Watanzania naomba muangalie hii picha.

Yap,halafu mtu akitoka Malaysia kuja Kenya kupanda mlima Kilimanjaro tunaanza kulalamika,malalamiko ya nini wakati mpaka Kahawa wanayokunywa toka Kenya inaeleza Kilimanjaro ipo Kenya.....
 
Kuna haja ya kutafuta hiyo haki miliki na kuizuia Kenya kufaidika kwa kutumia jina ambalo halihusiani na chochote kile ndani ya nchi yao. Usikute wameshatuzidi kete tayari wana haki miliki ya jina Kilimanjaro.

Labda Tanzania haina "haki miliki " ya neno "Kilimanjaro" kama ilivyo kwa kenya kwa neno "Harambee"
 
viongozi wa tanzania wao wanajua kugombea madaraka na labda kuomba misaada nje tu.
 
Viongozi wetu bado wako kny kampeni kunadi sera za ccm na uchaguzi ni 2015! Kenya wanaidi nchi yao kwa mbinu yoyote wanayo ijua kuwa italeta ushawishi, na uchaguzi wao ni march 2013!


Nadhani badala ya kuwatwisha viongozi wetu kila kitu, sisi kama raia mmoja mmoja tuwe chanzo cha mabadiliko, kwa kutoa elimu mbadala kwa wageni kwamba Mlima Kilimanjaro uko Tanzaniana sio Kenya.
 
kuna KIA ila haisaidii kuwafanya waache kuli2mia ilo jina. Hapa ni viongozi kufuatilia na ikiwezekana wanasheria wa intellectual properties watuhelp kwa hili.
 
Kuna haja ya kutafuta hiyo haki miliki na kuizuia Kenya kufaidika kwa kutumia jina ambalo halihusiani na chochote kile ndani ya nchi yao. Usikute wameshatuzidi kete tayari wana haki miliki ya jina Kilimanjaro.


Kweli mkuu labda jamaa wameshatuzunguka wakachukua haki miliki.
 
Dhaifu! Kwahiyo tumeshindwa kuregister Kilimanjaro kuwa trade mark, ili nchi yoyote ikitaka kutumia picha au jina watulipe kwanza? Anyway acha twende ivo ivo kwakuwa hata tukiregister tukalipwa trade mark yetu, hizo fedha hazitafika Hazina.
Dhaifu!
 
A rose by any name would smell as sweet.

Kenyans do not have to brand their products Kilimanjaro to sell, it smacks of insecurity.

Tanzanians do not need to cling to the Kilimanjaro name, it smacks of incompetence.
 
Mbona wengine wamevaa MAGWANDA huku mioyoni mwao ni MAGAMBA?,hilo mbona huliulizi?
 
Kilimanjaro sio registered trade mark

DID YOU MEAN THIS?
100px-Kilimanjaro_Lager_beer.JPG
 
wakuu wakenya ni ndugu zetu 2waachie na wao wafaidi mbona 2nakuwa wabinafsi watanzannia mmnaniudhi
 
Kama Kenya hiyohiyo na nchi zingine zinaweza kusema kuwa Tanzanite inapatikana kwao wakati dunia nzima inajua kuwa vito hivyo vinapatikana Tanzania tu, kwanini wasitumie nafasi hiyo ya ukilaza wa viongozi wetu?
 
Nadhani badala ya kuwatwisha viongozi wetu kila kitu, sisi kama raia mmoja mmoja tuwe chanzo cha mabadiliko, kwa kutoa elimu mbadala kwa wageni kwamba Mlima Kilimanjaro uko Tanzaniana sio Kenya.

Ushauri huu niosawa na ule wa raia kutaja majina ya mafisadi wenye pesa uswiss, serikali umeshindwa kuwajuwa !
 
Hivi huu mchezo wa Kenya kutumia jina la Kilimanjaro ili 'kuuza kwao' utaisha lini?

Mkuu, what is in a name. Sioni jambo baya ikiwa waafrika watatumia majina ya kiafrika kuuza bidhaa zao. kwa mfano neno kama safaricom......ukiivunja pande mbili utapata Safari (mwendo) + com (communication) mawasiliano. sikusikia mkenya au mpwani au muarabu yeyote kutoka oman akilalama. sijatembelea Tz lakini najua utakuta majina kama lamu mombasa yanatumika iwe ni dar au arusha.

kwangu mimi naona huku kulalama ndio njia pole ya kuua the spirit of integration.

Wazungu wa ulaya tayari huiga majina ya swahili bila copyrights na hamna chochote mnachofanya wala hamulalamiki. iweje mkenya aibue mvutano akitumia neno kilimanjaro?
 
Hivi huu mchezo wa Kenya kutumia jina la Kilimanjaro ili 'kuuza kwao' utaisha lini?

Hii ni majuzi Waziri Mkuu wa Kenya Mh Raila Odinga akiwa Malaysia....kahawa ni 'Kenya Coffee' lakini
mbona tena hapo juu naona 'Kilimanjaro'?

...ama nd'o ishatoka hii nayo?

8208518582_5e8dab2c29_b.jpg

Actually, what's has the business community done with regard to this. Its a business issues, if they are just sitting there and do nothing; what you think the govenment is gonna do. Kenya has been doing this for the longest time now. Its must stop and it must stop now. They need to use talent not cheating tanzania business and small farmers. Tusingojee Serikali itatue maswala ya biashara. Viongozi ni wenzetu kama hili jambo sisi wafanya biashara na wajasiriamali tunakaa kimya viongozi unadhani watafanyaje. Zipo njia wa kudhibiti haya maswala. Nahakika hata serkali hairidhiki na wizi huu.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom