Kinyungu
JF-Expert Member
- Apr 6, 2008
- 17,365
- 33,004
Ndugu wana JF pamoja na kujua kuwa kuna watu wangependa muungano wa Tanganyika na Zanzibar uendelee kuwepo nimeona nilete hii mada hapa ili nipate mawazo ya wadau wa JF juu ya muungano huu amabao kwangu naona ni wa gharama zisizo na lazima na usio na faida yoyote kwa pande mbili. Japo kuna mengi yanayonikera kwenye muungano huu haya hapa ndio haswa yanayonitia kichefuchefu:
Kwa nini Zanzibar imepewa upendeleo wa kuwa na wabunge wengi sana kwenye bunge la muungano ukilinganisha na idadi yao ya watu? Kwa maoni yangu ingetosha Zanzibar yote kuwa na wabubge watano tu. Wawili Pemba na watatu Unguja. Ukiangalia matokeo ya uchaguzi uliopita mbunge wa Zanzibar anachaguliwa kwa wastani wa kura 4000-6000 kwa mshindi. Idadi hii ni ndogo sana ukilinganisha na wabunge wa huku bara. Ndio kusema kama hali hii ingelikuwa huku kwetu basi labda kila mtaa ungekuwa na mbunge. Hizi ni gharama zisizo na maana na ni sababu moja ya kuvunja muungano.
Kila siku tumekuwa tukisikia malalamiko ya Wazanzibar kuhusu mafuta na rasilimali nyinginezo wakitaka ziwe zao kama dhahabu zilivyo zetu. Wanataka rais wao atambuliwe kama amiri jeshi mkuu na kupigiwa mizinga. Sasa kama wanataka mamlaka yote hayo kwa nini tusiachane nao wakaangali mustkabali wao na sisi tungahangaika na wetu?
Najua kero zipo nyingi lakini naomba tuchangie ili tujuzane kama kweli muungano huu una manifaa yoyote kwetu.
Kwa nini Zanzibar imepewa upendeleo wa kuwa na wabunge wengi sana kwenye bunge la muungano ukilinganisha na idadi yao ya watu? Kwa maoni yangu ingetosha Zanzibar yote kuwa na wabubge watano tu. Wawili Pemba na watatu Unguja. Ukiangalia matokeo ya uchaguzi uliopita mbunge wa Zanzibar anachaguliwa kwa wastani wa kura 4000-6000 kwa mshindi. Idadi hii ni ndogo sana ukilinganisha na wabunge wa huku bara. Ndio kusema kama hali hii ingelikuwa huku kwetu basi labda kila mtaa ungekuwa na mbunge. Hizi ni gharama zisizo na maana na ni sababu moja ya kuvunja muungano.
Kila siku tumekuwa tukisikia malalamiko ya Wazanzibar kuhusu mafuta na rasilimali nyinginezo wakitaka ziwe zao kama dhahabu zilivyo zetu. Wanataka rais wao atambuliwe kama amiri jeshi mkuu na kupigiwa mizinga. Sasa kama wanataka mamlaka yote hayo kwa nini tusiachane nao wakaangali mustkabali wao na sisi tungahangaika na wetu?
Najua kero zipo nyingi lakini naomba tuchangie ili tujuzane kama kweli muungano huu una manifaa yoyote kwetu.