Watanzania nani katuloga ?

Rufiji

Platinum Member
Jun 18, 2006
1,881
941
Wanabodi nimesoma hii habari kuhusu mpango wa serikali kuwakopesha wanafunzi waliopata division one kwa wanaume na division one na two kwa wasichana tuu ! Mimi bado aiingii akilini kabisa inawezekana vipi kwa mtanzania wa kawaida kuweza kumsomesha mtoto wake pale chuo ?

Hivi ni taifa gani hawa viongozi wanategemea kulijenga? Hivi hawa viongozi hatambui ya kuwa kima cha chini cha mshahara ni shs 60,0000?



Tutashauri serikali itoe mikopo kwa wote’

2006-08-16 08:35:15
Na Haji Mbaruku

Mwenyekiti wa Bodi ya Mikopo kwa Vyuo vya Elimu ya Juu nchini, Bw. Nimrod Mkono, amesema bodi yake inaendelea kuishauri serikali ili iweze kutoa mikopo kwa wanafunzi wote wanaoihitaji.

Bw. Mkono ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, alisisitiza kauli iliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete, wakati akizindua shule mpya ya kisasa huko Musoma wiki iliyopita, kuwa serikali haina fedha za kusomesha wanafunzi wote wa vyuo vya elimu ya juu.

”Serikali imesema kuwa haina fedha, tunaendelea kutafakari suala hili kwa vile linajadilika,” alisema.

Alikuwa akiongea na Idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), kuhusiana na malalamiko ya wanafunzi kuhusu utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.

Hivi karibuni Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu, wakati ikiwasilisha makadirio na matumizi ya bajeti yake bungeni, ilisema kuwa mikopo ilitolewa kimakosa, hivyo kuanzia sasa, watakaopewa mikopo ni wale watakaofaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza kwa wanaume na kiwango cha daraja la kwanza na la pili kwa wanawake.

Baadhi ya wanafunzi waliozungumza na BBC walipinga kauli hiyo ya serikali, wakisema kuwa kusomesha wanafunzi kwa misingi hiyo, kutaua maendeleo ya elimu nchini.

Pia, wanafunzi wanadai kuwa kutoa mikopo kwa vigezo hivyo kunaweza kuleta ubaguzi na kwamba Taifa litashindwa kuwapata madaktari, wanasheria, wakandarasi, wahandisi na watafiti wa kutosha.

Mmoja wa wanafunzi wanaosoma mchepuo wa Sayansi katika shule moja ya sekondari, Said Jumanne, alisema kuwa mara nyingi wanafunzi wa masomo ya Sayansi, hufaulu kwa kiwango cha daraja la pili na kuendelea, hivyo wengi wao watashindwa kupata mikopo kwa vigezo vya serikali.

”Kwa sababu wanafunzi wengi sasa watakimbilia kwenye masomo ya Sanaa, ambako wanaweza kupata daraja la kwanza na wanafunzi wa masomo ya sanaa hawawezi kusomea udaktari hata kidogo,” alisema mwanafunzi huyo.

Aliiomba serikali ifikirie upya suala la utoaji wa mikopo.
 
jibu ni simple!!

mchawi ni chukua chako mapema. ukipewa elimu ni sawa na dawa kwa hiyo mchawi anataka ufe!
 
Mkwawa,

Kuna njia kama mbili hivi inawezekana kutumiwa:

1. Wote waliokopeshwa na serikali warudishe mikopo, Serikali ina toa circular kwenda kwa waajiri wote, ku submit majina ya walio graduate vyuo vya Tanzania, basi uchambuzi unafanyika kisha wenye kudaiwa wanaambiwa waajiri wawakate kiasi fulani na kupeleka kwenye Bodi ya mikopo kila mwezi. Mtu akijiajiri pia anatakiwa alipe. Hii inawezekana kama serikali itahakikisha kuwa kila mtu mwenye umri zaidi ya miaka 18 anapata TIN (Tax identification Number), kama anasoma poa, akanza kuuza maji serikali ina mtrace. Uwanja huu ni mpaka mnaweza kuchangia namna ya kuboresha!

2. Pili ni kuongeza Skill and Development levy kwa angalau asilimia 2 (kwa sasa ni 6) na kugawana VETA (current recipient) na Bodi ya mikopo!! au hata kuongeza asilimia moja ya kodi kwa wafanyakazi kuchangia bodi ya mikopo

Vi mchango vyangu kiduchu

FD
 
Fikiraduni ,

Mawazo mazuri sana ! ila kitu ambacho kinaumiza kichwa ni watanzania wangapi wataweza kuwasomesha watoto wao chuo ? Kwa sababu JK alisema kule mwanza wale watakaokopeshwa ni wale waliopata daraja la kwanza tuu . Nikajaribu kufuatilia twakimu mbali mbali ili kuweza kujua watu wananaopata daraja la kwanza ni percent gani ya wanafunzi wanaoingia chuo , nikagundua aifiki hata theluthi.

Sasa kama aifiki hata theluthi then nini mpango wa serikali na wanafunzi wengine , Jee viongozi hawaoni ya kuwa wanataka kujenga nchi yenye matabaka ? na jee itawezekana vipi kwa mkulima kumlipia mtoto wake chuo ? Jee kuna financial institution yoyote itakayowezesha wananchi kukopa ili kuwasomesha watoto wao ?

Ndio maana niliposoma hii article nilikasirika sana , nadhani viongozi wetu wamesahau ya kuwa Tanzania ni maskini.
 
Mzee Rufiji,

Heshima mbele mkuu,

kuna kitu kimoja muhimu nikiseme ni kwamba katika hii enzi hatasoma mtu tena bure, kama zamani labda serikali tu ifikirie njia za kuwalipia wananchi wasiokuwa na uwezo, yaani somehow lazima kuwe na malipo kwa shule!

sasa hivi yanayofanyika Dodoma na chuo kipya pamoja na elimu pia kuna issue ya kuuendeleza mkoa huo kiuchumi kwa kukitumia chuo hicho, ndio maana ninasema kuwa ni lazima tulipie elimu, lakini zitafutwe njia za kuwasaidia wananchi wasiojiweza,
 
Mzee ES,

Nakubalina na kila kitu ulichosema kwamba ni muhimu kwa wananchi kulipia Elimu , ila serikali ni lazima ianzishe utaratibu utakaowezesha watu wenye uwezo mdogo kulipia ada za watoto wao . Na wale waliokopeshwa lazima walipe PERIOD

Ni majuzi tuu Rais wetu aliombwa abadilishe uamuzi wa serikali kuhusu KUWAKOPESHA wanafunzi wanaojiunga na vyuo vya elimu juu , Msimamo wa serikali ni kuwa wale watakaokopeshwa ni wale waliopata division one tuu kwa wanaume na division i na ii kwa wanawake, JK alikataa na akasemaa hiyo ndio kauli ya serikali . Mzee ES , hapa ninachojaribu kuzungumzia mimi sio kusomesha watu bure bali kutoa mikopo itakayowezesha watu kwenda vyuoni, kumbuka hapa tunazungumzia ada kati ya shs 700,000 mpaka milioni moja kwa mwaka kiasi ambacho ni impossible kwa mtu wa kima chini kukipata kwa mwaka .

Serikali ilitakiwa kuandaa utaratibu mzuri utakaowezesha watu kulipia mikopo yao mara tuu wanapoanza kazi na wakati huo huo kuwakopesha wale wote wanajojiunga na vyuo . Bunge letu lilitakiwa kujadili hii issue na sio kuzungumzia kikatuni !

By the way , Mzee ES hivi huko bungeni spika amekosa kazi au ? Utasemaje katuni imewatukana wabunge wakati mtu alichora picha yake tuu , na awaoni kwa kufanya hivyo ni kuingilia uhuru wa vyombo vya habari ?
 
Mzee Rufiji,

Unajua I wish kungekuwa Realty Show ya bunge na wabunge wakiwa bungeni, unajua kama unakumbuka mambo ya darasani wakati tunasoma either shule ya msingi au secondary, ni yale yale ndani ya bunge,

Mle ndani wabunge huwa kama watoto wadogo, na ndipo ninaposema kuna mama mmoja ambaye kazi yake ilikuwa kusambaza picha za porno na sasa ni waziri, halafu viongozi wote huwa kwenye level moja hata PM mwenyewe,

lakini kitu kimoja tu ni kwamba siku zote kuna arrogance ya wabunge kujiona kuwa ni viongozi muhimu sana, na utai-notice hiyo pale tu wanapokuja wageni ambao si wabunge, na ndipo inapokuja issue ya vikatuni ukweli response ya spika na baadhi ya wabunge ni motivated na hiyo arrogance, ndani ya bunge kulikuwa na upinzani mkubwa kuwa waiache hiyo issue na waandishi waendelee na uandishi wao,

lakini kuna kundi moja la wabunge wachache ambao hawataki mabadiliko na kuelewa kuwa times have changed na kwamba waandishi kama comedians wanayo haki ya kueleza jinsia zao na kero za wananchi kwa kutumia sanaa (vikatuni na etc), lakini wao wakanga'ng'ania tuu na ndio ukaona Spika akapiga kelele kwa hiyo ikabidi kumuarifu mzee JK haraka sana na issue ikaisha hapo hapo,

Hii ndio faida ya kuwachagua viongozi waliochoka, katika kasi mpya kwani wao hutaka kurudisha time nyuma tuuuuuu!, kwa hiyo JK akakumbushwa kuwa hayo malalamiko against vikatuni sio sambamba na kasi mpya!
 
mapendekezo yangu ni serikali iwalipie wanafunzi wote wanaochaguliwa kujiunga na vyuo vikuu vya serikali, yaani Mlimani,Ardhi,Muhimbili,Sokoine,na DIT. Ni watanzania wachache sana ndiyo wenye uwezo wa kujisomesha wenyewe, au kuchukua hiyo mikopo na kuweza kuirudhisha.

Watanzania tuna tabia ya kupenda kuiga mambo bila kuyafanyia uchunguzi kama yanaweza kufaa katika mazingira yetu. Kwenye zilizoendelea wanaoutaratibu rasmi wa kujua nani anaweza kujilipia Elimu ya juu, na nani hawezi. Sasa sisi tumekurupuka na kuiga Ulaya na Marekani, kana kwamba kila anayefaulu kujiunga chuo kikuu basi anauwezo wa kuchukua mkopo na kuurudisha.

We are acting utafikiri tumepiga hatua kuubwaa katika kutoa elimu kwa wananchi wetu. Serikali itafute mbinu za kuwezesha wanafunzi kusoma vyuo vikuu vya taifa bure sasa hivi. Isipofanya hivyo Tanzania itakuwa taifa la vibarua na manamba wa wakenya na waganda ndani ya EAC.
 
Mzee Joka Kuu,

Heshima mbele mkuu,

katika mazingara ya kiuchumi sasa hivi hatuwezi tena kuwa na wanafunzi kusoma buree, ni lazima walipiwe ada ambayo itakuwa ni mkopo ambao utakuwa na masharti nafuu ya kumruhusu mwanafunzi kuulipa baada ya kumaliza shule, akiwa kazini,

Tanzania ya leo hatuna jinsi tena, gharama za elimu ni kubwa mno serikali haiwezi kuzi-afford, I mean wanafunzi wetu nao wajifunze kufanya kazi na kujisomesha, meaning kwamba sometimes wanahitaji ku-sacrifice school time kwa kusogeza muda wa kujiunga na shule ili kufanya kazi kwanza wakusanye pesa za kujisomesha, I did that kule US, sioni sababu kwa nini isiwezekane hapa bongo,

lakini idea ya kusoma bure au kulipiwa na serikali bila ya kuzirudisha hilo leo haliwezekani tena, na hata wafadhili hawawezi kuturuhusu katika masharti ya kutupatia misaaada, ambayo ni mikopo, ni lazimka tutafute njia za kuwafanya wananfunzi nao wachangie kwa njia moja au nyingine kwenye karo zao!
 
Bado tuna safari ndefu! Lakini kwa kutoa data za mafanikio tuko juu. Kuna mwaka Former PM aliwahi kutoa amri kuhakikisha Shule zote zina Madawati.

Je walifanakiwa? Ila ukiangalia data utaambiwa hakuna wanafunzi wanaokaa chini!
 

