Watanzania huu mzimu umeanza kututafuna taratibu

Newbies

JF-Expert Member
Jul 13, 2018
1,476
2,147
images


Hujambo na karibu ndugu msomaji,
Leo sitaandika sana ili nisikuchoshe
Nitaeleza kwa ufupi sana lakini natamani sana unielewe.

Jisikie kuwa ni mwenye bahati kwa kupata kufunuliwa ufahamu huu kuwa Tanzania Tumevamiwa kuna mzimu unatunyemelea na kutumezea mate! Napengine bado kidogo tuu uanze kututafuna, na mbaya zaidi kuna watanzania wanajipeleka na kujisogeza karibu kabisa na mzimu huo wenye njaa Kali bila wenyewe kujua na pengine wewe ni mmoja wao.

Utani ni semi zenye lengo la kufurahisha na kupitisha muda, ajabu nikwamba utani unapozidi huwa ni uchokozi, na hutengeneza chuki ambazo ama kwa hakika madhara yake ni makubwa kuliko pengine wahusika wanavyo dhani. Kwa ujumla utani sio mbaya sana lakini huwa sumu pale unapoanza kuingia katika masuala nyeti ya kinasaba au kikabila, pale ambapo maandishi, maneno ama picha, au video kubeba dhana ya kutania, kudunisha, au mchoro wowote hasi juu ya kabila fulani, hii ni sumu ambayo inaweza kujenga chuki, kuvunja ushirikiano baina ya Jamii na Jamii, au Jamii ya watu Fulani kujiona duni kutokana na namna wanavyo chukuliwa na Jamii Nyingine. Na Mara nyingi katika hiki kizazi cha maendeleo ya TEHAMA.

Kama wewe ni mtumiaji mzuri Wa mitandao utakuwa umewahi kushuhudia picha, ama maneno au maudhui yeyote yanayo dhalilisha kabila au Jamii ya watu fulani, pengine uliichukulia poa, ukacheka ukafurahi, lakini napenda ufahamu Leo kuwa hii ni miongoni mwa masuala yanayo zusha uhasama, kuhasimiana kati ya Jamii na Jamii na inaweza kufika wakati ulee muunganiko wetu, ule uhusiano wetu, Yale maheshimiano yetu, na ule ukarimu wetu kati ya Jamii na jamii ukapotea kabisa nakubaki kuwa historia katika ardhi hii ya matumaini.

Katika karne hii hakuna haja yakulizungumzia kabila fulani kuwa nibora au kabila fulani ni washamba au hawa ni bora Bali tuzungumzie Utanzania wetu ili tuulinde ule muunganiko tuliojaaliwa

Inasikitisha katika karne hii ya maendeleo ya tehama mtu anathubutu kutamka oooh ofisi fulani wamejaa kina fulani ooo kabila fulani ni washamba Mara ooo kabila hili wanajigamba namengine mengi yakukera.

Sisi sote kabila letu ni watanzania tushirikiane, tuepushe chuki miongoni mwetu ili amani na ushirikiano uwepo na uendelee kuwepo baina yetu. FUTA DELATE KABISA , ujumbe, picha, video au matini yeyote yenye maudhui hasi juu ya kabila fulani.

Mwisho.
 
Hii ni hatari maana Kuna vikundi au vyama vya hayo makabila vimeshamiri Dar. Vikundi au vyama hivyo hudai kuwa ni wanaungana kwa ajili ya kusaidiana katika masuala ya kijamii. Kila mtu anajua kuna makabila makubwa hapa kwetu yana nguvu na hatari ninayoiona hapo mbeleni hivi vyama vikianza kujihusisha na masuala ya siasa vitaleta mkanganyiko na vyama vya siasa vilivyosajiliwa rasmi pamoja na Serikali. Tuwe makini kujigawa gawa mwisho wake ni mbaya zaidi
 
Kwa staili hii ya kuita 'vikundi' live kwa kutumia TEHAMA ktk mitandao, digital radio na online TV anamalizia hatua kwa hatua kuimaridha utawala wa kidiktekta bado imebaki kubadili katiba na kujitangaza Rais 'mpendwa na wote' wa maisha.

Maana kwa staili hii anajaribu kuonesha kwa watanzania baada ya kuliburuza Bunge linaonekana ni dhaifu, mdhibiti CAG asifanye kazi kwa uhuru,CCM ni dhaifu inabebwa na dola, kuminya vyama vya upinzani visifanye kazi ,mawaziri na wakuu wa mikoa ni dhaifu kilichobaki ni kuchukua vyeo vyote hivyo nakujitangaza Rais wa Maisha.

Hali hii siyo mpya ktk historia imewahi kutokea Venezuela ya Hugo Chavez / Maduro, Spain ya Jenerali Francisco Franco hivyo historia hii inashabiana na kinachotokea Tanzania ya awamu ya 5.
 
images


Hujambo na karibu ndugu msomaji,
Leo sitaandika sana ili nisikuchoshe
Nitaeleza kwa ufupi sana lakini natamani sana unielewe.

Jisikie kuwa ni mwenye bahati kwa kupata kufunuliwa ufahamu huu kuwa Tanzania Tumevamiwa kuna mzimu unatunyemelea na kutumezea mate! Napengine bado kidogo tuu uanze kututafuna, na mbaya zaidi kuna watanzania wanajipeleka na kujisogeza karibu kabisa na mzimu huo wenye njaa Kali bila wenyewe kujua na pengine wewe ni mmoja wao.

Utani ni semi zenye lengo la kufurahisha na kupitisha muda, ajabu nikwamba utani unapozidi huwa ni uchokozi, na hutengeneza chuki ambazo ama kwa hakika madhara yake ni makubwa kuliko pengine wahusika wanavyo dhani. Kwa ujumla utani sio mbaya sana lakini huwa sumu pale unapoanza kuingia katika masuala nyeti ya kinasaba au kikabila, pale ambapo maandishi, maneno ama picha, au video kubeba dhana ya kutania, kudunisha, au mchoro wowote hasi juu ya kabila fulani, hii ni sumu ambayo inaweza kujenga chuki, kuvunja ushirikiano baina ya Jamii na Jamii, au Jamii ya watu Fulani kujiona duni kutokana na namna wanavyo chukuliwa na Jamii Nyingine. Na Mara nyingi katika hiki kizazi cha maendeleo ya TEHAMA.

Kama wewe ni mtumiaji mzuri Wa mitandao utakuwa umewahi kushuhudia picha, ama maneno au maudhui yeyote yanayo dhalilisha kabila au Jamii ya watu fulani, pengine uliichukulia poa, ukacheka ukafurahi, lakini napenda ufahamu Leo kuwa hii ni miongoni mwa masuala yanayo zusha uhasama, kuhasimiana kati ya Jamii na Jamii na inaweza kufika wakati ulee muunganiko wetu, ule uhusiano wetu, Yale maheshimiano yetu, na ule ukarimu wetu kati ya Jamii na jamii ukapotea kabisa nakubaki kuwa historia katika ardhi hii ya matumaini.

Katika karne hii hakuna haja yakulizungumzia kabila fulani kuwa nibora au kabila fulani ni washamba au hawa ni bora Bali tuzungumzie Utanzania wetu ili tuulinde ule muunganiko tuliojaaliwa

Inasikitisha katika karne hii ya maendeleo ya tehama mtu anathubutu kutamka oooh ofisi fulani wamejaa kina fulani ooo kabila fulani ni washamba Mara ooo kabila hili wanajigamba namengine mengi yakukera.

Sisi sote kabila letu ni watanzania tushirikiane, tuepushe chuki miongoni mwetu ili amani na ushirikiano uwepo na uendelee kuwepo baina yetu. FUTA DELATE KABISA , ujumbe, picha, video au matini yeyote yenye maudhui hasi juu ya kabila fulani.

Mwisho.

MASHELE GASPER

Niandikie
info.masshele@gmail.com
Mzimu kaja nao kutoka alikotoka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Inasikitisha katika karne hii ya maendeleo ya tehama mtu anathubutu kutamka oooh ofisi fulani wamejaa kina fulani ooo kabila fulani ni washamba Mara ooo kabila hili wanajigamba namengine mengi yakukera.

Nakubaliana na hoja yako kuwa mambo ya kuzungumzia makabila ya watu mara nyinyi hayaleti umoja katika nchi. Amani tunayojivunia sisi hapa imejengwa kwa misingi ya USAWA katika nyanja zote na makabila rote na ndio maana toka enzi ya Mwalimu alikuwa anapiga vita sana upendeleo wa kikabila au dini.

Siku hzi inashangaza kuwa wananchi wameanza kuzungumzia ukabila wao na dini zao bila kificho; yote hayo yanatokana na viongozi wa nchi wa siku hizi kuwa mashabiki wakubwa wa ukabila kama inavyodhihilika katika teuzi mbali mbali za serikali ya awamu ya tano. Wananchi toka sehemu mbali na kanda ya ziwa wanaona kama vile wao ni wageni katika nchi yao jinsi wanavyotengwa. Sina haja ya kuthibitisha hili kwani liko wazi na wananchi wanalifahamu; kuwa wenye mamlaka wanauliza sehemu anayotoka mtu anayependekezwa kwa nafasi inayotakiwa kujazwa!!

