Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,060
- 22,755
Mtu unaamka nyumbani kwako asubuhi, pamoja na mawimbi na dhoruba hutulii kwako...unavuka bahari kuelekea nyumbani kwa mwenzio. Jioni baada ya kusetiriwa na kuchuma unachoweza huko ugenini unafunga safari, unavuka tena bahari hadi nyumbani kwako na kuuchapa usingizi mwonono ukisubiri kesho yake uende kuchuma tena.
Cha ajabu ni kuwa pamoja na kufaidi vya mwenzio, huachi kulalama kwamba kakung'ang'ania huku uhuru unao wa kuamua utakachoona kinakufaa! Ama ni kama yale ya kupe...jua linampiga mchana wote toka asubuhi hadi jioni lakini kamng'ang'ania ng'ombe kwani afanye nini? Aache kunyonya? Tofauti na Wazanzibari, kupe halalamiki.
Cha ajabu ni kuwa pamoja na kufaidi vya mwenzio, huachi kulalama kwamba kakung'ang'ania huku uhuru unao wa kuamua utakachoona kinakufaa! Ama ni kama yale ya kupe...jua linampiga mchana wote toka asubuhi hadi jioni lakini kamng'ang'ania ng'ombe kwani afanye nini? Aache kunyonya? Tofauti na Wazanzibari, kupe halalamiki.