Attachments

  • 72748kaa.jpg
    72748kaa.jpg
    15 KB · Views: 465
by Augustino Mosha
Naona lazima tujaribu kujiuliza kwa dhati namna tunavyotumia fedha zetu. Kufikia hapa, tumeona kwamba Zambia wanatumia 24% ya bajeti yao kwenye Elimu, Kenya wanatumia 27%. Sisi mwaka huu tunatumia 4.9% tu ya bajeti kwenye Wizara ya Elimu na Ufundi. Sijajua bado Wizara ya Sayansi na Elimu ya Juu imepangiwa kiasi gani. Naamini ukijumlisha zote, bado tutakuwa tunatumia chini ya 10% ya bajeti yetu kwenye Elimu.

Mzee ES,
kama madai ya Bw.Mosha ni kweli basi Tanzania tunao uwezo wa kuwasomesha bure wanafunzi vyuo vikuu vya taifa. tujaribu kupiga bongo ni jinsi gani tutafanikisha lengo hilo. we need to sacrifice.

fedha za kuwasomesha hao wanafunzi ni vizuri zikatokana na vyanzo vya ndani. huwezi kutegemea wafadhili wakusaidie katika jukumu la msingi kama hilo. vilevile nadhani wafadhili wanapiga kelele kwasababu tunajaribu kutumia fedha za msaada/budgetary supplement kulipia wanafunzi.

jamani, Wajerumani wanatoa elimu BURE kwa wananchi wao mpaka chuo kikuu. Marekani wanatoa elimu bure mpaka darasa la 12( High school), na hiyo ni kauli mbiu ya Taifa lao. Vilevile Marekani wanatoa msaada kwa wanafunzi wasio na uwezo kupata elimu ya chuo kikuu. HAYA NI MAMBO YA KUIGA.
 
Mimi Chifu Ihunyo nimesoma hoja zenu juu ya Serikali kusema kila mmoja alipie Elimu nimeshindwa kuelewa .Watoto wengi wanao ingia Chuoni wakisha struggle sana majumbani mwao wanashindia Mapanki, wale ambao ndugu zao wamewasaidia kusoma hadi kufikia hapo kuongia Chuo wana extended family yaani mbuzi kamzaa mbuzi kamza mbuzi ndiyo maisha yetu yalivyo waafrika .

Leo kuna neno Mkopo nao umekuwa na masharti kwamba serikali itawakopesha hao tu .Nina maswali mengi sana .

1.Hivi Serikali ina sababu ya kutowapa mkopo hawa watoto wa walala hoi wapate Elimu waijenge Tanzania kusaidia familia zao ?
2.JK hujui kwamba wengi wa watoto hawa ndiyo wazawa na wazalendo na Nchi kuliko kundi lako ambalo watoto wenu wanasoma Nje na hawajui shida yeyote kwa gharama za maisha ya Mlala hoi?
3.Kwenye ilani nya Uchaguzi ya CCM si nilisikia mnaongelea Elimu , Ukimwi , maisha bora nk ? Leo ni vipi hata mwaka hujamaliza madarakani?
4.Utakuja na nyimbo gani mwaka 2010 kuomba ama ndiyo utawatumia vijana wako wa Usalama na Polisi kukupa tena 80% ?

Hebu nisaidieni mwenye majibu badi nina maswali mengi sana
 
Chifu Ihunyo ,

Hili suala linaumiza sana na inaonyesha ni jinsi serikali ya CCM wasivyoitakia mema Tanzania siku za usoni . Rais wetu asingekuwa madarakani leo kutokana na system ya nyerere ya elimu kwa wote wazazi wake wasingeweza kumsomesha chuo, kama wazazi wake yeye wasingeweza iweje leo watoto wa walala hoi waweze ?

Nakubalina kabisa na mjumbe aliyesema Tanzania tunaiga mambo bila ya uchambuzi yakinifu aimaanishi kwa kuwa jambo fulani linafanywa marekani au uingereza basi na sisi tulifuate blindly ,huu ni ujinga ! Halafu hawa viongozi wasio na uwezo wa kuona mbali wanakimbilia kuingia kwenye umoja wa afrika mashariki wakati huu wakiaribu mfumo wetu wa elimu , sijui tutafaidikeje na huo umoja kama taifa litajaa vihiyo.


Mwisho napenda kutumia nafasi hii kumpongeza mheshimiwa Mbatia kwa kuliona hili , nadhani mheshimiwa naye siku moja moja huwa anapita hapa just kiddin! Tafadhali angalia attachment hapo chini.




http://ippmedia.com/ipp/nipashe/2006/08/21/72833.html
 
Wazee kwanza naomba kubisha hodi kuingia ndani ya forum.

Suala la elimu ya juu ukweli ni kwamba lazima tulipie, maana katika dunia ya leo hakuna cha bure na ndio maana kukawa na suala la mkopo. Sasa tatizo linakuja ku je kuna mechanism gani ya kurecover pesa ambazo zilikopeshwa kuanzia 1998 or so? maana by simple common sense tungetegemea kuwa hizo pesa zingekuwa kama revolving fund, kuwa unachukua na kurudisha ili wengine wachukue tena.

Suala jingine ni kwamba sisi watanzania hatuna utamaduni wa kuchangia masuala ya maendeleo hasa elimu. Tuko makini sana kwenye kuchangishana kwenye shughuli za ubatizo, kipaimara, arusi you name it all. Wenzetu Wakenya kwa hilo wako mbali na harambee zao.

All in all lazima serikali iwekeze zaidi kwenye elimu in this era of globalisation ili angalau tusiachwe nyuma sana. Ukiangalia sasa hivi kama mtu anataka kuinvest kwenye high technology industries, hatuna wataalam wakutosha. Kwa wenzetu Wachina na Wahindi hapo ndio wamepiga bao maana as production cost kwenye developed world zinavyoongezeka kila leo and demand for products keep on increasing, all production is moving to "developing countries" where production costs are low and yet the level of expertise is almost the same as in the developed countries. This is why the Chinese are trail blazing economically.
 
1.Wacha Vyuo Vikuu vifanye kazi ya Kuchuja nani anafaa kuingia chuo kulingana na vigezo/standards. Challenge kwa serikali yetu iwe ni kutoa mikopo kwa wale wote watakaofaulu kuchaguliwa Vyuoni.
Sasa anapokuja mtu na kusema eti daraja la kwanza pekee kwa wanaume na daraja la kwanza na pili kwa wasichana, huku ni kuwanyima haki vijana wengi tu wenye uwezo tena wakti mwingine mwisho wa kozi za chuo hufanya vizuri zaidi ya wale walioingia na daraja la kwanza, mifano ni mingi saaana. La sivyo tutaendelea kuwa nyuma kielimu siku zote za maisha ya kiuchumi ya dunia hii. Hivyo basi bajeti ya Elimu pia iongezwe to atleast 20%.

2. Ukikopa shurti kurudisha/kulipa, hilo halina ubishi/mjadala. watu walipe mikopo waliyochukua.
 
hivi karibuni niliongea na mwana mama mmoja ambaye ni lawyer!

Baada ya majadiliano marefu alikiri kwangu kuwa tumeparamia sana mabadiliko ya kuwapendela wanawake. Mabadiliko yaje lakini taratibu. Akaongezea kuwa hali ya Tanzania hivyo si zaidi ya miaka kumi ijayo Tanzania litakuwa taifa linaloongoza kuwa na vijana wa kiume wala unga au wa vijiweni maana hawatakuwa na elimu!!!!!!!!!

SIKU HZI KILA KITU WASICHANA, NAFASI ZA KAZI WASICHANA KIPAUMBELE, UBUNGE MAALUMU AKINA MAMA. TENA KIBAYA ZAIDI TUNAWAGAWIA VYEO KWA KUWAPENDA NA SIYO KWA UWEZO WAO. WENZETU UALYA AKINA MAMA WANAGANAGAMARA SANA NA KWELI MAJORIY WANAFIT. LAKINI SERIKALI YA BINGO MTU AKILALA CHUMBANI KWAKE NA KUONGEA NA MAMA WATOTO WAKE BASI KESHO INAKUWA AGENDA YA KITAIFA.!!!!