Hivyo basi kama amani na mshikamano wa taifa hili tunataka udumishshwe viongozi hawana budi kuonesha kwa vitendo na sio maneno kuwa kweli wanachukia ubaguzi wa watu kwa makabila au dini zao; sio busara viongozi wanapohutubia hadhara kuwataka wananchi wanapotaka kuzungumza au wanapoombwa kutoa kero zao kuwauliza makabila au sehemu wanazotoka, kufanya hivyo ni kueneza tabia ya watu kujitambua kwa makabila yao [ sehemu watokako]na sio UTANZANIA wao!! Haya sio mambo ya utani kwani yanaweza kuliangamiza taifa. Viongozi ni kioo cha jamii hawana budi kuonesha mfano kwa yale wanayohuburi.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hii hali mwenyewe inanikela sana,zamani kukutakana na mtu akuulize ww Kabila gani ilikuwa Hakuna, ila sasa hivi nijambo la kawaida, siku hizi mpaka kwenye form kuna vipengele vya dini, kabila, nilichoka nilipofika hospitali, fom inasehemu ya kujaza kabila na dini,
Ukabila unarud tz kwa kasi,siku hiz mavikund ya makabila yameibuka, vyama vya Kikabila vimeibuka kwaminajili ya Kwamba tunasaidiana huku ugenini,wewe Mtanzania uko Tanzania uko ugenini gani,viashilia vya kurudi kwa udini na ukabila, ni
Mihadhara ya kidini
Vikund na vyama vya kikabila
Uwepo wa kipengele cha kujaza dini au kabila kwenye Form Za makazin, shule,matibabu,
Tuchukue hatua mapema Kabla HAJAKOMAA HII KITU
 
images


Hujambo na karibu ndugu msomaji,
Leo sitaandika sana ili nisikuchoshe
Nitaeleza kwa ufupi sana lakini natamani sana unielewe.

Jisikie kuwa ni mwenye bahati kwa kupata kufunuliwa ufahamu huu kuwa Tanzania Tumevamiwa kuna mzimu unatunyemelea na kutumezea mate! Napengine bado kidogo tuu uanze kututafuna, na mbaya zaidi kuna watanzania wanajipeleka na kujisogeza karibu kabisa na mzimu huo wenye njaa Kali bila wenyewe kujua na pengine wewe ni mmoja wao.

Utani ni semi zenye lengo la kufurahisha na kupitisha muda, ajabu nikwamba utani unapozidi huwa ni uchokozi, na hutengeneza chuki ambazo ama kwa hakika madhara yake ni makubwa kuliko pengine wahusika wanavyo dhani. Kwa ujumla utani sio mbaya sana lakini huwa sumu pale unapoanza kuingia katika masuala nyeti ya kinasaba au kikabila, pale ambapo maandishi, maneno ama picha, au video kubeba dhana ya kutania, kudunisha, au mchoro wowote hasi juu ya kabila fulani, hii ni sumu ambayo inaweza kujenga chuki, kuvunja ushirikiano baina ya Jamii na Jamii, au Jamii ya watu Fulani kujiona duni kutokana na namna wanavyo chukuliwa na Jamii Nyingine. Na Mara nyingi katika hiki kizazi cha maendeleo ya TEHAMA.

Kama wewe ni mtumiaji mzuri Wa mitandao utakuwa umewahi kushuhudia picha, ama maneno au maudhui yeyote yanayo dhalilisha kabila au Jamii ya watu fulani, pengine uliichukulia poa, ukacheka ukafurahi, lakini napenda ufahamu Leo kuwa hii ni miongoni mwa masuala yanayo zusha uhasama, kuhasimiana kati ya Jamii na Jamii na inaweza kufika wakati ulee muunganiko wetu, ule uhusiano wetu, Yale maheshimiano yetu, na ule ukarimu wetu kati ya Jamii na jamii ukapotea kabisa nakubaki kuwa historia katika ardhi hii ya matumaini.

Katika karne hii hakuna haja yakulizungumzia kabila fulani kuwa nibora au kabila fulani ni washamba au hawa ni bora Bali tuzungumzie Utanzania wetu ili tuulinde ule muunganiko tuliojaaliwa

Inasikitisha katika karne hii ya maendeleo ya tehama mtu anathubutu kutamka oooh ofisi fulani wamejaa kina fulani ooo kabila fulani ni washamba Mara ooo kabila hili wanajigamba namengine mengi yakukera.

