Watanzania msiipigie kura CHADEMA 2015

Ni ukweli usiopingika kuwa CCM ni chama kongwe na hawakurupuki ktk maamuzi. We angalia mchakao wa kusuluhisha hili suala la madakitari, ni suala ambalo limefanywa kwa umakini na linaendelea kutatuliwa kwa umakini. Sasa hao kenya tangu waweke upinzani;
  1. Mwaikibaki na Raila waligombana
  2. Raila alijilimbikizia mali kwa kuchukua mikataba ya mafuta toka Arabuni,
  3. Mwaka 2007 wakenya wakachinjana kwa sababu ya uchu wa madaraka wa hao wapinzani
  4. Na sasa hawataki kuwasikiliza wanachi wanyonge waliowapatia kura na wameamua kuwafukuza kazi!
Je kumfukuza mtu au kumfuta mtu kazi ni suluhisho? si ni ujinga? Kwani serikali ya CCM wasingeweza kuwafukuza ma Dr? Mbona wameamua kutumia njia ya mahakama wakati huo wanaendelea na mazungumuzo! Msiniite kiduku, naomba mtafakari!!

Hivi Tz itajifunia lipi zuri ukifananisha na kenya mfano hela yao inapanda thamani kila kukicha japo wana vita na alshabab na ingekuwa Tz tuna vita kama wao shilingi yetu ingeporomoka zaidi ya ile ya zimbabwe, pia asilimia kubwa ya wananchi wa kenya wanatambua haki zao nikimaanisha elimu ya uraia yapo mambo mengi tu waliyotuzidi nayo hata export of Tanzanite wametuzidi, sisi labda tulichowazidi nacho ni rasilimali tulizonazo ambazo tumeshindwa kuzittmia ambazo siyo man effort bali ni baraka toka kwa Mungu tu ila kwa upande wa kenya man effort wapo juu kuliko ufikiriapo
 
Ukweli utajitenga, sioni haja ya kuupigia upatu upinzani. Wanamuda mrefu wa kujifunza!!! Ni labda baada ya 50 years ndiyo wanaweza kuwa na sifa za kuongoza nchi.

nape kajitahidi kuwapanga humu ila hamtoweza
 
uko sawa kabisa ccm kwa ukongwe wake kinatakiwa kuwapitisha wakonge ili wagombee kwa sababu kwa akili yako ukongwe ndiyo dawa.

ccm impitishe kingunge ngombale mwiru kuwa mgombea urais,waziri mkuu awe peter kisumo.

mawaziri wastaafu wote jumuiya ya afrika mashariki kwa sababu hawa machekbob walioishika ccm na upinzani hawafai.

Kifo ni kifo tu no matter how old are you
 
Kwa Afrika ni nadra upinzani kuleta maendeleo. Mfano halisi angalia Kenya ambapo hao raia waliouweka upinzani madarakani uliwasbabishia matatizo makubwa na hatimaye umefikia hatua ya kuwafukuza wafanya kazi wa sekta ya afya. Hii haikubaliki, mfano tizama jinsi chama cha mapinduzi kinavyo fanya mambo kwa kufuata sheria na ni chama kivumilivu. Nasaha zangu, watanzania msibabaishwe na vyama vya upinzani. Tujenge nchi na CCM!!
Kwanza mtoa mada nimeipenda sana signature yako. You are believer!!!!!!! Common features za believers ni kwamba kwanza ni waoga wa mabadiliko, pili wanachokiamini ndio hicho hicho hata kama kina upungufu fulani. Taifa ni kama mwanadamu alivyo, hafanani na mwanadamu mwingine (You may find similar persons, but you will never find equal persons). Tanzania ni Tanzania, duniani iko peke yake na ina tabia za kipekee zisizofanana na nchi nyingine, na watu wake ni tofauti kabisa na watu wa taifa linginee lolote. Na Kenya ni Kenya haifanani na Tanzania. Wakenya wana itikadi zao na style zao za maisha tofauti kabisa na Tanzania. Ndio maana maasai wa Kenya ni tofauti na maasai wa Tanzania. Hivyo CCM si KANU na CDM si ODM. Watanzania wenye mapenzi mema tunapigania mabadiliko na si machafuko. Dhana ya machafuko ni sera ya CCM na wala si ya upinzani kama unavyotaka kuwaaminisha wengine. Chukulia misemo hii, CCM "TUTAHAKIKISHA TUNASHINDA UCHAGUZI ILI TUONGOZE SERIKALI, USHINDI NI LAZIMA". CHADEMA "TUTATUMIA NGUVU YA UMMA HADI KIELEWEKE KUSHINDA UCHAGUZI, PEOPLES POWER". Ukiangalia kauli hizo mbili utagundua mwenye sera ya machafuko ni CCM, kauli yake ina maana kwamba lazima washike dola liwe liwalo, na ushindi kwao ni lazima, mnataka ama hamtaki lazima washinde tu. Lakini tunajua kwamba wanaochagua serikali ni watu walio wengi, kama unalazimisha wengi wakupigie magoti hata kama hawataki unamaanisha nini?
CCM si bwana Yesu, ni chama cha wanadamu na chaweza kushikwa na wezi, majangili, wala rushwa, wauza mihadarati na mafioso. CCM ya leo ni pango la wanyang'anyi wake up ndugu yangu.
 
Ni ukweli usiopingika kuwa CCM ni chama kongwe na hawakurupuki ktk maamuzi. We angalia mchakao wa kusuluhisha hili suala la madakitari, ni suala ambalo limefanywa kwa umakini na linaendelea kutatuliwa kwa umakini. Sasa hao kenya tangu waweke upinzani;
  1. Mwaikibaki na Raila waligombana
  2. Raila alijilimbikizia mali kwa kuchukua mikataba ya mafuta toka Arabuni,
  3. Mwaka 2007 wakenya wakachinjana kwa sababu ya uchu wa madaraka wa hao wapinzani
  4. Na sasa hawataki kuwasikiliza wanachi wanyonge waliowapatia kura na wameamua kuwafukuza kazi!
Je kumfukuza mtu au kumfuta mtu kazi ni suluhisho? si ni ujinga? Kwani serikali ya CCM wasingeweza kuwafukuza ma Dr? Mbona wameamua kutumia njia ya mahakama wakati huo wanaendelea na mazungumuzo! Msiniite kiduku, naomba mtafakari!!

Mkuu umakini ulioonesha serikali ni upi?

Kusambaza propaganda?, kuitumia mahakama? au kupotosha uma juu ya madai ya madaktari?, ubabe wa kutaka kupeleka wagonjwa hospitali za binafsi?. Kikwete alikuwa azungumze kama hayo na wazee wa CCM, ila TISS(wakapitia humu JF wakapata nondo) , na wazee wenye busara wakamuuma sikio, wakamwambia waite Ikulu uongee nao. Safari hii akashaurika.

Serikali makini ingekuwa imeanza kutekeleza makubaliano kwa kuanza yale hayaitaji muda mrefu kama la mawaziri kujiuzulu. Hata hivyo natoa pongezi kwa JK kwa kutambua umuhimu wa mazungumzo.
 
Chadema mpango mzima. Magamba subirin tuchukue kisu tuyakwangue 2015. Peoplez........power.
Watz msikubal kubakwa na siasa uchwara za mafisadi.
1.ccm ni chama cha mafisadi
2.magamba
3.majambazi
na kimeshindwa kazi. Mfano mzur watz wengi wanakufa kwa tatizo la mgomo wa madoctor, kisa ccm.
2015, chadema 1
4. Cha mawaziri wanaolizwa guest house na vyangudoa...,Labda ungeandika hivi hiyo thread yako, Wana ccm msiichague tena CUF imekufa...
 
Kwa Afrika ni nadra upinzani kuleta maendeleo. Mfano halisi angalia Kenya ambapo hao raia waliouweka upinzani madarakani uliwasbabishia matatizo makubwa na hatimaye umefikia hatua ya kuwafukuza wafanya kazi wa sekta ya afya. Hii haikubaliki, mfano tizama jinsi chama cha mapinduzi kinavyo fanya mambo kwa kufuata sheria na ni chama kivumilivu. Nasaha zangu, watanzania msibabaishwe na vyama vya upinzani. Tujenge nchi na CCM!!

matatizo ya kutumia supu ya nguruwe pori.
 
Mtoboasiri, sikiliza! Ukilinganisha upiznani wa hizo nchi ni stable, hwezi kulinganisha na upinzani wa TZ ambao wamejaa njaa (mfano David Kafulila alikuwa na haja gani ya kupiga magoti na kulia ili asamehewe?) na CHADEMA ni chama kilicho jaa migogoro ya hapa na pale, labda kikiundwa chama kingine chenye mlengo na dhamira ya dhati ya kusikiliza matatizo ya watanzania walio wengi na kisiwe na migogoro

ww mbumbumbu kwel,ccm kumeoza chama hakifai kuendesha nchi.Watz CHADEMA KWA MAENDELEO YA TZ
 
Aargh, nilidhani JF ni ya Great thinkers tu kumbe hata na wenye mfumo wa kufikiri kama huyu wamo!
Anatuhamasisha tuendelee kuwachagua wezi, vibaka, walaghai, vibakauchumi na wahuni wakubwa walioigandamiza nchi,kuifilisi na kutufikisha hapa tulipo? Tuendelee kuwachagua majambazi waliogawana na kuigawa kwa wageni ardhi yetu, waliouza na kuuziana viwanda, migodi, waliodiriki kukwapua fedha hadi kwenye kihenge cha taifa (Benki Kuu) hadi kugawana nyumba za serikali! Waliobuni na kuutumia vema msemo wa "kuchakachua" yaani kukwapua na kugeuza cha kwako kwa ustadi wa hali ya juu na kuziambukiza karibu asasi zote za kitaifa hivi kuligeuza taifa letu kuwa la majambazi na matapeli? Ni asasi ipi basi haijachakachuliwa au isiyojua uchakachuaji? Wizi wa mchana, ulaji rushwa wenye baraka za chama hiki umetamalaki katika kila asasi kiasi cha kutufanya watanzania kutoaminiana tena! Tuhuma za wizi, uhalifu zinawasakama karibu viongozi woote chini ya chama hiki na hakuna wa kumwamini kuanzia Rais hadi tarishi! Ni kichaa tu anayeweza hamasisha watu kuendelea kuchagua uongozi wa sampuli hii.
Hapo umemaliza yote! Sina la kuongeza Mkuu. Salute kwa uchambuzi wako. Naona mwanzishaji wa thread (magamba) hii atajuta kwa kuwa expose magamba wenziwe ili waumbuliwe na ma- Great thinkers wa humu kama ulivyofanya. Asante sana.
 
Kwa Afrika ni nadra upinzani kuleta maendeleo. Mfano halisi angalia Kenya ambapo hao raia waliouweka upinzani madarakani uliwasbabishia matatizo makubwa na hatimaye umefikia hatua ya kuwafukuza wafanya kazi wa sekta ya afya. Hii haikubaliki, mfano tizama jinsi chama cha mapinduzi kinavyo fanya mambo kwa kufuata sheria na ni chama kivumilivu. Nasaha zangu, watanzania msibabaishwe na vyama vya upinzani. Tujenge nchi na CCM!!

Hah hah duh hiki kweli kiduku napita nitarudi baadae:spider:
 
kiduku wewe ndio wale ambao huwa mnapewa takrima ya kofia na tshirt kisha unauza shahada yako ya kupiga kura, mtu kama wewe unayetumia teknohama bado unaleta hoja za ajabu hivi unashindwa hata na bibi na babu yako walioko kijijini tena watu wa mwaka 47 wanaelewa nini kinaendelea ndani ya jamuhuri tanzania sasahivi watu wanashindia mlo mmoja kwa siku! alaf unajenga hoja kwa kuangalia suala la madakrati peke yake ndio nchi iendeshwe na ccm peke yake. hivi bila chadema leo watanzania tungeweza kujua habari za richmond, EPA, kiwira na ANBEN company. Umeniudhi sana na nimekutoa maana kabisa bahati yako sikujui. JAMII FORUM mdelete huyu he/she does not deserve to sail on a boat of great thinkers.
 
Kwa Afrika ni nadra upinzani kuleta maendeleo. Mfano halisi angalia Kenya ambapo hao raia waliouweka upinzani madarakani uliwasbabishia matatizo makubwa na hatimaye umefikia hatua ya kuwafukuza wafanya kazi wa sekta ya afya. Hii haikubaliki, mfano tizama jinsi chama cha mapinduzi kinavyo fanya mambo kwa kufuata sheria na ni chama kivumilivu. Nasaha zangu, watanzania msibabaishwe na vyama vya upinzani. Tujenge nchi na CCM!!

Kwanza kabisa napenda nikujulishe kuwa hii dhana yako ya mtu kupigia kura chama badala ya mgombea ni dhana ya kizaman sana, hili wazo lilitakiwa lisiwepo kichwani mwa kizazi kilichopo hai nyakati hizi. Pili nadhan wewe ni myopic/short-sighted, yaani unadhani mipaka ya dunia imeishia Kenya, sumbua kichwa kiongozi. Je unasemaje nchi kama England/USA ambapo pia kuna vyama vya upinzani na vinabadilishana utawala kila wakati bila kuharibu kitu??au na huko upinzani unaleta shida???Upinzani kuharibu sio utaratibu rasmi, usikariri.
 
WeWE...hivi upo serious au..
Umetumwaa au umekuja mwenyewe yakhe!
 
[COLOR=#000000 said:
Ng`wanakid[/COLOR]uku;3463744].. labda kikiundwa chama kingine ...na kisiwe na migogoro

Kwa hiyo CCM unakubali haifai kwa 7bu ina migogoro! CUF mbona mmewalaza chali waka zaa katoto kanaitwa ADP hakina migogoro! Una uvivu wa kufikiri ngw'akiduku!
 
Back
Top Bottom