ETI MWAKA 2010 UWAKILISHI BUNGENI UTAKUWA 50% WANAWAKE NA 50% WANAUME. JE BAADA YA HAPO TUNAELLKEKA ASILIMIA 1OO% WANAWAKE!!!

TUMEPRTAAMIA MABADILIKO KWA KASI KUBWA KAMA YA ILE YA UUZAJI WA MADINI!
YANGU NI HAYO SICHUKII WANAWAKE LAKINI KASI HII INATISHA!

HUKO ULAYA WANAUME HAWANA SAUTI. UKIWAONA UTAWAHURUMIA.

NINADHANI TUJIANDAE SASA KUANZISHA NGO ZA KUTETEA MTOTO WA KIUME.
MAANA SI MUDA MREFU WATAKUWA KAMA MAYATIMA!!

AUMTU UTAONA ILI MTOTO WAKO ASOME BASI ZAA WA KIKE NA SIYO WA KIUME.

IWEJE DIV 1 AND 2 WASICHANA HALAFU DIV 1 WAVULANA! SI MUAMUE TU KUSOMESHA WASICHANA PEKEE KIELEWEKE!

KUNA WAKATI SCHOARSHIP ZILITOLEWA CHUO KIKUU NA SIDA SAREC ZILIKUWA 100. WAKASEMA KATI YA HIZO 50 NI ZA WASICHANA.

KWA HIYO 100-50=50.

NA HIZI 50 ZILIZOBAKI NI KWA AJIRI YA WANAUME NA WANAWAKE. CHA AJABU TENA KATI YA HIZO WAKSEMA WOMEN ARE OF THE HIGHEST PRIORITY.

HATA KAMA NI MASHARTI TUWE MAKINI.

IKO SIKU WATATOA HELA NA KUSEMA HIZI BWANA NI ZA KUSOMESHA HO... PEKA YAKE!!
 
Mpaka juzi yaani miaka 3 nyuma Spain walipeleka sheria Bungeni kusema ukimpiga mkeo sasa ufungwe na bado ikaleta matatizo maana walisema mwanamke anapewa nguvu kubwa haoatakuwa na maendeleo kwenyue familia na nk .

Hadi sasa hawa wazungu bado wanawake wanamtegemea mwanaume kwa kiasi kikubwa pamoja na kwamba wanalia na mambo gender lakinij haya yanakuja within a slow changing in the system.

CCM na JK wanakazania kuwapa ama kuwapigia kelele wanawake mwa kuwa ndiyo watu pekee ambao uwezo wa kuelewa ni mdogo na wanatumia mno kuwapa kura na baadaye wanawasahau .

Swala la jenda jamani tusilifuate toka kwa Wazungu na si kila wakisema wazunhgu basi lazima tufuate . Mbona wazungu wana sheria za wasenge wanaume kwa wanaume kuoana ama wanawake hilo tutalipokea na kuli adress lini ?

Kama tunaweza kulikataa hilo basi mengine mengi tuyakatae yote na si kufuatilia kila kitu .Nina uhakika kwamba kulipia shule ni lazima na muhimu sana sana lakini si kwa ubaguzi wa aina hii .Tunacholilia hapa ni ubaguzi kuliokoa Taifa kwenye ujinga maana asilimia kubwa ni ya watoto wa wakulima ambao ndiyo wapiga ambao wazazi wao hawana uwezo wa kulipia kama wale wa 10% ambao ndiyo akina JK & Co.
Waliokopeswa walipe na wenzao wakoe bila kusema mara wanawake wala nini . JK na CCM wanataka kutumia gender kwa manufaa binafsi kwenye uchaguzi kitu ambacho mimi sijaona faida ya Kuwa na Waziri wa fedha mwanamke kiibadilishe maisha ya mwanamke mwenziwe ambaye ni Mama yangu kijijini. Tuache siasa za kipuuzi na tuangalie Tanzania na mwelekeo wake .Wapewe mikopo na waache kuwaza kununua ndege mpya ya Rais wakati ana ndege mpya kabisa ambao hatujamaliza deni lake .
 
Muganyizi ,

i think a'm missing something did you say that our government is planning to buy another plane for our beloved president ? What happened to the Gulf Stream jet they recently bought ?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom