Watanzania tumekuwa watu wa kulalamikia pesa kila siku lakini ukweli ni kwamba pesa hatuna na ni wakati wa kufikiria pesa ifanye nini kwa jamii na iende wapi. Mfano nilimsikia Zitto akisema walimu wapandishie mishahara lakini hakueleza pesa itataka wapi! vilevile tutataka madaktari waongezewe mishahara lakini hatusemi pesa itatoka wapi?
Polisi na jeshi nao watataka kuongezewa mishahara na makundi mengine yanayotegemea serikali. Sisi Watanzania tuna wajibu wa kuja na jinsi ya kuweza kukuza uchumi ili kuongeza kipato na vilevile kupunguza shughuli na vitu serikali inavyofanya ili serikali iweze kuongeza mishahara na kushughulikia shughuli muhimu tu za jamii.
Hatuwezi kutaka serikali iendelee kujihusisha na vitu vya biashara na kupoteza pesa halafu tutegemee wafanya kazi wa serikali wawe na mishahara na mafao zaidi. Mfano serikali ingeweza kujitoa kwenye Tanesco, ATC, TRC n.k ambavyo vinachukua pesa za serikali nyingi bila kuongeza unafuu, kazi au ufanisi wa mashirika haya kwa jamii. Kwahiyo walimu wakitaka kuongezewa pesa ukweli ni kwamba pesa ya serikali imeenda Tanesco na ATC! huwezi kupata vyote.
Kwahiyo badala ya kulalamikia rushwa pekee ni lazima Watanzania tukubaliane kwamba serikali imejihusisha kwenye vitu vingi sana ambavyo si vya lazima kwa serikali kufanya na hatuwezi kuongeza ukubwa wa serikali na kuongeza mafao wakati huohuo.Matatizo ya Tanzania hayataweza kutatuliwa na serikali pekee bali serikali inatakiwa kuweka mazingira tu na Watanzania wenyewe watatatua matatizo yao.
Huwezi kufanikiwa kwenye mfumo huu wa sasa wa kibepari kwa kuwa na serikali kubwa kwani serikali kubwa inaleta rushwa, inadumisha ufanisi na vilevile haileti ugunduzi.
Swali langu.
1. Je Tanzania ifanye nini kuongeza kiwango cha elimu na kuongeza mafao ya walimu bila kuongeza Budget ya elimu?
2. Tanzania ifanye nini kuboresha sekta ya Afya na kuongeza mafao ya madaktari bila kuongeza budget?
3. Je Tanzania itaweza vitu kuongeza ufanisi wa Bank kwenye uchumi wetu wa Tanzania?
Tutaongeza maswali topic inavyoenda.
Polisi na jeshi nao watataka kuongezewa mishahara na makundi mengine yanayotegemea serikali. Sisi Watanzania tuna wajibu wa kuja na jinsi ya kuweza kukuza uchumi ili kuongeza kipato na vilevile kupunguza shughuli na vitu serikali inavyofanya ili serikali iweze kuongeza mishahara na kushughulikia shughuli muhimu tu za jamii.
Hatuwezi kutaka serikali iendelee kujihusisha na vitu vya biashara na kupoteza pesa halafu tutegemee wafanya kazi wa serikali wawe na mishahara na mafao zaidi. Mfano serikali ingeweza kujitoa kwenye Tanesco, ATC, TRC n.k ambavyo vinachukua pesa za serikali nyingi bila kuongeza unafuu, kazi au ufanisi wa mashirika haya kwa jamii. Kwahiyo walimu wakitaka kuongezewa pesa ukweli ni kwamba pesa ya serikali imeenda Tanesco na ATC! huwezi kupata vyote.
Kwahiyo badala ya kulalamikia rushwa pekee ni lazima Watanzania tukubaliane kwamba serikali imejihusisha kwenye vitu vingi sana ambavyo si vya lazima kwa serikali kufanya na hatuwezi kuongeza ukubwa wa serikali na kuongeza mafao wakati huohuo.Matatizo ya Tanzania hayataweza kutatuliwa na serikali pekee bali serikali inatakiwa kuweka mazingira tu na Watanzania wenyewe watatatua matatizo yao.
Huwezi kufanikiwa kwenye mfumo huu wa sasa wa kibepari kwa kuwa na serikali kubwa kwani serikali kubwa inaleta rushwa, inadumisha ufanisi na vilevile haileti ugunduzi.
Swali langu.
1. Je Tanzania ifanye nini kuongeza kiwango cha elimu na kuongeza mafao ya walimu bila kuongeza Budget ya elimu?
2. Tanzania ifanye nini kuboresha sekta ya Afya na kuongeza mafao ya madaktari bila kuongeza budget?
3. Je Tanzania itaweza vitu kuongeza ufanisi wa Bank kwenye uchumi wetu wa Tanzania?
Tutaongeza maswali topic inavyoenda.