Watanzania nani anaturoga? Kama hamtaki kila mtu ale urefu wa kamba yake, mnataka wale bila kamba?

Mwananchi Huru

JF-Expert Member
Nov 20, 2021
1,448
1,003
photo_2022-01-18_01-30-19.jpg
Majuzi wakati Rais Samia Suluhu Hassan anafanya kikao baina yake na Mawaziri na Manaibu wa Serikali ya awamu ya Sita aliowateua siku chache zilizopita,

Katika hotuba yake miongoni mwakauli zilizozua utata katika kikao kile ni pale Rais Samia Suluhu Hassan alipowaambia viongozi hao kuwa, " Lazima kila mtu ale kwa Urefu wa kamba yake "

Kauli hii imetafsiriwa na wengi hasa wasiofahamu maana za methali za kiswahili kuwa ni sawa na Rais Samia Suluhu Hassan kuruhusu Mawaziri kutafuna pesa ya Umma,

Nini maana halisi ya methali hii " Kila Mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake "

Kwanza,
maana yake kinadharia ni kwamba Mbuzi akifungwa kamba hawezi kula zaidi ya urefu wa ile kamba mpaka kamba ikatike,

Pili, Maana ya kimantiki ni kwamba kila kitu/mtu hufanya kile kilichopo kwenye uwezo wake au ruhusa yake au Mamlaka yake tu,


RAIS SAMIA ALIMAANISHA NINI?

Rais Samia Suluhu Hassan alipotoa kauli hii alilenga kuwafunda Mawaziri na Manaibu Mawaziri wasichote pesa ya Umma hata senti moja,

Ila waridhike na wachukue kile tu wanachostahili kama Posho za Safari na marupurupu mengine yaliyoanishwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za kiutumishi wa Umma kwa nchi yetu,

Sikia, Kila mtu kula kwa urefu wa kamba yake sio kauli inayoruhusu " Wizi au Ufisadi " ila ni kauli inayolenga kuwarudisha watu|Viongozi kuwa na hofu ya Mungu na kutambua dhamana walizonazo ipo siku watajibu walizitumiaje kwa Mungu,

Dunia hii kila mtu ni mwizi ndio sababu pakawepo na controls|Utaratibu au kwa lugha rahisi kama aliyoitumia Rais Samia Suluhu yaani " Kamba "

" Kula tu unachostahili, kula chako tu "


#Sasa kama kuna Waziri hafahamu kiswahili fasihi aguse pesa ya Umma ndio ataelewa Rais Samia Suluhu Hassan alimaanisha nini,
 
Wanataka kuleta ile weledi wa kitanzania, Ili kuihlalisha ukwapuaji Kwa kisingizio chakutoelewa maana ya kula kulingana na urefu wakamba.
 
Kudadeki.

Rudia tena kumsikiliza. Afu uje ufute na hizi pumba zako uandike upya.
 
labda tuwekane sawa ktk swala la wizi.Mm siamini kwamba dunia hii kila mtu ni mwizi bali wezi ndo wengi.
 
Wengi wamemuelewa vizuri tu raisi, lkn waliopindisha kuelewa huko, wamepindisha kwa sababu mbili. (1) kuna watu wameajiriwa humu na chama fulan kwa lengo la kupotosha umma. Hawa kazi yao kubwa ni kuja huku kuandika propaganda mbali mbali za kuichafua serikali na viongozi wa serikali hata kama serikali au viongozi hao wa serikali wanafanya mambo mazuri na yenye faida kwa taifa, wao watayageuza kuwa ni mabaya na hayana faida kwa taifa ili serikali na viongozi wake waonekane hawana maana mbele ya wanaowaongoza. (1) Hili kundi la pili ni bendera fata upepo. Kundi hili wao hawalipwi kitu, kwa sababu hawapo ktk system ya mikakati,na pia wengi hawajui kuwa wenzao hulipwa. Kwahiyo kundi hili hutumiwa tu kama daraja humu mitandaoni kwa faida ya watu au kundi fulani bila wao kujijua.
 
Watanzania Kiswahili ni shida, Ila umefafanua vizuri mleta mada
Kila mtu ale mezani kwake? Ndiyo maana yenu?
Kwa hiyo kwenye huo uzingo ( urefu) wa kamba utamruhusu mbuzi kutafuna chochote kwenye huo mzunguko hata majani ya mihogo, plastic, nknk.
Mama angesema lugha nyepesi " Ridhikeni na mkipatacho." Na ingewapa watawaliwa imani.
Lakini kwa kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba. HAPANA
 
Unachofanya ni kujilazimisha kuwa mpumbavu.

Kwenye hii video ndefu hapa chini Samia anazungumzia jinsi hela za miradi zinavyoliwa na watumishi hadi miradi kukwama(compromised).

Kumbuka budget ya posho ni tofauti na budget ya miradi.Uliwaji wa hela za posho haiwezi kukwamisha miradi.

Samia hapa anapozungumzia miradi ya Meli,Bandari,Barabara na mingineyo kukwama kutokana na fedha yake kutafunwa.

Anazungumzia fedha za miradi kutafunwa na kitendo hiki ndicho anachokiita kuwa ni kula hadi kuvimbiwa.

Ndipo akashauri kuwa fedha hizo zitafunwe bila kukwamisha miradi na ndipo kitendo hicho akakiita kuwa ni kujipimia.

Nasisitiza hapa mwishoni kuwa kwa kuwa budget ya posho ni tofauti na budget ya miradi,utafunwaji wa fedha za posho hauwezi kukwamisha miradi.Anachozungumzia Samia hapa ni miradi kukwama kutokana na fedha za miradi kutafunwa.
 
#Sasa kama kuna Waziri hafahamu kiswahili fasihi aguse pesa ya Umma ndio ataelewa Rais Samia Suluhu Hassan alimaanisha nini,
Ukiwafuatilia sana Watanzania utaugua Tezi Dume, ndugu Mwananchi...

JK kajisemea zake "Ukitaka kula nawe lazima uliwejapo kiduchu ", Hee! Wabongo si tutakaona JK katuambia ukitaka kula utamu nawe lazima uliwe utamu japo kiduchu.... astaghfirullah

 
Unachofanya ni kujilazimisha kuwa mpumbavu.

Kwenye hii video ndefu hapa chini Samia anazungumzia jinsi hela za miradi zinavyoliwa na watumishi hadi miradi kukwama(compromised).

Kumbuka budget ya posho ni tofauti na budget ya miradi.Uliwaji wa hela za posho haiwezi kukwamisha miradi.

Samia hapa anapozungumzia miradi ya Meli,Bandari,Barabara na mingineyo kukwama kutokana na fedha yake kutafunwa.

Anazungumzia fedha za miradi kutafunwa na kitendo hiki ndicho anachokiita kuwa ni kula hadi kuvimbiwa.

Ndipo akashauri kuwa fedha hizo zitafunwe bila kukwamisha miradi na ndipo kitendo hicho akakiita kuwa ni kujipimia.

Nasisitiza hapa mwishoni kuwa kwa kuwa budget ya posho ni tofauti na budget ya miradi,utafunwaji wa fedha za posho hauwezi kukwamisha miradi.Anachozungumzia Samia hapa ni miradi kukwama kutokana na fedha za miradi kutafunwa.View attachment 2086526
Kwanini Umsemee? Kwanini hamkusema Moja kwa Moja kuwa wale Mishahara yao kwani ndio Urefu wa kamba zao?
 
Back
Top Bottom