Watangazaji wetu na weledi wao!

K A B U R U

JF-Expert Member
Nov 24, 2011
817
1,067
Jana nilikuwa natazama taarifa ya habari saa moja usiku kupitia kituo cha luninga cha Channel Ten, nilipata ukakasi baada ya kumsikiliza mtangazaji wa habari za kimataifa akipata taabu kutamka mji wa Munich

Hili alilitaja kimakosa kama mara nne mpaka nikajiuliza ina maana hajawahi hata kulisikia neno hili kabla, ili ajisahihishe?

Leo ninasikiliza Radio Free Africa kipindi cha Watanzania Tuzungumze magazeti, mtangazaji ameanza na gazeti la Nipashe anatamka chama cha wanasheria Tanganyika kama TLC badala ya TLS. Amerudia tena kutamka TLC akipitia gazeti la Mtanzania.

MY TAKE:
Huwezi kujua kutamka maneno yote hasa yale ya lugha za kigeni kama kijerumani na kifaransa, lakini kama mtangazaji ni vizuri ukajiridhisha kama sehemu ya maandalizi ya kipindi jinsi ya kutamka maneno yaliyopo kwenye kipindi chako.

Tuweze kuwa mazoea ya kuwa na uwanja mpana wa ufahamu wa mambo yanayotuzunguka katika taaluma zetu, mfano mtangazaji wa taarifa za habari ni vema akawa mfuatiliaji wa habari mbalimbali zinazotangazwa na vyombo vingine hasa vya kimataifa badala ya kujikita kuchonga sauti peke yake.

The content is what matters the most.
 
Na mimi nimemsikia wa Rfa "Pique kataja Paku" sasa kimbembe ni kutaja "Solkjaer"(Sosha) katamka Soka na hana hata aibu.
 
Wana Matatizo sana ya kutokuwa watafiti na wachunguzi wa mambo yanaynhusu taaluma yao. Kituko Kingine ni utamkaji wa mji mkuu wa Ubelgiji, Brussels wanautamka isivyo. Hata Dar Es Salaam Kuna baadhi ya watangazazaji wanaitamka kwa ukakasi sana. Kukosa weledi kupo pia kwenye taaluma zingine nyeti kama ualimu. Unakuta Mwalimu anatia aibu kwenye mambo ya ufahamu kuhusu fani yake hajui mambo mengi yaliyopo yahusuyo taaluma yake. Wanataaluma Wanapaswa Kuwa Wadadisi wa mambo mengi yahusuyo fani zao (well informed ).
 
Cheap Labour Nalo Ni Tatizo. Mmiliki Wa Media Anajiwekea Ndugu Yake Anayeweza Kubabaisha.
 
Tatizo ni wamiliki wa vyombo husika unakuta mtu alikuwa mchekeshaji kapewa kazi ya utangazaji nn kinafuata kama si kuvurunda..... Juzi kuna mtangazaji wa redio kubwa tu hapa nchini... Jjna Haiti limemshinda na kuitaja Aiti karudia kama mara nne.... Tatizo ni cheap labour!
Jana nilikuwa natazama taarifa ya habari saa moja usiku kupitia kituo cha luninga cha Channel Ten, nilipata ukakasi baada ya kumsikiliza mtangazaji wa habari za kimataifa akipata taabu kutamka mji wa Munich, hili alilitaja kimakosa kama mara nne mpaka nikajiuliza ina maana hajawahi hata kulisikia neno hili kabla, ili ajisahihishe?
Leo ninasikiliza Radio Free Africa kipindi cha Watanzania Tuzungumze magazeti, mtangazaji ameanza na gazeti la Nipashe anatamka chama cha wanasheria Tanganyika kama TLC badala ya TLS. Amerudia tena kutamka TLC akipitia gazeti la Mtanzania.
MY TAKE:
Huwezi kujua kutamka maneno yote hasa yale ya lugha za kigeni kama kijerumani na kifaransa, lakini kama mtangazaji ni vizuri ukajiridhisha kama sehemu ya maandalizi ya kipindi jinsi ya kutamka maneno yaliyopo kwenye kipindi chako.
Tuweze kuwa mazoea ya kuwa na uwanja mpana wa ufahamu wa mambo yanayotuzunguka katika taaluma zetu, mfano mtangazaji wa taarifa za habari ni vema akawa mfuatiliaji wa habari mbalimbali zinazotangazwa na vyombo vingine hasa vya kimataifa badala ya kujikita kuchonga sauti peke yake. The content is what matters the most.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jana nilikuwa natazama taarifa ya habari saa moja usiku kupitia kituo cha luninga cha Channel Ten, nilipata ukakasi baada ya kumsikiliza mtangazaji wa habari za kimataifa akipata taabu kutamka mji wa Munich, hili alilitaja kimakosa kama mara nne mpaka nikajiuliza ina maana hajawahi hata kulisikia neno hili kabla, ili ajisahihishe?
Leo ninasikiliza Radio Free Africa kipindi cha Watanzania Tuzungumze magazeti, mtangazaji ameanza na gazeti la Nipashe anatamka chama cha wanasheria Tanganyika kama TLC badala ya TLS. Amerudia tena kutamka TLC akipitia gazeti la Mtanzania.
MY TAKE:
Huwezi kujua kutamka maneno yote hasa yale ya lugha za kigeni kama kijerumani na kifaransa, lakini kama mtangazaji ni vizuri ukajiridhisha kama sehemu ya maandalizi ya kipindi jinsi ya kutamka maneno yaliyopo kwenye kipindi chako.
Tuweze kuwa mazoea ya kuwa na uwanja mpana wa ufahamu wa mambo yanayotuzunguka katika taaluma zetu, mfano mtangazaji wa taarifa za habari ni vema akawa mfuatiliaji wa habari mbalimbali zinazotangazwa na vyombo vingine hasa vya kimataifa badala ya kujikita kuchonga sauti peke yake. The content is what matters the most.
kuna mmoja wa EAtv anaongea kiswahili af anasema" okey"
 
Channel ten ni ya CCM

Star tv-Mmiliki wake ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa mwanza.

So majibu umeshayapata mpk hapo.
 
Tuliaminishwa kuwa sheria ya huduma ya habari ingetatua mapungufu haya kwa kuwa na bodi ya waandishi wa habari kama ilivyo kwa wahasibu na wahandisi. Hili limekwama wapi?
 
Jana nilikuwa natazama taarifa ya habari saa moja usiku kupitia kituo cha luninga cha Channel Ten, nilipata ukakasi baada ya kumsikiliza mtangazaji wa habari za kimataifa akipata taabu kutamka mji wa Munich, hili alilitaja kimakosa kama mara nne mpaka nikajiuliza ina maana hajawahi hata kulisikia neno hili kabla, ili ajisahihishe?
Leo ninasikiliza Radio Free Africa kipindi cha Watanzania Tuzungumze magazeti, mtangazaji ameanza na gazeti la Nipashe anatamka chama cha wanasheria Tanganyika kama TLC badala ya TLS. Amerudia tena kutamka TLC akipitia gazeti la Mtanzania.
MY TAKE:
Huwezi kujua kutamka maneno yote hasa yale ya lugha za kigeni kama kijerumani na kifaransa, lakini kama mtangazaji ni vizuri ukajiridhisha kama sehemu ya maandalizi ya kipindi jinsi ya kutamka maneno yaliyopo kwenye kipindi chako.
Tuweze kuwa mazoea ya kuwa na uwanja mpana wa ufahamu wa mambo yanayotuzunguka katika taaluma zetu, mfano mtangazaji wa taarifa za habari ni vema akawa mfuatiliaji wa habari mbalimbali zinazotangazwa na vyombo vingine hasa vya kimataifa badala ya kujikita kuchonga sauti peke yake. The content is what matters the most.
Nami nimeskia hilo la TLC badala ya TLS

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo ni kuwa hawajiandai. Ilitakiwa kabla ya kwenda kusoma taarifa hizo kujiuliza hata kwa wenzake namna ya kutamka baadhi ya maneno. Wengi wanakosea sana
 
Tatizo ni moja tu - kutopenda kusoma. Na hali kadhalika tatizo linasambaa mpaka katika fani nyingine. Kujenga 'competency 'ni shughuli pevu kwa muafrika.
 
East Africa napo kuna mtangazaji anapenda kurudia maneno 'STILL BADO' hasa kipindi cha michezo. Sijui hajui matumizi ya haya maneno??

Sent using Jamii Forums mobile app
Wachambuzi wengi wame muiga Dr Liki ila hawajui jamaa ana exposure sasa wao ili waonekane wabobezi basi utakuta wana chomeka na english matokeo yake ni kituko. Ata sijui ni redio gani ila mara nyingi nasikiaga nikiwa saloon nanyoa, hao wa EATV wanakuaga watatu aisee huwaga ni aibu. Wachambuzi tumieni kiswahili mwanzo mwisho, mnazingua sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom