Watano wauawa huko Nyantorotoro - Geita

zomba

JF-Expert Member
Nov 27, 2007
17,240
3,910
Salama Mrisho wa Star TV ameleta habari sasa hivi za mauaji ya Raia 5 waliouliwa kinyama na magaidi bila ya hatia.

Magaidi watatu wanashikilwa na Polisi hadi sasa kwa tukio hilo.

Watanzania tuungane tuutokomeze ugaidi, wanatumalizia raia zetu wema hawa magaidi.

=====================
UHALISIA WA KILICHOTOKEA:

Mods huwa hawapotoshi, wako hapa kwa ajili ya kuhakikisha kila kitu kiko sawa humu jukwaani!

Wanaweza ku-verify mahali husika na kuweka sawa kama jambo halieleweki vizuri na mleta mada kama hili lako!

Lakini pia sisi wanachama wa JF tunaruhusiwa kufuatilia jambo na kuwaeleza mods kama unaweza kufanya hivyo kama kuna utata!

Sasa ngoja tukusaidie hili jambo vizuri:

Kwanza hakuna gaidi aliyeua, wala aliyeuawa!

Pili Watu waliouawa ni watano na ni vibaka ambao jana walikwenda kuvamia msibani na kukwapua sahani iliyokuwa na fedha za rambirambi shilingi 67,000 na wakaondoka nazo!

Tatu baada ya kuondoka uongozi wa Sungusungu wa katika kijiji hicho walianza msako na kubahatika kumpata mmoja wao ambaye baada ya kumhoji alikiri na kuwataja wenzake wanne!

Baada ya kuwataja wakakamatwa na sungusungu,wakati wanaendelea kuhojiwa wananchi wakapata taarifa wakawafuata wakaanza kuwasahambulia kwa mawe na silaha zingine za jadi!

Mmoja alivunjwa miguu yote mwiwili,waliotambuliwa majina ni wawili,mmoja ametambuliwa kwa jina moja na wengine bado hawajatambuliwa jina hata moja!

Hao ni vibaka,wawili waliotambuliwa majina nimMarwa Chacha, Shija Mlingwa, Ezekiel, wakazi wa Nyantorotoro wawili hawajafahamika.

Polisi wanawashikilia watu watatu akiwemo wa kiongozi mmoja wa sungusungu,wanaume wote wamekimbia familia zao kwa hofu ya kukamatwa.

Haya ni maelezo kamili niliyoyapata kutoka kwa kamanda wa Polisi mkoa wa Geita Leonard Paul katika mahojiano kati yangu na yeye kwa njia ya simu!

Mtoa mada alitaka tu kupamba habari ili ipate sapoti ya wana JF!

Kwa hiyo mods mnaweza kubadili kichwa cha habari vyovyote vile kulingana na hayo maelezo niliyowapa hapo juu,tusipende kuwapa watu presha huu ni mwisho wa mwaka.
 
Salama Mrisho wa Star TV ameleta habari sasa hivi za mauaji ya Raia 5 waliouliwa kinyama na magaidi bila ya hatia.

Magaidi watatu wanashikilwa na Polisi hadi sasa kwa tukio hilo.

Watanzania tuungane tuutokomeze ugaidi, wanatumalizia raia zetu wema hawa magaidi.

Speed yako kubwa sana mleta thread.. Au ulikuwa sehemu ya tukio? Hivi polisi wa Tanzania wanaweza kamata magaidi?
 
Salama Mrisho wa Star TV ameleta habari sasa hivi za mauaji ya Raia 5 waliouliwa kinyama na magaidi bila ya hatia.

Magaidi watatu wanashikilwa na Polisi hadi sasa kwa tukio hilo.

Watanzania tuungane tuutokomeze ugaidi, wanatumalizia raia zetu wema hawa magaidi.

nyantorotoro kaka,wamewauwaje?na kisa nini? Hebu tujuze zaidi maana tupo mbali na mkoa wetu mpya:.
 
Salama Mrisho wa Star TV ameleta habari sasa hivi za mauaji ya Raia 5 waliouliwa kinyama na magaidi bila ya hatia.

Magaidi watatu wanashikilwa na Polisi hadi sasa kwa tukio hilo.

Watanzania tuungane tuutokomeze ugaidi, wanatumalizia raia zetu wema hawa magaidi.

ni nyantorotoro..,wamewauwaje?na kisa nini? Hebu tujuze zaidi maana tupo mbali na mkoa wetu mpya:.
 
Bahati mbaya Sana vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ni reactive Sana badala ya kuwa proactive. Tutaangamia wengi bila kuuangalia upya mfumo wetu wa utendaji kazi wa vyombo hivi.
 
Salama Mrisho wa Star TV ameleta habari sasa hivi za mauaji ya Raia 5 waliouliwa kinyama na magaidi bila ya hatia.

Magaidi watatu wanashikilwa na Polisi hadi sasa kwa tukio hilo.

Watanzania tuungane tuutokomeze ugaidi, wanatumalizia raia zetu wema hawa magaidi.

Jamani kunatofauti ya magaidi na vibaka hawo ni vibaka tu
 
nyantorotoro kaka,wamewauwaje?na kisa nini? Hebu tujuze zaidi maana tupo mbali na mkoa wetu mpya:.

Yes, ni Nyantorotoro ni typo tu na nnadhani Moderator ataliona hilo na ku edit jina kwenye heading.
 
Last edited by a moderator:
Mmm sio wale walio iba shiingi elfu 60 wamechomwa moto? Sio magaidi jaman ni kifo cha simanzi sana.
 
Nasikitika na upotoshwa wa habari hii na mleta uzi watu hao ni wezi walienda kuiba pesa za rambi rambi kwa mzee mmoja hapo kijijini ndio wakakutana na dhahma hiyo jitahidi kuwa una sema facts hii taarifa nimeingalia punde na sasa ni habari za michezo
 
Salama Mrisho wa Star TV ameleta habari sasa hivi za mauaji ya Raia 5 waliouliwa kinyama na magaidi bila ya hatia.

Magaidi watatu wanashikilwa na Polisi hadi sasa kwa tukio hilo.

Watanzania tuungane tuutokomeze ugaidi, wanatumalizia raia zetu wema hawa magaidi.

Operesheni tokomeza nini?
 
BAKITA imekufa..kama ipo ianze mihadhara ya wazi kufundisha matumizi sahihi ya baadhi ya maneno ya Kiswahili.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Salama Mrisho wa Star TV ameleta habari sasa hivi za mauaji ya Raia 5 waliouliwa kinyama na magaidi bila ya hatia.

Magaidi watatu wanashikilwa na Polisi hadi sasa kwa tukio hilo.

Watanzania tuungane tuutokomeze ugaidi, wanatumalizia raia zetu wema hawa magaidi.

Taabu ya polisi wetu nina wasiwasi na definition yao ya gaidi (nisamehewe kwa hili). Wana uhakika ni magaidi na siyo MAJAMBAZI?? Hili jina la GAIDI tusilikimbilie kulitumia katika kila mauaji kabla ya kuwa na uhakika.....
 
kuteto wanauwana wale sio magaidi. Kilosa pia. Hata kama una chuki na uislam lkn sio kwa stahili hiyo.
 
Back
Top Bottom