Watanzania na kupinga vitu vipya bila elimu yake

Beberu

JF-Expert Member
Jan 26, 2017
3,935
7,915
Nawasalimu katika jina la jamhuri ya muungano wa Tz (Hata usipojibu mi naendelea tu)

Mwanzoni mwa miaka ya 2000 wakati Tv ndo zinapata umaarufu hapa nchini watu walipinga sana hii issue wakisema itatuharibu macho, maadili na pia ni kazi ya shetani

Wakati simu za mkononi zinashika kasi pia watu walisema hii ni kazi ya freemason anataka kutuua waafrica na wachungaji kwa masheikh mbalimbali walijitokeza kukemea waumin kumiliki simu kwa kuwa ni kazi ya shetani leo wote wanamiliki smartphone

Wakati Obama analeta vyandarua watu walisema ule ulikuwa mpango wa kutupunguza nguvu za kiume ili tusizaliane waje wachukue madini yetu watu walikuwa hawataki lalia vyandarua kisa hio na wengine wakavitupa kabisa wakihoji iweje marekani atupe vyandarua bure bure tu? leo wote wanalalia vyandarua sijui kama nguvu za kiume zimepungua au Lah

Wakati smartphone (simu za touch) zinaingia watu walizipinga wakidai zinanyonya damu + habari za ufreemason leo hii sitak kusema how wanatumia smartphone zao kwa burudani.

Wakati internet inapata umaarufu Tz hapa ndo palikuwa kasheshe kwa sababu watu wakatafsiri kuwa INTER ni kuingia na NET ni nyavu ko ukiingia internet jua upo nyavuni na umeshadakwa na freemason ko huwez toka hivo watu wakatumia mikutano na radio zao kuweza kukataza watu kutumia internet

Anyway nina mifano mingi sana jins waTz tunavyopenda kupinga kitu kipya bila kufanyia wala kutafuta maelezo ya kitaalamu
Mtu anasema vyandarua vinapunguza nguvu za kiume unamuuliza unajua dawa inayowekwa kwenye chandarua ni ipi na inafanyaje kazi ? Hajui anabaki kusema wazungu hawatupendi mara freemasons blah blah blah

Naomba niwashauri waTz wenzangu kabla hujatoa maoni kuhusiana na jambo lolote lile bas hakikisha una maarifa na ufahamu sahihi wa hilo jambo leo Gwajima anapinga chanjo ya corona lakini wote mnajua maelezo yake bungen alipotaka kuelezea mRNA zinavyofanya kazi yalikuwa utopolo wa kiwango cha juu kuonesha hakuna anachojua juu ya mRNA lakin anapenda tu kupiga kelele na kuleta umuch know kwenye mambo ya kitaalamu

NB: Tuheshimu taaluma za watu

Imeandikwa na Beberu mweusi
 
Kama uliingia mawazoni mwangu.

Nakumbuka miaka hiyo shule ya msingi tunapewa vidonge vya minyoo.

Mitaani tunaambiwa msile vidonge wazungu wanataka kutuua.

Kwanza 'midonge yenyewe mikubwa' we uogopi.

Mtashindwa kuzaa mkikua msile na blah blah za kutosha tu.

Ni mentality za kishamba za watu waliokimbia shule tu.

We mtu anakwambia 5G technology ndo inasababisha Corona mtu kama huyo unamuweka kundi gani kama sio kundi la mambumbu tu.
 
1.) Kama mnaongelea Chanjo, unahitaji elimu gani kujua Chanjo ni ya majaribio? ( Emergence Use Authorisation)

2.) Definition ya Chanjo kwa mujibu wa CDC marekani, waliotoa hicho kibali cha dharura, ni ipi?
 
Mmmh mkuu tv zimepata umaarufu kabla ya mwaka 2000 au ulikua vijijini wakakudanganya hivyo. Nakumbuka isidingo iliyoanza 1998 nilianza nayo mpaka ilipoisha mwaka jana na hapo tulichelewa kupata tv maana kwa jiran ikikuepo muda

Tetea chanjo kivingine mkuu . Nyie ndo mnaofurahia mabeberu kutuletea magonjwa ya ajabu ajabu
 
Nawasalimu katika jina la jamhuri ya muungano wa Tz (Hata usipojibu mi naendelea tu)

Mwanzoni mwa miaka ya 2000 wakati Tv ndo zinapata umaarufu hapa nchini watu walipinga sana hii issue wakisema itatuharibu macho, maadili na pia ni kazi ya shetani...
Chanzo cha matatizo yote ni CCM, Unaweza ukazunguka koote ila tatizo ndo hili
 
Mmmh mkuu tv zimepata umaarufu kabla ya mwaka 2000 au ulikua vijijini wakakudanganya hivyo. Nakumbuka isidingo iliyoanza 1998 nilianza nayo mpaka ilipoisha mwaka jana na hapo tulichelewa kupata tv maana kwa jiran ikikuepo muda

Tetea chanjo kivingine mkuu . Nyie ndo mnaofurahia mabeberu kutuletea magonjwa ya ajabu ajabu
Ona huyu, yaani ulikuwa unapenda kutumia TV made in Tanzania au ,halafu leo upinge chanjo iliyotoka wapi tena. Kama bendera fuata upepo Sawa. Kujitambua ni ndiyo afya bora ya akili.
 
