Watanzania amkeni, CCM inataka kujadili matukio na siyo record zao

politiki

JF-Expert Member
Sep 2, 2010
2,376
1,507
Jana niliandika kuwa ni chadema isipoangalia itakuwa inacheza ngoma ya CCM kwa maana ya kujadili matukio na issues kwa sababu ccm
haitaki kujadili issues kwa sababu hawana cha kujadili when it comes to kitchen table issues kwa maana ya maji, umeme, sukari, ajira na
ugumu wa maisha
kwa ujumla kwa sababu ni vigumu kuwadanganya watu maeneo hayo kwa sababu wenyewe wanajionea.

kama ilivyotabiriwa jana ile NGOMA YAO INAENDELEA LEO HII KWA TUKIO LA GARI chadema, watu na media inaacha kujadili issues
inajadili tukio kitu ambacho CCM ndio ingependa wapiga kura, chadema na media ndio vijadili na kuacha issues.

kwanini ccm inafanya hivi ?
kwa sababu hawataki record zao zijadiliwe na wataendelea KU STAGE MATUKIO ili watu waache kujadili issues wajadili matukio na bado
wataendelea na matukio haya hata watafikia kuuwa mtu/watu kwa ajili ya kiti cha ubunge ndio mafunzo waliyokuwa wakiwapa vijana wao
huko singida ukiona mpinzani wako anakushinda basi mpaka mavi (samahani kwa lugha hii) ile aonekane hafai/mbaya na wewe uonekane una nafuu upite pamoja na ubaya wako wote.
inawezekanaje mbunge na ccm wapange gari lao livunjwe kioo ?

Gari hilo ni la kwake la ubunge kwa maana linalipiwa kila kitu na serikali kuanzia mafuta mpaka matairi yakiisha na hicho kioo hatotoa hata
senti ntano yake nyekundu pesa yote italipwa na bunge why not sacrifice the side shield to gain sympathy from the people in order to
win the paliamentary seat afterall we have nothing to loss when it comes to paying for the damage.

Chadema nini wafanye ?
waendelee kuzungumzia issues zinazowagusa wana igunga na kuwaeleimisha wananchi kuwa CCM imeishiwa na matukio haya wasiyashangae ni mbinu mojawapo ya ccm kutaka huruma ya wananchi na muwaambie watarajie matukio mengine zaidi kutoka kwa ccm baada ya kuelezea record yao ya miaka 50 hapa Igunga ambayo imewaletea wananchi ufukura na umaskini wa kutupwa..
 
Wewe mtoa mada, naomba nikukumbushe nukuu hizi za wanafalsafa wa enzi hizooooo!!!!! Ndipo utakapogundua CCM wanajua wanachofanya, wala usiwadharau kiasi hicho. Angalia kama wanafanikiwa au hawafanikiwi kufikia malengo yao;
  • Political campaigns are designedly made into emotional orgies which endeavor to distract attention from the real issues involved, and they actually paralyze what slight powers of cerebration man can normally muster. ~James Harvey Robinson, The Human Comedy, 1937
  • Politics are almost as exciting as war, and quite as dangerous. In war you can only be killed once, but in politics many times. ~Winston Churchil
  • Politics is the gentle art of getting votes from the poor and campaign funds from the rich, by promising to protect each from the other. ~Oscar Ameringer
 
Jasiri haachi asili yake. Unawataka Chadema waache fujo na huo ni mitaji wao itawezekana? Chadema na fujo ni synonimous!
 
Ninakubaliana nawe kwa asilimia mia moja Politiki. Kushindwa kwa hoja za Msingi kunawapelekea CCM kutafuta huruma. Na wanapanga kila kitu ili waipate hiyo huruma kama sio kuonesha kuwa Chadema hawafai.

Watamtuma Mkuu wa Wilaya afanye upuuzi wa dhahiri kuwa-provoke Chadema, Watamwagiana tindikali ili ionekane chadema ni wabaya, watafanya mengi. Kimsingi hawana hoja, kwakuwa hoja zote, kama ulivyosema zinayeyushwa na ukweli wa rekodi yao.

Mfano Mzuri ni tukio la juzi la kuzama Meli. Kikwete badala ya kuzungumzia nini serikali imekosea kiasi ajali mbaya zinaendelea kutokea na namna akachofanya kuondosha hayo kabisa, anafanya kazi ya kusifu watu waliookoa watu.

Katika hali ya kawaida, kila aliye na uwezo akiona mwenziye anaangamia atamuokoa. Atakayeshindwa kufanya hivyo labda hana uwezo huo. Haihitajiki fadhira ya pongezi ili tuendelee kuokoa wale waliopata majanga. Kwakuwa hakuna cha kusema, ni lazima kusema hata ambayo labda si muhimu sana!
 
Na simba akitaka kummaliza swala au kiumbe yeyote anayemla anamkaba kwenye ule mshipa mkuu wa damu wa shingoni (jugular vein); na Chadema wakitaka kuimaliza CCM ni kushambulia records mbovu za kiutendaji zilizoifanya Igunga kuwa mojawapo ya Wilaya maskini nchini. Na kuonyesha kwa mifano halisi kwamba umaskinii na UCCM ni vitu sambamba, kama kunguni anavyopenda uchafu.
 
Na simba akitaka kummaliza swala au kiumbe yeyote anayemla anamkaba kwenye ule mshipa mkuu wa damu wa shingoni (jugular vein); na Chadema wakitaka kuimaliza CCM ni kushambulia records mbovu za kiutendaji zilizoifanya Igunga kuwa mojawapo ya Wilaya maskini nchini. Na kuonyesha kwa mifano halisi kwamba umaskinii na UCCM ni vitu sambamba, kama kunguni anavyopenda uchafu.

Unajua mimi nashangaa kitu kimoja. CCM wanasimamia ooh! vurugu, oh! uvunjifu wa Amani.... etc, hata hayo matukio wanayoonyesha hayana mvuto sio kwa watu wenye akili timamu bali hata kwa wale waliozoea kuwalaghai huko vijijini. Uzuri ni kuwa hakuna mwananchi wa kawaida aliyewahi kufanyiwa hizo vurugu au fujo wanazosema CCM. Wananchi wameendelea na shughuli zao kama kawaida, na CDM wameendelea kuonyesha nia ya dhati ya kuwaletea mapinduzi sio tu ya kisiasa bali pia Kiuchumi.

Laiti kama CDM wangekuwa wanapita kuwasumbua wananchi kama wafanyavyo CCM then tungesema kuwa CCM wana strategy ya ushindi, lakini kinyume chake CCM ndio wanawasumbua wananchi hasa kwa kupitia kwa watendaji wao kama Wajumbe wa nyumba kumi na wakuu wa mikoa. CDM wamekuwa na mikutano yao mingi bila hata polisi na hakujawahi kutokea case ya mtu kuumizwa, kuporwa au vyovyote vile, so kwa CCM kutafuta huruma wana address segment ambayo ina access na vyombo vya habari na wala arguments zao haziwezi kuwafikia wananchi wanaopata matatizo huko vijijini.

Kwa mtazamo wangu naona CCM wanapoteza Muda, na CDM wao waendelee kuwa makini na kutoruhusu hila za CCM kuingia kwenye taratibu za chama chao. Hizi mbinu za CCM zimeshindwa huko Pemba, na hata huku Bara tumeona uchaguzi uliopita walifanya vurugu mtu akafa huko Maswa, na Shibuda kuwekwa ndani, kuzuiwa kufanya campain lakini mwishowe walishindwa.

Kama CDM wakisimamia vizuri upigaji, uhesabuji na utangazaji (kama ilivyokuwa Mwanza, Arusha & Ubungo) basi hizo campain za matukio zitakuwa ni kwa ajili ya biashara ya wenye vyombo vya habari tu.
 
Mada nyingi nzuri za kujadidili kuhusu maisha, maendeleo, uchumi, siasa nk, watu hawapendi kujadili. Kwenye matukio na watu ndio kuchangia kumeshamiri na wanachangamkia hii imekaaje?

Sina maana ya kuwadhalilisha wanaJF, bali ni ukweli, kwani tunaonekana wengi kuangukia kwenye category ya pili ya matukio na category ya kwanza ya kuhusu watu, lakini la kuhusu category ya tatu kujenga maisha maisha na maendeleo tunapiga kikumbo jambo ambalo lingesaidia kutufungua zaidi akili katika kukabiliana na maisha iwe kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni nk. Ukileta mada ya kufikirisha hakuna wachangiaji, lakini mada ya matukio na kujadili watu ina wafuasi wengi hapa sijajua kwani nafahamu wadau wengi wa JF ni wasomi.
 
'ashakyum sio matusi naomba nisamehewe kama nitakua nimekosea' mimi sio mwandishi wa habari na sina utaakamu huo,nisamehewe tena kama nitakua nimekosea hebu tutafakari haya kidogo;
1.Wantanzania wenzangu mimi naumia sana kwa jinsi ambavyo mambo yanavyokua kwa sababu tunasukumwa na matukio zaidi kuliko uhalisia wa mambo yenyewe,kuna matukio mengi sana yametokea yakatikisa nchi na baadae yakapita,tumeyasahau na hatuna mpango wa kuyafanyia kazi tena.
MFANO:
1.suala la EPA tunakumbuka lilitingisha nchi kila mtu akawa attention kufuatilia lakini wapi , Anne Kilango aliapa nakusema zisipo rudi hapatatosha ! je kuna mwenye uhakika kuwa zulirudi? kama zilirudi ni kiasi gani na nani na zimefanyiwa nini?
2.RICHMOND,nani hakulifahamu hili mpaka mawaziri kujiuzuru na baraza la mawaziri kuvunjika nini matokeo yake?
3.DOWAN,huyu ni ndugu wa RICHMOND hakijaeleweka kama wamelipwa au hapana hakuna ajuaye sio mwakyembe wala sitta
4.UCHAKACHUAJI wa matokeo ya uchaguzi mkuu.
5.Suala la JAIRO (jairo scandal) nini hatima yake.
6.Wizi mkubwa na wa kiajabu wa T WIGA
7.NOTI mpya zisizo na ubora
8.MAJENGO pacha ya B. O .T kesi inayomhusu LIYUMBA
9.Mgogoro wa kwanza na huu wa sasa nao utapita.
10.Zanzibar na suala la muungano
11.Nyumba za serikali kuuzwa bei chee
ni hayo ni niliyoyakumbuka nini hatima yake jamani ?
Kama hatutafuatilia jambo moja hadi na jingine ili tupate suluhisho sahihi itakua imekula kwetu.....nawasilisha.
 
kisingi kutofuatilia kwetu kunafanya wanaotenda kufanya yaleyale wakijua udhaifu wa watz
 
Ukitafakari kwa kina jamii ya wa-tz tumekuwa kama mashabiki hivi. Linatokea tukio kubwa la kitaifa, linaandikwa sana na kujadiliwa sana mitaani, ghafla linatokea jingine, lile la kwanza kabla hatujajua hatma yake linasahaulika kabla hata ya kujua hatma yake. Nadhani tunapaswa kuwa makini zaidi. NASHAURI TUANZE HAPA Jf, KUWE NA PAGE YA KU-ANALYSE YALIYOTOKEA KWA MWEZI & THEN KWA MWAKA. Kwa kila tukio kuwe na updates issue yenyewe imefikia wapi.
 
Anzisha huo utaratibu kwa kuandika thread kila mwezi kukumbushia na kuulizia hatma ya matukio ya wiki!
 
Tatizo hata tukitunza kumbukumbu hakuna wa kumfunga paka kengere.Watawala a.k.a Viongozi hawawajibiki hata kwa mambo madogo yaliyo chini ya uwezo wao.
 
Wana JF hii ni hatari kwa matarajio na ndoto za kutokomeza vitendo vya kinyama na ubadhilifu hapa nchini. Kuna mambo mengi sana ya unyanyasaji,ufisadi,ubadhilifu na usultan hapa nchini. Hii inajirudia kwa watanzania kila linapotokea jambo moja tunalipigia kelele kwa muda mfupi na kulitupilia mbali hata kama halijarekebishwa.

Ilipotokea ubadhilifu na mikataba ya ulaghai ktk shirika la umeme na kampuni ya Richmond,ikaja, epa,dowansi na mingine mingi tulipiga kelele na kuacha bila hata kutatua tatizo,ikaja mawaziri kula rushwa mf wizara ya utalii,wizara ya nishati na madini,wizara ya fedha na wizara nyingine tumenyamaza huku watuhumiwa wakiishia kuachia ngazi bila kufilisiwa. Haya vikaja vitendo vya kinyama dhidi ya binadam kwa watu kuuawa,mf mauaji ya igunga,ruvuma,singida,arusha,dr Ulimboka, Ally zona, na Mwangosi.

Tumekuwa maarufu kwa kupiga kelele jamvini bila kuchukua hatua stahiki ili kuinusuru Tanzania kwa vitendo hivi haramu. Wito kwa watanzania wote ni kwamba tuwe tunaongea na kufuatilia na kuhimizana ili kutokomeza vitendo hivi hapa nchini. Hata watawala ona sasa Baba anakuwa mwenyekiti wa chama, Mama mjumbe wa Nec na mtoto ni Mjumbe wa Nec je,hivi kweli hii ni demokrasia? Maana hapo yatafanywa maamuzi ya kifamilia katika masuala nyeti ya kitaifa.

Naomba tuungane kuupinga utawala huu wa kisultani. Kukaa kwetu kimya kutawapa kiburi watawala kwani watajua kuwa huwa tunaongea kwa muda mfupi na kutoweka, naomba tusiwe watu wa kupigia kelele matukio na kuayasahau bila majawabu.
 
Tatizo watanzania wanakamatwa kwa kuanzishiwa tukio juu ya tukio ili wasahau matukio mengine ni juzi tu dowans wameambiwa walipwe hii ilikuja kufutia swala la daudi ila la daudi likazidi so dowans imepigwa chini
 
Wana JF hii ni hatari kwa matarajio na ndoto za kutokomeza vitendo vya kinyama na ubadhilifu hapa nchini. Kuna mambo mengi sana ya unyanyasaji,ufisadi,ubadhilifu na usultan hapa nchini. Hii inajirudia kwa watanzania kila linapotokea jambo moja tunalipigia kelele kwa muda mfupi na kulitupilia mbali hata kama halijarekebishwa.

Ilipotokea ubadhilifu na mikataba ya ulaghai ktk shirika la umeme na kampuni ya Richmond,ikaja, epa,dowansi na mingine mingi tulipiga kelele na kuacha bila hata kutatua tatizo,ikaja mawaziri kula rushwa mf wizara ya utalii,wizara ya nishati na madini,wizara ya fedha na wizara nyingine tumenyamaza huku watuhumiwa wakiishia kuachia ngazi bila kufilisiwa. Haya vikaja vitendo vya kinyama dhidi ya binadam kwa watu kuuawa,mf mauaji ya igunga,ruvuma,singida,arusha,dr Ulimboka, Ally zona, na Mwangosi.

Tumekuwa maarufu kwa kupiga kelele jamvini bila kuchukua hatua stahiki ili kuinusuru Tanzania kwa vitendo hivi haramu. Wito kwa watanzania wote ni kwamba tuwe tunaongea na kufuatilia na kuhimizana ili kutokomeza vitendo hivi hapa nchini. Hata watawala ona sasa Baba anakuwa mwenyekiti wa chama, Mama mjumbe wa Nec na mtoto ni Mjumbe wa Nec je,hivi kweli hii ni demokrasia? Maana hapo yatafanywa maamuzi ya kifamilia katika masuala nyeti ya kitaifa.

Naomba tuungane kuupinga utawala huu wa kisultani. Kukaa kwetu kimya kutawapa kiburi watawala kwani watajua kuwa huwa tunaongea kwa muda mfupi na kutoweka, naomba tusiwe watu wa kupigia kelele matukio na kuayasahau bila majawabu.

Hapo penye rangi ya blue, wajumbe waliopiga kura na kupitisha ndio wa kulaumiwa! Hata wao wangefanya nini wakati serikali imesimika mizizi ya kujuana na kutokosoana au kutokuangushana. Hata kama mtu anakosea eti unakaa kimya kwa sababu anatoka chama chako!! We need another system in power!!
 
tatizo za ccm ilisha kufa yani waliomo ndani hawajitambui kabisa hawawezi hata kujua nini wanafanya na kwa manufaa ya nani. wako radhi hata kuua ili wabaki madarakani
 
Kwa nini sisi watz tunapenda kuckia matukio tu na sio kufanya dialoges mara mwanahalisi lafungiwa,mara mwangosi kauwawa,mara sumaye,kigwangala,bashe,mkono watemwa.cjui what is next?
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom