Watanzania kuendelea kuibeba sana ya Afrika ya Kusini ni ushamba uliopitiliza

Alwayz patriotism come first!you can't feed your neighbour while your kid is hungry.!
Muziki ni chakula ya hisia za mtu. Muziki mtamu ni muziki mtamu hata kama hujui mashairi yanayoimbwa. TheDreamer Thebeliever tatizo kubwa la muziki wa bongofleva kutopigwa kwenye clubs nyingi hasa za usiku na kwenye baadhi ya media kwa hapa nchini ni kwa sababu miziki ya bongofleva watalaamu wa muziki wanasema "haichezeshi". Yaani % nyingi miziki ya "bongofleva haimfanyi mtu kunyanyuka na kucheza muziki. Na mingi imejaa mashairi mengi na wakati mwingine kuna beti au baadhi ya vitendo kwenye video zinakerehesha au kutia aibu! Lakini kwa SA, miziki yake mingi ina midundo inayochezesha na kuburudisha sana, yaani ukisikiliza mwenyewe unanyanyuka kucheza au kujitingisha tu kwa raha zako. Lakini vile vile ni lazima tukubali kuwa SA wana wasanii wa muziki mzuri unaochezesha kwa muda mrefu sana tangu enzi hizo za makaburu. Kuna mwanamuziki mmoja kutoka SA kwa jina kimemsahau wa kike na alisema aliwahi kuishi hapa bongo na aliulizwa ni kwanini miziki ya bongo haipewi nafasi kwenye clubs za usiku za SA. Nakumbuka alijibu kwa kusema "miziki mingi ya bongofleva haina midundo inayochezesha mtu". Miziki yetu iko slow na mashairi mengi! Hits yaani yale mangoma ya club yanahitaji midundo na melody za kufa mtu ili kuamsha hisia za mtu kucheza muziki!

Hivyo basi ni jukumu la wasanii wetu wa muziki na wale kwenye fani zingine kama comedy, movies nk kuwa wabunifu na bidhaa wanazoingiza katika soko la ushindani. Huu ndio uzuri wa market economy yaani nguvu ya soko. "Kizuri cha jiuza na kibaya cha jitembeza".
 
Back
Top Bottom