Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,708
- 5,711
- Thread starter
- #141
Hakuna mtu anayetaka kiongozi asujududiwe. Bali tunaeleza mambo mazuri aliyofanya. Ambayo hata wewe unasema yalicheleweshwa. Hakuna ulimbukeni hapo, hivi punde utakuwa unakula treni mpaka Dodoma, fasta tu.Ni kweli, ila sio kwa huku jukwaani kwa watu wenye uelewa wa mambo. Kwa huko vijijini na kwa watu wenye uelewa duni wa mambo, mnaweza kuchukua maksi, ila sio kwa watu wanaojitambua. Haya machache yanayofanyika sasa, ni mambo madogo yaliyochelewa. Ndio maana tukiona mmeamka sasa na kuanza kunajisi demokrasia eti kisa kuna hospitali za 1.2b@ tunawaona malimbukeni fulani. Kibaya zaidi mnataka kiongozi asujudiwe kwa mambo madogo hivyo. Hapo ndio ninajua bado mna mitazamo ya kichovu ya kikomunisti.