Ona huyu so unataka tuipende corona kisa ni gonjwa la kibeberu na chanjo yake kisa beberu kaleta?
Ona huyu, yaani ulikuwa unapenda kutumia TV made in Tanzania au ,halafu leo upinge chanjo iliyotoka wapi tena. Kama bendera fuata upepo Sawa. Kujitambua ni ndiyo afya bora ya akili.
 
Nawasalimu katika jina la jamhuri ya muungano wa Tz (Hata usipojibu mi naendelea tu)

Mwanzoni mwa miaka ya 2000 wakati Tv ndo zinapata umaarufu hapa nchini watu walipinga sana hii issue wakisema itatuharibu macho, maadili na pia ni kazi ya shetani...
Sawa Beberu.
 
Woooi kumbe hujui corona ilipotokea aiseee pole sana ndo nyie nyie akili ndogo mnataka katiba mpya huku mkiidhihaki katiba nzuriii tuliyopaste toka kwa mabeberu
Hata asili ya ugonjwa wa Corona huijui halafu unapinga chanjo.acha kufuata mkumbo
 
mimi nashauri tufuate ushauri wa gwajima.....
ILA WEE CHAGUA NI GWAJIMA YUPI??
IMG-20210727-WA0004.jpg
 
Nawasalimu katika jina la jamhuri ya muungano wa Tz (Hata usipojibu mi naendelea tu)

Mwanzoni mwa miaka ya 2000 wakati Tv ndo zinapata umaarufu hapa nchini watu walipinga sana hii issue wakisema itatuharibu macho, maadili na pia ni kazi ya shetani...
mtu yeyote mwenye akili zake lazima atilie mashaka kitu kipya, labda sisiem tu ndo wanafuata mkumbo
Hizo chanjo hata wazungu wenyewe wana mashaka nazo
 
Nawasalimu katika jina la jamhuri ya muungano wa Tz (Hata usipojibu mi naendelea tu)

Mwanzoni mwa miaka ya 2000 wakati Tv ndo zinapata umaarufu hapa nchini watu walipinga sana hii issue wakisema itatuharibu macho, maadili na pia ni kazi ya shetani..
Elimu yetu itusaidie kupambana na matatizo, ingependeza wataalamu wetu wawezeshwe ili watengeneze chanjo zetu badala ya kuletewa halafu wajifanye wanadhibiti viwango wakati hawaji imetengenezwaje ... mbaya zaidi hukohuko zinakozalishwa wanaathirika nazo
 
TUHESHIMU TAALUMA ZA WATU
Tuwekee hapa mfano wa mtaalam utuamishe kuwa wataalam mpo nchi hii, kama prof. anaweza kujitambulisha kuwa ameokotwa jalalani!!!
hivi aliyesoma zaidi ya profesa anaitwa nani vile?

Wakati mwingine mtengeneze magroup ya kuwa mnakanyana af ndo mje kutwambia tuheshimu taaluma.
Magu alilianzisha la kukagua vyeti mbona wapo waadhiri wa vyuo walioondoka kwa miguu bila hata kusubiri barua za kufukuzwa?๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
kwa ufupi msituchanganyeee,tumewachoka.

Nchi inapiga kwata pale pale sababu ya eti wataalamu.
Kila siku mnaibuka na misemo(MKUKUTA,MKURABITA,MCHAKATO,UPEMBUZI YAKINIFU...).๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚:rolleyes:) Hivi hamuoni aibu kujiita wenye taaluma?
Alipokuja magu akaondoa misemo angalia yaliyofanyika nchini
 
๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚Mtoa mada si ukwende ukachanjwe sindano yanini kuwapigia kelele wenzako. Wewe kimbia kachanjwe haraka.
 
Mmmh mkuu tv zimepata umaarufu kabla ya mwaka 2000 au ulikua vijijini wakakudanganya hivyo. Nakumbuka isidingo iliyoanza 1998 nilianza nayo mpaka ilipoisha mwaka jana na hapo tulichelewa kupata tv maana kwa jiran ikikuepo muda

Tetea chanjo kivingine mkuu . Nyie ndo mnaofurahia mabeberu kutuletea magonjwa ya ajabu ajabu

Ile massive usage of Tv mpaka kwa watu wa kawaida imetokea mwishon mwa 90s na mwanzon mwa 00s
 
Back
Top Bottom