G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Naam, watangazaji takribani watatu wa shirika la utangazaji nchini TBC wanawania nafasi za uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kwa sasa watangazaji hao sitaweza kuwataja hapa ingawa wengine tayari wamejiweka hadharani kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii.
Tuliwahi kusema kuwa wafanyakazi wa TBC wako pale siyo kikazi ila kuvizia! Wafanyakazi takribani wote wa shirika lile wanavizia nafasi za uteuzi za kichama au wengine ndiyo kama hivyo kutafuta fursa ya kuwania uongozi ndani ya CCM.
Hawa bila shaka watatumia kigezo cha "Nilikipa kipaumbele chama kwenye taaluma yangu" ili wapate kura. Huu ni ujinga mkubwa!
Kwenye nchi nyingi huwezi kuona vituko hivi wanavyoonyesha hawa watangazaji "wajinga" zaidi ya hapa kwetu. Mwisho wa siku ni kuharibu sura ya kituo hicho na kukifanya kuendelea kuonekana kituo cha hovyohovyo kisicho na ufanisi.
Tuliwahi kusema kuwa wafanyakazi wa TBC wako pale siyo kikazi ila kuvizia! Wafanyakazi takribani wote wa shirika lile wanavizia nafasi za uteuzi za kichama au wengine ndiyo kama hivyo kutafuta fursa ya kuwania uongozi ndani ya CCM.
Hawa bila shaka watatumia kigezo cha "Nilikipa kipaumbele chama kwenye taaluma yangu" ili wapate kura. Huu ni ujinga mkubwa!
Kwenye nchi nyingi huwezi kuona vituko hivi wanavyoonyesha hawa watangazaji "wajinga" zaidi ya hapa kwetu. Mwisho wa siku ni kuharibu sura ya kituo hicho na kukifanya kuendelea kuonekana kituo cha hovyohovyo kisicho na ufanisi.