Wengi mtakubaliana nami kuwa kwa sasa sio humu JF peke yake hata maofisini, nyumbani, vyuoni n.k. tumekuwa na ushabiki mwingi wa kisiasa na kutambiana kuwa chama flani kimeshinda bila kuangalia kimeshindaje na kinatupeleka wapi, mengiyamesemwa ya kweli na si ya kweli kuhusu vyama mbali mbali...sasa hivi tunacheka na kurelax, ila wakati utakapowadia tutalia na kusaga meno...hii nidhamu ya uoga tuliyo nayo ndo inayotufanya tukandamizwe na mfumo wa siasa uliopo madarakani. Simaanishi tuingie msituni, ila tuelimishane na kuhakikisha kuwa huu mfumo dhalimu unaondoka....Mi nshaanza kuchukua hatua kivyangu, soon mtanisikia nitakapolipuka. Nimechoka kuishi ka mkimbizi kwenye nchi yangu.