Watanzania hawana imani na Waziri wa Nishati January Makamba, anapaswa kuachia ngazi, asipoachia Rais amuondoe

Mkuu, umeelezea kwa uchungu na hisia kali kuhusu waziri mwenye dhamana kuwa ndiye pekee ambaye anapaswa kubebe zigo la lawama kuhusiana na matatizo ya kihistoria yanayoikabili TANESCO. Lakini nafikiri ni vyema pia hata ungetoa ushauri nini hasa kinapaswa akifanye.

Je! Ni vyema kulazimisha umeme upatikane kwa njia yoyote ile pasipo kujali ushauri na mazingatio ya kitaalamu? Ama la, ni vyema pia kuzingatia ushauri na mazingatio ya kitaalamu kwa kukata umeme kwa muda ili kutafuta suluhisho la kudumu?

Stitch in time saves nine! Waziri inampasa alipitishe Taifa katika njia sahihi bila ya kujali nani anasema nini na yupo wapi. Ni ukweli uliokuwa bayana kuwa hawezi kumridhisha kila mtu.
Huyo mwamba anataka kuendesha shirika kwa siasa kama awamu ile ambayo watu walifikia kugawana hela za michongo yani ESCROW! Umeme ulikuwa kero balaa kumbe ni juhudi za makusudi za watawala kutuangamiza.

Watanzania wa mwaka 2021 sio wale wa 2007 ambao unaweza kuwapiga sound za kishamba eti kuwa kiangazi ndio kimefanya umeme usiwe wa uhakika au service ya mitambo. Kinachofanya statement za utetezi huo ziwe ngumu ni vile JPM alipohakikisha umeme hauzimwi kipumbavu na kila ulipozimwa kulikuwa na sababu ya msingi! Kwa hizi kelele za sasa laiti kama hayati angekuwepo Waziri wa nishati angeshakuwa kapigwa chini!
 
Kila kona manug'uniko ya Watanzania ni juu ya dalili za wizara nyeti ya nishati na umeme kuwa na waziri ambae watu hawana imani nae. Tangu ateuliwe kuwa waziri basi taifa limekuwa na mauzauza tu juu ya upatikanaji wa umeme na hata uongozi na uendeshaji wa Tanesco.

Kitendo cha watanzania kutokuwa na imani na waziri huyu ni sababu tosha kabisa ya kujiuzulu au kuwajibishwa maana ni muda mfupi tu ameprove failure

Mtangukilizi wake Dkt Kalemani alisimamia vizuri Tanesco na kudhibiti ukatikaji hovyo wa umeme, pia aliwahakikishia watanzania kuwa mradi wa kuzalisha umeme wa JNHP utakuwa tayari ifikapo juni 2022.

Lakini tangu ateuliwe January Makamba kuwa waziri mradi wa JNHP umeanza kupata mauzauza, ujazaji maji kwenye mabwawa umechelewa kwa sababu zisizo za msingi, huku kukiwa na harufu ya ufisadi.

Nishati ya umeme ni muhimu sana kwa maendeleo ya taifa letu. Hii wizara haipaswi kuwa na waziri anayetiliwa shaka na umma kuwa mpiga madili.
Tz ya sasa hakuna kiongozi mzalendo wote ni wezi hivi unatengemea Makamba ajiuzulu au waziri wa kulimo pamoja nakuitwa nonsense hapa bila katiba mpya au sisi wana wa nchi hii kuchukua maamuzi magumu watafanya wanavyotaka kama alivyowahi kusema Kheri James cha kuwafanya hatuna
 
Mnawakumbuka waliobatizwa jina la Lumumba buku 7,
Naona kama kuna harufu ya Kalemani kuajiri vijana ili kuchafua hali ya hewa kwa mrithi wake,wapo wengi humu wanajikuta wametekwa na kuitikia mapambio kwa nyimbo wasizozijua,

Ni dhahiri kwamba kama unauwezo wa kuajiri vijana 20 humu mitandaoni wanatosha kabisa kuchafua hali ya hewa nchi nzima.

Plz kalemani pumzika kwa amani fanya mambo mengine tambua hujazaliwa uwe waziri wa nishati.
 
Usiwe kama mkoonduw wewe jamaa! Bwawa linajengwa na sehemu ya kuhifadhia maji ili kusudi kipindi cha kiangazi flow iendelee kuwepo!

Umeme wa maji ndio umeme wa bei nafuu kama hujui sasa ni natural source of energy isio na madhara yeyote kwa jamii na mazingira kwa ujumla.

Kuhusu madhara miti inayokatwa Iringa kwa kuchana mbao kwa mwaka ni Mingi kuliko hio iliokatwa huko kwenye mradi wa JNHPP. Kwa eneo lililojengwa mradi limetumika almost 5% tu na 95% imebaki bila kuathiriwa! Sasa unaposema kiangazi kimesababisha na kukatwa miti 3000 unakuwa hueleweki na wakati mvua zinanyesha tayari!
Mkuu kunamajitu ya kiitwa NONSENSE ni kawaida kabisa
 
Moja, umeme umeanza kukatika baada ya Makamba kuingia madarakani. Hiyo ni rebuttable presumption kwamba tatizo ni yeye.

Mbili, hajui, hajatulia akaisoma TANESCO, ama hasemi ukweli kuhusu kiini cha matatizo ya TANESCO. Alisema sababu za kukatika kwa umeme ni kukosekana kwa ukarabati wa mitambo, siku tatu baadae tukaambiwa tatizo ni mabadiliko ya tabia nchi. Wiki moja baadae bosi wake akasema tatizo ni ng'ombe za wasukuma na binadamu wakaidi. Wiki moja baadae tukaambiwa tabia nchi imetengemaa, mabwawa yamekaa sawa. Jana Dar es Salaam maji yamekatika kutwa. The leadership is clueless.

Tatu, hajui ama ali underestimate majukumu yake: alisema kama Waziri hataki kupelekewa matatizo ya umeme kwa sababu hataki TANESCO iingiliwe na wanasiasa. Siku hizi anazunguka kwenye mabwawa na karakana za TANESCO.

Nne, anafanya mzaha na teuzi za watendaji. Kamweka Mkurugenzi rafiki yake ambae hana background ya kumwezesha kuendesha taasisi ya kibiashara kubwa kuliko zote nchini. CEO wa Makamba, Chande Maharage, kasema kiini cha tatizo la TANESCO ni wafanyakazi kutolipwa kutokana na utendaji. Toka lini mshahara wa mtumishi wa umma ukabadilika kila mwezi based on performance ?

Tano, ni mzembe, anatupa excuses za hovyo na za kitoto kila wanaposhindwa kusimamia miradi. Makamba kasema Nyerere Hydropower haitakamilika kwa wakati kwa sababu vyuma ni vizito na crane hatuna. Atulie akasome mikataba kwanza, project planning ya contractor inasemaje, walikubaliana watatumia nini kubeba nondo za ujenzi, vichwa vya waponda zege ?

January Makamba does not know which end is up at Ministry of Energy. His boss is just as clueless, and Makamba knows the boss is a lightweight.
Makamba ione hii kwenye faili lakie.hakika umeeleza vyema sana na juzi kaingia mkataba wa 30USD kwa kufunga tu software ya kawaida ambayo wataalam wtu wanaweza kuifanya .alipo maliza akakimbilia tweeter kwenda kutweent kwa mbwembewe kama vile hiyo software ni suluhisho la msingi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi watu hawaoni ya kuwa January na uongozi mpya wa Wizara ya Nishati pamoja na TANESCO wapo katika nafasi walizo kuwanazo kwa muda mfupi uliopita! Katika kipindi kama hicho ni lazima tuwe wavumilivu na wapewe muda ili kuweka mambo sawa.

Unapo kabidhiwa uongozi wa wizara kubwa na nyeti kama hiyo ya nishati, ni vyema kiongozi mpya akajifunza kwanza kuhusu mambo ya "efficiency & productivity" ya mfumo alioukuta, nafikiri hiki ni kitu ambacho January amekuwa akikifanya. Pia anapaswa kufanya mabadiliko kwa tahadhari kubwa ili kuleta matokeo lengwa.

January aliukuta mfumo ambao unaendeshwa tu kwa amri tu za kisiasa bila kujali "technical environment" ili watu wapate umeme. Mfumo alioukuta haukujali kabisa kuhusu athari hasi na za muda mrefu kwa mitambo iliyolazimishwa kuendelea na uzalishaji pasipo kuzingatia tahadhari za kitaalamu.

