changamoto
Member
- Aug 26, 2008
- 11
- 0
NIA na shabaha ya mada hii ya Watanzania na Kiswahili ni kujaribu kufufua mada yangu ya awali wakati nikiwa mwandishi wa habari juu ya umuhimu wa Kiswahili katika kuleta maendeleo ya kweli ya watu na nchi yetu.
Kwanza, tutambue kuwa lugha ni roho ya taifa. Na nchi yoyote inayotumia lugha ya Kigeni ni kwamba haina roho. Haina tofauti na msukule ambaye kwa kawaida hana itihari katika kuamua au kufanya jambo lolote wakati wa uhai wake ambao sio uhai bali ni umauti unaotembea na kuhudumia wengine lakini sio kujihudumia mwenyewe.
Ninadhani nipange mada yangu katika sehemu zifuatazo:
. Historia ya Kiswahili kabla ya Uhuru
. Historia ya Kiswahili baada ya Uhuru na kabla ya Kufariki kwa baba wa Taifa.
. Historia ya Kiswahili toka Mwinyi hadi Kikwete.
. Ni nini faida za kuwa na Kiswahili kama lugha ya Kufundishia toka Msingi hadi sekondari
. Nchi ngapi za Kiafrika zinazotumia Kiingereza au Kiswahili zilizoendelea?
. Japan, China, India, Sweden, Denmark, Norway wanatumia lugha gani?
. Tanzania kama nchi inayoua lugha zake za asili-kikiwemo Kiswahili
. Utamaduni wa Kitanzania unavyopotea kwa mauaji hayo ya lugha
. Nafasi ya Kiswahili katika shule za msingi
. Kiswahili katika sekondari-majaribio yanayopigwa vita
. Kiswahili vyuoni
. Uchumi na Kiswahili
. Menejimenti na Kiswahili
. Sheria na Kiswahili
. Jiografia na Historia kutofundishika kwa Kiswahili
. Sayansi, ufundi na teknlojia kwa Kiswahili
. Lugha sasa sio Kiingereza ili kina Asha Rose Migiro wawe wengi....
. Mikakati ya Maendeleo ya Kweli na ya Uhakika tokana na Kiswahili
. Sio wote katika jamii wanaweza kuwa na uwezo wa lugha za Kigeni au hata lugha yao wenyewe
. Maendeleo ya Lugha zingine sanjari na Kiswahili
. Uendelezaji Istilahi kwa somo na jinsi kunavyoweza kuandikwa kwa vitabu vya masomo ya aina yote.
MATUMAINI yangu ni kuwa baada ya majadiliano mapana na ya kina tutaweza kuchapisha kijitabu tutakachowazawadia viongozi wetu wote na hasa Wabunge ambao kwa sababu moja au nyingine wameonesha udhaifu mkubwa katika kupigania lugha ya Kiswahili kuwa lugha ya kufundishia ili kasi ya maendeleo yetu iweze kukua kwa haraka zaidi.
NITAFURAHI kupata zaidi hoja za kupinga Kiswahili kuwa lugha ya kufundishia ili niweze kuandika kile kilicho bora zaidi. Kama una sifa basi wasifie wengine lakini sio mimi!
Kwanza, tutambue kuwa lugha ni roho ya taifa. Na nchi yoyote inayotumia lugha ya Kigeni ni kwamba haina roho. Haina tofauti na msukule ambaye kwa kawaida hana itihari katika kuamua au kufanya jambo lolote wakati wa uhai wake ambao sio uhai bali ni umauti unaotembea na kuhudumia wengine lakini sio kujihudumia mwenyewe.
Ninadhani nipange mada yangu katika sehemu zifuatazo:
. Historia ya Kiswahili kabla ya Uhuru
. Historia ya Kiswahili baada ya Uhuru na kabla ya Kufariki kwa baba wa Taifa.
. Historia ya Kiswahili toka Mwinyi hadi Kikwete.
. Ni nini faida za kuwa na Kiswahili kama lugha ya Kufundishia toka Msingi hadi sekondari
. Nchi ngapi za Kiafrika zinazotumia Kiingereza au Kiswahili zilizoendelea?
. Japan, China, India, Sweden, Denmark, Norway wanatumia lugha gani?
. Tanzania kama nchi inayoua lugha zake za asili-kikiwemo Kiswahili
. Utamaduni wa Kitanzania unavyopotea kwa mauaji hayo ya lugha
. Nafasi ya Kiswahili katika shule za msingi
. Kiswahili katika sekondari-majaribio yanayopigwa vita
. Kiswahili vyuoni
. Uchumi na Kiswahili
. Menejimenti na Kiswahili
. Sheria na Kiswahili
. Jiografia na Historia kutofundishika kwa Kiswahili
. Sayansi, ufundi na teknlojia kwa Kiswahili
. Lugha sasa sio Kiingereza ili kina Asha Rose Migiro wawe wengi....
. Mikakati ya Maendeleo ya Kweli na ya Uhakika tokana na Kiswahili
. Sio wote katika jamii wanaweza kuwa na uwezo wa lugha za Kigeni au hata lugha yao wenyewe
. Maendeleo ya Lugha zingine sanjari na Kiswahili
. Uendelezaji Istilahi kwa somo na jinsi kunavyoweza kuandikwa kwa vitabu vya masomo ya aina yote.
MATUMAINI yangu ni kuwa baada ya majadiliano mapana na ya kina tutaweza kuchapisha kijitabu tutakachowazawadia viongozi wetu wote na hasa Wabunge ambao kwa sababu moja au nyingine wameonesha udhaifu mkubwa katika kupigania lugha ya Kiswahili kuwa lugha ya kufundishia ili kasi ya maendeleo yetu iweze kukua kwa haraka zaidi.
NITAFURAHI kupata zaidi hoja za kupinga Kiswahili kuwa lugha ya kufundishia ili niweze kuandika kile kilicho bora zaidi. Kama una sifa basi wasifie wengine lakini sio mimi!