Watanzania naomba sana taarifa za nyie kutotupigia kura ziwe za uwongo maana nitawachukia sana ndugu zetu

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,748
48,371
Humu JF sisi ni watani, na hata nje ya JF huwa watani wa jadi, tunaringishiana maendeleo ila kwa nia njema, pamoja na haya matani ila binafsi huwa sina kinyongo na Watanzania na wengi ni marafiki zangu, kunao hata leo nina ukaribu nao hata kuzidi ndugu zangu, yaani tunaweza kupigiana simu na kusaidiana hata hela, ila hili la UNSC limenishtua sana, sikujua inawezekana mkawa na chuki kiasi hiki, sitaki kuamini na mpaka itolewe taarifa rasmi sitaamini.

Jameni acheni kuwa serious kwamba hamkutupigia kura, yaani mataifa yote ya SADC na EAC yatupigie kura nyie mbaki na waarabu huko pekee yenu, kama hii kweli itakua aliyekwenda kupiga kura kajichanganya, sitaki kuamini Magufuli na uongozi wake wote waliidhinisha kitu kama hiki, siamini na sitaamini mpaka taarifa rasmi zitoke.

Jameni turingishiane mazuri, tupige biashara na kushindana lakini tusifike mpaka wa kuoneana wivu kiasi hiki, nitachukia sana nikizingatia kwamba nina jamaa zangu wa karibu sana huko Tanzania, hivi tulifikia kiasi hiki lini na ilianza vipi, waziri wenu bwana Kabudi tena namheshimu sana maana ni kichwaa, mwenyewe aliahidi mtatupigia kura.

Bado naomboleza kwa hili, sitaki kuamini.
 
Mbona mnapiga kelele?

Kama mmeshinda zogo la nini.

Jua na huo ni utani maana tulijua mtashinda! Halafu msipopigiwa na tz mnang'aka kweli sijui hata shida iko wapi au mnawashwawashwa tuwakune? Kuweni wawazi shida wapi wazee wa nikikupea utawezana.😂😜
 
Mkuu usipate shaka. Hizo taarifa ni feki na ndio maana zina makosa. Kura tuliwapa. Hatuna maslahi na Djibouti ila Kenya yapo. By the way tuliwaahidi.

Serikali yetu ikiona kuna haja ya kutolea ufafanuzi katika hili watatoa.

Ila amini hichi ninachokwambia.
 
Mbona mnapiga kelele? Kama mmeshinda zogo la nini.
Jua na huo ni utani maana tulijua mtashinda! Halafu msipopigiwa na tz mnang'aka kweli sijui hata shida iko wapi au mnawashwawashwa tuwakune? Kuweni wawazi

Hata Uganda au Rwanda asingetupigia kura dah sipati picha jinsi tungewasema. Sio kila upigaji wa kura unazingatia demokrasia za kwenye vitabu, kuna mengine huwa hayaendi kihivyo, ni kama leo rais wenu aje kugundua kuwa mkewe au ndugu yake kapigia kambi ya upinzani kura na kumnyima yeye, japo ndio uhuru wa demokrasia ila patachimbika.
 
Uchukie, usituchukie we don't care. Who are you!? Na baada ya uchaguzi, tunawasaka kila kona na kuwaondoa.

Bahati nzuri ni kwamba maamuzi ya nani wa kupigiwa kura huwa hayafanywi na makajamba wa Tandale, ni level nyingine ambayo hauna uwezo wa kufika hata kwenye gate.
 
Mkuu usipate shaka. Hizo taarifa ni feki na ndio maana zina makosa. Kura tuliwapa. Hatuna maslahi na Djibouti ila Kenya yapo. By the way tuliwaahidi.

Serikali yetu ikiona kuna haja ya kutolea ufafanuzi katika hili watatoa.

Ila amini hichi ninachokwambia.

Aisei shukrani.
 
We mpumbavu kweli sasa ukituchukia kwan anaemtegea mwenzake Zaid c nyie ! Mimi naomba ziwe za kweli kwa kiuhalisia tu haiwezekani TZ wawapigie kura wakenya ,ni wazi hatujawapigia hilo moja ,pili hata ukichukia ukitoka hapo unaenda kusubir chakula kilichotoka Tanzania ule ili upate nguvu ya kupiga domo humu Jf sasa itakua unachukia kinafiki . Haiwezekani uchukie lakini unaishi kwa vyakula vya Tanzania, mitandao unayotumia kupiga kelele ya Tanzania c upumbavu huu!!
 
  • Thanks
Reactions: Oii
Bahati nzuri ni kwamba maamuzi ya nani wa kupigiwa kura huwa hayafanywi na makajamba wa Tandale, ni level nyingine ambayo hauna uwezo wa kufika hata kwenye gate.
Pwahahaha!! Unachekesha sana kijana.
You are so obsessed with Tanzania.
Najua inawauma sana Tanzania inapiga hatua kubwa kwa haraka sana.

Semeni mabaya yote kuhusu Tanzania. But joto mnalipata sawa Sawa.
Fanyeni Kazi acheni kupiga kelele.
Nchi yenu kila mwaka watu wanakufa na njaa.
 
MK254,
Wakenya hamna lolote jema enzi zile za urafiki na Kenya zimepita kwani mmetuibia vya kutosha.
 
Huo ukaribu wa Kenya na Tanzania mnaouongelea ni myth, haupo kwani inategemea na Jiografia ya mahali unapoishi ukiuliza wachaga ndiyo watakwambia kuna ukaribu wa Tanzania na Kenya ukiuliza kwetu Rufiji mpaka Kusini mwa Tanzania hawajui Kenya wanajua Msumbiji, ukienda Mbeya, Iringa au Songea hawajui chochote kuhusu Kenya, ukienda Bukoba wako karibu zaidi na Uganda na Rwanda kuliko na Kenya haiwahusu, Kigoma wako na Kongo/Burundi hivyo ni sehemu ndogo sana ya Tanzania ndiyo ina ,,ukaribu'' na Kenya hivyo msikuze haya mambo kiasi hicho
 
Back
Top Bottom