Ni lazima kijana apewe "benefit of doubt" ili apate kutimiza yale aliyoyakusudia kuyafanya na timu yake. Hapo alipo yupo kwenye mipango ya muda mfupi, yaani STP ambayo matokeo ya ni magumu kuyaona. Isipokuwa akiingia katika MTP na hatimaye LTP watu ndipo wanaweza kumpa stahiki yake ya pongezi ama lawama.
Napata wakati mgumu kuamini kinachosemwa kuendesha mitambo bila kujali maintenance. Kwangu naona ni kichaka cha watu kujifichia. Kwani mwendazake angetawala miaka 10 mgao ungekuepo? Hao wanaosema walikuo wakiogopa utawala wangemuaminisha vipi kwamba hawakufanya maintenance bali waliendelea kuzalisha umeme kuepusha mgao? Salama yao ingekuaje mitambo ingeharibika?

Namnukuu mzee kikwete " Zakuambiwa changanya na zako "
 
Sina uhakika kama huyu bingwa anajua anachofanya na ninaanza kuamini anahusika kutopatikana kwa umeme, atueleze ukweli sio story za magufuli alikataza maintenance au hakuna crane ya kufanyia kazi
Hapo kwenye crain ndio kuna uozo kabisa. Huyo aliyepewa hiyo kazi alitarajia aifanyeje? Bila aibu waziri anatetea ujinga.
 
Naona mnaanzisha nyuzi kibao za January Makamba kwa Nchi ya Tanzania yenye msururu wa kodi kwenye bidhaa zetu toka enzi na enzi mnamzungumzia Makamba wa leo.

Kwenye magari huko kuna kodi utadhani Wananchi wanaleta ndege bado wakileta hayo magari yaliyotumika kutoka Japan wanakutana na Ewura kuwapandishia bei kila mwezi...Zambia mafuta yapo bei nafuu kuliko Tanzania nadhani tumerogwa sio bure.
Nenda kahamie Zambia.
 
Kwa hiyo kwa akili yako huu umeme tunaotumia unatoka Stiglers Gorge kule DIKTETA MAgufuli alikokata miti Milioni 26 yenye ukubwa DSM?

Kwa taarifa yako 60% ya umeme wa national grid unazakishwa Kinywrezi 1& 2 kwa gesi ya Mtwara aliyokuwa anaiponda Mwendazake
Huna akili.
 
Tushushieni bei ya petrol kwani si mlisema January bei ingeshuka mbona badoooooo......
Mkasema mmeongea na wauza mafuta wenyewe mbona badoooooo......
Serikali tusaidieeee..... We can't breath Mrs.government!!!!!!
 
Katika mitandao ya kijamii waziri makamba ameonekana kutotisha katika wizara hiyo mara nyingi malalamiko yamekuwa mengi jinsi anavyoondesha wizara yake ilianza bwala la nyerere visingizio kuhusu ujazaji wa maji vilikuwa vingi hadi sasa bwawa hilo halijakamilika na maradi unasuasua , tozo ya tsh100/= hiyo ilifutwa na waziri huyo ndiye aliyesema raisi kamtuma kutekeleza na baadae raisi mwenyewe amerudisha tozo hiyo na huku ikisemekana kwamba sheria ya kupitisha tozo hiyo ilipitishwa na bunge ambazo fedha hizo zingeenda kufanya shughuli za serikali. Makamba tayari inasemekana kwamba alikodi software kutoka india $30milion hadi sasa hatujajuwa ukodishwaji huo unaisha lini na nini kilichopelekea kukodi software hiyo.

Aidha kinachoshangaza zaidi amejikita kwenye miradi ya gesi LNG huku miradi mingine kama bwawa la umeme mradi huo ukisusua .kufanya MHESHIMIWA RAISI KUKAA KIMYA KWA JAMBO HILO INAONESHA KUWA WAZIRI HUYO HAGUSIKI NA TAYARI KUNA MANENO KUTOKA KWENYE MEDIA MBALIMBALI ZIKISEMA KWAMBA KIJANA HUYO NA KUNDI LAO NDIO WATAKAOMPIGANIA RAISI 2025 KURUDI MADARAKANI NDIYO SABABU RAISI HASEMI CHOCHOTE KUHUSU WAZIRI HUYO.

Binafsi natoa ushauri kuwa raisi anawajibu wakuamua yeye mwenyewe bila kulazimishwa na mtu nink afanye kwa kelele zinazoandama wizara hiyo anayoiongoza january makamba kwani makamba hawezi kuamua mawazo ya watanzania milion 60.
 
Back
Top Bottom