Sisi sote kabila letu ni watanzania tushirikiane, tuepushe chuki miongoni mwetu ili amani na ushirikiano uwepo na uendelee kuwepo baina yetu. FUTA DELATE KABISA , ujumbe, picha, video au matini yeyote yenye maudhui hasi juu ya kabila fulani.

Mwisho.

MASHELE GASPER

Niandikie
info.masshele@gmail.com
Kuna changamoto kubwa huko tuendako
 
..mimi kinachoniudhi ni salamu za KIDINI ktk shughuli za SEREKALI.

..utamaduni huu aliuanzisha mwanasiasa mmoja wa Kusini, lakini umekuja kuota mizizi awamu hii.

..pia kuna kiongozi amekuja na tabia ya kuuliza makabila ya watu. Siyo mara moja amesikika akiuliza wewe ni wa mkoa fulani, au wewe kabila fulani.

..mambo ya utani wa makabila nayo yameanza kuibuka ktk shughuli za serekali. Miaka ya zamani utani wa kikabila ulikuwa kwenye misiba na harusi tu.
 
images


Hujambo na karibu ndugu msomaji,
Leo sitaandika sana ili nisikuchoshe
Nitaeleza kwa ufupi sana lakini natamani sana unielewe.

Jisikie kuwa ni mwenye bahati kwa kupata kufunuliwa ufahamu huu kuwa Tanzania Tumevamiwa kuna mzimu unatunyemelea na kutumezea mate! Napengine bado kidogo tuu uanze kututafuna, na mbaya zaidi kuna watanzania wanajipeleka na kujisogeza karibu kabisa na mzimu huo wenye njaa Kali bila wenyewe kujua na pengine wewe ni mmoja wao.

Utani ni semi zenye lengo la kufurahisha na kupitisha muda, ajabu nikwamba utani unapozidi huwa ni uchokozi, na hutengeneza chuki ambazo ama kwa hakika madhara yake ni makubwa kuliko pengine wahusika wanavyo dhani. Kwa ujumla utani sio mbaya sana lakini huwa sumu pale unapoanza kuingia katika masuala nyeti ya kinasaba au kikabila, pale ambapo maandishi, maneno ama picha, au video kubeba dhana ya kutania, kudunisha, au mchoro wowote hasi juu ya kabila fulani, hii ni sumu ambayo inaweza kujenga chuki, kuvunja ushirikiano baina ya Jamii na Jamii, au Jamii ya watu Fulani kujiona duni kutokana na namna wanavyo chukuliwa na Jamii Nyingine. Na Mara nyingi katika hiki kizazi cha maendeleo ya TEHAMA.

Kama wewe ni mtumiaji mzuri Wa mitandao utakuwa umewahi kushuhudia picha, ama maneno au maudhui yeyote yanayo dhalilisha kabila au Jamii ya watu fulani, pengine uliichukulia poa, ukacheka ukafurahi, lakini napenda ufahamu Leo kuwa hii ni miongoni mwa masuala yanayo zusha uhasama, kuhasimiana kati ya Jamii na Jamii na inaweza kufika wakati ulee muunganiko wetu, ule uhusiano wetu, Yale maheshimiano yetu, na ule ukarimu wetu kati ya Jamii na jamii ukapotea kabisa nakubaki kuwa historia katika ardhi hii ya matumaini.

Katika karne hii hakuna haja yakulizungumzia kabila fulani kuwa nibora au kabila fulani ni washamba au hawa ni bora Bali tuzungumzie Utanzania wetu ili tuulinde ule muunganiko tuliojaaliwa

Inasikitisha katika karne hii ya maendeleo ya tehama mtu anathubutu kutamka oooh ofisi fulani wamejaa kina fulani ooo kabila fulani ni washamba Mara ooo kabila hili wanajigamba namengine mengi yakukera.

Sisi sote kabila letu ni watanzania tushirikiane, tuepushe chuki miongoni mwetu ili amani na ushirikiano uwepo na uendelee kuwepo baina yetu. FUTA DELATE KABISA , ujumbe, picha, video au matini yeyote yenye maudhui hasi juu ya kabila fulani.

Mwisho.

MASHELE GASPER

Niandikie
info.masshele@gmail.com
"FUTA DELATE KABISA "sijaielewa hii kauli mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom