Donatila
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,557
- 21,512
Watanzania 12 wanashikiliwa na mamlaka nchini Msumbiji baada ya kwenda nchini humo kwenye shughuli za uwindaji bila kuwa na vibali.
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Homera amesema amezifikisha taarifa hizo kwa mkuu wa MKoa wa Ruvuma ili hatua zichukuliwe
Watanzania ambao wanashikiliwa nchini Msumbiji ni wakazi wa kijiji cha Mkapunda na wenje wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma ambapo vijiji hivyo vipo mpakani na kijiji cha Luimila cha wilaya ya Niassa nchini Msumbiji, Vijiji hivyo vya Tanzania na Msumbiji vinatenganishwa na Mto Ruvuma.