu walimsifia.
Na usifananishe Sweden na Tanzaniam
 
Sweden nchi ambayo kodi yake inatumika inavyotakiwa. Watu wasiseme kweli kuwa serikali inatimiza wajibu vizuri? Maana Sweden mtu akikosa hata dawa ni kashfa kubwa. Kwa hiyo kutimiza wajibu ipasavyo lazima watu wajadili ukweli.

Sina tatizo na kodi kutumika kufanya baadhi ya mambo, maana hayo ndio matumizi ya kodi, na hayo hata wakoloni walifanya. Ila nisichounga mkono ni uonevu, kuchafua demokrasia ya nchi, na kulazimisha watu wote kutawaliwa kwa shuruti kwa mitazamo ya rais, kisa kajenga hospitali, barabara, reli nk. Sio kila mtu anaamini itakadi ya rais na chama chake, yeye atekeleze wajibu wake, na atuache tuishi kwa mitazamo yetu, na tumchague tumtakaye, na sio amtakaye yeye.
 
Unakosea sana kusema viongozi wanasujudiwa. Hata Usa Trump amekalia kuti kavu. Lakini Obama alifanya mazuri kama Obamacare na watu walimsifia.
Na usifananishe Sweden na Tanzaniam

Sikosei chochote maana kila kitu kiko wazi, kuna shuruti ya wazi na ya kificho kuwa kiongozi huyu asujudiwe. Ndio maana taasisi zote za kimamlaka zinaweza kumuonea yoyote asiye upande wa rais, na kutia wananchi hofu ili watawaliwe kwa lazima bila ridhaa yao. Chaguzi zetu zinajieleza wazi, uhuru wa vyombo vya habari uko hoi, labda uwe kundi la kusifia ndio salama yako.

Watu walimsifia Obama kwa ridhaa yao na sio kwa shuruti. Hapa ni kinyume chake.
 
Sikosei chochote maana kila kitu kiko wazi, kuna shuruti ya wazi na ya kificho kuwa kiongozi huyu asujudiwe. Ndio maana taasisi zote za kimamlaka zinaweza kumuonea yoyote asiye upande wa rais, na kutia wananchi hofu ili watawaliwe kwa lazima bila ridhaa yao. Chaguzi zetu zinajieleza wazi, uhuru wa vyombo vya habari uko hoi, labda uwe kundi la kusifia ndio salama yako.

Watu walimsifia Obama kwa ridhaa yao na sio kwa shuruti. Hapa ni kinyume chake.
Hapa Tanzania nani anasurutishwa kusema ukweli? Ni aibu watu kutokuitakia mema nchi yenu.
 
Uzalendo ni itikadi ya kuweka maslahi ya taifa lako mbele ili liweze kufanikiwa kwa kila namna. Lakini inatia aibu sana CHADEMA na wanachama wake pamoja na wafuasi wake hawana uzalendo kabisa na hawalitakii mema taifa letu.

Kwa mwananchi mzalendo ambae unalitakia mema taifa lako huwezi kubeza mambo ambayo CCM imelifanyia taifa hili tangu tunapata uhuru mpaka sasa. Serikali ya CCM inaimarisha sekta ya afya kwa kujenga vituo vya afya na hospital, mnasema eti ni maendeleo ya vitu. Kwani hawatakuja kutibiwa watu?

Serikali ya CCM inajenga mradi wa JNHPP ili taifa lipate umeme mwingi na wa uhakika. Mnasema eti ni Mega structures na hazina manufaa kwa watu. Kwani huo umeme nyie wanaChadema hamtautumia? Tena kwa bei rahisi! Mradi wa Sgr mnasema ni maendeleo ya vitu sio watu. Kwa hiyo hiyo treni hamtaipanda? Hamtasafirishia mizigo yenu?

Kwa ujumla watanzania wameshawajua ninyi ni wapiga dili na chama chenu kipo kimaslahi binafsi. Sio kuwaletea watanzania maendeleo kwa maslahi mapana ya taifa letu.

Natoa ushauri tu Oktoba msijaribu kugombea nafasi yoyote maana watanzania hawawataki tena.

Siasa sio chuki na uadui.
Uzalendo wa kizuzu tena nyinyi ni wasakatonge tu wabunge wenu hawasomi miswaada wala kuchambua niwabunge wa ndio Mzee kina Steve Nyerere, Mc pilipili mmefanya mpaka watu wameushusha hadhi ubunge kila mtu anataka kuwa mmbunge nonsense
 
Serekali sio nchi, usitake kuchanganya haya mambo mawili.
[/QUOTE
Sijachanganya,serikali ya Ccm inaongoza taifa letu . Nchi yetu ipo mikononi mwa serikali ya Ccm. Ukiombea mabaya Ccm ni sawa na kuliombea mabaya taifa letu.
 

Ccm hawako madarakani kwa ridhaa ya wananchi, bali wako kupitia chaguzi za kishenzi na kihayawani. Ndio maana tunataka tume huru, ili anayekaa madarakani awe na ridhaa ya walio wengi kihalali.
 
Ccm hawako madarakani kwa ridhaa ya wananchi, bali wako kupitia chaguzi za kishenzi na kihayawani. Ndio maana tunataka tume huru, ili anayekaa madarakani awe na ridhaa ya walio wengi kihalali.
Mh... Kwa hiyo 2015 haukufanyika uchaguzi?
 
Huo uhuru unataka uwe vipi? Maana hata sasa tume ni chombo huru kinachofanya kazi kwa mujibu wa katiba na sheria. We unataka uhuru wa namna gani? Fafanua.

Mimi sio mtoto boss, tume iliyo huru, na tume inayoshiriki ushenzi wa kunajisi uchaguzi naweza kuzitenganisha vizuri sana. Tume hii ni sehemu ya ushenzi wa wazi unaoendelea kwenye chaguzi zetu.
 
Back
Top Bottom