Watanzania amkeni

Novatus

JF-Expert Member
Jul 28, 2007
330
37
Napenda kuwajulisha kuwa kizazi kipya kimeamka kinataka mabadiliko. Anzia kwenye kura za maoni za CCM vijana ndio waliowabwaga vikongwe, Ukija sasa kwenye uchaguzi wenyewe wote mmshuhudia vijana wakivyofanya. wengi wa wabunge wateule wa Chadema ni vijana.

hii ni nguvu ya umma. Na nimwanzo tu. CCM walilewa madaraka hadi wabunge kujitangazia kuwa mjimbo ni mali yao. wakadiriki kuwaita wenzao wanaotaka kugombea mavuvuzela. wengi tumeshuhudia pesa zilivyotumika ili kushinda bahati nzuri vijana wameamka wamefanya kweli kuwa fedha ni adui ya haki. vijana wa chadema hawakuwa na pesa ila wamepita katika sehemu ambazo watanzania wameamka kwa sasa liwe fundisho kwa wengine waache kupokea shs 2000 na kanga ili kuendelea kututesa na mafisadi.
 
Naskia hadi JK ni kijana!!
Akina Makamba wanamwita 'rais kijana'
Na huu ndio ujinga mwingine wa watanzania. Kiongozi mmoja wa sisi m aliwahi kuitisha kikao cha vijana katika jimbo lake na akanitaka na mimi mzee nihudhulie. Nikamuuliza mimi ni kijana? akasema katika chama chao wazee mara nyingine uitwa vijana.
 
Back
Top Bottom