John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, Sunday Deogratias ametoa onyo kwa watu watakao onekana kung'oa vibao vya anuani ya makazi na kwenda kuuza kama vyuma chakavu na kwa watakaobainikia watachukuliwa hatua za kisheria.
Hayo ameyasema alipokuwa katika hafla ya siku ya wanawake wilayani humo na kuongeza kuwa kuna mikoa ambayo zoezi hili la vibao vya makazi tayari lilifanyika lakini watu waling'oa vibao na kuviuza hivyo katika Halmashauri yake hatarajii jambo hilo litokee ambapo amewataka viongozi wote wa ngazi ya kata na vijiji pamoja na wananchi kuvilinda vibao hivyo ili visiharibiwe.
"Viongozi wote wa kata na vijiji ninaomba mkahakikishe vibao hivi vinakaa katika hali ya usalama, nanyi wananchi mnatakiwa kila mmoja awe mlinzi wa mwenzie ili kuhakikisha Halmashauri yetu inakaa katika mpangilio mzuri wa mitaa," Amesema Mkurugenzi.
“Tunataka tutambue nyumba na barabara zetu, mfano unaweza kuagiza kitu mtandaoni unaletewa hadi nyumbani kwako.”
Source: Wasafi FM
Hayo ameyasema alipokuwa katika hafla ya siku ya wanawake wilayani humo na kuongeza kuwa kuna mikoa ambayo zoezi hili la vibao vya makazi tayari lilifanyika lakini watu waling'oa vibao na kuviuza hivyo katika Halmashauri yake hatarajii jambo hilo litokee ambapo amewataka viongozi wote wa ngazi ya kata na vijiji pamoja na wananchi kuvilinda vibao hivyo ili visiharibiwe.
"Viongozi wote wa kata na vijiji ninaomba mkahakikishe vibao hivi vinakaa katika hali ya usalama, nanyi wananchi mnatakiwa kila mmoja awe mlinzi wa mwenzie ili kuhakikisha Halmashauri yetu inakaa katika mpangilio mzuri wa mitaa," Amesema Mkurugenzi.
“Tunataka tutambue nyumba na barabara zetu, mfano unaweza kuagiza kitu mtandaoni unaletewa hadi nyumbani kwako.”
Source: Wasafi FM