FrediusSnowden
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 269
- 224
Habari za asubuhi wakuu. Natumaini kwamba mko salama kabisa. Ni jambo la heri sana kwake Mungu kwetu sisi wanawe. Basi kwa kuanza niwapongeze wote kwa kuadhimisha kumbukizi ya Mwl J.K. Nyerere alifariki mnamo mwaka 1999, mwezi wa kumi tarehe 14. Ni wazi kwamba Mwl J.K. Nyerere ni ICON kwa viongozi wengi na pia ameleta heshima ya kipekee kwa taifa letu hili kongwe kiumri changa kimaendeleo.
Katika pitia zangu katika mitandao ya kijamii kuona ni namna gani viongozi kiserikali wanamuenzi Mwl J.K. Nyerere, ndipo nilipo pata mshangao wangu na kufanya kichwa kufikiri kisha kuandika uzi huu.(kama wewe ni kiongozi naomba tulia, na kisha yaa he hapa).
Maswali ni kama yafuatayo..
1. Kwanini siku ya kumuenzi Mwalimu Nyerere iingiliane na shughuli za mwenge?
2. Mwalimu alikuwa ni kiongozi wa iliyokuwa Jamhuri ya Tanganyika, kwanini maadhimisho haya hayajafanyika Tanganyika (Tanzania Bara)?
3. Kwanini shughuli hii haikunakishiwa na mabango jumbe na picha za Mwalimu Nyerere?
4. Kwanini hapakuwa na mijadala mikubwa juu ya kumbukizi hili?
5. Kwanini mashati ya vitenge ya mwenge zaidi kuliko mashati ya vitenge ya mwalimu?
6. Kwanini kuingiza siasa na shughuli za chama katika shughuli za kitaifa kubwa kama hizi?
7. Kwanini kupanga makusudi mwingiano mkali kama huu wa tarehe za hii shughuli na masuala ya mbio za mwenge?
8. Kwanini kutokutaka mualiko wowote katika shughuli za maadhimisho hayo?
9. Kwanini sisi kama watanzania tuko kimya katika hili;au ni bumbuwazi la sintofahamu fahamu?
10. Kwanini kwanini ziko nyingi?
Basi niishie hapo. Taarifa ni kwamba shemeji yenu kajiunga baada ya pilikapilika nyingi za hapa na pale. Tulipima mkojo na nk mambo sasa mswano. Nawafikishia salamu zake kwenu. Ni mapacha? Tutajuzana.
Katika pitia zangu katika mitandao ya kijamii kuona ni namna gani viongozi kiserikali wanamuenzi Mwl J.K. Nyerere, ndipo nilipo pata mshangao wangu na kufanya kichwa kufikiri kisha kuandika uzi huu.(kama wewe ni kiongozi naomba tulia, na kisha yaa he hapa).
Maswali ni kama yafuatayo..
1. Kwanini siku ya kumuenzi Mwalimu Nyerere iingiliane na shughuli za mwenge?
2. Mwalimu alikuwa ni kiongozi wa iliyokuwa Jamhuri ya Tanganyika, kwanini maadhimisho haya hayajafanyika Tanganyika (Tanzania Bara)?
3. Kwanini shughuli hii haikunakishiwa na mabango jumbe na picha za Mwalimu Nyerere?
4. Kwanini hapakuwa na mijadala mikubwa juu ya kumbukizi hili?
5. Kwanini mashati ya vitenge ya mwenge zaidi kuliko mashati ya vitenge ya mwalimu?
6. Kwanini kuingiza siasa na shughuli za chama katika shughuli za kitaifa kubwa kama hizi?
7. Kwanini kupanga makusudi mwingiano mkali kama huu wa tarehe za hii shughuli na masuala ya mbio za mwenge?
8. Kwanini kutokutaka mualiko wowote katika shughuli za maadhimisho hayo?
9. Kwanini sisi kama watanzania tuko kimya katika hili;au ni bumbuwazi la sintofahamu fahamu?
10. Kwanini kwanini ziko nyingi?
Basi niishie hapo. Taarifa ni kwamba shemeji yenu kajiunga baada ya pilikapilika nyingi za hapa na pale. Tulipima mkojo na nk mambo sasa mswano. Nawafikishia salamu zake kwenu. Ni mapacha? Tutajuzana.