Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,377
- 58,384
Watanzania kuonja shubiri ya mafuta ya taa wiki hii | Send to a friend |
Tuesday, 28 June 2011 20:25 |
0digg Leon Bahati WATANZANIA wataanza kufaidika na punguzo la mafuta ya petroli na dizeli kuanzia keshokutwa kutokana na kuanza kutumika kwa sheria mpya ya punguzo la kodi iliyopitishwa bungeni wiki iliyopita.Pia, siku hiyo watumiaji mafuta ya taa wataanza kuonja shubiri ya bei kubwa ya bidhaa hiyo kutokana na serikali kupandisha kodi yake kwa Sh400.30 kwa lita. Hayo yamebainishwa katika mkutano wa wadau wa sekta ya mafuta nchini uliofanyika Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), Haruna Masebu, aliweka wazi jinsi mkakati huo utakavyotekelezwa. Tayari sheria hiyo imepitishwa na kutangazwa kwenye gazeti la serikali na itaanza kutumika rasmi Julai Mosi (kesho kutwa), alisema Masebu. Aliweka wazi kuwa kodi inayotozwa kwenye mafuta ya dizeli itapungua kutoka Sh314 hadi Sh215, hivyo bei mpya itapungua kwa wastani wa Sh100 kwa lita, wakati kwenye mafuta ya taa kodi imeongezwa kutoka Sh52 hadi kufikia Sh400 kwa lita.Kulingana na takwimu za mkurugenzi huyo, punguzo la mafuta ya dizeli ambayo Dar es Salaam inauzwa kwa wastani wa Sh2,000 inatarajiwa kushuka kufikia kadirio la Sh1,900 kwa lita. Takwimu hizo zinaashiria bei ya mafuta ya taa itaongezeka kutoka Sh1,500 kwa lita hadi kufikia Sh1,900 kwa lita, bei ambayo haitakuwa na tofauti na ile ya petroli na dizeli. Kwa mujibu wa Masebu, bei ya mafuta ya taa itakuwa chini zaidi ya ile ya dizeli kwa wastani wa Sh15 kwa litaMasebu alifafanua kuwa lengo la serikali la kupandisha kodi ya mafuta ya taa siyo kuwakomoa watumiaji wa bidhaa hiyo inayotumika kwa wingi, hasa maeneo ya vijijini wanapoishi Watanzania wengi na ambako hakuna umeme, bali ni kukabiliana na tatizo la uchakachuaji mafuta. Alisema tatizo kubwa la uchakachuaji lilikuwa likifanywa na wafanyabiashara kwa kuchanganya dizeli na mafuta ya taa, wakati huo serikali ikiwa inatoza kodi kidogo kwa bidhaa hiyo inayotumiwa na sehemu kubwa ya Watanzania ambao ni maskini."Kwa sasa bei ya mafuta ya taa haitatofautiana sana na ya dizeli," alisema Masebu akifafanua kuwa anatarajia bei ya mafuta ya taa itakuwa chini kidogo. Kulingana na utaratibu uliowekwa na Ewura, Masebu alisema punguzo hilo litafanyika kwa awamu mbili, Julai Mosi na Agosti Mosi, mwaka huu. Masebu alisema awamu ya kwanza itatokana na mafuta yanayouzwa nchini kushuka bei kulingana na kupunguzwa kwa kodi kwenye mafuta na awamu yapili itazingatia gharama za uagizaji mafuta wa pamoja. Mchakato wa kuelekea kwenye mkakati wa wafanyabiashara kuagiza mafuta kwa pamoja, utaanza Jumatatu ijayo na watachagua bodi ya usimamizi ya watu sita miongoni mwa wafanyabiashara.Masebu alisema bodi hiyo itashirikiana na serikali kupanga bei na kuchagua zabuni kwa wafanyabiashara watakaoonyesha uwezo wa kununua mafuta kwa pamoja. |