Ncha Kali
JF-Expert Member
- Sep 19, 2019
- 14,501
- 27,000
Ndugu zangu!
Ni kawaida kwa kila kiongozi akishika hatamu kujifanyia namna yako ya uongozi/utawala, huku akizingatia mwongozo wa katiba.
Lakini pia katika kuunda serikali, kiongozi mkuu (kwa kesi hii ni Rais) anayo nafasi ya kuweka watu wake kwenye mfumo (cycle) ili kupata urahisi wa hapa na pale.
Kwa kufanya hivyo, wengi hupendelea zaidi walio watiifu kwao (the yes man kind of) hivyo kiongozi hutawala kwa kusifiwa na kuabudiwa sana na hao wateule/wapambe (in some ways).
Wengi tumeshuhudia hili pengine zaidi katika awamu hii iliyokoma, wapambe walienda mbali zaidi kiasi cha kutuaminisha kuwa HAKUTATOKEA tena kiongozi wa kaliba ya JPM (Rest in Power).
Kwamba viongozi wa aina yake hawazaliwi kila wakati (one of his kind), hivyo tumshukuru Mungu kwa tunu hii. Huku wengine wakimtaka Mungu amshukuru JPM!
Wakati SIFA zote hizo zikimwagwa kwa JPM, mama yetu Samia alikuwepo kando yake (just a heartbeat away) lakini hazikuwahi kumhusu hata KIDOGO!
Sasa, baada ya mama kuapishwa, huku akijua kabisa hakuwahi kusifiwa (kuaminiwa) kutosha VIATU vile. Leo atapata wapi nguvu ya kuamini kuwa anaweza?
Inabidi sasa wapambe tukubaliane ya kuwa sio JPM tu aliyekuwa na uwezo wa kutuvusha, kwamba ilifanyika hivyo kwa unafiki tu ili kumtia moyo (kama si kumjaza upepo) mkuu ili achape kazi.
Na sasa tutarajie SIFA zile zile kumrudia Mama yetu, na kwa rekodi zake, basi iwe ZAIDI kwa maana nchi haijapata kuongozwa na Rais mwanamke hapo kabla.
Basi nawasihi tubadili beti tu, ila kiitikio kibakie kile kile. Tuna imani na uwezo wa mama, piga kazi kazi kwa kumtanguliza Mungu na kuzingatia misingi ya utu na utawala bora.
Kila la kheri katika uongozi wako, tunaamini tuko mikono salama. Tuvushe tuifikie nchi ya ahadi.
Ncha Kali.
Ni kawaida kwa kila kiongozi akishika hatamu kujifanyia namna yako ya uongozi/utawala, huku akizingatia mwongozo wa katiba.
Lakini pia katika kuunda serikali, kiongozi mkuu (kwa kesi hii ni Rais) anayo nafasi ya kuweka watu wake kwenye mfumo (cycle) ili kupata urahisi wa hapa na pale.
Kwa kufanya hivyo, wengi hupendelea zaidi walio watiifu kwao (the yes man kind of) hivyo kiongozi hutawala kwa kusifiwa na kuabudiwa sana na hao wateule/wapambe (in some ways).
Wengi tumeshuhudia hili pengine zaidi katika awamu hii iliyokoma, wapambe walienda mbali zaidi kiasi cha kutuaminisha kuwa HAKUTATOKEA tena kiongozi wa kaliba ya JPM (Rest in Power).
Kwamba viongozi wa aina yake hawazaliwi kila wakati (one of his kind), hivyo tumshukuru Mungu kwa tunu hii. Huku wengine wakimtaka Mungu amshukuru JPM!
Wakati SIFA zote hizo zikimwagwa kwa JPM, mama yetu Samia alikuwepo kando yake (just a heartbeat away) lakini hazikuwahi kumhusu hata KIDOGO!
Sasa, baada ya mama kuapishwa, huku akijua kabisa hakuwahi kusifiwa (kuaminiwa) kutosha VIATU vile. Leo atapata wapi nguvu ya kuamini kuwa anaweza?
Inabidi sasa wapambe tukubaliane ya kuwa sio JPM tu aliyekuwa na uwezo wa kutuvusha, kwamba ilifanyika hivyo kwa unafiki tu ili kumtia moyo (kama si kumjaza upepo) mkuu ili achape kazi.
Na sasa tutarajie SIFA zile zile kumrudia Mama yetu, na kwa rekodi zake, basi iwe ZAIDI kwa maana nchi haijapata kuongozwa na Rais mwanamke hapo kabla.
Basi nawasihi tubadili beti tu, ila kiitikio kibakie kile kile. Tuna imani na uwezo wa mama, piga kazi kazi kwa kumtanguliza Mungu na kuzingatia misingi ya utu na utawala bora.
Kila la kheri katika uongozi wako, tunaamini tuko mikono salama. Tuvushe tuifikie nchi ya ahadi.
Ncha Kali.